Honestty, No, si kweli! Nchi yetu sio masikini. Nchi yako labda. Sema sisi watanzania ni masikini wa akili lakini sio nchi. Sisi hatuna tofauti na ma zombies ambao, waswahili wanasema, tulio bweteka bwa! Tukisubiri kufukiwa mkaburini
Uingereza kwa mfano ilikuwa nchi masikini sana Europe karne za huko nyuma. Haikuwa na kitu chochote isipokuwa kisiwa, mild weather, ardhi yenye rutuba na coal. Lakini kupitia ujasiri na uthubutu wa viongozi wake kama; King Henry wa nane ambaye alimdindia Pop wa Rom na baadae kuanzisha madhehebu yake ya kianglican, the Virgin Queen Elizabeth I. (binti wa mwisho wa King Henry VIII.) na Queen Victoria na wingi wa maarifa ya watu wake kama; Sir Francis Drake, Thomas Newcomens, James Watt, Robert Stephenson with the Rocket locomotive na wengineo wengi.
Wajerumani wana msemo unaosema; "Not macht erfinderich",(Necessity is the mother of invention, kwa nyie waingereza). Hapa namaanisha kuwa ulimwengu including us, tuko katika matatizo makubwa, kwa hiyo sisi watanzania hatuna budi nasi kutumia hili janga kama njia moja wapo ya kutuwezesha sisi kukusanya nguvu zetu pamoja na kujitahidi kufanya mambo ambayo yatatusaidia sisi wenyewe badala ya kukaa na kusubiri watu wa kutoka nchi tunazo ziita zimeendelea waje kutusaidia.
Waziri mkuu wa Great Britain Sir Winston Churchill mwaka 1941 wakati wa vita kuu ya pili ya dunia, aliwakusanya kwenye Bletchley Park watu tofaut wanaume kwa wanawake karibu 1,000 hivi ambao walifanya kazi moja tu muhimu ya kutafuta ufumbuzi wa mawasiliano ya majeshi ya Hitler wa Ujerumani.
Kabla ya vita, wakati wa amani, watu hawa walikuwa na professions tofauti; walikuwa waalimu wa vyuo vikuu, maafisa wa jeshi, watafsiri, Bankers, Ches Masters, wanasayansi wana mahesabu, wanafunzi, na wasanii. Kitu kilicho angaliwa hapa ni intuition na silaha zao kubwa zilikuwa ni mantiki, hisabati, fikra na uvumbuzi. Na kweli baada ya kuhangaika mda mrefu hatimaye walifanikiwa ku i cracke mashine ya mawasiliano ya jeshi la Hitler "ENIGMA" na hapo kuifanya vita iwe rahisi kwao mpaka kumshinda Hitler.
Na sisi kikubwa tunacho hitaji ni kutengeneza device yetu wenyewe ambayo itatuwezesha ku scann magonjwa kama haya ya mlipuko ki sawa sawa au tutumie njia nyingine ku mitigate mlipuko kama huu badala ya kukubali kuwa mazombie wa Mutants.
List ya watanzania wenye utaalam tofauti is very long. Kwa nini tusikusanye hizi nguvu pamoja na kuanza kufanya utafiti wetu sisi wenyewe?
Rais Magufuli fanya kitu cha maana Mzee!
Sent using
Jamii Forums mobile app