Mzalendo Uchwara
JF-Expert Member
- Jan 26, 2020
- 4,437
- 13,836
- Thread starter
-
- #21
Uzuri JPM alikuwa hawezi kukaa nalo moyoni. Alituambia ukweli, gesi tusahau, tumeshapigwa. Wahuni wanataka kuuza mpaka bandari.alishasema magufuli gesi sio yetu ipo siku atakuja rais mwingine na kusema bandari sio yetu wahuni hawa tunaishi nao humu humu
Mnoo na tatizo lililopo ni mfumo!!Nchi masikini lakini viongozi wake wanapenda anasa.
Anasema gesi ya wapi ??😅😅Amka usingizini ndugu😂
Bila hata ya aibu anasema "Gesi yetu"😆😆Anasema gesi ya wapi ??😅😅
Ziara za viongozi wote ni zile zile na zina uzito uleule wa kiitifaki lakini tofauti zinaweza kuonekana kutokana na ukubwa wa Taifa husika. Kwa hiyo unataka Rais wa Tanzania afanye ziara yenye malengo Yale Yale na Rais wa Marekani? Unapozungumzia tija kwenye ziara ya Rais wa Tz usiangalie tija inayopatikana na Rais wa Marekani. Ziara zina tija kubwa sana na faida ni nyingi, kwanza nchi inafunguka na bidhaa za Tanzania zinatambuliwa kimataifa. Kwa mfano Rais anapoenda kwenye maonesho makubwa ya kimataifa, anaenda na watu ambao watatangaza utamaduni wetu na hivyo kufanya hata vinyago vya mmakonde kupata soko la kimataifa.1. Kuna tofauti kubwa kati ya safari ya Biden nje ya nchi yake na safari ya rais wetu. USA anamaslahi mengi nje ya nchi, wana makampuni makubwa yanayaiingizia Marekani mabilioni ya fedha yanayofanya operations zake nje ya Marekani.
Safari zetu sisi ni kwenda kuvutia wawekezaji, kwenda kuomba misaada na mikopo. Matunda ya safari za SSH ndio hayo mauzauza ya DPW na madeni makubwa. Hazina tija!
2. Bwawa la umeme na reli havijengwi kwa mwaka mmoja. Hizo gharama ulizozitaja ni makadirio ya mradi wote ambao utachukua karibu miaka 10. Kwakuwa inajengwa na wakandarasi wa nje ni kweli kwamba lazima tutalipa kiasi fulani kwa fedha za kigeni. Lakini tunaweza kuhakikisha materials zote zinazopatika ndani basi zinanunuliwa ndani ( vitu vingi tu kwenye hiyo miradi vinatoka nje wakati tunavyo viwanda vya ndani vyenye uwezo wa kuzalisha), pamoja na subcontractors wote wa ndani wenye uwezo kufanya baadhi ya kazi wanapewa kipaumbele.
Lakini pia, miradi niliyokuwa nimeilenga zaidi ni ya barabara na majengo ya serikali. Hayo tunao wakandarasi wenye uwezo wa kujenga mingi ya miradi hiyo. Wapewe kipaumbele.
Hoja ya kukopa ili kuharakisha maendeleo haina maana kama mikopo hiyo inageuka kuwa mzigo kwenye uchumi wa nchi.
Hoja ya wizara ya fedha kuwekwa chini ya Dr. Mpango ni jambo la kutumia rasilmali ukizonazo kwa wakati huo. Rais angeweza hata kumwondoa Mwigulu na kumweka mtu mwingine pale, lakini itakuwa ni kama kufanya majaribio. Hiki ni kipindi cha mpito, serikali inaye mtaalamu wa uchumi ambaye amethibishwa kwa vitendo uwezo wake mkubwa wa kusimamia uchumi wa nchi, naye ni makamu wa rais. Kushindwa kumtumia kuzisimamia hizo wizara ni kushindwa kutumia rasilmali ulizonazo kutatua matatizo.
Naongezea1. Serikali isitishe kwa muda matumizi yasiyo ya lazima (anasa) yanayohitaji fedha za kigeni kama vile kununua magari ya kutembelea viongozi na safari za nje ya nchi (zote mpaka za SSH hazina tija).
2. Kampuni za ndani zitakazolipwa kwa shilingi zipewe kipaumbele kwenye miradi ya ujenzi na uwekezaji mwingine.
3. Serikali isitishe kukopa mikopo ya nje. Kwasasa mapato yetu ya fedha za kigeni mengi yanaishia kuhudumia madeni ya nje yaliyokopwa kwa pupa na serikali hii ya SSH kwa ushauri mbovu wa Mwigulu. Serikali isiongeze mzigo mwingine. Ikope ndani kwa kuuza bondi na njia nyinginezo.
4. Wizara ya fedha na wizara ya mipango ziwekwe chini ya ofisi ya makamu wa rais. Ni wazi kuwa hizo wizara mbili wameshindwa kujisimamia, na mamlaka kuu haina ujuzi wala uwezo wa kuzisimamia. Ni vema kazi hiyo apewe Dr. Mpango kwa wizara hizo kuwekwa chini yake rasmi.
5. Tunakaribia kutumbukia kwenye mgogoro mkubwa wa kiuchumi, majibu ya kisiasa na shortcuts haziwezi kusaidia. Siasa maji taka za kutoa "ufafanuzi" na matamko ya kijingajinga hayatatufikisha popote. Na wala kuvutia uwekezaji wa nje kwa njia za kihuni na rushwa hauwezi kutufikisha popote zaidi ya kutengeneza matatizo mengine.
Hauwezi kuuficha mdororo wa kiuchumi, sote tunaona kinachoendelea kwenye upatikanaji wa mafuta. Serikali ichukue hatua haraka.
Ni kweli, hususani wachimbaji / wafanyabishara wadogo na wakati. Itaweza kununua kwa shilingi na kuuza kwa Dollar.Naongezea
1.BOT inunue madini Kwa wafanyabiashara au makampuni alafu iuze Kwa Dora
Ni hatari sana pale serikali inapokuwa inawaza namna ya kuiba uchaguzi ujao muda wote badala ya maendeleo.Ccm wanaficha hela na kuiba ili 2024&2025 wazitumie kuiba uchaguzi kwa kuhonga wapiga kura na wasimamizi
Yule mchumi sijui anachangamoto gani?? Darasani alikuwa na akili sana tu, lakini inaonekana akili za darasani sio sawa kabisa na mafanikio ya mtaani.Halafu Mchumi namba moja anakwambia hatuwezi kufanya kitu kwasababu dolla siyo zetu.
Naam, ukiwagusa tu unaondolewa kwenye nafasi yako. Kuna watu hiyo ndio shughuli yao, wanafanya juu chini wawepo serikali ili waibe kwa manufaa yao na vizazi vyao.Hii nchi ina wezi waliokubuhi ,,,na wana mbinu za kuiba wamebobea. Hebu tafakali mtu Kama tutuba ( Gavanna BOT ana uwezo mkubwa sana lakini anawatazama tuuu .Nan kama mama
1.Umewahi kumuona Rais alifanya safari za anasa?1. Serikali isitishe kwa muda matumizi yasiyo ya lazima (anasa) yanayohitaji fedha za kigeni kama vile kununua magari ya kutembelea viongozi na safari za nje ya nchi (zote mpaka za SSH hazina tija).
2. Kampuni za ndani zitakazolipwa kwa shilingi zipewe kipaumbele kwenye miradi ya ujenzi na uwekezaji mwingine.
3. Serikali isitishe kukopa mikopo ya nje. Kwasasa mapato yetu ya fedha za kigeni mengi yanaishia kuhudumia madeni ya nje yaliyokopwa kwa pupa na serikali hii ya SSH kwa ushauri mbovu wa Mwigulu. Serikali isiongeze mzigo mwingine. Ikope ndani kwa kuuza bondi na njia nyinginezo.
4. Wizara ya fedha na wizara ya mipango ziwekwe chini ya ofisi ya makamu wa rais. Ni wazi kuwa hizo wizara mbili wameshindwa kujisimamia, na mamlaka kuu haina ujuzi wala uwezo wa kuzisimamia. Ni vema kazi hiyo apewe Dr. Mpango kwa wizara hizo kuwekwa chini yake rasmi.
5. Tunakaribia kutumbukia kwenye mgogoro mkubwa wa kiuchumi, majibu ya kisiasa na shortcuts haziwezi kusaidia. Siasa maji taka za kutoa "ufafanuzi" na matamko ya kijingajinga hayatatufikisha popote. Na wala kuvutia uwekezaji wa nje kwa njia za kihuni na rushwa hauwezi kutufikisha popote zaidi ya kutengeneza matatizo mengine.
Hauwezi kuuficha mdororo wa kiuchumi, sote tunaona kinachoendelea kwenye upatikanaji wa mafuta. Serikali ichukue hatua haraka.
Ni mpuuzi huyo jamaa1. Hakuna safari ya kikazi ya Rais ya nje isiyo na tija, kama hufuatilii ni uvivu wako lakini mara kwa mara zinatolewa press conference na DPC Zuhuru kuhusu ziara hizo na faida zake. Dunia ya Sasa inahitaji mazungumzo lakini anapokwenda nje kuzungumza ina tija zaidi kuliko kuwakilishwa bila hivyo tusingesikua Rais wa Marekana anazuru katika nchi za Afrika.
2. Hoja ya pili ni mpaka pale nchi itakapokuwa na wawekezaji wengi na wenye uwezo wa ndani wa kuwekeza kwenye miradi mikubwa. Kwa mfano uwekezaji kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee unagharimi Zaidi ya Dola za kimarekani billion 7 ambazo ni sawa na Trillion 16 za kitanzania. Kwa wawekezaji waliopo ni nani ambaye ana hiko kiwango Cha pesa kutukamilishia ujenzi huo? Hata matajiri 10 wakubwa wakawekeza Kila kitu Chao Bado hawawezi kufanya mradi kama huo. Ingefaa kweli miradi ijengwe na wazawa ili malipo yafanyike Kwa shilingi lakini tuseme kweli tutachelewa Zaidi.
Hoja ya Tatu, Serikali inakopa ili kuharakisha maendeleo na zaidi mikopo hiyo ni Ile yenye riba nafuu sana au isiyo na riba kabisa. Pia, tunakopa ili tuwe na akiba kubwa ya fedha za kigeni kwa ajili ya manunuzi ya nje, bidhaa na Teknolojia. Ingefaa utupe na ufafanuzi, Serikali itumie njia Gani kugharamia Kwa haraka miradi mikubwa kama Tukiachana na mikopo.
Hoja ya nne, umemtaja Makamu wa Rais Dkt.Mpango kama mtu mwenye uwezo wa kusimamia wizara ya fedha na wizara ya mipango na uwekezaji Kwa uwezo wake wa kitaaluma kwenye masuala ya uchumi na fedha na ndio maana ukataka wizara hizo ziwe chini yake lakini umesahau jambo Moja kubwa ambalo litahitaji majibu baadaye, je asipokuwepo Dkt Mpango katika ofisi ya Makamu wa Rais na akawepo mtaalamu wa Sanaa ofisi ya Makamu wa Rais, je Bado itahitajika wizara hizo chini ya ofisi ya Makamu wa Rais?
Hoja ya Tano, siamini kama unaendesha asasi yoyote ya kufanya tathmini ya uchumi mpaka uje na hoja ya kwamba tunakwenda kutumbukia kwenye mdororo wa kiuchumi. Ni vema hoja yako hii ingejikitika kwenye takwimu halisi Zaidi ya blabla Kwa sababu uchumi ni namba na namba hazidanganyi.
AmemezwaYule mchumi sijui anachangamoto gani?? Darasani alikuwa na akili sana tu, lakini inaonekana akili za darasani sio sawa kabisa na mafanikio ya mtaani.
Kwani hujui kwamba vipande vingine vimeongezeka?Miradi ya reli na bwawa ilikuwepo hata awamu ya tano. Kiasi cha fedha tunacholipa huko hakijabadilika sana.
Ni kweli ila Kwa nn analea weziMbuzi kama wewe huwezi elewa kitu,Rais Samia hajawahi fanya safari ya hasara
Kwamba tatizo la Dola ni Kwa sababu Wataalamu hawajatumika au? Mbuzi ni.wengi.sana Nchi hii.1. Kuna tofauti kubwa kati ya safari ya Biden nje ya nchi yake na safari ya rais wetu. USA anamaslahi mengi nje ya nchi, wana makampuni makubwa yanayaiingizia Marekani mabilioni ya fedha yanayofanya operations zake nje ya Marekani.
Safari zetu sisi ni kwenda kuvutia wawekezaji, kwenda kuomba misaada na mikopo. Matunda ya safari za SSH ndio hayo mauzauza ya DPW na madeni makubwa. Hazina tija!
2. Bwawa la umeme na reli havijengwi kwa mwaka mmoja. Hizo gharama ulizozitaja ni makadirio ya mradi wote ambao utachukua karibu miaka 10. Kwakuwa inajengwa na wakandarasi wa nje ni kweli kwamba lazima tutalipa kiasi fulani kwa fedha za kigeni. Lakini tunaweza kuhakikisha materials zote zinazopatika ndani basi zinanunuliwa ndani ( vitu vingi tu kwenye hiyo miradi vinatoka nje wakati tunavyo viwanda vya ndani vyenye uwezo wa kuzalisha), pamoja na subcontractors wote wa ndani wenye uwezo kufanya baadhi ya kazi wanapewa kipaumbele.
Lakini pia, miradi niliyokuwa nimeilenga zaidi ni ya barabara na majengo ya serikali. Hayo tunao wakandarasi wenye uwezo wa kujenga mingi ya miradi hiyo. Wapewe kipaumbele.
Hoja ya kukopa ili kuharakisha maendeleo haina maana kama mikopo hiyo inageuka kuwa mzigo kwenye uchumi wa nchi.
Hoja ya wizara ya fedha kuwekwa chini ya Dr. Mpango ni jambo la kutumia rasilmali ukizonazo kwa wakati huo. Rais angeweza hata kumwondoa Mwigulu na kumweka mtu mwingine pale, lakini itakuwa ni kama kufanya majaribio. Hiki ni kipindi cha mpito, serikali inaye mtaalamu wa uchumi ambaye amethibishwa kwa vitendo uwezo wake mkubwa wa kusimamia uchumi wa nchi, naye ni makamu wa rais. Kushindwa kumtumia kuzisimamia hizo wizara ni kushindwa kutumia rasilmali ulizonazo kutatua matatizo.