Sanitaiza huwa mnatumia?
Vipi na faida ya kuchambia mawe bado mwaijua?
Kwenye kiswahili sijawahi kuliona neno alhamudilal.
Mnatawadha ili kujikinga na magonjwa? Je Koran imeyaainisha hayo magonjwa ni yapi au ya aina gani?
Hilo la viatu sahau, Israel wameshagundua chanjo ya Corona na hata isipofanikiwa, watu hawawezi kuamriwa kutembea peku au kuingia mahala fulani peku.
Biologically tutatengeneza tatizo jingine kubwa sana watu wana mifangasi miguuni, na kunawa hakuondoi fangasi.
Burqa ndio Barakoa uko sawasawa kweli?
Burqa na Barakoa ni vitu viwili tofauti.
Barakoa zinatumika mahospitalini miaka mingi sana.
Kuna athari za kutumia Barakoa moja kwa muda mrefu kubwa tu kama zile anazozipata mtu anayejifunika kichwa wakati wakulala.
Unaweza kutueleza hiyo burqa moja mnaivaa kwa muda gani kabla hamjavaa nyingine?
Na unafahamu kwanini kuvaa burqa mataifa yenye jangwa kuna faida nyingi kama Yemen, Saudia, Djibouti, Sudan, Qatar n.k kuliko kuvaa burqa San Diego?