Sakata la Kupotea Rajab Omari Mtana na Hukumu ya Kunyongwa kwa Masheikh 10 Tanga

Sakata la Kupotea Rajab Omari Mtana na Hukumu ya Kunyongwa kwa Masheikh 10 Tanga

Umemueleza barabara!! na bayana.

Seme alishajichagulia upande so hamtoelewana.

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
Mazi...
Hakuna asiyekuwa na upande.
Upande wangu ni huu kuwa historia iliyoandikwa ina makosa.

NImeandika kitabu kusahihisha makosa hayo.

Hajakuja mwandishi mwingine kusema kuwa historia niliyoandika si kweli.

Hapa nani hataki kumwelewa nani?

Ukimya huu wa kutojibu kitabu changu nini maana yake?
 
Political history inayoanza kwa ku classify wahusika kwa dini zao??? What a shame kutoka kwa mtaaluma kama wewe.
Masta....
Naam anaandika Kleist Sykes katika mswada wa kitabu alioandika kabla ya kufariki kwake 1949 anasema waasisi wa African Association wengi ni Waislam kwa kuwa wamishionari walikwakataza waumini wao wasijiingize katika siasa.

(AD Sykes "The Life of Kleist Sykes" Ref. No. JAN/HIST/143/15 1968 East Africana, University of Dar-es-Salaam).
 
Masta....
Naam anaandika Kleist Sykes katika mswada wa kitabu alioandika kabla ya kufariki kwake 1949 anasema waasisi wa African Association wengi ni Waislam kwa kuwa wamishionari walikwakataza waumini wao wasijiingize katika siasa.

(AD Sykes "The Life of Kleist Sykes" Ref. No. JAN/HIST/143/15 1968 East Africana, University of Dar-es-Salaam.
Nonesense. Hao waislamu walikua watanganyika au waburundi?
 
... kila penye neno muislamu hapo nadhani ungefaa kuweka mtanzania..
...
Mkuu waislamu siyo raia wa kawaida wao wana dunia yao ndiyo maana wanaonekana kujitenga na ngano.

All in all namfikilia yule mgambo aliyefariki ambaye ndiye chanzo toka anakamata gari, kwa nini achukue maamuzi ya kwenda kwa mkulima ambaye hausike kwenye bidhaa iliyonunuliwa kwake?.

Hakika baadaye ndipo naona njia ya kifo kinavyokuja, yaani naamini kauli ya Allah kuwa 'laiti ungejua siku ya kuja mwivi usiku ungekesha'.
 
Mzee kashupaza shingo. Akiambiwa anaendekeza udini, anakimbilia kwenye historia ya TANU. Huko tukishatoka, tunataka tuishi bila haya mapazia ya dini. Kama tunavyopanda mabasi pamoja, kama tunavyoshabikia mpira pamoja, kama tunavyojitambukisha kama Watanzania pamoja, bila kuweka udini mbele, ndivyo tunavyotaka kuishi. Hizi chokochoko kwamba wengine wanaonewa kwa sababu ya dini yao, hazitujengi shehe wangu. Tumia kipawa na kalamu yako kusambaza upendo. Wanasema, ukiona unafuatwa na kundi la nzi, usiulize hawa nzi wana nini, bali jiulize wewe una nini kinachowavutia hao nzi. Wengi humu wamekuhukumu kwa kusambaza udini, lakini kwa sababu umeshupaza shingo, unahisi wote wanakosea. Inasikitisha sana mzee kukosa busara
 
SAKATA LA KUPOTEA RAJAB OMARI MTANA KIJIJI CHA LULAGO HANDENI 2013

Waislam 10 wamehukumiwa kunyongwa kwa tuhuma za kuua mlinzi mmoja.

Kufikia hukumu hii kuna mengi na chanzo chake kilianzia katika biashara ya hiliki na malipo ya ushuru kijijini Lulago.

Ninaanza leo kueleza kisa hiki kama nilivyotafiti na kuweka kumbukumbu miaka 10 iliyopita.

Rajab Omar Mtana alikuwa mwanakijiji wa kawaida tu akiishi kijijini Lulago, Handeni kama wanavijiji wengine wanavyoishi na alikuwa na biashara yake ya kuuza hiliki kama mkulima wa zao hilo.

Siku moja akaja mnunuzi mfanyabiashara wa hiliki nyumbani kwake kununua hiliki na akamuuzia.

Yule mfanyabiashara alipokuwa anatoka na gari yake akasimama kwenye kizuizi cha kulipia ushuru.

Alipotakiwa kulipa ushuru akasema kuwa si hiliki yote amenunua katika kijiji hicho kwa hiyo hawezi kulipa ushuru wa hiliki yote.

Hapo palitokea ubishi na mfanyabiashara yule akagonga lile geti na akaondoka.

Hii ikapelekea kwa wakusanya ushuru wa hapo kijijini kwenda nyumbani kwa Rajab Omar Mtana kumkamata na kumweka chini ya ulinzi katika ofisi ya serikali ya kijiji hadi hapo atakapolipa ushuru ambao yule mfanyabiashara alitakiwa alipe.

Ndugu zake Rajab Omar Mtana wakaenda pale ofisini kwa nia ya kumtoa ndugu yao na hapo pakatokea vurugu na mapigano.

Katika mapigano hayo, mgambo ambae ndiye aliyekuwa akishughulika na kudai ushuru akauawa.

Kisa hiki cha ushuru wa hiliki ndicho kilichozua balaa kubwa la mauaji na uchomwaji moto nyumba za Waislam wa kijiji cha jirani cha Madina na kuvunjwa kwa misikiti katika vijiji ambavyo vilikuwa na idadi kubwa ya wakazi wake Waislam.

Baada ya haya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akatoa amri kuwa hapana ruhusa tena ya sehemu hizo kuwa makazi kwa kuwa hizo ni kambi za ugaidi.

Mkuu wa Mkoa alisema mengi ambayo takriban yote yamedhihirika baadae kuwa hayakuwa na ukweli.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa wapo Al Shabab vijijini, kumechimbwa mahandaki ya vita katika vijiji na kuna silaha za kutungulia ndege nk. nk.

Mkuu wa Mkoa alizungumza na Radio Nuur, Tanga inayomilokiwa na Msikiti wa Ibadh.
Nilifunga safari hadi Radio Nuur Tanga kwa nia ya kupata taarifa kamili yalivyorushwa.

Radio Nuur waliogopa kunipa juu wala kuniruhusu kusikiliza kipindi hicho cha Mkuu wa Mkoa ingawa kabla sijahama Tanga nilikuwa mmoja wa Wakurugenzu wa radio hiyo.

Lakini niliwahoji watu waliosikia kipindi hicho.

Katika Waislam waliokamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani Handeni ni huyu kijana Rajab Omari Mtana.

Baada ya kukaa rumande alipata dhamana yeye pamoja na wenzake na akawa nje.
Rajab Omar Mtana alirejea kijijini kwake.

Wakati anakaribia kuingia kijijini alisimamishwa na askari wa kijiji akapekuliwa na akanyang'anywa simu yake na fedha taslimu.

Baada ya mkasa huu walimwachia na yeye akaendelea na safari yake.

Lakini wakati akiwa rumande nyumba yake ilikuwa imevurugwa haifai kuishi mtu kwa hiyo alifikia kwa dada yake.

Akiwa nyumbani kwa dada yake alifatwa na watu wa serikali ya kijiji usiku akatolewa ndani na kuanza kupigwa kwa bakora na kisha kwa mapanga.

Kujitetea kijana huyu alikimbia huku akikimbizwa.
Asubuhi kulipokucha palionekana damu nyingi sana.

Taarifa ilitolewa polisi lakini hakuna kilichofanyika.
Polisi walitoa taarifa (SON/RB346/2014).

Dada yake na mumewe walikamatwa na kushitakiwa katika mahakama ya hapo kijijini na wakapigwa faini ya kila mtu shs. 20.000.

Kosa lao ni kumleta kijiji Rajab Omari Mtana mtu asiyetakiwa.

Miaka 10 imetimia Rajab Omar Mtana hajulikani alipo na inasadikiwa ameuawa na wale waliokuja kumtoa nyumbani kwa dada yake.

Rajab Omar Mtana ametafutwa kote hajapatikana na waliompiga na kumjeruhi wako huru nje hawajaguswa wala kuhojiwa na polisi.

Lakini wale waliotumiwa kwa mauaji ya mlinzi wa kijiji wamehukumiwa kifo.

Hapa kuna mengi sana ya kufikirisha mbali ya yale kuwa kulikuwapo na silaha za kutungua ndege katika vijiji hivi vya Waislam wa Handeni vilivyokuwa na nyumba za nyasi na udongo.

View attachment 2668468
Kwenye hili bila kupepesa naiona state crime hususan kwa viongozi ngazi za kijiji hadi mkoa.

Mungu awasimamie masheikh.
Mungu afunue ukwelli wa kilichomsibu Rajab Omari Mtana
 
80% na zaidi ya wakazi wa mkoa wa Tanga na wilaya zake ni waislamu.

Yawezekana mtana alipigwa au kuuwawa na waislamu wenzake.

Ila inatafuta sababu hapa au Kuna dini au kikunda Cha watu kinatafutwa kipewe lawama Ili kuonekana waislamu wanaonewa na dini zingine au mamlaka.

Hizi ni propaganda za kidini zenye kueneza chuki na kuharibu mshikamano kayiia Taifa.



Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
Na hawatafanikiwa. Ukiisoma hii thread, unaona kama ukosefu wa busara. L:eo kama mtu ameuwawa, basi tunaanza kwanza kuangalia dini yake, ili tujikite katika kuhalalisha ujinga wetu, kama aliyeuwawa ni wa dini yetu.
Bila hata kujali alifanya nini
 
Mzee kashupaza shingo. Akiambiwa anaendekeza udini, anakimbilia kwenye historia ya TANU. Huko tukishatoka, tunataka tuishi bila haya mapazia ya dini. Kama tunavyopanda mabasi pamoja, kama tunavyoshabikia mpira pamoja, kama tunavyojitambukisha kama Watanzania pamoja, bila kuweka udini mbele, ndivyo tunavyotaka kuishi. Hizi chokochoko kwamba wengine wanaonewa kwa sababu ya dini yao, hazitujengi shehe wangu. Tumia kipawa na kalamu yako kusambaza upendo. Wanasema, ukiona unafuatwa na kundi la nzi, usiulize hawa nzi wana nini, bali jiulize wewe una nini kinachowavutia hao nzi. Wengi humu wamekuhukumu kwa kusambaza udini, lakini kwa sababu umeshupaza shingo, unahisi wote wanakosea. Inasikitisha sana mzee kukosa busara
Vangi...
Sikimbilii historia ya TANU.

Historia ya TANU ndiyo yenye misingi ya umoja na laiti kama ungeijua historia hii ungejiuliza imekuwaje tumefika hapa nchi imegawanyika?

Kikao cha kumtia Julius Nyerere katika uongozi wa TAA kilifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu (1913 - 1962) Nansio Ukerewe.

Waliokuwa katika kikao hicho ni Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Ndugu yangu ushajiuliza kwa nini historia hii haijulikani?

Athari ya kukosa kutambua misingi hii ndiyo haya unayoeleza wewe hapo juu.
 
Wewe ni mbilikimo wa akili pia.
Wewe jamaa inabidi ukapimwe akili kwa sababu unaonyesha kila dalili ya ukichaa. Inakuwaje unamtukana mtu kwa sababu tu hoja yake huipendi? Kwani lazima ujibu si upige kimya tu? Kama umesoma basi elimu yako haina maana yoyote na ni mzigo kwa nchi.
 
Wewe jamaa inabidi ukapimwe akili kwa sababu unaonyesha kila dalili ya ukichaa. Inakuwaje unamtukana mtu kwa sababu tu hoja yake huipendi? Kwani lazima ujibu si upige kimya tu? Kama umesoma basi elimu yako haina maana yoyote na ni mzigo kwa nchi.
Kuwa na adabu unapoona comment yangu. Kwa akili zako zilivyo ndogo unaona anachofanya Mzee Mohamed ni kitu sahihi. Unadhani machafuko yanavyotokea ni jambo la siku moja tu? Inaanza polepole na mambo kama ya huyu Mzee Mohamed.. kupandikiza chuko taratibu. Siwezi kukaa kimya pale mtu anapoichezea amani ya nchi hii.
 
Ralph...
Tundu Lissu hanihitaji mimi kumsemea halikadhalika Freeman Mbowe.
Hawa wana watu wa kutosha kuwasimamia.

Nakuwekea hapo chini kisa kingine ambacho hakuna chombo cha habari kiliripoti ingawa walikuwa na taarifa zote:

Mauaji ya Hamisi Ramadhani na Abu Zubeir wa Kijiji cha Madina

Tarehe 25 Oktoba 2013 siku ya Ijumaa Waislam katika kujiji cha Madina walishambuliwa na askari na Waislam wawili waliuawa kwa kupigwa risasi.

Waislam hao ni Hamisi Ramadhani na Abu Zubeir.
Hamisi Ramadhani amezikwa Handeni katika makaburi ya hospitali maiti ilipokuwa imehifadiwa.

Abu Zubeir maiti yake ilihamishwa kutoka Handeni kwa kuwa hospitali haikuwa na chumba cha barafu cha kuhifadhi maiti ikapelekwa Korogwe.

Ndugu zake Abu Zubeir waliogopa kujitokeza kuchukua maiti yake kwa kuwa askari walikuwa wakimkamata kila aliyefika hospitali kuuliza taarifa za maiti hao.

Haijulikani nani wamemzika Abu Zubeir na hadi sasa ndugu zake hawajajitokeza kujua ndugu yao kazikwa wapi kwa hofu ya kukamatwa.

Sheikh Waziri anasema yeye na wenzake walikabidhiwa maiti ya Hamisi Ramadhani siku ya Jumapili na siku hiyo hiyo walimzika katika makaburi ya hospitali sanda yake ikiwa shuka ile iliyofunika maiti yake.

Sheikh Waziri anasema juu ya kuwa maiti zile zilikuwa hazikuhifadhiwa katika baridi hali ya maiti ilikuwa nzuri kabisa.

Mashuhuda wa kifo cha Hamisi Ramadhani wanasema alipopigwa risasi Hamisi Ramadhani alishahadia kwa sauti na kila mtu alisikia shahada ile.

Allah awalaze mahali pema peponi.
Amin.

Maelezo Mafupi ya Sheikh Waziri Shuza

Siku ile ya mashambulizi tarehe 25 Oktoba 2013 Sheikh Waziri akiwa kama kiongozi wa Waislam alipigiwa simu yeye akiwa Mkata katika shughuli za biashara kujulishwa kuwa kuna watu wameuawa kwa hiyo akaombwa aende Hospitali ya Wilaya Handeni akaagalie waliouawa na majeruhi.

Taarifa zilizomfikia alipofika Handeni jioni ile zilikuwa taarifa za kuogofya.

Hali pale hospitali ilikuwa ya kutia hofu palikuwa na ulinzi mkali hospitali nzima imezungukwa na maaskari. Kwa ajili hii Sheikh Waziri hakuweza kwenda hospitali siku hiyo na hata siku ya pili yaani Jumamosi hakuweza kwenda.

Waislam walibakia majumbani kwao wakisubiri na kuomba dua.

Sheikh Waziri akiwa kiongozi alipiga marufuku shura ya aina yoyote msikitini kuhusu mauaji yale kutafuta salama.

Waislam walikuwa wanakuja kuswali na wakimaliza wanaondoka kurudi majumbani kwao.

Lakini Sheikh Waziri akawa na wasiwasi kuwa ikiwa hatafanya jambo kuna hatari ya wale marehemu kutozikwa Kiislam.

Sheikh Waziri ilipofika Jumapili ikamjia fikra ya kumpigia diwani Mushashi. Alimweleza diwani huyu kuwa Waislam wangeshukuru kama serikali wangeruhusu maiti zile wapewe ili wazizike.

Haukupita muda diwani akamfahamisha Sheikh Zuberi kuwa anaweza kwenda hospitali na kuonana na Mganga Mkuu kwa ajili ya kupewa zile maiti mbili.

Lakini Mganga Mkuu akasema kuwa amri aliyopewa na Mkuu wa Mkoa Bi. Chiku Galawa ni kuwa maiti zile zipelekwe Tanga kwa mazishi ikiwa ndugu zao hawajajitokeza na huko maiti hizo zitachangwanywa na maiti nyingine za wasio na ndugu na zitazikwa na serikali.

Ikawa sasa lazima Mkuu wa Mkoa asubiriwe ili abatilishe amri yake ya awali na endapo ruksa itatoka Waislam wa Handeni watazizika maiti hizo.

Sheikh Hamisi akaondoka kusubiri amri ya Mkuu wa Mkoa.

Mwishowe maiti ilitolewa kwa Sheikh Waziri baada ya mazungumzo marefu kati ya Mganga Mkuu na Sheikh Waziri ikizingatiwa kuwa kwa siku tatu hakuna ndugu wa marehemu aliyejitokeza kuchukua maiti.

Sheikh Waziri alifunuliwa maiti ya Hamisi Ramadhani na Mganga Mkuu mbele ya askari.akaonyeshwa jeraha la mguuni alipopigwa risasi.

Shuka haikufunuliwa kuoneshwa majeraha mengine...
Sheikh Waziri hakuwa na haja ya kutaka mengi lililomshughulisha ilikuwa ni kupata maiti ili waisiitiri.

Sheikh Waziri anasema ilikuwa wazi kuwa Polisi na Mganga Mkuu walikuwa wameshakubaliana nini cha kufanya wakati watakapoonyesha maiti kwa ndugu zao.

Mganga Mkuu alionyesha jeraha la risasi mguuni akisema kuwa hapo ndipo zilipotoka damu nyingi kusababisha kifo cha Hamisi Ramadhani.

Lakini wao walikuwa na habari kamili kutoka kwa mke wa marehemu na jamaa wengine kuwa ndugu yao alikuwa amepigwa risasi katika kibofu cha mkojo na kwa hakika sehemu ile ingawa ilikuwa imefunikwa na shuka palikuwa na uvimbe mkubwa.

Sheikh Waziri na Waislam wachache walimzika ndugu yao usiku katika makaburi hapo hospitalini.
Kama walitishia usalama wa nchi lazima wangeuawa
 
Kuwa na adabu unapoona comment yangu. Kwa akili zako zilivyo ndogo unaona anachofanya Mzee Mohamed ni kitu sahihi. Unadhani machafuko yanavyotokea ni jambo la siku moja tu? Inaanza polepole na mambo kama ya huyu Mzee Mohamed.. kupandikiza chuko taratibu. Siwezi kukaa kimya pale mtu anapoichezea amani ya nchi hii.
Wewe huna akili ndiyo maana unatumia lugha za matusi na zisizo za kistaarabu. Kama hukubaliani na hoja ya mtu tumia lugha za staha kumnasihi na siyo kumtukana. Unamwitaje binadamu mwenzio nguruwe?
 
Huyu Mzee anatabia za chuki za kidini kama yule sheikh ilunga alikuwa anahamasisha mauaji ya mapadri
 
SAKATA LA KUPOTEA RAJAB OMARI MTANA KIJIJI CHA LULAGO HANDENI 2013

Waislam 10 wamehukumiwa kunyongwa kwa tuhuma za kuua mlinzi mmoja.

Kufikia hukumu hii kuna mengi na chanzo chake kilianzia katika biashara ya hiliki na malipo ya ushuru kijijini Lulago.

Ninaanza leo kueleza kisa hiki kama nilivyotafiti na kuweka kumbukumbu miaka 10 iliyopita.

Rajab Omar Mtana alikuwa mwanakijiji wa kawaida tu akiishi kijijini Lulago, Handeni kama wanavijiji wengine wanavyoishi na alikuwa na biashara yake ya kuuza hiliki kama mkulima wa zao hilo.

Siku moja akaja mnunuzi mfanyabiashara wa hiliki nyumbani kwake kununua hiliki na akamuuzia.

Yule mfanyabiashara alipokuwa anatoka na gari yake akasimama kwenye kizuizi cha kulipia ushuru.

Alipotakiwa kulipa ushuru akasema kuwa si hiliki yote amenunua katika kijiji hicho kwa hiyo hawezi kulipa ushuru wa hiliki yote.

Hapo palitokea ubishi na mfanyabiashara yule akagonga lile geti na akaondoka.

Hii ikapelekea kwa wakusanya ushuru wa hapo kijijini kwenda nyumbani kwa Rajab Omar Mtana kumkamata na kumweka chini ya ulinzi katika ofisi ya serikali ya kijiji hadi hapo atakapolipa ushuru ambao yule mfanyabiashara alitakiwa alipe.

Ndugu zake Rajab Omar Mtana wakaenda pale ofisini kwa nia ya kumtoa ndugu yao na hapo pakatokea vurugu na mapigano.

Katika mapigano hayo, mgambo ambae ndiye aliyekuwa akishughulika na kudai ushuru akauawa.

Kisa hiki cha ushuru wa hiliki ndicho kilichozua balaa kubwa la mauaji na uchomwaji moto nyumba za Waislam wa kijiji cha jirani cha Madina na kuvunjwa kwa misikiti katika vijiji ambavyo vilikuwa na idadi kubwa ya wakazi wake Waislam.

Baada ya haya Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Galawa akatoa amri kuwa hapana ruhusa tena ya sehemu hizo kuwa makazi kwa kuwa hizo ni kambi za ugaidi.

Mkuu wa Mkoa alisema mengi ambayo takriban yote yamedhihirika baadae kuwa hayakuwa na ukweli.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa wapo Al Shabab vijijini, kumechimbwa mahandaki ya vita katika vijiji na kuna silaha za kutungulia ndege nk. nk.

Mkuu wa Mkoa alizungumza na Radio Nuur, Tanga inayomilokiwa na Msikiti wa Ibadh.
Nilifunga safari hadi Radio Nuur Tanga kwa nia ya kupata taarifa kamili yalivyorushwa.

Radio Nuur waliogopa kunipa juu wala kuniruhusu kusikiliza kipindi hicho cha Mkuu wa Mkoa ingawa kabla sijahama Tanga nilikuwa mmoja wa Wakurugenzu wa radio hiyo.

Lakini niliwahoji watu waliosikia kipindi hicho.

Katika Waislam waliokamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani Handeni ni huyu kijana Rajab Omari Mtana.

Baada ya kukaa rumande alipata dhamana yeye pamoja na wenzake na akawa nje.
Rajab Omar Mtana alirejea kijijini kwake.

Wakati anakaribia kuingia kijijini alisimamishwa na askari wa kijiji akapekuliwa na akanyang'anywa simu yake na fedha taslimu.

Baada ya mkasa huu walimwachia na yeye akaendelea na safari yake.

Lakini wakati akiwa rumande nyumba yake ilikuwa imevurugwa haifai kuishi mtu kwa hiyo alifikia kwa dada yake.

Akiwa nyumbani kwa dada yake alifatwa na watu wa serikali ya kijiji usiku akatolewa ndani na kuanza kupigwa kwa bakora na kisha kwa mapanga.

Kujitetea kijana huyu alikimbia huku akikimbizwa.
Asubuhi kulipokucha palionekana damu nyingi sana.

Taarifa ilitolewa polisi lakini hakuna kilichofanyika.
Polisi walitoa taarifa (SON/RB346/2014).

Dada yake na mumewe walikamatwa na kushitakiwa katika mahakama ya hapo kijijini na wakapigwa faini ya kila mtu shs. 20.000.

Kosa lao ni kumleta kijiji Rajab Omari Mtana mtu asiyetakiwa.

Miaka 10 imetimia Rajab Omar Mtana hajulikani alipo na inasadikiwa ameuawa na wale waliokuja kumtoa nyumbani kwa dada yake.

Rajab Omar Mtana ametafutwa kote hajapatikana na waliompiga na kumjeruhi wako huru nje hawajaguswa wala kuhojiwa na polisi.

Lakini wale waliotumiwa kwa mauaji ya mlinzi wa kijiji wamehukumiwa kifo.

Hapa kuna mengi sana ya kufikirisha mbali ya yale kuwa kulikuwapo na silaha za kutungua ndege katika vijiji hivi vya Waislam wa Handeni vilivyokuwa na nyumba za nyasi na udongo.

View attachment 2668468
Hawa ni waumini wa kawaida au Mashehe?
 
Vangi...
Sikimbilii historia ya TANU.

Historia ya TANU ndiyo yenye misingi ya umoja na laiti kama ungeijua historia hii ungejiuliza imekuwaje tumefika hapa nchi imegawanyika?

Kikao cha kumtia Julius Nyerere katika uongozi wa TAA kilifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu (1913 - 1962) Nansio Ukerewe.

Waliokuwa katika kikao hicho ni Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Ndugu yangu ushajiuliza kwa nini historia hii haijulikani?

Athari ya kukosa kutambua misingi hii ndiyo haya unayoeleza wewe hapo juu.
You really didn't get my point. Na inawezekana utaendelea kutonielewa. Binafsi, nimekiri kwenye post zangu mbili huko juu kwamba kwa suala la historia ya TANU, uko vizuri. Inawezekana nilichojifunza shule hakikuwa sahihi, ingawa hainipi madhara yoyote. Point yangu kubwa ni namna ulivyotumia kisa hiki kuonyesha kwamba madhira waliyoyapata hao Watanzania wa Handeni, yametokana na Uislamu wao. Hapa ndipo wote waliokupinga, wameparejea. Hili halihusiani na Nyerere na TANU. Hili halihusiani na nani alidai uhuru wa Tanganyika. Hapa tunaongelea Watanzania. Nilitabiri utashupaza shingo, umeshupaza. Bado nakushauri, soma maoni ya waliokukosoa kwa utulivu, bila kimue cha kutaka kuprove kuwa uko sahihi. Unaweza kujifunza kitu
 
You really didn't get my point. Na inawezekana utaendelea kutonielewa. Binafsi, nimekiri kwenye post zangu mbili huko juu kwamba kwa suala la historia ya TANU, uko vizuri. Inawezekana nilichojifunza shule hakikuwa sahihi, ingawa hainipi madhara yoyote. Point yangu kubwa ni namna ulivyotumia kisa hiki kuonyesha kwamba madhira waliyoyapata hao Watanzania wa Handeni, yametokana na Uislamu wao. Hapa ndipo wote waliokupinga, wameparejea. Hili halihusiani na Nyerere na TANU. Hili halihusiani na nani alidai uhuru wa Tanganyika. Hapa tunaongelea Watanzania. Nilitabiri utashupaza shingo, umeshupaza. Bado nakushauri, soma maoni ya waliokukosoa kwa utulivu, bila kimue cha kutaka kuprove kuwa uko sahihi. Unaweza kujifunza kitu
Nasikitika kuwa Mohammed ameamua kuwa mpuuzi wa kudumu
Mjinga wa muda wote

Wapumbavu huwa na 'confidence' sana. Sijui hii inatokana na nini!
 
Back
Top Bottom