Sadaka kumpa mzazi ni bora kuliko kuipeleka kwenye nyumba za ibada

Watu walioanzisha makanisa watakanusha hoja yako . Mimi nakuunga mkono , ukishawapa wazazi , angalia majirani wenye shida uwasaidie kuliko kuwapelekea mchwa waliojificha makanisani. Wengi wakiitikia wito wako makanisa mengi yatafungwa. Hawa watu wanakula kilaini Sana , eti kitendo Cha kunikumbusha Mungu anakupenda umpe sadaka ! Mimi ninajua Mungu anakupenda .
 

Uzuri ni kwamba imani zetu zinatufundisha kila kitu. Katika kutoa ili sadaka yako ipokelewe kitu cha kwanza kabisa unatakiwa kutoa kwa imani huku ukiwa na upendo na watu wako

Kumbukumbu la torati 14: 22-24
22 Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi (10%) katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka. 24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako; 25 ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako;


Hagai 1: 5-10
"5 Basi sasa, Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. 6 Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka. 7 Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. 8 Pandeni milimani, mkalete miti, mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana. 9 Mlitazamia vingi, kumbe vikatokea vichache; tena mlipovileta nyumbani nikavipeperusha. Ni kwa sababu gani? Asema Bwana wa majeshi. Ni kwa sababu ya nyumba yangu inayokaa hali ya kuharibika, wakati ambapo ninyi mnakimbilia kila mtu nyumbani kwake. 10 Basi, kwa ajili yenu mbingu zimezuiliwa zisitoe umande, nayo nchi imezuiliwa isitoe matunda yake."


Mungu wetu ni Mungu wa kiasi, na aliweka taratibu katika kutoa.....

Marko 12:17 anatuambia​

"Yesu akajibu, akawaambia, Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu. Wakamstaajabia sana."



Ukitoa sadaka vibaya Mungu hapokei ni kujichosha tuu

1 Timotheo 5:8 anatuambia​

"Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

Hakuna anayeweza sema ametoa sadaka hadi kushindwa kumtunza mzazi wake au kusaidia watu wa nyumba yake na wahitaji"


Tusimtafute Mungu sababu ya kutuwahudumia wazazi
 
Na wazazi wahakikishe shida zote za watoto na wanandugu nyumbani zimetatuliwa tayari ndipo waanze kujazia vipato kina gwaji boy.
 
Sadaka kanisani(unapo weka imani yako hata kama ni kwa mganga)
msaada kwa wasio huwez
a
Matumizi kwa familia (wazazi ndugu jamaa na marafiki)

Usichanganye
 
Majirani unawajua vizuri wewe!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Haws ndo nawakusudia mimi.

Mzazi ana hangaika huku wewe unafurahisha waumini.

Aisee Mungu hayupo hivyo bhana.
 
Haws ndo nawakusudia mimi.

Mzazi ana hangaika huku wewe unafurahisha waumini.

Aisee Mungu hayupo hivyo bhana.
 
Hagai kamaliza kabisa, hawajui kila mtu ataubeba msalaba wake, mazazi hatabeba maovu ya mtoto wala mtoto hatabeba ya mzazi, kila kitu kifanyike kwa nafasi yake! Mzazi ni MUNGU wa pili hivyo wakwanza yupo pia.

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Safi mkuu

Bila shaka kwa uislamu sadaka ni tofauti sana na zaka tena sana.

Sijajua katika ukristo ,ila uislamu zaka na sadaka ni tofauti,zaka wanatoa watu waliofikia kiwango fulani cha pesa kila mwaka wanatoa,hii iwe wanasaidia wazazi au laa lazima watoe.

Kwenyw uzi nimegusia sadaka sio zakka
 

Hakuna excuse kwenye kutoa. Mungu na serikali wana miongozo yao iliyo rasmi kabisaaa

Mungu alishasema Kipimo chake ni 10% ya kila tunachoingiza iwe ni pesa au bidhaa au mazao...
Serikali nayo TRA ameshaweka viwango vyake

Na kinachobaki bado kikubwaaaa ndio tuwaangalie wazazi, ndugu na wahitaji wengine
Hapa ni kujiongeza na kujiongoza mwenyewe kwa kuangalia uhitaji wa mtu
 

Zaka ni tofauti na sadaka...

Zaka ni 10% ya kipato chochote anachotakiwa kutoa mtu yoyote anayelipwa kama ujira au anachozalisha. Iwe ni mshahara, mazao, mifugo....

Sadaka inatolewa kwa kiasi unachojaaliwa.......

Ila hili ya kutokutoa huduma kwa mzazi sababu eti unamtolea Mungu limekaa upandeupande
 
Sijajua umeupokea vipi uzi wangu ama umeufahamu vipi lakini makusudio tangu kama nilivyosema ni hivi..

Jamaa anamsahau mama anaona kwa kuwa haombwi basi hatoi kwa mama,lakini ibadani ikiitajika sadaka huyo wa mwanzo kutoa ilhali wazazi wake hawana hali.

Huyu ndio niliyemkusudia,sio kwamba anasema mwenyewe kwamba anashindwa kuwapa wazazi kwa sababu ya sadaka no,bali anasahau kama wazazi wake nao wana shhida zao.

Wazazi wengi sasa hivi hawawaombi sana watoto wao kwa sababu wanajua kuwa ukiwaomba utaonekana mswahili,wengi wanakufa na tai shingoni.
 
Unajua unaweza ukamuona mtu hasaidii wazazi wake, lakini kilichopo ndani hukijui, familia hizi zina mambo mengi sana, kuna mtu alikuwa anawapa kama kawaida mpaka yeye mwenyewe anakosa au anapungukiwa, Baba kaoa mama anakusanya watoto wa ndugu lakini akiuliza anajibiwa mimi sijawabagua nyie ,siku kakosa lawama anawanyima au wakigawana kile kidogo wazazi wanalalamika na hao wazazi tuseme vipi?

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Nimekuelewa safuher


Ulweso umeongea ukweli....
Wakati mwingine unakuta wazazi walifanya yao yasiyompendeza Mungu sasa wako kwenye kutumikia adhabu ya Mungu.
Mambo ya rohoni ni magumu sanaaaa, tumwombe Mungu ufahamu na hekima ya kuishi ndani ya mapenzi yake

Kutoka 34: 6-7
"Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili,

si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;
mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu,
mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi;
wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe;
mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne."
 
Lengo la sadaka ni kuwasaidia wasiojiweza, sasa kama mzazi wako naye hajiwezi msapoti.
Hilo sio lengo la sadaka. Kutoa sadaka kuna lengo la kumrudishia Mungu sehemu ya baraka alizokujalia, ambapo zinatakiwa zisaidie kueneza utukufu na ukuu wake
 
Hilo sio lengo la sadaka. Kutoa sadaka kuna lengo la kumrudishia Mungu sehemu ya baraka alizokujalia, ambapo zinatakiwa zisaidie kueneza utukufu na ukuu wake
PEngine tunatofautiana imani mkuu.

mimi siamini kama lengo la sadaka ni kumrudishia MMunguMungu yeye hanufaiki na sadaka zetu na wala hadhuriki na ubakhili wetu.

pengine tunatofautiana imani.

sadaka inatolewa ili iwasaidie wengine pasi na kuangalia kipimo fulani cha pesa zako.
 
Unajua unaweza ukamuona mtu hasaidii wazazi wake, lakini kilichopo ndani hukijui,
Ni kweli ulweso,lakini mimi uzi wangu haugusii hii situation.
Mtu ataangalia mwenyewe na hali ya familia yake ijapokuwa hakuna kosa ambalo atakufanyia mzazi alafu ikawa umhukumu kwa kumnyima matumizi.
Bado huu sio kisingizio cha kumnyima mzazi mahitaji mkuu.

Unajua tumeamrishwa na Dini zetu kuwatendea wema wazazi,Dini haikusema kuwa umfanyie wema mzazi ambae ni mwema na usimfanyie wema au kumhudumia mzazi mbaya.

Sasa unapovunjika moyo kumsaidia mzazi ambaye unaona kuna vitu anakosea basi ujue na huyo mzazi anahitaji huduma yako pia

Kama ambavyo sisi tulihudumiwa na wao utoto wetu haina maana kuwa tulikuwa wasafi tu,tulikosea sana lakini waliendelea kutuhudumia,na sisi tuendelee na moyo huu.

Hivyo ndugu ulweso hakuna nyudhuru ya maana ambayo mtu atasema kwa hili baba namweka na njaa,no no no.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…