Sakata la Zumaridi na namna alivyokamatwa na polisi ni kichefuchefu, sheria haikuzingatiwa

Sakata la Zumaridi na namna alivyokamatwa na polisi ni kichefuchefu, sheria haikuzingatiwa

Hata mimi sioni sababu.
Halafu Tanzania uwa inafurahisha. Akikamatwa mtu wanayempenda bila kufuata sheria, raia inalalamika, akikamatwa mtu wasiyempenda bila kufuata sheria, raia inasema hata kama ache akamatwe.
Halafu sijui kwa nini huyu dada wanamsumbua hivi. maana kama issue ni misukule makanisa yoteeee yana misukule maana Hata kuna baadhi ya wakatoliki huwa na ubishi wa ajabuajabu wanapolezwa kuhusu matukio yanayofanywa na makasisi wao....
 
Halafu sijui kwa nini huyu dada wanamsumbua hivi. maana kama issue ni misukule makanisa yoteeee yana misukule maana Hata kuna baadhi ya wakatoliki huwa na ubishi wa ajabuajabu wanapolezwa kuhusu matukio yanayofanywa na makasisi wao....
Hata mm sioni kwanini wanamsumbua, anachofanya wakifanya wengine ni sawa.
Hapa kuna double standards
 
Hatu kama hao sio wa kuchekea
Wanamambo yao ya siri sana
Tuangalie kwa upande wa pili
 
Mhalifu hawi mhalifu hadi pale itakapothibitika!

Sakata la mfalme Zumaridi (Kiongozi wa kanisa la Zumaridi huko Mwanza) Linaacha midomo wazi kwa wapenda haki na utii wa sheria!

Sipo hapa kumtetea Mfalme Zumaridi, Bali nashangaa namna ya uharamu wa ukamtaji!

Taratibu za ukamataji kwa mujibu wa sheria ziko wazi kabisa lakini mamlaka zimekuwa zikionesha kufeli Mara kwa Mara kutekeleza sheria hiyo jambo ambalo limekuwa likitweza utu wa watu wasio na hatia.

MFANO! mambo kama haya yalitokea huko mtwara hadi kufedhehesha uongozi wa polisi ambayo yalianza hihivi kwa kufumbafumba mambo,

Mfano 2. Ni huko ARUSHA Kuna taarifa ya askali mzalendo kulalamika kutaka kuuwawa na polisi wenzake kwa mambo Yale Yale kama ya mtwara na serikali iko kimya.

SASA NI HILI SAKATA LA TATU LINALOTIA KICHEFCHEFU

Ni TUKIO LA zumalidi Siku ya kwanza inaripotiwa kwamba polisi waliruka ukuta/geti ili kuingia kwa Zumalidi! Kitendo hiki kilitakiwa kulaaniwa na kila mtu! (Waliruka kwa Zumalidi kesho wataruka kwako)

Kama kulikuwa na ulazima wa kufika pale kwanini hawakufuata utaratibu wa upekuzi unavyotaka? Kwanini hawa kumshirikisha mwenyekiti wa mtaa/mjumbe? Kwanini waliruka ukuta kama jambazi! (VIPI KAMA ZUMARIDI ANGEJIBU MASHAMBULIZI KWA KUFYATUA RISASI KWA POLISI ALIYEVAA KIRAIA ALIPORUKA UKUTA?) Ina maana wangejibu kwamba walikuwa kwenye mapambano na majambazi au?

Kwa utaratibu walio utumia polisi hauna tofauti na utarabu wa kijambazi! Na hili linachangia sana siku hizi RAIA kutokutofautisha kati ya jambazi na polisi.

Tukiachana na mbinu ya ukamataji!

Riport ya polisi ina ukakasi mkubwa juu ya mtuhumiwa Zumaridi!

Kosa walilo utaarifu Umma kwamba anasafilisha BINADAMU 149, kosa hilo Linatia aibu nyingine!

Hivi tangu lini watu wanaokusanyika kusali pamoja imekuwa kosa la jinai?

Mbona jumuiya na taasisi kibao tunawaona wanakusanyika na kukesha na haijawahi kutajwa kuwa ni kosa?

Zumalidi kasafirisha binadamu kutoka wapi kwenda wapi kwa lengo gani? Kuna jinai gani pale?

Hapo taifa juzi wakatoliki walikusanyika mbona haikutamkwa kuwa ni usafirishaji wa binadamu?

Kina mwingira na wachungaji kibao Tanzania kila kutwa wanakusanya watu na haisemwi ni usafirishaji,

INAKUWAJE JAMBO LILE LILE LIWE HALALI KWA MWAMPOSA LAKINI LIWE HARAMU KWA ZUMARIDI?

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Nawashauri TAKUKURU WAINGILIE KATI!
Haiwezekani sheria zipo wazi, kwanini zisingefuatwa kama kweli ZUMALIDI anamakosa makubwa hivyo!

Mimi kwa utashi wangu nahisi sakata la Zumaridi lina maslahi binafisi!

TUKIRUHUSU HAYA YA UKIUKWAJI WA SHERIA HAKUNA ATAKAYEBAKI SALAMA!

Itakuwa mtu akikosana na polisi wanakuja kuluka ukuta! Na majambazi nao watatumia mwanya huohuo kufanya uharifu!
Huyu mama ameonewa kinoma, huyu zumaridi huwa ana utaratibu wake wakualika watu mbalimbali kwake ili wanywe na kunywa, ata kama anapiga pesa lakini huwa anakumbuka kuzirudisha kwa maskini ni tofauti na manabii wote hapa Tanzania waliojaa ubinafsi, hii nazan ni hujuma dhidi yake, mimi nashauri na wachungaji wote na wanaojiita manabii nao wanakamatwe.
 
Lakini mbona anaenenda kimataifa .
1.Mavazi na dansi zake ni chukizo mbele za Mungu, kuna tofauti ya mavazi ya Mkristo na mpagani.
2.Anajiinua yeye zaidi kuliko Mungu Jehovah ana kaa mahali pa Mungu Jehovah kwa kujiita Mungu
1.Je!Biblia ilieleza style ya kudance unapomtukuza Mungu?kiungo chochote unachokiona kwenye mwili wa binadamu kimeumbwa kwa mfano wa Mungu,hata akikata mauno ni kiungo cha Mungu sema binadamu mmetunga sheria zenu,sijaona kwenye amri kumi za Mungu sehemu iliyokataza kucheza kwa kutumia style Fulani na viungo fulani tu. Kuhusu mavazi hakuna sehemu imesema haya ni mavazi ya kikiristo au haya ni kipagani....

2.Yehova kampa kila binadamu utashi wa kuchagua mema na mabaya. na kila mtu atalipwa ujira wake sawasawa na matendo yake... Wale watu kwa hiari Yao wameamua kumuamini nyie wana dunia mnaanza kuwahukumu,je? hiyo ni kazi yenu kuhukumu au kazi ya Yehova?Jamani tusiwe kama mafarisayo
 
Hata mm sioni kwanini wanamsumbua, anachofanya wakifanya wengine ni sawa.
Hapa kuna double standards
Waanze na Mwamposa pale wanakula Hadi nauli in the name of sadaka ya kujimaliza,afuatwe Gwajima nae ndio muasisi wa kufufua misukule... kama vipi wampotezee tu huyu bibie
 
Polisi ya Tanzania imeshamtoa mfalme damu.
AemeU.jpg
 
Kwa taarifa yako ni kwamba polisi huwa hawakamati waharifu huwa wanawakamata watuhumiwa wa uharifu,ambao bado uharifu wao haujathibitishwa kwa kuwa kazi ya kuthibitisha uharifu wa mtuhumiwa ni mahakama.

Kazi ya polisi ni kumkamata mtuhumiwa kulingana na tuhuma zilizopatikana kutoka kwa raia wema au kwa askari wenyewe,na kukusanya ushahidi utakao tumika kuthibitisha tuhuma za mtuhumiwa mahakamani kutoka vyanzo mbalimbali.

Katika suala la ukamataji, mtuhumiwa ndiye anayemshawishi askari polisi atumie nguvu ya namna gani katika ukamataji wake, ndio maana kuna usemi unaosema tii sheria bila shuruti, ukionyesha utii kwa askari aliyekuja kukukamata kutokana na tuhuma zako hakuna askari atakayetumia nguvu kukusurutisha kwa sababu tayari umeshafuta kipengera cha askari kukushurutisha kwa kuwa umechagua kutii pasipo kushurutishwa,mtuhumiwa ndiye anayechaguwa atendeweje na polisi.

Mtuhumiwa ndiye anayemjengea askari polisi mazingira ya kumkamata, ni nguvu ya kiasi gani itumike katika ukamataji mataji wake.

Mtuhumiwa akitaka akamatwe na askari polisi kama watu wanaokwenda pamoja kanisani kusali ni juu ya mtuhumiwa mwenyewe,jinsi atakavyoonyesha mwitikio wake wa kutii sheria pasipo shuruti kwa askari.

Matumizi ya nguvu/kuruka ukuta kwa askari polisi vinakuja pale ambapo mtuhumiwa anapokataa kuonyesha ushirikiano wa kutii sheria bila shuruti na njia zote hizi za mtuhumiwa kutii sheria,pasipokushurutishwa na kutii sheria kwa kushurutishwa zote ni njia za kisheria.

Ndio maana polisi kapewa rungu ili alitumie kwa mtuhumiwa ambaye amegoma kutii sheria bila kushurutishwa, kapewa silaha za moto, kapewa mabomu ya machozi, kapewa mabomu ya kubomoa kuta na kuvunja milango kwa lengo hilohilo la kutumia kumlazimisha mtuhumiwa atii sheria,na hakuna sheria inayomtaka askari polisi katika ukamataji wake akamchukue kiongozi wa mtaa au akamchukue jirani aje athibitishe ukamataji unavyofanyika.

Na hakuna hati ya kumpekulia mtuhumiwa anapokamatwa isipokuwa kuna hati ya kufanya upekuzi kwa ajili ya kutafuta mali zilizoibiwa au zimefichwa kwa nia ovu na hapo ndipo anapotakiwa kuhusika kiongozi yeyote wa mtaa au jirani kuja kuthibitisha upekuzi huo.
Nonsense.
 
Nakubaliana na wewe hapo kwenye kumkamata zumaridi hata Mimi niliona Sheria ilipindishwa Sana lakini hii huwa inatokea Mara nyingi hasa kwa jeshi la polisi hapa Tanzania askari anakuja tu anamkamata raia bila kufuata taratibu maalum.
Hapo kwenye mashtaka ya mtuhumiwa kuhusu kusafirisha watu nadhani wamemaanisha human trafficking? ambayo tafsiri yake kisheria inaweza kua Pana sana, wataalam washeria watatusaidia.
Kuhusu ibada ni kweli kuabudu sio kosa kisheria lakini umefuata taratibu? Kumbuka zumaridi alikua na kanisa na likafungiwa kwa sababu zilizowekwa wazi kisheria na zilizokua na mashiko kabisa na alitii amri, so kitendo Cha yeye kuanza kufanya ibada nyumbani kwake maana yake kahamishia kanisa pale ambapo kwanza sio eneo la kanisa ni eneo la makazi na pia bado vigezo vilivyofanya afungiwe Mara ya kwanza hajavitimiza lakini analazimisha kuendelea na kanisa lake.
Kama anataka kuabudu bila kusumbuliwa afuate Sheria asajili kanisa lake na afuate taratibu zote za kisheria hakuna atakayemsumbua hata wakitaka kulala humo kanisani hakuna atakayewafuatilia.
Yes,unaongea vitu vinamake sense.
 
Acha kuwa bendera kufuata upepo,Leo kwa Zumaridi kesho kwako... wafuate sheria waache uonezi
Kabisa! Akiguswa wanaempenda kwa kuvunja wanalia, lakini kwa mbinu ileile akiguswa wasiye mpenda wanashangilia!

Wanasahau kuwa KUNA MSEMO USEMA WAKIZOEA KUNYONGA , KUCHINJA KWA KISU WANAONA TABU!
Watanyonga kila anaekatiza
 
Huyo Mganga wa kienyeji, wakiweza wamfunge jiwe shingoni na kumtosa baharini tu.
 
Kwani kiongozi mzuri wa dini ni mpaka atoke kwenye haya makanisa ya wazungu..au wewe kiongozi wa dini unampima kwa vigezo gani..je huko unakoamini kuna viongozi sahihi wa dini mbona kila siku wamejaa maovu na mazambi mengi.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna sehemu hakuna maovu......ila sehemu nyingi ni taasisi,siyo mtu anaabudiwa kama Mungu na mambo mengi ya ajabu kinyume hata na sheria za nchi......
 
Back
Top Bottom