Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa hiyo kumbe USA ni chanzo Cha vurugu,vita na fujo zote dunianiSaudi Arabia hana uwezo wa kumdindia USA, US atafungulia Houthi rebels ndani ya siku 2 Saudi inakuwa Libya
Amdindie Mara ngapi? Kagoma kupokea hata simu yake.Saudi Arabia hana uwezo wa kumdindia USA, US atafungulia Houthi rebels ndani ya siku 2 Saudi inakuwa Libya
BBC, CNN na ALJAZEERA ni majanga tu kuhusu Africa kama njaa, magonjwa COVID-19, vimbunga, vita, tetemeko la ardhi, mafuriko, mateka ya Boko Haram, mtifuano wa wanasiasa na ukame jangwani....[emoji849]Sema hizi habari huwezi kuzkuta BBC news[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
ExactlyKwa hiyo kumbe USA ni chanzo Cha vurugu,vita na fujo zote duniani
Halafu tunaoongea sasa na kuanza kumwambia US atakoma tupo madongo kuinama huku Ulimwengu wa tatu kwenye dhiki tele hata kodi ya chumba kimoja kulipa ni shida.Nasoma comment za huu uzi huku nacheka sana 😀😀Tunavyoongea utafikiri USA ni ka center flani hivi ambayo wanaishi watu wasiodizi 30 wenye njaa sana, jamiiforum Kuna watu kwelikweli.
US hawezi kugusa Saudi Arabia maana pale Kuna miji mitakatifu, Islam wako siriazi na dini yao sio Kama sisi wakristo Mara Mwamposa na Nabii Shila,Saudi Arabia hana uwezo wa kumdindia USA, US atafungulia Houthi rebels ndani ya siku 2 Saudi inakuwa Libya
Kwa ujuaji tunaounyesha hapa 😁Mnapenda futuhi wabongo
Habari yako haiko sawa na imekaa kichuki sana...Iko hivi, Marekani kwa kutaka kuikomoa Urusi wakapata mawazo ya kugomea kununua mafuta Yao. Lakini kabla hawajafikia muafaka wa kugomea mafuta ya Urusi wakaona watafuta chanzo mbadala Cha mafuta. Hapo ndio wakapata wazo la kuiomba Venezuela kwa Raid Maduro waweze kuànza téna kuchukia mafuta huko ambako mwanzo waliyagomea kwa kutokumtamvua Rais Maduro badala yake wakaamua kumtambua mpinzani wake aliyekuwa ameshindwa vibaya kwenye uchaguzi aitwaye Guaido.
Wakaona ni afadhali wameangukie Maduro kuliko kuendelea kununua mafuta ya Urusi. Ili kutekeleza sdhima hiyo, Marekani ikayuma ujumbe mzito kwa Rais Maduro wa Venezuela ambaye aliwaambia hakuna shida njoni tuyajenge (si unajua kwenye siasa hakuna sdui wa kudumu au rafiki wa kudumu, kinachoangaliwa ni maslahi!).
Kweli ujumbe mzito ukaenda na Rais Maduro akawapokea kwa bashasha na tabasamu la kufa mtu. Akawaambia hakuna shida mafuta nitawapatia. Wageni hao wa Rais Maduro wakarudi Marekani na moto wa kugomea mafuta ya Urusi maana wameshapata mafuta mbadala. Walipofika tu Marekani, Rais Biden wa Marekani akatoa amri ya kupiga marufuku ununuaji wa mafuta Toka Urusi.
Maduro akasubiri siku mbili Kisha akaioiga mkwara Marekani:
1. Nitawauzia mafuta lakini kwa masharti yafuatayo:
(i). Itabidi mnitambue rasmi kuwa Mimi ndiye Rais halali wa Venezuela tangu baada ya uchaguzi mkuu uliopita.
(Ii). Wakati nawaauzia mafuta Hilo halitaathiri ushirika wangu na Urusi na nitabaki mwamininifu kwa Nchi ya Urusi!!
Hayo masharti yakawa magumu Sana kwa Marekani na akashindwa kuyatekeleza wakati tayari ameshatangaza kugomea mafuta ya Urusi!! Bei ya mafuta Marekani ghafka ikapanda juu Sana!!
Rais Biden akaamua aiombe Saudi Arabia waongeze uzalishaji wa mafuta Ili kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya Marekani lakini mfalme wa Saudia akamchunia na hakukubali kupigiwa simu na Biden!! Sasa hivi huu ko Marekani Biden anahaha!
Kaingizwa mkenge na kiburi hakimruhusu kuyakubali téna mafuta ya Urusi.
kwan hana namba yake ya watsap akmchek king mojakwa mojaaa si rahis fastaAisee.. Noma sanaa
Niliiona hiyo ya Saudia kuwachunia ku pickup simu zao ila kuhusu venezuela sikujua kabisa..
No way itabidi akubali masharti ya venezuela tuu...
Nenda katafute mzee hifadhi ya mafuta ya us ina iwezo wa kukaa kwa muda gani ndo uje u commentHabari yako haiko sawa na imekaa kichuki sana...
Sasa ni hivi...Marekani ina hifadhi kubwa ya mafuta kuliko nchi yoyote duniani
Nimecheka sana mkuu hii comment yako.Tunavyoongea utafikiri USA ni ka center flani hivi ambayo wanaishi watu wasiodizi 30 wenye njaa sana, jamiiforum Kuna watu kwelikweli.
Ongezea sukari kidogo kwenye kahawaBado nasisitiza tu kwamba vijana wa kitanzania bado ni shida sana kwani hawapendi kusoma na kutafuta taarifa ila wao ni kukariri tu na ushabiki kama wa Simba na Yanga.
Marekani ni taifa lenye watu "Think Tanks" na ni taifa ambalo vitabu walivyoandikia mipango yao ya maendeleo kwa miaka 200 ijayo vinaweza vikajaza semi trela hata kumi hivyo kutegemea kwamba mambo yake yanaweza yakakwamishwa na tu-nchi kama Venezuela au sijui Saudi Arabia ni kufikiria kitoto sana.
Sasa hivi wameshaanza mpango wa kutoa mapipa milioni mbili za mafuta ghafi kila siku kutoka kwenye akiba yao ya Strategic Oil Reserve ilioko Alaska na kufanya bei ya mafuta ghafi ipungue kwenye soko la dunia kutoka USD 124/bbd mpaka USD 106/bbd (High) na USD 98.6/bbd (Low) bei ya leo na bado itaendelea kushuka unafuu ambao hata sisi tutanufaika nao.
Wenzetu walishajipanga siku nyingi na kujiwekea Contingency Plans kwa kufahamu kwamba kuna kipindi lazima watakutana na taharuki fulani fulani.
Itakumbukwa kwamba Marekani ndio taifa la pili duniani, nyuma ya Russia, kwa kuwa na akiba kubwa ya mafuta ghafi kwa hiyo wanaofikiria kwamba wanaweza wakakwama kwa kukosa hiyo rasilimali watakuwa wanakosea sana.
Habari za kubumba tupu. Habari hazina kichwa wala miguu. Ulimwengu wa sasa taarifa yoyote isiyo na chanzo inabaki kuwa story za kijiweniSema hizi habari huwezi kuzkuta BBC news[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]