Uchaguzi 2020 Sera ya majimbo itaua utaifa na uzalendo

Uchaguzi 2020 Sera ya majimbo itaua utaifa na uzalendo

Ulinganisho wa ukubwa sio issue, Logic inabakia pale pale kuwa, nchi inagawanywa katika kanda zenye mifumo ya kujitawala ndani kwa ndani ili kurahisha maendeleo ya watu badala ya kuwa na mtawala mmoja (Rais) mwenye kuamua hadi choo cha kijiji kijengwe wapi na lini.
Issue sio kujitawala ni mapato yao wana ya kutosha mfano kagera uchumi unategemea kilimo cha ndizi hasa sasa mikungu mingapi uuze upate pesa ya kujenga barabara? Kilomita moja tu pesa zaidi ya shilingi bilioini moja hapo mikungu mingapi?

Chadema hii sera itaumiza mikoa mingi mno kuwarudisha chini kwenye umaskini wa kufa mtu

Issue sio maamuzi bali ni kwa pesa ipi uliyonayo ya kwako ya source ya eneo lako?

Hiyo ya kuuza ndizi?
 
Vipi unafikiri sera ya nchi katika Afrika Mashariki inaua uafrika mashariki,

Je sera ya nchi Afrika, inaua uafrika,

Je sera ya vijiji inaua uzalendo kikata?

Je, sera ya mikoa nayo inaua utaifa?

Je sera ya kuwa na wilaya, inaua uazlendo kimkoa?

Tumia akili, acha propaganda.
Nimesikia chama kimoja kinazungumzia nchi kuigawa kwenye majimbo ya kiutawala na uendeshaji. Kwangu mimi kwa nchi ambayo imekuwa kwenye utawala wa mikoa kwa miaka zaidi ya 50 na kwa mfumo wa kugawana mapato kupitia serikali kuu na serikali za mitaa kwa baadhi ya mapato haileti mantiki kubadili mfumo kwenda kwenye majimbo ambayo yanaweza kuua utaifa na kuleta mfarakano. Mfumo wa sasa unaondoa u-mimi na maendeleo ya uchumi yanayopishana- Regional economic imbalances - ambao utaacha baadhi ya maeneo kwenye umasikini mkubwa. Baadhi ya athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na:

1. Maeneo yenye raslimali kidogo kuendelea kuwa maskini na maeneo mengine kuwa tajiri na hivyo kuwa na mchango mdogo wa GDP

2. Ajira ndogo kwenye baadhi ya maeneo yenye raslimali chache na hivyo ongezeko la idadi ya watu kwenye maeneo yenye utajiri wa raslimali

3. kila jimbo kuwa na sheria zake za kiutawala, bunge dogo, polisi nk hali inayoweza kujenga mwelekeo wa kujitenga. Rejea matatizo yakujitenga kwa Biafra Nigeria miaka ya nyuma.

4. Nchi zenye majimbo mf Msumbiji hazina hakikisho la maendeleo endelevu kuzidi ambazo hazina utaratibu huo ie Tanzania

5. Mfumo huo utakuwa na gharama kubwa kuuanzisha

Kimsingi hadi sasa mfumo uliopo hauna shida changamoto kubwa ni kuweka mifumo mizuri ya udhibiti matumizi na mapato ya serikali kwa kuyagawa kwa haki ili kila eneo la serikali liweze kunufaika. Na hususani kuimarisha mfumo wa Halmashauri uweze kukabiliana na changamoto za kiuchumi kwa kila eneo. Iwapo kuna changamoto za mgawanyo sawia basi tupitie upya sera na sheria zetu ndani ya mfumo uliopo tuboreshe.

6. Hata hivyo, Kwa maoni yangu badala ya utawala wa majimbo ni afadhali kuweka kanda za kiuzalishaji ili kuchochea uchumi wa kimaeneo kulingana na mazingira ya kiuchumi na uzalishaji kwa kila eneo.
 
The objective of AU is to defend territorial integrity, kama hujui territorial integrity ni nini, nenda google wameidadavua. Hakuna mtu anayeweza kugawa mipaka ya nchi kirahisi rahisi na dunia ikanyamaza never, sera ya majimbo ni kurahisisha tu na namna ya utawala yaani kwa kifupi ni kugawa majukumu so msitumie nguvu kubwa kupiga proganda ya kipuuzi eti majimbo yatagawa nchi
Eritrea ilijitenga kutoka Ethiopia sijui kama unakumbuka hilo na sasa ni mwanachama wa AU. Pia kuna Simaliland na Putland zimejimegua toka Somalia huku hiyo AU ikiangalia. Morocco iliivamia Sahara Magharibi kinyume na mkataba wa OAU wakati huo ambao ulikuwa na clause inasema nchi za Africa haziruhusiwi kubadili mipaka iliyowekwa na wakoloni kwa kutumia nguvu. Ndugu yangu ukipenda masuala haya take time kusoma.
 
Kuna majimbo yatakuwa maskini hasa kuna yale wategemea alizeti kama Singida kuna yale wategemea mbao mahindi na maharage kama mkoa wa njombe na Iringa na Ruvuma nk. Pesa hizo haziwezi jenga barabara wala miradi mikubwa lazima watoe kwingine

Kigoma na mawese yatawapeleka wapi watakuwa na umaskini wa kufa mtu



Swala sio tu kujiamulia kwa pesa ipi?

Nenda hata marekani uone majimbo yalivyo kuna yenye umaskini wa kufa mtu hata ukitoka Tanzania ukiambiwa kaishi kule bure utagoma
Hawa wanaokuja na sera za majimbo ndio hao wanaowakejeli watu wa Dodoma kuwa ni maskini mpaka wanakula wadudu.

Ndio hao wanaosema uwanja wa ndege Chato hautakuwa na faida baada ya rais kuondoka ikulu.

Halafu wanataka majimbo hayo yasiyokuwa na chochote yajitegemee!!.

Ni sera ambayo imejificha kwenye moyo wa uchoyo. Watanzania tunategemeana na tumekuzwa katika misingi ya kutegemeana hatuwezi kukwepa kuwa kitu kimoja.
 
Kwako utaifa ni wananchi kuwa mafukara na ombaomba wa magufuli?

Huo ndio utaifa kwa mujibu wa ilani ya CCM?
Mafukara na ombaomba wapo nchi hii kabla wazazi wetu hawajazaliwa na tutakufa tutawaacha, hakuna mfumo wa maisha utakaomaliza umaskini wa binadamu.
 
Wewe ulitaka tulinganishe na nini??? Endeleeni kupiga kelele tunajua kisu cha Lissu kimegusa mfupa. Ndo mwisho wenu kutapanya hela za kodi za watanzania mtakavyo
Lissu mwepesi tu kwa wenye kuielewa dunia. Kwenu labda ndio anaonekana superstar.
 
We jamaa huna unachokifahamu unabisha kitu usichokielewa UN kuisapoti AU kibajeti haimanishi AU haiwezi kutekeleza kazi zake, so unataka kuniambia kundi la kagame linalotaka kuimega kongo, ni wanajeshi wa kizungu ndo walikuja kupambana na waasi wa kitusi?
Nimeanza kufuatilia haya mambo ya siasa kabla hujazaliwa.
Nimekuuliza wale wanajeshi wa Tanzania waliokwenda Kongo walienda kwa mandate ipi ya UN au AU? Pili nani alitoa vifaa na kugharimia uwepi wao kule Kongo ni AU au UN?

OAU na sasa AU haijawahi kutatua mgogoro wowote zaidi ya maneno matupu. Kila mgogoro wa bara hili uluowahi kutatuliwa ni UN ndio walihusika tena kwa kusaidiwa na nchi za magharibi.
 
tanzania hii hakuna mkoa ambao ni masikini wa rasilimali
kila mkoa una rasilimali ambazo kama zikitumika ipasavyo basi kila maendeleo yatakuja katika mkoa husika
 
Mfano mzuri wa maendeleo katika majimbo ni kama hivi; ichukue Rwanda au Burundi irudi Tanzania then baada ya miaka 10 iangalie maendeleo yake, Rwanda au Burundi zingekuwa upande wa Tz toka uhuru zingekuwa zinafanana na Kagera au Singida, je kwa sasa Rwanda na Burundi kimaendeleo unaweza kuzilinganisha na hiyo mikoa niliyoitaja?
 
Mitanzania tu kulipa kodi hamtaki hayo maendeleo hao mnaowasadiki/kuwapenda waume zenu hao wagombea urais wote/chama chochote ndo watawaltea pesa mifukoni? Fanyeni kaz kwa bidii mtaji ikowa jamii yako unatusua....mnapenda bata kuliko kazi
 
......
FB_IMG_1600761592882.jpg
 
Eritrea ilijitenga kutoka Ethiopia sijui kama unakumbuka hilo na sasa ni mwanachama wa AU. Pia kuna Simaliland na Putland zimejimegua toka Somalia huku hiyo AU ikiangalia. Morocco iliivamia Sahara Magharibi kinyume na mkataba wa OAU wakati huo ambao ulikuwa na clause inasema nchi za Africa haziruhusiwi kubadili mipaka iliyowekwa na wakoloni kwa kutumia nguvu. Ndugu yangu ukipenda masuala haya take time kusoma.
Kazi ya AU na UN ni kulinda territory za nchi wanachama, kesi ya eritrea ni kwamba AU na UN zilisimama na Eritrea ili liwe taifa make Ethiopia ni mvamizi alilazimisha muungano, hata zanzibar ikitaka kuvunja muungano, AU na UN hawatakuwa na pingamizi coz since day one tanganyika na zanzibar zilikuwa separated territories. Kuhusu kesi ya somalia nadhani kila mtu na ulimwengu unatambua somalia ni failed states kila jimbo linaibuka na kujitangazia uhuru, lkn pamoja na hayo somalilanda na puntland AU na UN haizitambui hizi nchi
 
Ukiangalia kwa makini utaona CCM ndio inatengeneza mazingira ya watu kutaka majimbo.

Rais anasema kama huchagui chama chake hakuna maendeleo. Kuna maana gani kwa wakazi wa Mbeya Mjini kulipa kodi zoooote na wasipate maendeleo badala yake zipelekwe kwa wanaompenda Rais na chama chake?

..kwa majibu haya, ungekuwa karibu yangu ningekununulia kinywaji baridi, nusu kuku, na chipsi.
 
Nimesikia chama kimoja kinazungumzia nchi kuigawa kwenye majimbo ya kiutawala na uendeshaji. Kwangu mimi kwa nchi ambayo imekuwa kwenye utawala wa mikoa kwa miaka zaidi ya 50 na kwa mfumo wa kugawana mapato kupitia serikali kuu na serikali za mitaa kwa baadhi ya mapato haileti mantiki kubadili mfumo kwenda kwenye majimbo ambayo yanaweza kuua utaifa na kuleta mfarakano. Mfumo wa sasa unaondoa u-mimi na maendeleo ya uchumi yanayopishana- Regional economic imbalances - ambao utaacha baadhi ya maeneo kwenye umasikini mkubwa. Baadhi ya athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na:

1. Maeneo yenye raslimali kidogo kuendelea kuwa maskini na maeneo mengine kuwa tajiri na hivyo kuwa na mchango mdogo wa GDP

2. Ajira ndogo kwenye baadhi ya maeneo yenye raslimali chache na hivyo ongezeko la idadi ya watu kwenye maeneo yenye utajiri wa raslimali

3. kila jimbo kuwa na sheria zake za kiutawala, bunge dogo, polisi nk hali inayoweza kujenga mwelekeo wa kujitenga. Rejea matatizo yakujitenga kwa Biafra Nigeria miaka ya nyuma.

4. Nchi zenye majimbo mf Msumbiji hazina hakikisho la maendeleo endelevu kuzidi ambazo hazina utaratibu huo ie Tanzania

5. Mfumo huo utakuwa na gharama kubwa kuuanzisha

Kimsingi hadi sasa mfumo uliopo hauna shida changamoto kubwa ni kuweka mifumo mizuri ya udhibiti matumizi na mapato ya serikali kwa kuyagawa kwa haki ili kila eneo la serikali liweze kunufaika. Na hususani kuimarisha mfumo wa Halmashauri uweze kukabiliana na changamoto za kiuchumi kwa kila eneo. Iwapo kuna changamoto za mgawanyo sawia basi tupitie upya sera na sheria zetu ndani ya mfumo uliopo tuboreshe.

6. Hata hivyo, Kwa maoni yangu badala ya utawala wa majimbo ni afadhali kuweka kanda za kiuzalishaji ili kuchochea uchumi wa kimaeneo kulingana na mazingira ya kiuchumi na uzalishaji kwa kila eneo.
Sidhani kama kila jimbo litakuwa na askari wake watakufafanulia lakini
 
Nimeanza kufuatilia haya mambo ya siasa kabla hujazaliwa.
Nimekuuliza wale wanajeshi wa Tanzania waliokwenda Kongo walienda kwa mandate ipi ya UN au AU? Pili nani alitoa vifaa na kugharimia uwepi wao kule Kongo ni AU au UN?

OAU na sasa AU haijawahi kutatua mgogoro wowote zaidi ya maneno matupu. Kila mgogoro wa bara hili uluowahi kutatuliwa ni UN ndio walihusika tena kwa kusaidiwa na nchi za magharibi.
Objectives za AU na UN almost the same, AU for Africa na UN for world, so if UN is for world manake AU ipo ndani ya UN, wachama wa AU ni wachama wa UN so suala la kongo UN iliamua kulisimamia AU ingiwezaje kujitenga na UN?
 
Kazi ya AU na UN ni kulinda territory za nchi wanachama, kesi ya eritrea ni kwamba AU na UN zilisimama na Eritrea ili liwe taifa make Ethiopia ni mvamizi alilazimisha muungano, hata zanzibar ikitaka kuvunja muungano, AU na UN hawatakuwa na pingamizi coz since day one tanganyika na zanzibar zilikuwa separated territories. Kuhusu kesi ya somalia nadhani kila mtu na ulimwengu unatambua somalia ni failed states kila jimbo linaibuka na kujitangazia uhuru, lkn pamoja na hayo somalilanda na puntland AU na UN haizitambui hizi nchi
Hufahamu historia vizuri, unakumbuka Mwalimu Nyerere aliwahi kuwa msuluhishi wa huo mgogoro ikashindikana? Eritrea walifanikiwa kimapambano wakateka eneo lao lote na wakajitangazia uhuru.. OAU ililazimika kuitambua Eritrea; Ethiopia hawakuivamia Eritrea ila Eritrea ikiwa sehemu ya Ethiopia iliwahi kutawaliwa na Italy hivyo walivyoondoka ndipo Mfalme Haileselassie akunganisha. Ni kama case ya Caameroun ile iliyotawaliwa na wafaransa na ile iliyotawaliwa na waingereza lakini zote ziliunganishwa kuwa nchi moja wakati wa uhuru.
 
Hivi mfumo wa Majimbo wa Kanisa Katoliki, Lutherani (kule unaitwa Dayosisi), Moravian, SDA, TAG nk. nao huwa unaua uzalendo wa kiimani miongoni mwa wakristo?

..hata benki kuu imegawanywa kikanda/kimajimbo.

..tra nao wamegawanywa kikanda/kimajimbo.

..wakati wa muingereza kulikuwa na majimbo, lakini Watanganyika tulikuwa wazalendo, na tulikuwa na umoja, tukaweza kudai uhuru.
 
Back
Top Bottom