Sakata la Zumaridi na namna alivyokamatwa na polisi ni kichefuchefu, sheria haikuzingatiwa

Sakata la Zumaridi na namna alivyokamatwa na polisi ni kichefuchefu, sheria haikuzingatiwa

Pale walipokutwa watu sio kanisa, ile ni nyumba ya makazi. watu 149 kwenye nyumba ya mtu binafsi walikua wanafanya nini kama huduma zake za kikanisa zimefungiwa? Na kwanini polisi walivyofika nyumbani kwake walitoka hao misukule yake kuwazonga hadi kumdondosha mmoja wa polisi. Hata ingekua mimi unanifanyia ule ujinga niko mwenyewe nikienda kubeba kikosi changu itakua mbwai tu.
Kisheria watu wangapi wanaruhusiwa kuwa nyumbani kwenye makazi binafsi ya mtu?
 
Kosa walilo utaarifu Umma kwamba anasafilisha BINADAMU 149, kosa hilo Linatia aibu nyingine!

Hivi tangu lini watu wanaokusanyika kusali pamoja imekuwa kosa la jinai?

Hapa naona upotoshaji wa makusudi ili kujenga hoja yako. Kosa ni anasafirisha binadamu wewe unasema kukusanyika
Mtoa mada anatetea hata Mambo ya hivyo, huu Ni upotoshaji wa makusudi
 
Swali la kwanza hujanijibu..

2. Wakristo wote Tanzania sijaona wanajisitiri naongea kwa Experiences kila siku naenda kanisani,kujisitiri wanajisitiri waislamu tu...haya Zumaridi kavaa nini cha ajabu pale?nimepita you tube mbona hakuna la ajabu pale,kama ana mapaja manene sio yeye wa kilaumiwa.... msikuze mambo jamani.... Acheni kutoka vibanzi wenzenu wakati nyie mna maboriti

Inatakiwa uelewe kwanza kuwa kanisani hakumaanishi wewe ni Mkristo, makanisa mengi ni makanisa ya shetani viongozi vyake uogopa kuwaudhi waumini Ili wasikimbie makanisa sadaka zikapungua.
Lakini wakafundisha ile kweli wengi awatoenda kanisani.
 
Usirudie Tena kumfananisha YESU na Uyo mfalme wenu.
Sio ajabu lakini,hata huyo Yesu alikataliwa na bado anakataliwa mpaka Leo hii na ndugu zake huko Uyahudi.... Ukienda huko Israeli na habari za Yesu wanakushangaa
 
Waanze na Mwamposa pale wanakula Hadi nauli in the name of sadaka ya kujimaliza,afuatwe Gwajima nae ndio muasisi wa kufufua misukule... kama vipi wampotezee tu huyu bibie
Mwamposa alisababisha hadi vifo Moshi kisa kugombania kukanyaga mafuta na sidhani kama alifunguliwa hata kesi ya manslaughter.
 
Swali la kwanza hujanijibu..

2. Wakristo wote Tanzania sijaona wanajisitiri naongea kwa Experiences kila siku naenda kanisani,kujisitiri wanajisitiri waislamu tu...haya Zumaridi kavaa nini cha ajabu pale?nimepita you tube mbona hakuna la ajabu pale,kama ana mapaja manene sio yeye wa kilaumiwa.... msikuze mambo jamani.... Acheni kutoka vibanzi wenzenu wakati nyie mna maboriti
Pumzika sasa wacha mfalme Zumaridi apambane nayo yeye ndio mungu wenu. Kama wewe ni mkristo kweli usingemtetea sijali kuhusu mavazi yake kwanza libaya tu Ila ewe mkristo usikubali kumuita binadamu mwenzio au kumfananisha na Mungu.

Mie sijali anafanya mambo gani, anavaa nini, anaongea nini, anakaa na akina nani nk Ila kujiita Mungu aisee huyu hafai hata robo. Kwani angefanya hayo mazingaombwe yake bila kujiita hayo majina Kuna ubaya gani?

Kwani kuliita jina la Mungu kwa mizaha namna hii ni katazo kubwa kwenye biblia Kama wewe ni mkristo kweli basi kwako inatosha kuwa chukizo mbele yako kwakuwa hata mbele yake mwenye jina lipitayo majina yote ni chukizo na ubatili mkubwa kwa yite yanayofanyika pale.

Sijali anavaa nini Kama wengine wengi wanavyoisema in my view halitamanishi chochote libaya tu, Ila naudhika mtu kujiita Mungu.
 
Kitendo walichofanya polisi ni kuingilia uhuru wa kuabudu. Mbona wakatoliki wanafanya jumuia majumbani? Leo watamsakama Zumaridi sababu ni mdogo. Kesho watakuja kwenye dini kubwa zaidi.
Kosa sio kukusanyika, kosa ninkusafirisha watu 149.

Ndivyo hati ya mashtaka yake ilivyoandikwa.

Tusilete upotoshaji wa maksudi Hapa[emoji3525]
 
Sio ajabu lakini,hata huyo Yesu alikataliwa na bado anakataliwa mpaka Leo hii na ndugu zake huko Uyahudi.... Ukienda huko Israeli na habari za Yesu wanakushangaa
Leo umefeli sana
 
Inatakiwa uelewe kwanza kuwa kanisani hakumaanishi wewe ni Mkristo, makanisa mengi ni makanisa ya shetani viongozi vyake uogopa kuwaudhi waumini Ili wasikimbie makanisa sadaka zikapungua.
Lakini wakafundisha ile kweli wengi awatoenda kanisani.
Sasa tunaenda sawa,kwa kuwa umekiri kwa kinywa chako kwamba makanisa mengi ni makanisa ya shetani,sasa kwa nini anaonewa mmoja? kwa nini Zumaridi?si wakamatwe wote?
 
Mhalifu hawi mhalifu hadi pale itakapothibitika!

Sakata la mfalme Zumaridi (Kiongozi wa kanisa la Zumaridi huko Mwanza) Linaacha midomo wazi kwa wapenda haki na utii wa sheria!

Sipo hapa kumtetea Mfalme Zumaridi, Bali nashangaa namna ya uharamu wa ukamtaji!

Taratibu za ukamataji kwa mujibu wa sheria ziko wazi kabisa lakini mamlaka zimekuwa zikionesha kufeli Mara kwa Mara kutekeleza sheria hiyo jambo ambalo limekuwa likitweza utu wa watu wasio na hatia.

MFANO! mambo kama haya yalitokea huko mtwara hadi kufedhehesha uongozi wa polisi ambayo yalianza hihivi kwa kufumbafumba mambo,

Mfano 2. Ni huko ARUSHA Kuna taarifa ya askali mzalendo kulalamika kutaka kuuwawa na polisi wenzake kwa mambo Yale Yale kama ya mtwara na serikali iko kimya.

SASA NI HILI SAKATA LA TATU LINALOTIA KICHEFCHEFU

Ni TUKIO LA zumalidi Siku ya kwanza inaripotiwa kwamba polisi waliruka ukuta/geti ili kuingia kwa Zumalidi! Kitendo hiki kilitakiwa kulaaniwa na kila mtu! (Waliruka kwa Zumalidi kesho wataruka kwako)

Kama kulikuwa na ulazima wa kufika pale kwanini hawakufuata utaratibu wa upekuzi unavyotaka? Kwanini hawa kumshirikisha mwenyekiti wa mtaa/mjumbe? Kwanini waliruka ukuta kama jambazi! (VIPI KAMA ZUMARIDI ANGEJIBU MASHAMBULIZI KWA KUFYATUA RISASI KWA POLISI ALIYEVAA KIRAIA ALIPORUKA UKUTA?) Ina maana wangejibu kwamba walikuwa kwenye mapambano na majambazi au?

Kwa utaratibu walio utumia polisi hauna tofauti na utarabu wa kijambazi! Na hili linachangia sana siku hizi RAIA kutokutofautisha kati ya jambazi na polisi.

Tukiachana na mbinu ya ukamataji!

Riport ya polisi ina ukakasi mkubwa juu ya mtuhumiwa Zumaridi!

Kosa walilo utaarifu Umma kwamba anasafilisha BINADAMU 149, kosa hilo Linatia aibu nyingine!

Hivi tangu lini watu wanaokusanyika kusali pamoja imekuwa kosa la jinai?

Mbona jumuiya na taasisi kibao tunawaona wanakusanyika na kukesha na haijawahi kutajwa kuwa ni kosa?

Zumalidi kasafirisha binadamu kutoka wapi kwenda wapi kwa lengo gani? Kuna jinai gani pale?

Hapo taifa juzi wakatoliki walikusanyika mbona haikutamkwa kuwa ni usafirishaji wa binadamu?

Kina mwingira na wachungaji kibao Tanzania kila kutwa wanakusanya watu na haisemwi ni usafirishaji,

INAKUWAJE JAMBO LILE LILE LIWE HALALI KWA MWAMPOSA LAKINI LIWE HARAMU KWA ZUMARIDI?

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Nawashauri TAKUKURU WAINGILIE KATI!
Haiwezekani sheria zipo wazi, kwanini zisingefuatwa kama kweli ZUMALIDI anamakosa makubwa hivyo!

Mimi kwa utashi wangu nahisi sakata la Zumaridi lina maslahi binafisi!

TUKIRUHUSU HAYA YA UKIUKWAJI WA SHERIA HAKUNA ATAKAYEBAKI SALAMA!

Itakuwa mtu akikosana na polisi wanakuja kuluka ukuta! Na majambazi nao watatumia mwanya huohuo kufanya uharifu!
Dah... Hivi Ni Zumaridi au Zumalidi?....maana mnanichanganya😊🤭
 
Kosa sio kukusanyika, kosa ninkusafirisha watu 149.

Ndivyo hati ya mashtaka yake ilivyoandikwa.

Tusilete upotoshaji wa maksudi Hapa[emoji3525]
Kawasafirisha kutoka wapi kwenda wapi jamani?
 
Pumzika sasa wacha mfalme Zumaridi apambane nayo yeye ndio mungu wenu. Kama wewe ni mkristo kweli usingemtetea sijali kuhusu mavazi yake kwanza libaya tu Ila ewe mkristo usikubali kumuita binadamu mwenzio au kumfananisha na Mungu.

Mie sijali anafanya mambo gani, anavaa nini, anaongea nini, anakaa na akina nani nk Ila kujiita Mungu aisee huyu hafai hata robo. Kwani angefanya hayo mazingaombwe yake bila kujiita hayo majina Kuna ubaya gani?

Kwani kuliita jina la Mungu kwa mizaha namna hii ni katazo kubwa kwenye biblia Kama wewe ni mkristo kweli basi kwako inatosha kuwa chukizo mbele yako kwakuwa hata mbele yake mwenye jina lipitayo majina yote ni chukizo na ubatili mkubwa kwa yite yanayofanyika pale.

Sijali anavaa nini Kama wengine wengi wanavyoisema in my view halitamanishi chochote libaya tu, Ila naudhika mtu kujiita Mungu.
Kuna watu wanaudhika pia wewe ukila Kitimoto. Lazima tujifunze kuishi kwa kuvumiliana imani na itikadi tofauti ilimradi watu hawavunji sheria wala kudhuru wengine.
 
Sasa tunaenda sawa,kwa kuwa umekiri kwa kinywa chako kwamba makanisa mengi ni makanisa ya shetani,sasa kwa nini anaonewa mmoja? kwa nini Zumaridi?si wakamatwe wote?
Simply fulani anafanya uasherati na hajakamatwa na mke au mume wake haimaanishi nawe hautakamatwa.
 
Back
Top Bottom