Sasa nahitaji ndoa kuliko kitu kingine chochote. Siwezi tena kusubiri

Shauri yako kua makini mkuu
 
Mambo mazuri hayataki haraka.Naomba usome huu mstari,Methali(Mithali)24:27 "Tayarisha kazi yako ya nje,na utayarishe Kila kitu shambani,Kisha uijenge nyumba yako". Mm nakukumbusha uwe na shughuli ya kuingiza kipato Cha kulea hiyo familia ndio mengine yafwate.
 
Bwana mdogo kwa umri huo Tena jobless na kibunda huna achana na mawazo ya ndoa au nenda morogoro ndanindani kwa wazee wa kiruguru wakuonzeshe demu alotoka kuchezwa
 
Usihofu Mungu atakupa hitaji lako Cha kwanza
1.Hudhuria sana kanisani
2.Mfate msichana unaeona angalau ana muelekeo sawa na wewe mwambie hitaji lako la kuoa
3.msichana awe angalau 25 kwenda juu ukipata mwenye 28 huyo atafaa zaidi
4.usiwe muhitaji sana as if unataka kuhurumiwa onesha manhood kwenye utaempata
 
Mtihani ni kumpata wa kukupenda kwa dhati without conditions. Naamini Mungu ataniletea.
Watu muna expectations za ajabu kwa Mungu!!!

Jamani Mungu hafanyi kazi ya kugawa wanawake kwa waume! Never
Ingekuwa anafanya hio kazi, kungekuwa na reserve ya wanawake mabikira kwa ajili ya mgao kwa wale waombao mke!

Mungu ametoa akili kwa watu, ili wazitumie kwenye shughuli zao zote za kijamii, kiuchumi n.k
Anayeoa atumie akili zake kupanga anaoa lini, anamuoa nani, anazaa wangapi, atakula mbususu kwa staili gani, kwa wakati gani,
Yaani waafrika, kilakitu Mungu, Mungu, mwisho wa siku ndo wanaongoza kwa umaskini, na vifo!

Akili, Akili, Akili, Akiliiiiii

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwahio ukikaa Kati ya wanaume inatakiwa kusema shida Ni nini Mkuu?
 
Kwahio ukikaa Kati ya wanaume inatakiwa kusema shida Ni nini Mkuu?
Inabid useme hivi mimi sikuwa tayari kubeba majukumu, maana wapo vijana wanatembeza mitumba wana Mke na watoto, wapo waha wanafanya kazi ya kukopesha wana Mke na watoto.

sema hivi ndugu zangu mimi sikuwa tayari kubeba majukumu full stop.

Kama watu wanaponda Kokoto na wana familia, kama kijana anauzwa pweza na kacholi na ana Mke na mtoto unataka kusema nini wewe?
 
Bro, una miaka 40, jobless, kipato kidogo, halafu unatafuta mke wa kuoa? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Bro ndoa kwa mwanamke ndio lazima kwa mwanaume ni choice.

Huyo mwanamke utakae oa sijui unatafuta mkafanyaje saa hii, hiyo miaka yako iliyobaki hebu tulia mwenyewe tafuta jambo serious la kukuingizia hata 20,000 per day uwe inasave hata 15,000 kwa siku halafu baada ya miaka 5 toka sasa jaribu kutafakari tena kama upo serious na hoja ya kuoa.

Unatafuta mwanamke sababu unaogopa upweke ila sio kwasababu upo serious na kutafuta ndoa.

Wanawake wa sasa uishi nae na hauna kazi nini mtafanya hapo ndani zaidi ya kugombana na kuharibiana focus?

Hebu kuwa serious.
 
Muombe Mungu
Tembea tembea
Angalia mrembo anayekupendeza macho na roho. Dada wa level yako
Mwambie haja ya moyo wako
Basi jambo limeisha
 
Na ambao ndio hao watoto wao wanalilia elimu bure sio?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…