Sabaya na wenzake washinda Rufaa dhidi ya Serikali kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

Sabaya na wenzake washinda Rufaa dhidi ya Serikali kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

Mahakama ya Rufaa ya Tanzania imetupilia mbali Rufaa iliyokatwa na Upande wa Jamhuri, ikipinga uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Arusha, kumuachilia huru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili waliokuwa wamehukumiwa Kifungo cha miaka 30 jela.

Hukumu hiyo iliyosomwa na Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Abesiza Kalegeya, leo Ijumaa Novemba 17, 2023, imesema hakukuwepo na tukio la unyang’anyi wa kutumia silaha, badala yake Mjibu rufani wa kwanza Lengai Ole Sabaya, alikuwa katika majukumu yake halali ya kufuatilia Makosa ya uhujumu uchumi kama ilivyoelezwa na Mashahidi wenyewe wa upande wa mashtaka.

Mahakama hiyo ya rufaa iliyokaa chini ya Mwenyekiti wake Jaji Jacob Mwambegele imeeleza zaidi kwamba, Mahakama ya Hakimu Mkazi iliyomtia hatiani Sabaya na wenzake, ilikosea kutochambua ushahidi unaoonyesha wazi kwamba, haiijawahi kutokea Jambazi akamate Mtuhumiwa, amnunulie Ndizi na baadae kumpeleka Polisi kama Mashahidi wenyewe walivyoelezwa kutendewa na Sabaya.

Majaji wameeleza hiyo ni aina ya kwanza ya unyang’anganyi wa Majambazi kuepeleka waliowaibia Mahakamani, na kuhitimisha kwamba Wajibu rufaa waliachiwa kihalali na Mahakama Kuu.

Mkurugenzi wa Mashtaka alikata Rufaa kupinga uamuzi wa Jaji E. Kisanya, kuwaachilia huru Lengai Ole Sabaya, Sylivester Nyegu na Daniel Mbura, waliokuwa wamehukumiwa Kifungo cha miaka 30 jela na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Arusha.
Mbwa wa msoga wanazidi kuaibika na bado kesi ya uhaini ya jiwe inawangoja
 
Lilikuwa swala la muda tu, mahakama zetu zipo kwaajili ya wanyonge ila sio wanasiasa au watu wenye pesa.
 
The expected! Mahakama za kishenzi. Kama walitoa hukumu kuwa Wakurugenzi kusimamia kura haina shida kwa vile wameapa kutenda haki, basi ujue hakuna mahakama ni takataka tu mbona wanajeshi wanapindua serikali ingawa wamaepa? chini ya viapo vyao?
Sio Mahakama za kishenzi, ni waendesha mashtaka wabovu. Kanuni ya mahakama, hata kama Baba Yako ameshitakiana na shetani, shetani aka argue vizuri Kesi yake, basi shetani atapewa Haki.

(Sasa, jambazi linakuwa huru, na huenda likapewa tena nafasi Fulani. Na safari hii litataka kutoa watu Roho. Tusubiri tu)
 
Kweli wema n akiba jamaa kapangua kesi kwa ndiz alzonunua kumpa mshitak😂 huyu wakil n James bond kabsa
 
Mtu tangu azaliwe hajawahi ondoka Songea bomba mbili, lakini amekazana Kuwa Sabaya Yupo guilty.
How yaani? Ulimuona wapi? Akifanya huo uhalifu?
Tujichunge Tusipandikiziwe Chuki, mchukie mtu ukiwa una uhakika unachochukia ni nini
Sio kwa sababu watu wanachukia basi na wewe unachukia tu.
 
Viongozi wa nchi hii ovyo kabisa! Afu bila aibu waweza mpa cheo kama walivyofanya kwa makonda! na watanzania kwa ujinga wao, watashabikia kama wanavyofanya kwa konda!
 
The expected! Mahakama za kishenzi. Kama walitoa hukumu kuwa Wakurugenzi kusimamia kura haina shida kwa vile wameapa kutenda haki, basi ujue hakuna mahakama ni takataka tu mbona wanajeshi wanapindua serikali ingawa wamaepa? chini ya viapo vyao?
Una Wakati mgumu sana wewe kilaza wa mbowe

Yajayo yatakufanya uitafute milembe mwenyew
 
Viongozi wa nchi hii ovyo kabisa! Afu bila aibu waweza mpa cheo kama walivyofanya kwa makonda! na watanzania kwa ujinga wao, watashabikia kama wanavyofanya kwa konda!
Peleka mashitaka mahakamani.. pumbavu
 
Mahakama ya Rufaa ya Tanzania imetupilia mbali Rufaa iliyokatwa na Upande wa Jamhuri, ikipinga uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Arusha, kumuachilia huru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili waliokuwa wamehukumiwa Kifungo cha miaka 30 jela.
Unaweza kuona ameshinda kwa maelekezo ya Mwenezi
 
Majaji wanaosubiri wapigiwe simu toka Ikulu ili kujua watoe hukumu ya namna gani, wana faida gani kwa Taifa?

Mtu wa karibu na ikulu, Rostam Aziz alikwishaeleza kuwa hakuna mwekezaji anayeweza kuja kuwekeza Tanzania, halafu akubali mgogoro usuluhishwe na mahakama za Tanzania ambazo hutoa hukumu kwa maelekezo ya Serikali.

Serikali aliamua kumkomesha Sabaya, iliporidhika amesota vya kutosha ilimwachia. Sabaya alipotaka kukoa wakamnyamazisha kwa tishio la rufaa. Aliposujudia, wameamua kumwachia tena. Akizidi kusujudia, atapewa ukuu wa mkoa.
 
Back
Top Bottom