Sanamu la Magufuli na ukarabati wa kumbi za kisasa kujengwa kwa Tsh milioni 420 viwanja vya Sabasaba

β€œUsijifanyie sanamu ya kuchonga….” Hilo sanamu la nini sasa?
 
Ndio maana tunasema tunataka katiba MPYA!!

Magufuli katusababishia hasara kubwa ktk nchi hii, kaiba sana, kanyanyasa sana raia wa nchi hii na ujinga mwingine mwingi kafanya,

Kwa heshima gani hasa hadi pesa ya wananchi itumie kumjengea sanamu? Ndio maana waTanzania wengi hawalipi kodi, kodi tunalipa ila inaelekezwa kwa mambo ya kipuuzi na ya kishamba kama haya!?

Huu ujinga upo Tanzania tuu na ni sababu ya hii katiba butu na ya kikoloni tulio nayo.

Ni mtu mjinga tu anaweza kubeza mchakato wa katiba mpya.
 
Tuendelee kuwa wazalendo
 
Kwa msingi na mantiki hiyo basi ni vizuri aidha usiweke bango lolote humu JF au ukaandike ambao watu/mtu hata comment au kuuliza! Vinginevyo utajibiwa tu, aidha kwa kukufurahisha au kwa kukukera.
Kile kinachokupa furaha kifanye ila kwangu mimi sipo hapa kukufurahisha. Bahati mbaya sana unapambana na mtu asiyeelewa katika kile unachokiamini.
 
Mtakufa kwa pressure nyau nyie
Nadhani wewe si mwenyeji wa huko na naamini huishi huko, vinginevyo, unapaswa kujua kuwa hicho kijiji cha Liangweni kimetengewa fedha kiasi cha shilingi 210milioni kwa ajili ya hiyo zahanati, madawa na vifaa tiba. Kama hujui cheki na Mbunge wako au TAMISEMI.
 
Kile kinachokupa furaha kifanye ila kwangu mimi sipo hapa kukufurahisha. Bahati mbaya sana unapambana na mtu asiyeelewa katika kile unachokiamini.
Pole sana humu JF hatunaga "mapambano" ila tunakwenda kwa hoja, tena zile hoja zenye nguvu yaani tunakwenda kwa nguvu ya hoja na siyo kwa hoja za nguvu na za kufurahishana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…