Serikali ikiondoa unafiki na chuki bado Kagera inaweza kuchomoza, Chalamila unatakiwa kujua haya

Ego na ubishi wa kuamini tunajua kila kitu. Unamchukua mtoto wa mjomba au shangazi yako kutoka nyumbani kabisa, akifika Dar anakuwa wa kwanza kukuhujumu hapo nyumbani.

Ndio hulka zetu watu wa Kagera, RC Chalamila sio wa kuchukiwa, ametupa changamoto nzuri.
 
Ukiona mtu anazungumzia Umalaya,mashoga, na uvivu kwamba ni sifa ya mkoa flan ndani ya tz, jua
1.akili yake kaifungia kwenye sanduku, alipo anatembea yeye tu,.
Hakuna mkoa haya Mambo hayapo
Huwezi kujiona mpaka uambiwe ndiyo maana tulifuta uchifuu
 
We ni mpuuzi sio kawaida yangu jibiza na wapuuzi,unamtisha nani umekaa Mikoa mingi na kuja na matusi hapa mwanaharam mkubwa, Kama ni laana zako za ukoo kaa nazo huko,binfsi sio mtu wa matusi
Kaliwe mbele hamna unachojua mpumbavu kabisa

Kasome hyo report hujui kitu unajua umaskini nenda longido ukaone umaskin usidanganywe na magorofa investment za watu wa juu kabisa wachache
 

Attachments

  • Screenshot_20220904-142845.png
    94 KB · Views: 7

Kaliwe mbele hamna unachojua mpumbavu kabisa

Kasome hyo report hujui kitu unajua umaskini nenda longido ukaone umaskin usidanganywe na magorofa investment za watu wa juu kabisa wachache
Wewe jamaa Shamba Sana alikwambia Kama mtu mmoja kipato chake sh 300 KWA siku na mwingine 500 KWA siku basi Hawa wote sio maskini ni nani,? Mnakuja na vipeperushi vya kuokoteza hapa ,
Hiyo ni Mikoa kiwango Cha umaskini akiwezi lingana ila Mikoa maskini ,
Alafu jitu linakuja na matusi alafu eti nimekaa Mikoa kibao,
Sasa nakuonya binafsi sio mtu wa matusi ,Sasa hutaki endelea na matusi upate haki yako live pitia hapa jf , wenda ipo laana ya ukoo inakutafuna , ni swala la kuiongezea
 
kama kuna mikoa imeminywa na serikali ni mikoa ya nyanda za juu kusini, mbeya, iringa, rukwa , songwe, lakini tofauti yenu na mikoa ya huko ni nyinyi kuzidisha ujuaji kuliko kazi, nimekaa na wahaya na nimefika hadi kagera umaskini ni mkubwa sana aisee, ni watu wanaomini sana maisha yanapatikana kupitia shule tu na tatizo linanzia hapo, miaka hii aliyesoma na asiye soma ujanja ni kuwa na akili ya utafutaji nje ya mfumo, hangikieni masoko y bizaa zenu ,
 
🤣🤣🤣Acha mkwara tafuta wajinga wenzio ndo uwadanganye sio mbele yangu...kama hujielewi lazima ukumbushwe sio unaropoka Kuna watu kibao tafuta wenzio kuwadangany watuw anafanya research Kuna sehemu watu wanaoga mpaka mkojo wa ng'ombe ndo maisha yao unaongea ebu tembea uone uache kukariri
 
Chalamila kawaambia ukweli mtupu.
 
Kwa hiyo nyie wananchi wa Kagera mnajadili miaka Sita wapi mjenge soko na stand?
Mko very serious aisee
Kazi ya kwanza ya Serikali& viongozi wake ni kuwaletea wananchi Maendeleo . Na Hilo ndo Huwa wanaliombea kura! Huo ndio MKATABA WA SERIKALI NA WATU WAKE, SIO MKATABA WA WASOMI NA WATU. WASOMI wanaweza kushirikiana na Serikali ila HAWAWIWI kwa mjibu wa uongozi. Wanasiasa watata sana. Wanafanya agenda ya wasomi kumbe sio. SERIKALI itimize wajibu wake kwa wananchi wake na KUWAOMBA WASOMI kusaidia kwa Kisomo Chao.
 
Yote uliyoandika, la maana ni hilo hasa ambalo hao wa kagera hawana
 
Wahaya wanapenda sifa za kijinga sana. Sifa zao za kijinga ndizo chanzo cha umaskini wao wa kutupwa. Ovyo kabisa nshomile.
 
Basi endeleeni na vingereza vyenu na sifa za kijinga. Chalamila kawashauri mfanye kazi, nyie mnatokwa na povu!
 

Katika wote naunga mkono hoja. Miji yote watu wanaojigamba kuwa imeendelea(kwa kibongo bongo) imefanywa na Serikali. Bila serikali ni zero. Leo hii Serikali ikiamua Singida kwa mfano liwe jiji itakua na itachangamka. Mfano wa Dodoma,bila msukumo wa Serikali Dodoma haina ubavu wowote kuizid mikoa ya kimkakati kama Iringa tu kwa mfano.
 
Changamoto zifuatazo, zinafanya Kagera tuwe nyuma. Tuache visingizio.

1. Ardhi ni ndogo
Kupata mkulima mwenye acre 2 au zaidi ni shida. Maeneo mengi yaliyotumika na jamii kwa kuchungia, kulima nafaka kama karanga n.k. yalichukuliwa na watu wachache wakapanda miti ya mbao, na kuacha watu wengi wakabaki wanahangaika.

2. Utamaduni wa kilimo cha migomba.
Migomba ni utamaduni wa Mhaya. Migomba hii haizalishi tena kwa wingi. Mashamba mengi ni yamechoja. Siyo rahisi kuwashauri watu kung'oa na kupanda mazao yenye tija. Hii ni crop rotation ambayo ingesaidia kurudisha rutuba na kutokomeza mnyauko.

3. Matumizi ya mbolea
Watu wengi wanaamini kwamba, mbolea inaharibu ardhi. Kwa hiyo, mapinduzi ya kilimo kwa kutumia ardhi iliyochoka ni ngumu.

4. Kaitu kaila
Acceptance ya aina mpya ya mazao ni ngumu. Tukubaliane, Mhaya anapenda sana migomba.

Pia, Takwimu zinaonyesha Kagera unaoongoza uzalishaji wa maharage kitaifa. Tatizo kubwa ni kwamba hawalengi soko. Maharage yanalimwa kwa wingi, lakini ni local na mchanganyiko. Yaani kila variety kidogo kidogo kiasi kwamba ukiyachambua na kukusanya, kiasi kinachopatikana hakikidhi soko individually.

5. Vijana na akina baba kutoshiriki kilimo
Mathalani, vijana wengi wilaya ya Missenyi hasa Kiziba na Kibumbilo, wamejikita sana kwenye kunywa karadarugo ambayo ni starehe ya vijana wengi. Hii inua nguvukazi.

Fursa za masoko

Masoko siyo shida. Kuna kipindi nimeshuhudia mihogo inatoka Lindi na Kigoma kupita Mutukula kwenda South Sudan. Vivyo hivyo, maharage na mahindi kutoka Rukwa na Mbeya. Halafu, wakati wa vita ya Rwanda, Kulikuwa na soko kubwa la WFP. Waliofaidi ni watu wa mbali.

Kuna mashule ya bweni pamoja na majeshini. Maharage yanayotumika huko ni ROZIKOKO. Soko siyo shida.

Kwa hiyo, swala la Stendi au Soko Kuu, havitaongeza chochote kwenye mfuko wa mwananchi. Vitabadili mandhari tu na kuongeza mapato ya serikali. Ni sawa na kuvaa suti huku una njaa.

Ili kubadili wananchi, inatakiwa nguvu kiasi, hasa ya kisiasa. RC ameanza vizuri japo tunataka zaidi action.

Nashauri kampeni kubwa iwe ni kubadili mindset za watu. Mfano, badala ya radio nyingi(Kasibante, Fadeco n.k) kushinda wanajadili mpira na miiziki, wajikite kutoa elimu ya kilimo na uchumi muda mwingi.

Ianzishwe TV station ya Kagera. Hii itakuwa na muda mwingi wa kutoa elimu kwa vitendo. Mpaka sasa kuna watu hawajui hata namna ya kupanda mahindi na maharage kitaalamu!. Watu hawajui kama kuna aina mpya za migomba na kahawa inayogawiwa bure.

Nashauri vikundi vya kilimo, vilivyo na uwezo wa kuunganisha wakulima pamoja, kama kule Kenyana Kilimilile, vipewe elimu na misaada ili kuleta chachu kwa wakulima wengine.

Nashauri pia, Maafisa ugani wapewe mafunzo ambayo ni 'tailor made' kwa ajili ya kupeleka elimu sahihi kwa wakulima.

Inawezekana. Hapo chini ni shamba la maharage katika kijiji cha Kenyana, 2021
 
Haya Sasa. Huyo ni kiongozi na kaonyesha wazi chuki dhidi ya wahaya. Pia naona michango mingi unakuja against wahaya. Sasa wahaya tafuteni jinsi ya kubadilisha majina yenu. Msitegemee kupata ajira na kushinda interview kama watu wenyewe ndo hao. Kazi kwenu akina Mutashobya, Mwijage, Karugendo nk
 

Hoja ya Wazawa kwa maana ya kuwekeza haina mashiko. Kila mkoa upambane kuleta ushawishi wa wawekezaji haijalishi ni wwzawa au Mtanzania yeyote. Dar kwani ni wazaeama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…