Senzo aomba kutokuongezewa mkataba wake na Yanga, Akubaliwa ombi lake

Protect

Senior Member
Joined
Apr 4, 2020
Posts
103
Reaction score
362

Afisa Mtendaji Mkuu wa Yanga, Bw Senzo Mazingiza ameomba kutokuongezewa mkataba wake na Yanga kwa sababu za kifamilia

Kutokana na ombi hilo kamati ya utendaji ya Yanga ilikutana leo katika Hotel ya Serena na kukubali ombi hilo la Bw Senzo

Mkataba wa Senzo na Yanga unamalizika tarehe 31/07/2022

Yanga yamteua Wakili Simon Patrick kuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Mpito
 
Hii tarehe tu ni ya wapi
 
Ametutoa mbali sana.

Leo hii tusingefikia "Mabadiliko kamili ya uendeshaji wa klabu bila yeye"

Amekuja amekuta klabu ikiwa na mapato ya mwaka Bil 1.8.

Anaondoka akiwaacha wanajangwani wakiwa na vyanzo vya mapato vya mwaka vyenye thamani ya Bil 9.9
 
Afisa Mtendaji mkuu wa Yanga Senzo amewasikisha ombi la kutokuendekea na kazi baada ya mkataba wake kuosha. 31/7/2022
 
😝😝😝 byuti byuti maji yanaanza kujitenga na mafuta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…