Sayansi ya uumbaji ndani ya Qur'an/Koran: Sehemu ya 01

Sayansi ya uumbaji ndani ya Qur'an/Koran: Sehemu ya 01

JINSI MVUA INAVYO SABABISHA MMEA KUOTA KWA HATUA KATIKA QUR'AN

Kwa maelezo ya Qur-an na Sayansi


Allaah anasema katika Qurani

“... Na unaiona ardhi imetulia kimya, lakini tunapo yateremsha maji juu yake husisimka na kututumka, na kumea kila namna ya mimea mizuri.”(Quran 22:5)

Inafahamika kuwa hakuna uhai pasina maji na hewa. Lakini je imepata kupita kwenye akili ya yeyote kuwa udongo nao unayo sehemu yake kwenye hili? Quran hapa imetaja hatua tatu muhimu kwenye maisha ya udongo.

(1)Kutetema
(2) kuvimba (kututumka)
(3) kutoa mimea ya aina kwa aina (dume na jike)

Kwa kulinganisha maelezo ya wana sayansi na hatua zilizo tajwa kwenye Quran

Hatua ya kwanza mvua inapodondoka, chembe, chembe tofauti zinazo tengeneza chembe moja ya mchanga, zinaanza kutetema na kupokea au kupunguza chaji zake za kiumeme kutokana na matone ya mvua yanayo dondoka. Mwaka 1828, mtetemo huu wa udongo kutokana na matone ya mvua uliitwa ‘Brown Movement’ baada ya Robert Brown kufanya ‘uvumbuzi’ huo na kuieleza dunia kuwa matone ya mvua yanapo shuka vichembe, vichembe tudogo, tudogo, vinavyo tengeneza chembe moja ya mchanga vinatetema.


Hatua ya pili, Quran inazungumzia kuvimba au kuongezeka ukubwa kwa chembe hizo za mchanga au mchanga kwa ujumla. Chembe ya mchanga hutengenezwa na tabaka mbili, baina ya tabaka hizo kuna nafasi ambayo inaruhusu maji na chaji zinazo tokana na matone ya mvua kupenya, kisha kutokana na athari hiyo udongo unatanuka au unavimba.

Hatua ya tatu, baada ya hapo ni udongo ulio kuwa umekufa, unapata uhai, na kutoa uhai kwa mimea ambayo nayo itasababisha kupatika uhai kwa viumbe wengine akiwemo binadamu.


Zama zote binadamu tumekuwa tukifahamu kuwa mvua ndiyo inayo sababisha mimea kuota, lakini hatukuwa hata kidogo, tukifikiria ni hatua gani au ni kitu gani kinacho tokea kabla ya mimea kuchomoza. Lakini ni vipi katika zama za Muhammadi binadamu angeweza kuzitambua hatua hizo zinazo pitiwa na udongo kabla ya kuanza kuotesha mimea yake?


Kama tulivyo ona, hatua hii ya muhimu sana, tunaikuta inavumbuliwa mwaka 1828, na kutokana na heshima na thamani uvumbuzi huo, tendo lenyewe linapewa jina la mvumbuaji, lakini Muhammad alishakisema karne zaidi ya kumi kabla, sasa inakuwaje? Vipi Muhammad aliweza kuliona hili, ni wapi alipatia taarifa hizi, ni vipi hazipingani hata kidogo na uvumbuzi wa zama zetu?
 
Kuongea kitu pasi na ushahidi/elimu maana yake unafanya mambo kishabiki.

Kukataa kusoma kuhusu kitu fulani huko ni kubagua/kuvunja misingi ya elimu.mtu wa hivyo Mimi namuona mtu flani anayeogopa kujifunza kitu kipya kwa hofu kuharibu imani ya kitu alichokuwa anakiamini mwanzo.

Unakataa kuwa miujiza ya kisayansi kwenye Quran sio ya kweli lkn hautuambii ni uongo kivipi.

Tafuta kitabu ; "The Quran unchangeable miracle " only 2gb
 
Habari za kisaayansi kwenye ni nyingi sana haiwezekani ikawikaw yote imetokea kwa bahati nasibu , yani iwe imeandikwa kwa kukisiwa
nipe muujiza mmoja wa kisayansi wa Quran nisilim
 
nipe muujiza mmoja wa kisayansi wa Quran nisilim
Asili ya chuma in quran

“...Na tumeteremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu...” Qur’an 57:25


Kisayansi Chuma ni matokeo ya kupasuka pasuka kwa Nyota zilizoko angani, nyota ambazo ni kubwa sana kuliko Jua . Hali hiyo ya kutokea hayo mapande, yanayosababisha sisi wakazi wa dunia yetu kupata chuma,

yanatokea baada ya nyota hizo kufikia hali ya uzee (Nova stage) kipindi ambacho joto katika nyota hizo hufikia nyuzi joto zinazo kadiriwa kuwa zaidi ya nyuzi digirii 100m Wakati huo chuma kinakuwa kingi sana katika nyota hizo. Joto linapokithiri kwa kiwango hicho, nyota hizo zinashidwa kuvumilia na hapo ndipo zinapo pasuka mapande mapande,

mapande hayo ambayo hutawanyika huku na huko na kuelekea mielekeo tofauti tofauti. Na hapo basi mapande mengine ndio huelekea huku katika dunia yetu. Na yanapokaribia anga la dunia yetu baadhi yake huvutwa na nguvu ya mvutano (gravitation force), na hii ni baada ya kupungua sana kwa ukubwa wake, na ni nadra sana mapande haya kushuka kwa ukubwa wa kuonekana. Bali mengi yao huja kwa mfumo wa kama vumbi. Na kupitiliza hadi chini ya ardhi na huko ndiko ujiunda pamoja na kujitengeneza majabali.

Huu sio muijuza pekee kwenye quran Bali nimeleta huu kwasababu swali lako halipo wazi (hujataja muujiza kuhusu nini)

na sijakujibu kwa sababu umetishia kusilimu Bali kukuonyesha huo muujiza
 
Asili ya chuma in quran

“...Na tumeteremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu...” Qur’an 57:25


Kisayansi Chuma ni matokeo ya kupasuka pasuka kwa Nyota zilizoko angani, nyota ambazo ni kubwa sana kuliko Jua . Hali hiyo ya kutokea hayo mapande, yanayosababisha sisi wakazi wa dunia yetu kupata chuma,

yanatokea baada ya nyota hizo kufikia hali ya uzee (Nova stage) kipindi ambacho joto katika nyota hizo hufikia nyuzi joto zinazo kadiriwa kuwa zaidi ya nyuzi digirii 100m Wakati huo chuma kinakuwa kingi sana katika nyota hizo. Joto linapokithiri kwa kiwango hicho, nyota hizo zinashidwa kuvumilia na hapo ndipo zinapo pasuka mapande mapande,

mapande hayo ambayo hutawanyika huku na huko na kuelekea mielekeo tofauti tofauti. Na hapo basi mapande mengine ndio huelekea huku katika dunia yetu. Na yanapokaribia anga la dunia yetu baadhi yake huvutwa na nguvu ya mvutano (gravitation force), na hii ni baada ya kupungua sana kwa ukubwa wake, na ni nadra sana mapande haya kushuka kwa ukubwa wa kuonekana. Bali mengi yao huja kwa mfumo wa kama vumbi. Na kupitiliza hadi chini ya ardhi na huko ndiko ujiunda pamoja na kujitengeneza majabali.

Huu sio muijuza pekee kwenye quran Bali nimeleta huu kwasababu swali lako halipo wazi (hujataja muujiza kuhusu nini)

na sijakujibu kwa sababu umetishia kusilimu Bali kukuonyesha huo muujiza
neno "Anzal" lililo tumika kwenye hio aya inamaa kuwa ni “Kushushwa kwa kitu au kuletwa kwa kitu toka angani (Sent down)
 
nipe muujiza mmoja wa kisayansi wa Quran nisilim

Na kwa hakika tumemuumba binaadamu kwa asili ya udongo - Quran 23: 12

Kisha tukamjaalia awe mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti - Quran 23: 13

Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyoganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka mwenyezimungu m’ bora wa uumbaji. - Quran 23: 14.

Haya maandiko kama tuyasoma kwa mazingatio utakuta yanaelezea utungaji wa mimba huko tumboni.

Sasa niambie kwa kipindi hicho cha muhammad (s.a.w) kuna mwanasayansi gani alikaa na kutoa maelezo juu ya utungaji wa mimba jee hiyo sio sayansi?
 
Mkisikia habari za Quran roho zenu huwa zinawakeleketa sana

Aya za sayansi zipo nyingi sana katika Quran ukizitaka zitakuja kama mvua maana aliyeumba ulimwengu ndio huyohuyo aliyeileta Quran

Chukua na hi nakupa kama zawadi

Quran 21:33.
Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi, vyote katika anga vinaogelea.
Huwezi kupata wasomi bila kuwa na uwekezaji wa elimu,sasa kama quran ndio chimbuko la sayansi mbona wagunduzi si wenye quran?
 
Huwezi kupata wasomi bila kuwa na uwekezaji wa elimu,sasa kama quran ndio chimbuko la sayansi mbona wagunduzi si wenye quran?
Quran sio kitabu cha sayansi Bali ni muongozo , kama kuna waislamu wanaamini hivyo basi wanakosea hio tunayoiita miujiza ni sehemu ya ukuu wa Mwenyezi Mungu kwamba yy ananafanya mambo makubwa.
 
Asili ya chuma in quran

“...Na tumeteremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu...” Qur’an 57:25


Kisayansi Chuma ni matokeo ya kupasuka pasuka kwa Nyota zilizoko angani, nyota ambazo ni kubwa sana kuliko Jua . Hali hiyo ya kutokea hayo mapande, yanayosababisha sisi wakazi wa dunia yetu kupata chuma,

yanatokea baada ya nyota hizo kufikia hali ya uzee (Nova stage) kipindi ambacho joto katika nyota hizo hufikia nyuzi joto zinazo kadiriwa kuwa zaidi ya nyuzi digirii 100m Wakati huo chuma kinakuwa kingi sana katika nyota hizo. Joto linapokithiri kwa kiwango hicho, nyota hizo zinashidwa kuvumilia na hapo ndipo zinapo pasuka mapande mapande,

mapande hayo ambayo hutawanyika huku na huko na kuelekea mielekeo tofauti tofauti. Na hapo basi mapande mengine ndio huelekea huku katika dunia yetu. Na yanapokaribia anga la dunia yetu baadhi yake huvutwa na nguvu ya mvutano (gravitation force), na hii ni baada ya kupungua sana kwa ukubwa wake, na ni nadra sana mapande haya kushuka kwa ukubwa wa kuonekana. Bali mengi yao huja kwa mfumo wa kama vumbi. Na kupitiliza hadi chini ya ardhi na huko ndiko ujiunda pamoja na kujitengeneza majabali.

Huu sio muijuza pekee kwenye quran Bali nimeleta huu kwasababu swali lako halipo wazi (hujataja muujiza kuhusu nini)

na sijakujibu kwa sababu umetishia kusilimu Bali kukuonyesha huo muujiza
Mmmmh!
 
Huwezi kupata wasomi bila kuwa na uwekezaji wa elimu,sasa kama quran ndio chimbuko la sayansi mbona wagunduzi si wenye quran?

Hata hivyo kitabu cha Qur’an sio kitabu cha sayansi bali ni kitabu chenye muongozo wa maisha. Lakini hiyo Camera unayoifahamu pengine isingezumbuliwa kama Ibn alhaytham ambae ni muislam asingeanzisha concept mpya ya jicho linavyoakisi mwanga katika kitabu chake kinachojulikana kama the book of optics na hiyo imekuwa mchango mkubwa mpaka kupatikana Camera.
 
Hata na mimi huwa natamani sana kuuliza swali hili sema sijawahi mpata mtu mwenye hekima na aliyeshiba Quran nikamuiliza
Wewe uliza maswali yako muislamu mwenye elimu nayo atakujibu .dini yetu hailazimishi mambo kitu kama huna elimu nalo basi usikitolee maelezo
 
HESABU NA UWIANO NDANI YA QURAAN

Miujiza ya Qur’an

Shukrani zote ni zake Allah(subhana wataala) tunamshukuru, tunategemea msaada wake, tunafuata muongozo wake, tunajilinda Kwake kutokana na shari za nafsi zetu, amali zetu ovu Na shari ya alivyo viumba .

Nashuhudia kwamba Hapana anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allah(subhana wataala) na kwamba Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam) ni mja Wake na mwisho wa Mitume yake na mjumbe wake, na kipenzi chake na mbora wa viumbe vyake.

Watu wengi wanaposkia hesabu wanapeleka fikra zao kwenye vitabu vingine tafauti na quraan, bila ya kuelewa kama mfumo wa kisasa kabisa unaotumika kuthibiti mambo ya kimasiliano kimahesabu upo ndani ya quraan...

Hesabu ndio lugha peka yake ambayo inaweza kutuwezesha dunia nzima tukawasiliana bila kujalisha utaifa wetu, ukabila wetu wala lugha tunazozungumza kwa sababu hesabu ndio ukweli unaothibutishika (provable facts)

SABABU ZA KUELEZEA HESABU NDANI YA QURAAN

1: Tunaeleza hesabu ndani ya quraan kwa kuthibitisha hifadhi ya quraan kwa maana kama ndani ya quraan hakuna kilichoongezeka wala kilichopungua hivyo kwa kutumia hesabu tunaweza kulithibitisha hili.
Hii inatufahamisha kwamba quraan yoote ni kama sentensi moja iliyobeba ujumbe mmoja kimaana na kimaandishi

Katika hili tunaweza kupata (balance perfection of words) uwiano uliitimia wa maneno yoote katika quraan

Hii ina maana kwamba kila kitu kiko mahali pake na hakuna kinachostahili kuongezwa wala kupunguzwa na kama itatokea kutaongezwa ama kupunguzwa chochote huu uwiano uliotimia wa kimahesabu katika quraan woote utaparaganyika.

Kama anavyosema Allah (subhana wataala)

Quraan 4 : 82

"Hebu hawaizingatii hii Qur'ani? Na lau kuwa imetoka kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka wangeli kuta ndani yake khitilafu nyingi. "

Hii ina maana kama ile quraan iliyoshuka wakati wa mtume (sallah llahu alayhi wassalam) ndio quraan ambayo tuko nayo sisi leo hii.

Hivyo kwa wale ambao wataifuata quraan kikamilifu leo hii hawatakuwa na tafauti na wale waliokuwepo wakati wa mtume wetu (sallah llahu alayhi wassalam) sote tunapokea ujumbe mmoja kutoka kwa Allah(subhana wataala) .

2: Hesabu ndani ya quraan ni (intelectualy defence) ni hoja ya kiakili kwetu dhidi ya wapinzani wa quraan.

Leo tunashuhudia mashambulizi dhidi ya mtume wetu ( sallah llahu alayhi wassalam) uislam na quraan katika vyanzo mbali mbali vya habari, hivyo hesabu ndani ya quraan ni hoja nzito kwetu kwa wale wapinzani wa Uislam.

Uwiano wa kimahesabu katika quraan ni mwingi sana ni wa kushangaza na pia uko juu sana ya akili za kibinaadamu.

Miaka 1400 iliyopita katika jangwa la arabuni ambapo hakukuwa na teknolojia yoyote ile hakuna ambae angeweze kutengeneza uwiano wa kimahesabu kama uliopo kwenye quraan. Lakini katika zama zetu tulizokuwa nazo leo hii ambapo tuna program maalumu kabisa zenye uwezo wa kunyambua na kuainisha maneno, pamoja na program hizi kushindwa lakini pia program hizi zimetusaidia kujua kwamba hata katika zama hizi hakuna ambae anaweza kuleta mizani ya maneno kimahesabu iliyokamilika kama iliyokuwepo ndani ya quraan.

Allah (subhana wataala) anasema katika quraan katika sura ya 17: 88

88." Sema: Wangeli kusanyika watu na majini ili walete mfano wa hii Qur'ani basi hawaleti mfano wake, hata wakisaidiana wao kwa wao."

________________________

Zifuatazo ni baadhi ya hesabu na uwiano wa kimahesabu ndani ya quraan

1. Neno adhabu katika quraan limetajwa mara 117
Neno msamaha limetajwa mara 134
Ukichukua 117+117=134

2. Neno "Sema" limerudiwa mara 332 na neno "Wamesema" limerudiwa mara 332

3. Malaika limetajwa mara 88 na neno shetani limetajwa 88

4. Dunia mara 115 na akhera mara 115

5. Peponi mara 77, motoni mara 77

6. Zaka mara 32, Baraka mara 32

7. Tajiri mara 26, Masikini mara 13
13+13=26

8. Mwanaume mara 23 Mwanawake 23
Je! Kuna uhusiano wowote na maumbile ya binandamu

Naam! Kisayansi idadi ya chromosomes(chembe hai) za binadamu ni 46 mtoto anarithi nusu kwa nusu kutoka kwa baba na mama, ukijimulisha idadi ya wanaume na Mwanawake iliotajwa kwenye quraan unapata idadi kamili ya chromosomes 23+23=46

Subhanallah!!

9. Neno bahari limerudiwa mara 32 na Neno inchi kavu (ardhi) limerudiwa mara 13

Je! Kuna maana na mahusiano yeyote na dunia yetu ? Shuhudia muujiza huu wa Quraan

ukitafuta uwiano kwa asilimia kati ya landmass(inchi kavu) na sea(bahari) inakuwa kamaifuatavyo:

32+13 = 45

Tunagawanya 45 kwa kila mamba (32 na 13) kisha tunazidisha na 100%

[32÷45x100% = 71.1111111% Sea]

na ukichukuwa

[13÷45x100% = 28.888888889% Landmass]

na kwa mahesabu ya karibu tunakadiria (approximation) kuwa

71.111111~ 71%
na hii ndio uwingi wa maji katika Dunia yetu.

Na

28.88888889% ~ 29%
na hii ndio ukubwa wa ardhi tulio kuwa nayo.

71+29=100

Na wana jografia wana tuambia hivyo hivyo kuwa maji yamechukua nafasi 71% na Ardhi imechukua 28%

10. SURAT AS-SAJDAH

Zipo aya katika quraan tunapozisoma tunalazimika kusujudu aya hizi zinaitwa ayaatul sajdah

Pia katika quraan ipo sura inaitwa surat as-sajidah katika mpangilio wa sura katika quraan ni sura ya 32

Pamoja na kuwa sura hii ni ya 32 lakini asili ya neno hili (root word) limekuja pia katika quraan mara 32

Neno hili sajadah limekuja katika quraan mzima mara 15

Katika sura hii neno sajadah limekuja kwenye aya namba 15

Na aya hii ina maneno 15

Surat As-sajadah ina aya 30 tukianza kuhesabu maneno kuanzia mwanzo mpaka tukifika neno sajad tutakuta ni neno la 186

Na tukianza kuhesabu baada ya neno sajad mpaka mwisho wa quraan tutapata maneno 186

Hii inaonyesha kuwa pamoja na neno sajad kuwa katikakati katika sura hii lakini pia lipo katikati ya maneno ya sura nzima...


Tukumbuke kama hii quraan haikushuka kwa mtindo wa maandishi ila imeshuka kama ( speech)

Quran 6 : 115

"Na yametimia maneno ya Mola Mlezi wako kwa kweli na uadilifu. Hapana awezaye kuyabadilisha maneno yake. Na Yeye ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua."


11. SURAT RRAD

Katika mpangili wa sura katika quraan sura hii ni ya 13

Pamoja na kuwa ni sura ya 13 lakini pia Aya iliyotaja neno RRAD ni Aya ya 13

Na Sura hii ipo katika juzuu ya 13

Neno RRAD Limekuja katika Quraan nzima mara mbili...

Katika sura hii ya 13 aya ya 13

Na katika sura ya 2 aya ya 19

Tukisebu maneno katika sura hii ya 13 aya ya 13
Tunapata maneno 19 yenye herufi 83

Na tukihesabu maneno katika sura ya 2 aya ya 19

Tunapata pia ina maneno 19 na herufi 83

"Na walisema :Mbona hukuteremshiwa kutoka kwa mola wako mlezi ishara??
Sema: Ishaza ziko kwake Allah ; ama mimi kwa hakika ni muonyaji mwenye kubainisha tu. Je! Kwani hayakuwatosha ya kwamba tumekuteremshia kitabu hiki wanachosomewa? Hakika katika haya zipo rehema na mawaidha kwa watu wanao amini"

12. SURAT NAHAL

Katika mpangilio wa Quraan hii ni sura ya 16

Sura hii ina jumla ya aya 128

Je kuna uhusiano kati ya jina la sura Nahal na namba ya sura (16) na namba za aya (128)

Naam upo uhusiano mkubwa sana;

Kisayansi Nahal (Nyuki dume) ana chromosomes 16 ambayo ndio namba ya sura.

Nyuki jike ana jumla ya chromosomes (2n) ambayo ni 32 ambayo ni sawa na (16 x 2 ) yaani mara mbili ya nyuki dume

Kwa hio namba ya sura 16 inaonyesha chromosomes za nyuki dume na nyuki jike.
Sura ina aya 128 hii ina maana ni mara 8 ya nyuki dume na mara 4 ya jumla ya gawio (Proportion) ya namba za Chromosomes.

Namba ya Chromosomes ni kama namba ya element haibadili popote pale duniani:

Chromosomes kwa kiswahili ni chembehai walizokuwa nazo viumbe na kwa kawaida hubeba wasifu mzima wa kiumbe huyo.

Neno Nahl limekuja mara moja tu katika Quraan yote la limekuja katika aya namba 68

Katika aya hii (68) jumla ya maneno yoote ni 13

Ukichukua namba ya aya 68 ukizidisha kwa namba ya maneno 13 utapata 884 !!!

Cha kushangaza hapa ni kwamba ukianza kuhesabu maneno kuanzia mwanzo wa sura mpaka ukifika neno Nahal utapata vile vile 884 !!!

Lakini utashangaa zaidi kuona kama idadi ya aya namba 16 katika Quraan nzima ni 85 na jumla ya maneno katika aya zote hizi pia inakuja 884 !!!

Na cha kushangaza kingine ni kuwa idadi ya aya namba 68 katika Quraan nzima ni 13 na ukizidisha hizi namba yaani 13 x 68 unapata tena 884 !!!

Jumla ya aya katika sura hii zinazogawanyika kwa 16 ni 16, 32, 48, 80 96, 112 na 128 ukihesabu jumla ya maneno yoote katika aya hizi utapata 119 !!!

Chakushangaza ni kuwa gramatic value ya neno nahl ni 119 !!!

Cha kushangaza tena hapa ni kuwa idadi ya sura zinazogawanyika kwa 16
kuanzia mwanzo wa Quraan mpaka sura hii pia ni 119 !!!

Tumeona kama Jumla ya aya zinagawanyika kwa 16 ni aya 85 ukizidisha 16 x 85 tunapata 1360 na tuliona kuwa jumla ya maneno katika aya hizo ni 884

Tukijumlisha 1360 na 884 tunapata 2244

Jumla ya maneno katika sura hii ni 1844 idadi ya maneno ukijumlisha na namba ya sura 16 unapata 1860

Mwanzo tulipata 2244 tukijumlisha na 1860 utapata 4,104

1; 4,104 = 19 x 216

216 = 6 x 6 x 6

Hii namba 6 inakuwa ni namba ya pembe kwenye (hexagon) pembe 6 ambayo ndio umbo la Asali

2; Namba hii pia ni jumla yaani (numerical value) ya aya namba 68 aya ambayo jina la (Nahal) nyuki limetajwa.

Numerical value ni namna ya neno linalovoadikwa katika mfumo wa namba.

Quraan 11 :13 - 14

"Au wanasema: Ameizua? Sema: Basi leteni Sura kumi zilizo zuliwa mfano wa hii, na waiteni muwawezao badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa mnasema kweli."

"Na wasipo kuitikieni, basi jueni ya kwamba (hii Qur'ani) imeteremshwa kwa ujuzi wa Mwenyezi Mungu, na kwamba hapana mungu ila Yeye. Basi je! Nyinyi ni Waislamu? "

Quran 12 : 37

"Na haiwezekani Qur'ani hii kuwa imetungwa na haitoki kwa Mwenyezi Mungu. Lakini hii inasadikisha yaliyo tangulia, na ni mfafanuo wa Kitabu kisicho na shaka ndani yake, kutokana na Mola Mlezi wa viumbe vyote. "

Alhamdulilah Tunakushukuru Allah(subhana wataala) kwa neema hii ya kutufanya sisi kuwa ni Waislamu.

Unaweza ku-share
 
Wewe uliza maswali yako muislamu mwenye elimu nayo atakujibu .dini yetu hailazimishi mambo kitu kama huna elimu nalo basi usikitolee maelezo

Ndiyo unambie kuwa kuna ukweli kwamba " Kitabu cha Quran takatifu mtume alishushiwa moja kwa moja kutoka Mbinguni kikiwa na makaratasi yake " kuna ukweli katika hili ?
 
Asili ya chuma in quran

“...Na tumeteremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu...” Qur’an 57:25


Kisayansi Chuma ni matokeo ya kupasuka pasuka kwa Nyota zilizoko angani, nyota ambazo ni kubwa sana kuliko Jua . Hali hiyo ya kutokea hayo mapande, yanayosababisha sisi wakazi wa dunia yetu kupata chuma,

yanatokea baada ya nyota hizo kufikia hali ya uzee (Nova stage) kipindi ambacho joto katika nyota hizo hufikia nyuzi joto zinazo kadiriwa kuwa zaidi ya nyuzi digirii 100m Wakati huo chuma kinakuwa kingi sana katika nyota hizo. Joto linapokithiri kwa kiwango hicho, nyota hizo zinashidwa kuvumilia na hapo ndipo zinapo pasuka mapande mapande,

mapande hayo ambayo hutawanyika huku na huko na kuelekea mielekeo tofauti tofauti. Na hapo basi mapande mengine ndio huelekea huku katika dunia yetu. Na yanapokaribia anga la dunia yetu baadhi yake huvutwa na nguvu ya mvutano (gravitation force), na hii ni baada ya kupungua sana kwa ukubwa wake, na ni nadra sana mapande haya kushuka kwa ukubwa wa kuonekana. Bali mengi yao huja kwa mfumo wa kama vumbi. Na kupitiliza hadi chini ya ardhi na huko ndiko ujiunda pamoja na kujitengeneza majabali.

Huu sio muijuza pekee kwenye quran Bali nimeleta huu kwasababu swali lako halipo wazi (hujataja muujiza kuhusu nini)

na sijakujibu kwa sababu umetishia kusilimu Bali kukuonyesha huo muujiza
Unaiamini sayansi kua ni nyenzo ya uhakika kwa kujua ukweli wa kitu?
 
Ndiyo unambie kuwa kuna ukweli kwamba " Kitabu cha Quran takatifu mtume alishushiwa moja kwa moja kutoka Mbinguni kikiwa na makaratasi yake " kuna ukweli katika hili ?
Maswali mengine ni kama ridiculous tu

Hivi hata katika fikra zako za uhalisia unaweza uka imagine na ukapima mwenyewe, toka nje kisha anagalia anga halafu anza ku imagine kua kuna kitabu kilishushwa kutoka juu

Unaweza ukaniambia ni kiasi gani umejiona ni mjinga

Sasa kwanini swala hili lionekane kawaida machoni mwa waumini wa hizi hadithi? Ni kwasababu ya hofu ya kuhoji waliyopandikizwa nayo ndio inayo run vichwani mwao
 
Ndiyo unambie kuwa kuna ukweli kwamba " Kitabu cha Quran takatifu mtume alishushiwa moja kwa moja kutoka Mbinguni kikiwa na makaratasi yake " kuna ukweli katika hili ?
Si kweli hakuna mahali kunaeleza jambo kama , kushuka kwa Quran si kwa maana ya kwa kuporomoka karati kutoka juu Bali ni ufunuo ambao alikuwa anashshiwa kutoka kwa Mungu kupitia jibril ..karatasi zilitumika kwenye uandishi ambao yy mtume alisomea huo ufuno nao wakawa wanaundika chini ya usimamizi wake
 
Si kweli hakuna mahali kunaeleza jambo kama , kushuka kwa Quran si kwa maana ya kwa kuporomoka karati kutoka juu Bali ni ufunuo ambao alikuwa anashshiwa kutoka kwa Mungu kupitia jibril ..karatasi zilitumika kwenye uandishi ambao yy mtume alisomea huo ufuno nao wakawa wanaundika chini ya usimamizi wake

Hapa nitakuelewa, maana kuna muislam mmoja aliwahi kunambia kuwa
"Wakristo Biblia yenu mmeandika wenyewe sisi Quran yetu ilishushwa toka mbinguni moja kwa moja"

Actually nili- wonder nikawa nasubirigi mtu mwenye busara za dini nimuulize
 
Na ule ujinga wa bibilia unao wazulia mitume ya mungu ujinga eti mara daudi alilala na mke wa mtu akapatikana king solomon, mara Noah alikaa uchi ufukweni akiwa analewa, mara king solomon akaabudia masanamu yaani ujinga ujinga
Msipende kuamini hizi dini za kuletewa na maboti, hazina mshiko wowote kwetu. Sisi Waafrika ndiyo wa kwanza kuumbwa na Mwenyezi Mungu hapa duniani, iweje Myahudi, Mzungu na Mwarab aje kutufundisha namna ya kusali wakati tuna njia zetu wenyewe za kusali?
 
Asili ya chuma in quran

“...Na tumeteremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu...” Qur’an 57:25


Kisayansi Chuma ni matokeo ya kupasuka pasuka kwa Nyota zilizoko angani, nyota ambazo ni kubwa sana kuliko Jua . Hali hiyo ya kutokea hayo mapande, yanayosababisha sisi wakazi wa dunia yetu kupata chuma,

yanatokea baada ya nyota hizo kufikia hali ya uzee (Nova stage) kipindi ambacho joto katika nyota hizo hufikia nyuzi joto zinazo kadiriwa kuwa zaidi ya nyuzi digirii 100m Wakati huo chuma kinakuwa kingi sana katika nyota hizo. Joto linapokithiri kwa kiwango hicho, nyota hizo zinashidwa kuvumilia na hapo ndipo zinapo pasuka mapande mapande,

mapande hayo ambayo hutawanyika huku na huko na kuelekea mielekeo tofauti tofauti. Na hapo basi mapande mengine ndio huelekea huku katika dunia yetu. Na yanapokaribia anga la dunia yetu baadhi yake huvutwa na nguvu ya mvutano (gravitation force), na hii ni baada ya kupungua sana kwa ukubwa wake, na ni nadra sana mapande haya kushuka kwa ukubwa wa kuonekana. Bali mengi yao huja kwa mfumo wa kama vumbi. Na kupitiliza hadi chini ya ardhi na huko ndiko ujiunda pamoja na kujitengeneza majabali.

Huu sio muijuza pekee kwenye quran Bali nimeleta huu kwasababu swali lako halipo wazi (hujataja muujiza kuhusu nini)

na sijakujibu kwa sababu umetishia kusilimu Bali kukuonyesha huo muujiza
hii miujiza sijui ina miujiza gani...Mara nyingi huwa haiwekewi aya yote...lazima aya ikatwekatwe.
ukiendelea kusoma aya apo Allah anasema alileta chuma ili watu wauane wapigane kwa ajili yake(ibn kathir)..si ushetani huu?.
ingekhii miujiza sijui ina miujiza gani...Mara nyingi huwa haiwekewi aya yote...lazima aya ikatwekatwe.
ukiendelea kusoma aya apo Allah anasema alileta chuma ili watu wauane wapigane kwa ajili yake(ibn kathir)..si ushetani huu?
na ukiangalia tafsirs kwanini izo aya zilikuja utagundua haihusiani kivyovyote na sayansi na hata muhammad mwenyewe hakuelewa wala hakuelezea kama nyie wanasayaIslam wa sikuhizi mnavyopindisha...pale ambapo actually muhamad na quran yake aliongelea sayansi explicitly(mfano issue ya jua kuzama kwenye dimbwi) lazima alikosea.

anyway turudi kwa mada
neno la kiarab 'anzalna' lililotumika hapo lina maana nyingi sio lazima hiyo kuteremshwa..sawa ni mojawapo ya maana yake lakini most credible tafsirs hawajatumia neno 'sent down' kwenye hio aya...wengi wametumia maneno kama provided,bestowed etc.
tukisema kila tunapoliona hilo neno basi tuapply logic yako basi madudu yatatokea.
your explanations actually create more problems for the quran than it solves.

mfano hata Qran 39:6
He created you (all) from a single person: then created, of like nature, his mate; and he sent down for you cattle…(Surah 39:6)

kwahyo according to the Qur’an na logic yako, Allah, aliyeteremsha chuma
(Surah 57:25), pia alimteremsha na ng'ombe(39:6)..

Au soma Surah 7:26
O children of Adam! We have sent down for you clothing to cover your nakedness

inamaana nguo nazo zinashushwa kutoka kwenye manyota?

Fthermore ata tukigrant ivo ndo alimaanisha, Wamisri na jamii nyingine nyingi tu zilijua na kuamini kuwa chuma nyingi duniani ilianguka kutoka kwenye vimondo karibia miaka 3000BCE...
sijui muujiza uko wapi apo

The quran is not a science book and most verses you are reaching for scientific arguments aren't even talking about science but you force them to be about science because [all] the verses that actually do talk about science got the facts wrong.
Tatzo mna'reach sana kucheza na reinterpretetions ili kufukuzana na sayansi.
Leta aya nyingine iliyo wazi...sio izo za kutaftia maana kwa tochi
 
Back
Top Bottom