Uchaguzi 2020 Sababu zinazofanya Magufuli apendwe na Watanzania wengi

Uchaguzi 2020 Sababu zinazofanya Magufuli apendwe na Watanzania wengi

Mishahara hewa ilianza kushughulikiwa toka enzi za JK, labda kwakuwa yeye alipoingia ndio alikuta utaratibu umeenza akatembeans mchakato.
Ni jambo zuri pia kama lilishaanza kushughulikiwa na JK, lakini yeye JPM amekuja kulimzaliza na amerudisha nidhamu katika utendaji.
 
Weka deni la taifa kwenye kipindi chake, linganisha na deni alilokuta la miaka 50+, kisha nipe return ya miradi aliyojenga kuendana na deni alilokopa. Sina hakika kama unajua terms za mikopo ya sasa na marejesho yake. Kama unamudu hoja hizo rejea.

Nina uwezo wa kutosha na ndio eneo nililo bobea. Nitakuacha njiani ama utaleta ubishi wa kitoto.
 
Mkuu tumia akili tu ya kawaida, umeshasema vyombo vya ulinzi na usalama, hivi unawezaje kutumbua vyeti fake? Na ikiwa kuna watu wameingia kwenye majeshi n.k kwa vipaji vyao tu. Lazima uzingatie usalama wa nchi.
Hii sio sababu
 
Hakuna wilaya ambayo haijaguswa na miradi yenye faida kwa wananchi kipindi hiki Cha awamu ya tano
 
Kaondoa rushwa yote. Karejesha maadili kazini, kayabana majizi na mafisadi. Kazuia upoteaji wa mapato, kajenga viwanda, Kathubu kwenye mradi mkubwa wa umeme, kathubutu kuhamishia makao makuu ya serikali Dodoma, Karudisha elimu bure, karudisha heshima kazini, kazuia uizi wa madini yetu.
Eti elimu bure michango kibao
 
Mkuu tumia akili tu ya kawaida, umeshasema vyombo vya ulinzi na usalama, hivi unawezaje kutumbua vyeti fake? Na ikiwa kuna watu wameingia kwenye majeshi n.k kwa vipaji vyao tu. Lazima uzingatie usalama wa nchi.

Kwahiyo hao wa vyeti fake huko taasisi nyingine hakukuwa na wenye vipaji? Ukitaka sifa ya utendaji fulani hupaswi kuacha shaka ya maamuzi yako, Double standard ile haikuwa sawa, labda kwakuwa vyombo vya dola wanaweza kutumika kukandamiza wananchi na kumlinda kiongozi, na sio usalama wa nchi kama unavyotaka kusema.

Kwa mfano mimi nilitaka wanaopunguzwa isiwe kwa kigezo cha vyeti fake, bali rekodi ya uchapa kazi, na isiwe na macho. Kisha wote wanaoajiriwa kuanzia sasa vyeti halali iwe ni kigezo namba moja.

Nitakupa mfano mzuri wa kisemacho, kuna jamaa yangu ni daktari tena bingwa, alifukuzwa kazi maana kuanzia A level alitumia cheti cha mtu mwingine. Lakini form VI alifaulu vizuri, na chuoni alifanya vizuri sana.

Nje ya matokeo mazuri ya shuleni ukiachia form IV, alikuwa ni doctor mzuri hasa. Na mchapa kazi. Huoni hapo tulipoteza mtu mzuri kwa kosa dogo sana la huko nyuma?
 
Wanaomchukia JPM ni wivu tu, hawana sababu nyingine.
 
Kura atakazopata mgombea wenu mwaka huu ni zile atakazo zawadia na Tume ya Uchaguzi.
Hata mumpambe vipi, HAKUBALIKI. Na sababu kubwa ni hulka yake ya ubabe na kupenda kujiamulia kila kitu.
Serikali hii, haina mambo ya kuunda tume kufatilia uozo, Ni tit for tat,unapomuona jamaa amefika sehemu ujue data zote anazo A-Z, kinachofata Ni maamuzi tu, kulingana na mamlaka aliyonayo kikatiba.
 
  • Thanks
Reactions: Dua
Njaa itatawala kwa wavivu, wanaosubiri kutafutiwa na wanasiasa.
Njaa itatawala pale ambapo mtashindwa kuwalipa wakulima wa korosho pesa zao,kuwalipa wakulima wa pamba pesa zao,mtashindwa kuongeza watumishi mishahara, mtashindwa kuweka mazingira mazuri ya ukuzaji wa sekta binafsi.
 
Kwahiyo hao wa vyeti fake huko taasisi nyingine hakukuwa na wenye vipaji? Ukitaka sifa ya utendaji fulani hupaswi kuacha shaka ya maamuzi yako, Double standard ile haikuwa sawa, labda kwakuwa vyombo vya dola wanaweza kutumika kukandamiza wananchi na kumlinda kiongozi, na sio usalama wa nchi kama unavyotaka kusema...
Mkuu kwa hali ya kawaida huwezi kutumbua jeshi, kama nilivyosema kwa sababu za kiusalama.

Tambua pia wapo wasomi wazuri mitaani ambao wana vyeti vizuri na taaruma nzuri lakini hawakupata nafasi kwa sababu ya watu waliokua na vyeti fake ambao wapo makazini.
 
Niko zangu zenji huku tunaimba UBWABWAAAAAA na Rais wangu kipenzi Hashim Rungwe Spunda . Sababu inanifanya nimkubali Rungwe ni vile hana stress kabisa yaani nchi itakuwa shwari no Stress ukitaka bahari unaletewa tu kamfereji 😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Nina uwezo wa kutosha na ndio eneo nililo bobea. Nitakuacha njiani ama utaleta ubishi wa kitoto.

Unachekesha kwelikweli, kwani hoja unazokuja nazo ni msahafu au biblia kwamba nitakubaliana na kila usemacho? Nina akili timamu, utakachoniambia ni lazima nipime na sio uje na hoja unazotaka nikubaliane na ww kama toy. Una hoja weka, upotoshaji wowote utakutana na mapingamizi makali.
 
Mkuu kwa hali ya kawaida huwezi kutumbua jeshi, kama nilivyosema kwa sababu za kiusalama.

Tambua pia wapo wasomi wazuri mitaani ambao wana vyeti vizuri na taaruma nzuri lakini hawakupata nafasi kwa sababu ya watu waliokua na vyeti fake ambao wapo makazini.

Sielewi usemayo kuhusu kuwatumbua wanajeshi ni hatari kwa usalama. Mbona wanastaafu lakini hakuna kitisho cha usalama? Au ukiwa mwanajeshi unakuwa na kinga ya kuvunja sheria? Hao wanajeshi wameogopwa kwakuwa madictor huwatumia kutawala kwa mkono wa chuma. Hivyo kutokutumbuliwa ilikuwa ni kwa manufaa binafsi ya aliyeendesha zoezi la utumbuzi.

Narudia tena,vyeti sio vinavyofanya kazi bali uwezo. Kigezo sahihi kilipaswa kuwa kiwango cha uchapa kazi na weledi, kisha wale wote wenye uwezo duni wangewapisha wenye vyeti halali. Nimekupa mfano wa huyo jamaa yangu daktari ili ujue nini ninasema.
 
Kuna wanawake wengi wa Afrika wanapenda mwanamme mbabe, mwenye maneno ya kibabekibabe, hususan akiwa na madaraka.

Hawa wengi wana saikolojia na baiolojia ya kutaka kuwa na mtu mbabe anayeweza kuwatetea.Hiyo ni saikolojia ya muda mrefu, si kwa watu tu, bali hata wanyama wanayo.

Hivyo, kuna wanawake wengi wanampenda bila hata kujua hilo.

Wanaume wengine pia wana saikolojia ya kumkubali "Alpha male in the pack".

Washajua usipomkubali unaweza kupigwa risasi ukajeruhiwa au kuuawa.

Tabia hii si kwa watu tu, hata nyani na sokwe wanayo.

Nyani mdogo anatakiwa kumkubali Alpha male wa eneo, ama kama hamkubali ahame eneo atafute eneo lake jipya.

Ndiyo maana utasikia "Magufuli babalao, kama hamtaki hameni nchi".

Hizi si sababu zote, na kuna wengi wanampenda kwa mengi.

Lakini nimewaangalia watu wengine, hususan watu masikini ambao utawala wa Magufuli haujawasaidia lolote binafsi, na bado wanamshabikia, nikagundua kuna watu wengi wanataka kuwa sehemu ya "timu ya ushindi" tu, wampigie jarambe "Magufuli babalao, Alpha Male.Tingatinga".

By the way hata Malecela alishaitwa Tingatinga, alivyoshikishwa adabu, na jina akanyang'anywa.

Hilo linaonesha jinsi gani kuna watu wanaopenda viongozi wababe nchini mwetu.
 
Niko zangu zenji huku tunaimba UBWABWAAAAAA na Rais wangu kipenzi Hashim Rungwe Spunda . Sababu inanifanya nimkubali Rungwe ni vile hana stress kabisa yaani nchi itakuwa shwari no Stress ukitaka bahari unaletewa tu kamfereji 😂😂😂😂😂😂😂😂
😂😂😂😂😂😂😂😂😂 Rungwe anacheza game la siasa kama Messi yaani
 
Hapo kwenye namba 10 napinga kabisa hakuna elimu ya bure, hivi mtoa post unajua maana ya neno bure basi waulize majiran zako watakumbia maana yake.
 
Back
Top Bottom