Saudi Arabia, UAE, Iran, Egypt, Ethiopia na Argentina zakubaliwa kujiunga BRICS

Saudi Arabia, UAE, Iran, Egypt, Ethiopia na Argentina zakubaliwa kujiunga BRICS

Kinapungua kwa kiwango gani na ukilinganisha na sarafu zipi??

US Dollars katika foreign currency reserves zinazohifadhuwa na nchi mbalimbali duniani ni takribani 60% kwa sasa, inafuatiwa na Euro 20%, Yen ya Japan 6%, Paundi ya UK 5%, Yuan ya Mchina ni 3%
Ilikuwa ni 78% miaka ya nyuma kufikia mwaka 2021 imefikia 59% kulinganana ripoti ya IMF
 
View attachment 2727274

Sasa BRICS itakuwa na wanachama wenye sifa zifuatazo

●BRICS itakuwa na mataifa 6 kati ya 9 ambayo ni wazalishaji wakubwa wa mafuta na gesi duniani.

●BRICS itakuwa na mataifa ambayo yana 80% ya oil reserve duniani.

●BRICS itakuwa na mataifa yenye jumla ya GDP $30.76 trillion. Asilimia 36% ya uchumi wa dunia utakuwa mikononi mwa mataifa ya BRICS.

Zaidi ya mataifa 40 tayari yameonyesha nia ya kujiunga na BRICS.

Watafiti wa mambo ya kiuchumi wanasema uwepo wa mataifa makubwa yanayozalisha nishati ya mafuta ndani ya BRICS kutadhoofisha mfumo wa PetroDollar ikizingatiwa baadhi ya mataifa hayo yameanza kutumia sarafu zao katika biashara ya nishati hiyo.

Je jina lao litabadilika akutokana na current name kuundwa na hizo nchi 5?
 
Hii si habari njema kwa mataifa ya G7

Ikumbukwe kuwaweka pamoja Iran na Saudi Arabia hapo ni juhudi za China za kuyapatabisha mataifa hayo mawili wakati Marekani alitamani mataifa hayo yaendelee kuwa hasimu

Egypt na Ethiopia zimekuwa na msuguano kwenye bwawa la GERD kuyaleta pamoja mataifa hayo ni juhudi nzuri za BRICS

Kikubwa zaidi ni uwepo wa mataifa ya Africa inapendeza sana
Yaani kama vile anaongea mchambuzi wa maswala ya kimataifa BBC, Professor Boaz
 
ndani ya miaka miwili hadi mitano Ijayo, US atakua ameshamtengeneza India kiwa mbadala wa China
Mchina anauza bidhaa zake China-based products. Kwa mujibu wa forecast za IMF wanasema kuwa kufikia 2040 mataifa makubwa kiuchumi yatakuwa
●China
●India
●Marekani

Sasa kati ya wewe na IMF ni nani tuchukue projections zake?
 
View attachment 2727274

Sasa BRICS itakuwa na wanachama wenye sifa zifuatazo

●BRICS itakuwa na mataifa 6 kati ya 9 ambayo ni wazalishaji wakubwa wa mafuta na gesi duniani...
Ni lini watanzania nao wataingia BRICS au wamekaa tu kama mafisi wanasubiri mkono udondoke waokote. Nchi hii ngumu sana
 
Unajua kuwa kiwango cha reserve ya US Dollars katika foreign currency reserves za mataifa mbalimbali duniani kinapungua

Unafikiri sababu ni nini?
Kupungua kwa US Dollars reserve kunaifaidisha sarafu ipi? Halafu US $ reserve ikipungua unadhani madeni yenu mtalipa na nini na services na purchases mtafanya kwa currency gani?

US kawasaidieni kujibu hilo swali, ameamua kupunguza hela yake kutoka kwenye mzunguko, umeona matokeo yake?

...and BRICS haiendi popote sababu kati ya wanaotegemewa zaidi India ni mmoja wapo na India inapewa nguvu kubwa na kiuchumi, technology, Intelligence na US.
 
India ni mmoja wapo na India inapewa nguvu kubwa na kiuchumi, technology, Intelligence na US.
Mbaya kuliko, Mexico, Argentine, Brasil hao kamwe na kamwe hawawezi kuwa kusimama upande mmoja na Russia na China na Waarabu
Hivi mkuu hayo mataifa yaliyojiunga na wewe ni nani mwenye anajua faida ya huo muungano?

Umekuwa mkosoaji wa hayo mataifa kwamba walikurupuka?

Ok Kwani hiyo EU na G7 si kuna mataifa yaliwahi kuwa maadui miaka hiyo na wakazichapa sana kwenye WWI na WWII mbona hatusikii mkisema hawawezi kusimama upande mmoja

Nikurekebishe kidogo Mexico sio member wa BRICS
 
Angalia mtazamo wa vijana wanaiponda BRICS kwenye huu uzi hoja zao ni za kipuuzi sana. Ndio ujue Tanzania funa safari ndefu sana.
Sasa km vijana wenyewe ndiyo hawa wanaolawitiana, kusagana, kuvaa milegezo na vikuku miguumi unategemea wachangie nini positive. Wao muda wote wanawaza kunyanduana tu.
 
Baada ya kumiliki Nishati ya mafuta duniani, BRICS wanalenga kumiliki Dhahabu na Uranium hasa toka nchi za Africa. Madini kama Ntantalum na Cobalt nayo yanatafutwa kuingizwa katika BRICS. Hii inamaana kwamba hata US akitaka kuhamia kwenye Magari ya kuchaji Bado atatakiwa kufuata masharti ya BRICS
 
Kinapungua kwa kiwango gani na ukilinganisha na sarafu zipi??

US Dollars katika foreign currency reserves zinazohifadhuwa na nchi mbalimbali duniani ni takribani 60% kwa sasa, inafuatiwa na Euro 20%, Yen ya Japan 6%, Paundi ya UK 5%, Yuan ya Mchina ni 3%
Kiuchumi iko hivi kadiri mataifa yanapoamua kutumia sarafu zao kwenye international transactions au kuamua kutumia sarafu zingine ndivyo utegemezi wa US Dollar unapungua ndivyo na kwenye foreign reserves hupungua kwa sababu demand yake inashuka
 
Hivi mkuu hayo mataifa yaliyojiunga na wewe ni nani mwenye anajua faida ya huo muungano?

Umekuwa mkosoaji wa hayo mataifa kwamba walikurupuka?

Ok Kwani hiyo EU na G7 si kuna mataifa yaliwahi kuwa maadui miaka hiyo na wakazichapa sana kwenye WWI na WWII mbona hatusikii mkisema hawawezi kusimama upande mmoja

Nikurekebishe kidogo Mexico sio member wa BRICS
Kabla ya BRICS kulikuwepo na movement ya umoja wa Shanghai
 
Ilikuwa ni 78% miaka ya nyuma kufikia mwaka 2021 imefikia 59% kulinganana ripoti ya IMF
Hiyo 78% ni takwimu za miaka ya 1975 kurudi huko nyuma. Miaka 50 ambayo ni nusu karne mambo yalipaswa yawe yamebadilika kabisa, dola imesahaulika na kusiwepo tena na hii mijadala inayotokana na mihemko ya kuachana na matumizi ya US dollar.
 
Hiyo 78% ni takwimu za miaka ya 1975 kurudi huko nyuma. Miaka 50 ambayo ni nusu karne mambo yalipaswa yawe yamebadilika kabisa, dola imesahaulika na kusiwepo tena na hii mijadala inayotokana na mihemko ya kuachana na matumizi ya US dollar.
Lakini imeanza kushuka kwa kasi miaka ya late 1990s
 
Back
Top Bottom