Seneti ya Marekani yapitisha msaada wa trilioni 152 Ukraine, Trilioni 35 Israel, Trilioni 22 Palestina, Trilioni 12 Taiwan

Seneti ya Marekani yapitisha msaada wa trilioni 152 Ukraine, Trilioni 35 Israel, Trilioni 22 Palestina, Trilioni 12 Taiwan

Lend lease kwa Soviet Union ilikuwa ni msaada. Marekani ilitoa ndege za kivita zaidi ya 10,000 na vifaru zaidi ya 6,000 pamoja na mambo mengine kwa Urusi na haikuwa loan

Lend or lease. Marekani alikuwa anaweza kuchukua kitu chochote cha kutumia kwenye vita ile dhidi ya Nazi Germany ila sababu Urusi haikuwa na lolote la hadhi ya kuchukuliwa na Marekani, na Marekani ilijitosheleza ndio maana Urusi ikapokea tu kama Burundi inavyopokea misaada. Baadae mkataba ni wa kukodisha na kukodi, aya umekodisha ndege bure na umeziharibu au zimeharibiwa na adui, zilipe. Ndio hapo nchi zikailipa Marekani tena kwa riba ndogo sana, kwa msamaha wa deni na kwa kupewa miaka hata 40. Tabia za superpower hizo.

Taiwan ina privilege ya kuuziwa baadhi ya silaha za Marekani zisizowekwa open market. Sio kila mwenye hela anaenda US kumwaga mabilioni kununua silaha, kwa miaka kadhaa US iliblock Turkey kununua F-16 mpya mpaka mwaka huu, vilevile Turkey ilikataliwa kuuziwa Patriot ikaenda kununua S-400, Turkey hiyohiyo ilitolewa kwenye mradi wa F-35 ikarudishiwa hela. US hawauzi silaha kwa njaa.

Pia Taiwan inapewa misaada kama training ngumu ambazo sio kila nchi inapewa, na zina gharama kubwa. Inahesabika in monetary terms.
Americant haijahawahi kuisaidia Russia acha kupotosha watu
 
Ukraine itaendelea kupigwa kama ngoma maadam tu NATO wanaiogopa Russia basi Ukraine itapondwa pondwa sanaaaaaaaa
 
Marekani iliwahi saidia Urusi, China, Japan, South Korea, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Israel, etc.

Taiwan inahitaji msaada wa Marekani, na huwa inaomba kabisa.
Si wana fanya kuPrint tu!!!. Sasa hapo zinaenda kuprintiwa rundo la $ wanakwenda kuzigawa wenyewe wanaita misaada.
 
Aliyekuambia ya kwamba nchi ikiwa inadaiwa ndio inakosa bajeti ni nani?

Kumbuka wenzetu Sio kama wabongo yaani mtu akikukopa laki moja na akianza kukuona unanenepa,unakula na kuvaa vizuri na huna stress ni anamaind na kuanza kukudai hela yake kwa fujo sana,
Wenzetu kitu kilicho ndani ya bajeti na matumizi ya muhimu hua hawahesabu
Na hua hawachukui inahesabika hauna kitu mpaka upate akiba yaani imagine wadeni wa bongo wanachukuliwa hadi masufuria!
😁😁
Umenikumbusha jamaa yangu aliyepandishiwa kodi ya nyumba baada ya kununua gari😂😂. ....mwenye nyumba alisema tushirikishane maendeleo.
 
Swali la kijinga sana hili ni sawa na kuuliza unataka wafanye nini kwa mtu mwenye njaa? Obviously unakiwa umpe chakula ale
Watu wenye njaa Marekani hupewa chakula wale kupitia food stamps lakini bado hawajaona ni sahihi kuwapa watu nyumba za bure pamoja na maji na umeme vya bure. Kuna wanasiasa wengi Marekani wanopinga raia kupewa huduma au pesa za bure bila kufanya kazi.
 
Ni ajabu kabisa! Ni tabia mbaya ya ubinafsi na kujionesha tu mbele ya watu. Jitosheleze na kutunza kwanza nyumbani kwako kabla ya kuwasaidia wengine. Huo ndio umwamba unaofaa - kuijali familia yako kwanza.
Misaada ya kinchi huwa ni zaidi ya misaada, misaada ni sehemu ya soft power za nchi katika nyenzo za kidiplomasia. Ni uwekezaji wa muda mrefu sana.
 
Si wana fanya kuPrint tu!!!. Sasa hapo zinaenda kuprintiwa rundo la $ wanakwenda kuzigawa wenyewe wanaita misaada.
Taiwan haihitaji cash, inahitaji material things. Hapo sanasana ni silaha, nazo unaprint tu kama makaratasi?
 
Ingekuwa hizi pesa wanazo Irani au Talibani au Iraq au Afghanistan.


Zingetumika kuchinja wanaowaita Makafiri, kama wangegoma kusilimu na kuikubali inayoitwa Dini ya Haki.

Dola la Dini lingetawala Dunia kwa mabavu.

Asante Mungu uliyeumba Mbingu na Nchi kwa kuwapa uwezo wanaokujua.[emoji255]
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Americant haijahawahi kuisaidia Russia acha kupotosha watu
Bila Marekani kuhusika, Urusi yangekuwa mashamba ya Ujerumani na hao kina Putin wangekuwa manamba.
Lengo la Nazi Germany lilikuwa kuitumia USSR kama sehemu ya kuzalisha chakula na mafuta kwa uchache.
 
Jamaa ni hatari sana hawa wa Asia hata madikteta wao kuna namna unaona wanavyo waza ni tofauti pamoja ya kwamba kuna muda wanapata madikteta vichaa haswa.

Mfano ukiondoa ujinga ujinga wa kina familia ya kina Kim ila kuna kitu kidogo wanakosa nacho kujifungua kimataifa na kuanza kushirikiana na mataifa mbalimbali tena NK kwa level wakijifungua sidhani kama ishi ya viwanda itakuwa vikwazo kwao.

Licha ya kwamba jamaa wametengwa haswa ila wanajitahidi ukilinganisha hata na sisi ambao hatuja tengwa na yoyote

Nina hakika NK ametuacha sisi katika maeneo mengi sana pamoja na upuuzi puuzi wa familia ya Kim lakini Asians wapo smart s
Sisi Waafrika bado tunaelekea kuwa binadamu kamilifu, hili utaliona kwenye tabia zetu na ufanyaji wa maamuzi. Hata wakosefu wa Kiafrika na wa races nyingine wanatofautiana sana.

Gaidi la Uarabuni linatetea utamaduni wake, rasilimali zake, mali zake. Gaidi la Kiafrika linatetea mali zake kwenda kwa fulani badala ya kwa fulani (wote sio wazawa), kwa kutumia dini iliyoletwa kwa jahazi na majambia.
 
kwamba Urusi alisaidiwa kama Burundi tu ? wavaa kobaz wamekusikia kwel ?
Warusi walikuwa na jeshi la wakulima na wawindaji wengi hawana viatu wala uniforms. Alafu jeshi linaongozwa na makamisaa wa chama (machawa), hawajui lolote kuhusu jeshi ukitaka kuretreat kujipanga upya wanaona unatoroka wanakuchapa risasi.
Wakati upande mwingine Ujerumani walikuwa na professional military hadi uniforms wanatengenezewa na designer Hugo Boss, brand ya Boss hadi leo ni levels za kina Louis Vuitton.

Soviet Union walikuwa na enormous land alafu wanatembea kwa treni, kama hamna reli wanachapa mguu. Marekani kupitia kampuni yake ya General Motors ikawapa malori 150,000 ya kivita.

Hawakuwa na ndege za mizigo wakati wana ardhi kubwa sana kufikiwa kwa haraka. Marekani ikawapa ndegevita zaidi ya 14,000 hasa bombers na airlifters. Warusi kipindi hicho wana ndege zina parts zenye mbao ikipigwa risasi na ndege za Mjerumani kwenye dogfight inasambaratika. Walikuwa wana very limited resources kufanya mass production ya kila kitu. Marekani hadi mafuta iliwapa, hata vyakula, hata nguo.

Yani walikuwa njaa kali watoto wadogo hao. Unadhani Ujerumani ingewavamia kama wangekuwa wanajiweza. Alafu baadae wanajikuta wajuaji wakabanwa kwenye bei ya mafuta wakagawana mbao. Leo wanapigana waliokuwa muungano.
 
Haters wa magharibi wanachekesha kwelikweli, marekani na washirika wake wasipotoa msaada hasa kwa ukraine utasikia wanasema wameshamchoka na kumtelekeza zelensiky..,acha watoe msaada Sasa, utasikia mara ooh [emoji44] [emoji44] si wanaprint tu pesa wale? [emoji28]

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Marekani utafikiri wanafyatua pesa kwa kutumia Press Machine na kisha kugawa, hata waarabu wanaosemwa kwamba wana hela lakini ni bahiri kama mpare huwezi kuona hela yake.

NB: Hakuna nchi isiyo na deni duniani kila nchi inadaiwa ila viwango ndio tofauti.
Mnufaka mkubwa WA hizo pesa ni military industry ya marekani.
Hata hivyo kwa yeye Dola ni yake Wala Hilo deni halimsbui ni issue ya kuprint na kulipa tu.
 
Back
Top Bottom