DOKEZO Serikali chukueni hatua za haraka dhidi ya Nabii Dominiki "Kiboko ya Wachawi"

DOKEZO Serikali chukueni hatua za haraka dhidi ya Nabii Dominiki "Kiboko ya Wachawi"

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kushughulikia wachawi kama ni wachawi kweli binafsi sinaneno.

Tena awashughulikie hasa. Lakini kuchomoa watu Hela ndio naona si Sawa .

Halafu atakuwa na pepo la utambuzi anajua mwenye Hela na asokuwa nayo.
 
Huyu jamaa kama hatumii nguvu za giza basi atakua mchawi. Si kwa nyomi lile analoingiza. Ajabu yuko machokoloni lakini anajaza uwanja full haus.


Ni kweli.
Maana anaweza kutambua mwenye Hela na asokuwa nazo.
Yaani ukifika pale kwanza wale wakongo wenzio ni wa jeuri jeuri tu.
Very aggressive utasema hauko mazingira ya kanisani.

Wanataka waogopwe.
Ukishanidai Hela maana yake nakuwa mteja wako , kama ni mteja Kwanini unifokee, Kwanini unidumie kama hisani?!

Kuna jamaa aliwazingua kinoma!
 
Kuna masai alienda kuombewa ndugu wakachanga watu wenyewe wamechoka maskini ya Mungu!

Wakatoa Hela kwenda kumuona akasema wakaongeze Hela na hapo Hela ya awali walishampa,

Huduma hawa kupata akawaambia wakalete Hela nyingine waje amponye,

Masai wakasema Hawana akawafokea tokeni nje kama hamna Hela .

Huruma imagine Hela ya awali imeenda bure bila huduma yoyote na kufukuzwa .
 
Kuna masai alienda kuombewa ndugu wakachanga watu wenyewe wamechoka maskini ya Mungu!
Wakatoa Hela kwenda kumuona akasema wakaongeze Hela na hapo Hela ya awali walishampa,
Huduma hawa kupata akawaambia wakalete Hela nyingine waje amponye,
Masai wakasema Hawana akawafokea tokenu nje kama hamna Hela .
Huruma imagine Hela ya awali imeenda bure bila huduma yoyote na kufukuzwa .


Nazani ndio maana anadharau sababu watu wanaendelea kupigwa na hawastuki na vyombo vya doła vyenye dhamana ambavyo tuna ani viko kazini 24/7 lakini havistukii wananchi kuibiwa kwa njia ya ulaghai?
 
Nawasalimu wote kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania​

Utangulizi
Mimi ni raia wa Tanzania, Mkristo kwa imani. Lakini nasikitishwa na kile kinachoendelea katika huduma ya Nabii wa Uongo anayejiita “Nabii Dominiki, Kiboko ya Wachawi”, mwenye Huduma yake DSM, WILAYA YA TEMEKE, BUZA – MTAA WA LULENGE. Kwa bahati mbaya Serikali ya Tanzania imekuwa kimya, bila kuchukua hatua zozote dhidi ya huduma hii potofu. Je, serikali inasubiri yatokee maafa kama ya Kibwetere (Uganda) au Mchungaji Makenzie (Kenya) ndipo ishtuke? Kwa uchache tutaorodhesha yale yahusuyo huduma hii potofu (CULT):

B. Upotofu wa Huudma ya Nabii Dominiki

- Matangazo ya Uongo Redioni

Nabii Dominiki amerubuni kituo kimoja cha redio hapa Dar es Salaam kinachorusha SHUHUDA ZA UONGO, muda wa Usiku na kupotosha kuwa zipo familia zinatuhumiana kwa mambo ya uchawi (Kinyume na Maadili ya Watanzania). Redio hiyo hurusha Vipindi na kujifanya wanawahoji mashuhuda LIVE, na kumbe siyo kweli. Kupitia njia hii, mtu huyu anazidi kujijengea umaarufu na kupata watu wengi (waislamu kwa Wakristo) wenye shida za kuuguliwa au kufiwa na ndugu zao kwa matarajio kuwa watarudishiwa AFYA / UHAI pindi wakikutana na huyu Nabii feki, lakini kumbe siyo kweli.

- Wizi Ulio Wazi wa Ada za Viingilio
Katika eneo analofanyia hii huduma (Buza kwa Lulenge), ameweka raia wenzake wa nchi jirani ya DR-Congo kukusanya pesa za viingilio vya kumuona. Hadi mwezi Januari 2024, kiingilio cha kuonana naye ofisini kilikuwa Tsh. 200,000/- (Laki mbili) bila RISITI wala kuandikishwa majina yako kuonesha malipo uliyotoa. Changamoto ni kuwa, endapo nabii atachelewa kuja ofisini, au ukipatwa na dharura, pesa hii huwezi kuidai. Kwa sasa (Aprili 2024) zipo fununu kuwa kiwango cha Ada ya Kiingilio kimeongezeka zaidi ya Tsh. laki mbili (>200,000/=).

- Masharti magumu baada ya Kumuona Ofisini kwake
Kwa wale wanaopata fursa ya kuonana naye uso kwa uso, ni lazima uandikishe JINA lako, na KAZI unayofanya. Lengo kuu ni kutaka kulinganisha UWEZO wako wa kutimiza masharti ya pesa utakayotajiwa pindi ukiingia ndani kukutana naye.

- Mafundisho ya Imani Potofu (Cultism) – Kinyume na Mafundisho ya Ukristo
Imani ya Ukristo inayohubiriwa mahali hapa ni tofauti na mafundisho mama ya Biblia,inayosema kama ni kipawa chochote kile cha miujiza, “mmepewa bure na hivyo toeni bure” (Mathayo 10:8). Kwa huyu Nabii endapo utaingia Ofisini kwake kumuona na kwa shida yako, atahakikisha ili kutatua shida yako anakupa sharti gumu ikiwemo Kiwango cha Pesa kinachoendana na kazi au biashara unayofanya.

C. Nini Kifanyike?
Pesa inayokusanywa mahali hapa BUZA - MTAA WA LULENGE ni nyingi na wizi wa wazi. Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) na TAKUKURU chukueni hatua, kufanya upelelezi wenu na kuwasweka ndani hawa Manabii Wahuni. Hii ni filimbi ya kuiamsha serikali (WHISTLE BLOWER), na Andiko hili litabaki kama kumbukumbu na ushahidi kwamba Vyombo vya Serikali vilitahadharishwa kabla kwa lengo zuri tu la kuchukua hatua stahiki.

=====

Pia soma:
Hakuna utapeli hapo ,umejipeleka mwenyewe ukishindwa acha
 
Nabii anajichubua balaa. Jana nilikuwa saluni natengeneza kucha watu wanabishana kuhusu huyu tapeli wa dini yaan nikawaambia mwenyewe anajichubua wakaniwakia balaa eti tayari anajua ulichomsema😂😂...Tanzania nchi yangu wajinga ndio waliwao.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Lengo la huh Uzi ni nini..!?

Ni Nabii kutumia Matangazo unayoyaita Fake Radioni ama..!?

Ni kitendo cha Kuwalipisha kiwango kikubwa cha pesa watu wanaoenda kuonana nae face to face...!?

Ama malalamiko yako yanamaanisha kwamba Ni Nabii Taperi asiye na ukweli wowote.....!?

Binafsi sikubaliani na namna yeye anavyowalipisha Watu pesa ili kumuona, Angetumia Ubunifu kama wa Mwamposa, pale anapowataka watu kuchangia kusambaza Injili, kwa sababu kuna gharama kubwa kurusha Matangazo iwe TV ama Radio...!

Aisifuye Mvua imemnyea, yakikukuta wewe mwenyewe utajua Manabii wote wanapatikana wapi.....!

Kile watu wasichojua Kuna mstari mdogo sana kati ya Nabii na Mganga wa Kienyeji, Mganga wa Kienyeji mpiga Ramli akiamua kuokoka akitaka kumtumikia Mungu, anakua Nabii straight, utofauti ni kwamba akiwa Mganga alikua anafanya kazi kwa Usaidizi wa Mizimu na Majini, na sasa ni Nabii anafanya kazi kwa usaidizi wa Roho Mtakatifu.

Kuna Matatizo ya Watu yanawahitaji Manabii moja kwa moja, kumsaidia mtu atoke shimoni then uanze kumfundisha kuomba, kufunga n.k....!

Mtu ana matatizo lukuki, ni Mgonjwa, hatembei, Macho hayaoni kwa sababu ya Husda za Wanadamu,hafu unamwambia asome Biblia, afunge, akemee, anaanzia wapi.... Unahitaji Nabii atayekwambia tatizo lako na kutatua then akufundishe kumtegemea Mungu.
Siyo kila anayejiita nabii na anahubiri jina la Yesu ni mkristo. Ukristo una principles zake. Ndiyo maana Yesu alisema siku ya mwisho kuna watu atawakataa lakini watamjibu walifanya miujiza kwa jina lake lakini ajibu SIWAJUI. Miujiza SI KIGEZO CHA UKRISTO au kwamba mtu ameitwa/ametumwa na MUNGU
Aisifuye Mvua imemnyea Mkuu, mimi ni Mhanga wa Matatizo ya Kiroho, na hao Manabii ndo walinisaidia.....!!

Watu wote wanaojaa kwenye hayo Makanisa, sio Wajinga, yamewafika.....! Ndo maana Bulkdozer huwa anasema Makanisani ni "Mtakuja" yatakapokufika wewe mwenyewe utaongoza njia...! Ama ndugu zako watakubeba kukupeleka ukiwa hujiwezi.
Sawa. Hayo ndiyo Yesu aliyoyaita KIZAZI CHA ZINAA. Kizazi cha kutafuta miujiza. No matter who performs the miracles in no matter who's power basi wataifuata hiyo miujiza huko. Hata kama inatendeka kwa nguvu za shetani comouflaged in the name of Jesus, poteleambali. A really bad generation!
 
Huduma zote za kinabii ,kichungaji ,kikanisa kiutume na kiroho nikilainishi cha serikali ili kuwatiisha chini ya mamlaka ,serikali haiwezi chukua hatua mpaka nabii aanze kuua kondooo ,kiunafki serikali itamshika shika kufunika kombe mwanaharamu apite.
 
wacha afanye mambo ata kama ni uongo,mtaani tunaumizana sana,wakati mwingine mikwala ni muhimu sana!!!
 
Wewe umeona kosa kwake, ila Serikali haijaona kosa kwake, usidhani kwamba hayo uyasemayo Serikali haijui, inajua, kama kuna uvunjifu wa sheria ama la, na ipo makini kuliko unavyofikiri na kama kuna kosa itachukua hatua dhidi yake, muhimu utoe ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama uhitajikapo kama kweli una nia njema.
 
Wewe ni suguye ,Mwamposa au malisa au Musa naona amewazidi ,jamaa anaouwezo Mkubwa sana yule sio level zenu

Nitajie nabii ambapo kuniona ni bure


USSR
 
Wewe umeona kosa kwake, ila Serikali haijaona kosa kwake, usidhani kwamba hayo uyasemayo Serikali haijui, inajua, kama kuna uvunjifu wa sheria ama la, na ipo makini kuliko unavyofikiri na kama kuna kosa itachukua hatua dhidi yake, muhimu utoe ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama uhitajikapo kama kweli una nia njema.
Hakuna alicho andika cha kweli kwani wananyang'anywa watu wanapona wewe unaleta siasa


USSR
 
Wajinga ndio waliwao

Lakini hii inaonesha wazi jinsi watu walivyo na shida pamoja na kukosa tumaini, lakini ukiwaambia mwende katika makanisa ambayo yanafuata misingi ya Kristo wanatafuta shortcut

Waache wale jeuri yao
Hayo makanisa mafuata misingi ya Kristo yatoe solution basi kwa matatizo yao basi

Wao ndio tatizo la kusababisha waumini wazurure

Sidhani kama kanisa lina majibu na matatizo yao hawawezi zurura kutafuta solution hata kwenye imani potofu watatulia

Mwenye shida hana dini atasaka ufumbuzi kokote atakapoona kuna msaada
 
Back
Top Bottom