Serikali ikiondoa unafiki na chuki bado Kagera inaweza kuchomoza, Chalamila unatakiwa kujua haya

Serikali ikiondoa unafiki na chuki bado Kagera inaweza kuchomoza, Chalamila unatakiwa kujua haya

Acheni majivuno fanyeni kazi unataka kusingizia vita ya miaka 42 ndiyo imeleta umasikini. Kwani Kagera ina shida ya watu wa nguvu kazi.


Kazi kwani hatufanyi? Umemsikia mwenda zake akitaja kuwa miundo mbinu inaletwa na serikali sasa hiyo stand mnataka ijengwe na wananchi wakati tunakatwa tozo na kodi lakini bado hatupewi hizo fedha
 
Ninasema hata sie wa ,Njombe, Iringa, Songea n.k tulitakiwa shirikishwa wapi masoko na Stendi vijengwe, hili la Kagera ni mfano tu unaonesha ni KWa namna GANI wananchi Tunaburuzwa na Serikali, kwamba kwenye Miradi inayotugusa moja kwa moja hatushirikishwi, sawa WENDA miaka sita ikawa mingi tokana na malumbano wapi Mradi utajengwa ,ila ni kazi ya viongonzi kupima hoja na kuja na suruhu sio toa maneno ya hovyo,
Kuna pengine yamejengwa ayo masoko tz hii na stendi tena KWa gharama kubwa ila yatachukua miaka hata 30 bila kutorudisha gharama, Sasa nijibu,
Lipi zuri ,jenga mradi KWa mwaka au mda mfupi ila ufanisi wake unakua sufuli, au chelewa kujenga na ukajenga pale ambapo ufanisi ni 100% jibu mkuu
Bora hata uko wanapoijenga stendi ya bukoba sio mbali sana na kushangamka sasa...tatizo la Bukoba ni ccm ..imagine toka 2020 ujenzi ulisimamishwa kwa sababu uongozi wa Bukoba ulibadirishwa toka chadema to ccm.

Soko kuu Bukoba litajengwa hapo hapo mjini kati...lakin wanalumbana kila siku wafanyabiashara wawaweke wap kwa muda...

RC MWENYE WAJIBU WA KUSOLVE HAYO..ASHAANZA KUWAOGOPA WAHAYA NA USOMI WA KUJUA SHERIA...

Huyu chalamila baada ya kuja kagera ndo nimejua yuko weak..anajifisha kwa kuongea sana tu

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Bora hata uko wanapoijenga stendi ya bukoba sio mbali sana na kushangamka sasa...tatizo la Bukoba ni ccm ..imagine toka 2020 ujenzi ulisimamishwa kwa sababu uongozi wa Bukoba ulibadirishwa toka chadema to ccm.

Soko kuu Bukoba litajengwa hapo hapo mjini kati...lakin wanalumbana kila siku wafanyabiashara wawaweke wap kwa muda...

RC MWENYE WAJIBU WA KUSOLVE HAYO..ASHAANZA KUWAOGOPA WAHAYA NA USOMI WA KUJUA SHERIA...

Huyu chalamila baada ya kuja kagera ndo nimejua yuko weak..anajifisha kwa kuongea sana tu

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Ni imani yangu Mikoa mingi inapata viongozi ambao wao ubunifu, burasa katika kutatua kero nyepesi upo chini,
Siku moja nikashangaa katika Mapato eti Dodoma jiji ikawa juu ya Mwanza,!!
Leo Kagera, Ruvuma, Tanga , Tabora, kigoma ,KWA nini ziwe maskini? alafu unalaam Elim za watu,
Chalamila wakati anafundisha moja ya chuo hapo IRINGA, alikua anafundisha kwa KIBENA? maana vingereza hataki, na ni kwanini watoto wake awapeleke kwenye shule za kulipa, lengo siwajue vingereza

Kagera Kama ilivyo Mikoa mingine, vipo vyanzo vingi vya kuongeza mzunguko na Mkoa ukapaa ni swala la kuwa na viongozi wabunifu,
 
Bora hata uko wanapoijenga stendi ya bukoba sio mbali sana na kushangamka sasa...tatizo la Bukoba ni ccm ..imagine toka 2020 ujenzi ulisimamishwa kwa sababu uongozi wa Bukoba ulibadirishwa toka chadema to ccm.

Soko kuu Bukoba litajengwa hapo hapo mjini kati...lakin wanalumbana kila siku wafanyabiashara wawaweke wap kwa muda...

RC MWENYE WAJIBU WA KUSOLVE HAYO..ASHAANZA KUWAOGOPA WAHAYA NA USOMI WA KUJUA SHERIA...

Huyu chalamila baada ya kuja kagera ndo nimejua yuko weak..anajifisha kwa kuongea sana tu

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Umeona anaanza kwa kuponda badala ya kutafuta nini chanzo cha haya mambo. Ameferi kabla ya hata kuanza.
 
Ni imani yangu Mikoa mingi inapata viongozi ambao wao ubunifu, burasa katika kutatua kero nyepesi upo chini,
Siku moja nikashangaa katika Mapato eti Dodoma jiji ikawa juu ya Mwanza,!!
Leo Kagera, Ruvuma, Tanga , Tabora, kigoma ,KWA nini ziwe maskini? alafu unalaam Elim za watu,
Chalamila wakati anafundisha moja ya chuo hapo IRINGA, alikua anafundisha kwa KIBENA? maana vingereza hataki, na ni kwanini watoto wake awapeleke kwenye shule za kulipa, lengo siwajue vingereza

Kagera Kama ilivyo Mikoa mingine, vipo vyanzo vingi vya kuongeza mzunguko na Mkoa ukapaa ni swala la kuwa na viongozi wabunifu,
Watupe DC wa Malinyi asimame jiji bila kumwingilia alaf miaka mitatu waje kuangalia mambo.
 
Fainal hata mfanyeje serikali ndo Ina uwezo kufanya mkoa fulani uwe juuu kwa vile kibongo hatuna matajiri wakubwa wakasimama kuwezesha mikoa, mfano kanda ya ziwa mwanza iwezeshwa kaskazini Arusha na pwani ni dar ,hyo ni plan ya serikali na sasa wanawezesha Dodoma ambapo mnadai wakazi wake ni omba omba ila mtakuja kuona maendeleo mpaka mshangae ..

Ujinga unabaki vichwani kwamba kagera hawaendelei ila wahaya Wana manyumba ya kifaharu sio kosa lao ni mpango wa serikali ... wajinga wengi mmekariri eti uchapa kazi sijui wengin wavivu maendeleo sio kiivyo ndo maana mnakufa maskini eti uchapakazii !!Hkuna sehemu iliyoendelea bila ya sapot ya serikali kama unabisha niambie ukitaka kujua maendeleo y watu binafsi angalia ubora wa makazi na per Capital income kama Kilimanjaro hapo ndo utajua kwamba wanafight hata kagera pia, ila kwa image ya mji mzima na mkoa ni juu ya serikali.
 
Ni imani yangu Mikoa mingi inapata viongozi ambao wao ubunifu, burasa katika kutatua kero nyepesi upo chini,
Siku moja nikashangaa katika Mapato eti Dodoma jiji ikawa juu ya Mwanza,!!
Leo Kagera, Ruvuma, Tanga , Tabora, kigoma ,KWA nini ziwe maskini? alafu unalaam Elim za watu,
Chalamila wakati anafundisha moja ya chuo hapo IRINGA, alikua anafundisha kwa KIBENA? maana vingereza hataki, na ni kwanini watoto wake awapeleke kwenye shule za kulipa, lengo siwajue vingereza

Kagera Kama ilivyo Mikoa mingine, vipo vyanzo vingi vya kuongeza mzunguko na Mkoa ukapaa ni swala la kuwa na viongozi wabunifu,
Tafuta mikoa maskini list umekosea yaani Tanga unaumwa sio bure
 
Watupe DC wa Malinyi asimame jiji bila kumwingilia alaf miaka mitatu waje kuangalia mambo.
Ipo mashine nyingine hivi, MTAKA yule anafaa Sana kuwa mkuu wa Mkoa wa Mwanza au Kagera, hii Mikoa inategemeana,
Mwanza mzunguko wa pesa ukiwa juu vile Kagera mzunguko utapaa,
lakini pia badala ya viongozi toa lawama tu, fungua Milango ya mkoa wa Kagera kibiashara kupitia mipaka ya nchi jirani, watu wafanye biashara na serikali ipate kodi, wananchi pia wapate fedha,

Mkoa upo mpakani ila mmeutia pingu ukiritimba pale mpakani Kama wote, ila wenzetu pitia Mikoa iliyo mipakani wanaingia wanafanya biashara ,hii imekaa vipi?
 
Tafuta mikoa maskini list umekosea yaani Tanga unaumwa sio bure
Mkuu tatizo mnadanganywa na tafiti za Twaweza, wenda mnazungumzia tu kipi kinapatikana kule katika changia kwenye mfuko wa serikali kuu, kisa hivyo viwanda vichache vinavyofanya kazi

Maana vingi ni maghofu,

Pili utazungumzia labda kilimo Cha mkonge ambacho nacho kinasuasua, mashamba yale yaliyokua yakiajili watu wengi mengi yamebaki Kama sanam,ila wachache pitia hatimiliki walishachukulia mamikopo wanakula KWA urefu wa kamba zao,

Utazungumzia kilimo Cha machungwa, ambapo wengi wenye mashamba pale sio wazawa ni Wakinga, wazawa walisha uza

Bandari pia utaizungumzia lakin je imeajiri watu wanagapi?

Pale katika uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja ni wakimaskini wa kutupa,ndo maana linaitwa jiji ila bodaboda za baiskeli ni Kama zote,

Sasa niambie nyie kipimo Cha umaskini katika mkoa mnaangalia kile mkoa inachangia katika mfuko wa serikali kuu au pato kwa mwananchi mmojammoja
 
Kinachosikitisha ni kwamba kila anayepanda jukwaa kuelezea kinachoitwa umaskini wa Mkoa wa Kagera anakuja na ngonjera za wingi wa maprofesa na ma-PhD holders kutoka mkoani mwetu. Lawama zote zinarundikwa kwa watu hao na Wanakagera kwa jumla.

Huo ndio ukasuku na unafiki wa watawala wetu ambao tumezoea kwa miaka mingi sasa. Watawala wanajifanya kama hawajui chanzo halisi cha kile wanachokiita umasikini uliokithiri mkoani humo. Bila tafakuri yoyote ya "tafiti" zinazodaiwa kufanywa na Serikali, wanakuja tu na porojo za jumlajumla kuhusu "umasikini" huo. Tafiti hizo za kimangumashi hazielezei chanzo cha tatizo la mkoa wa Kagera.

Haziangalii matokeo ya vita vya Kagera na uharibifu wa usalama na miundombinu uliosababishwa na ugomvi wa Serikali na Iddi Amin. Kwamba shughuli za uzalishaji na kiuchumi zilikufa kabisa kutokana na vita hiyo.

Hawaoni kwamba serikali ilikosea (kwa makusudi) kutotangazwa kwa hali ya hatari mkoani humo, kwa maana ya kujenga miundombinu upya na kuwasaidia wanakagera kurudia maisha yao ya kabla ya vita. Hawasemi Serikali ilifunga mpaka na Uganda, hivyo kusitisha shughuli zote za kiuchumi, ambapo soko kuu la mkoa wa Kagera lilikuwa Uganda. Baada ya vita Ukimwi uliotokea Uganda ulimaliza nguvukazi kubwa ya mkoa huo kwa kupuputisha maisha ya maelfu ya nguvukazi wa Kagera.

Wanajifanya hawajui kwamba MV. Bukoba ilizama na kuua mamia ya watu, wengi wao wakiwa Wanakagera. Hapohapo, MV. Victoria "iliharibika" na kufanya Wanakagera kukosa kabisa usafiri wa kuwaunganisha na nchi yao, huku mazao yao ya kiuchumi yakishindwa kusafirishwa kwenda kwenye masoko makubwa ya kibiashara ya hapa nchini kama Mwanza na Dar es Salaam. Serikali haikuona umuhimu wa kuwapa Wanakagera vyombo vingine vya usafiri ili wajimudu kiuchumi.

Ndipo pia ulipoingia "Ugonjwa wa Mnyauko" wa migomba uliopigilia msumari wa mateso na umasikini wa wanakagera. Yapata sasa zaidi ya miaka 15. Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwasaidia wakulima wa kilimo cha migomba mkoani Kagera? Hakuna! Wakati huohuo Wanakagera walikatazwa kuuza kahawa yao nchini Uganda ambako walikuwa wanapata bei nzuri kulingana na gharama za uzalishaji. Waliopatikana na uvushaji wa zao hilo waliadhibiwa, ikiwemo vifungo au kufilisiwa, huko kahawa ikilimbikiziwa "tozo" lukuki bila kutilia maanani gharama za wakulima za uzalishaji.

Hiyo ni mifano michache tu ya hujuma ya serikali dhidi ya mkoa wa Kagera kwa miongo mingi sasa. Matokeo yake ni nini, Wananchi wa mkoa wa wa Kagera waliona serikali ilikuwa haiwataki, haiwapendi. Wakasema isiwe taabu, wakaamua kuhamia mikoa nyingine nchini na kuwekeza huko. Je, serikali inajifanya haioni uwekezaji wao mkubwa na uliotukuka katika mikoa mingine nchini, ikiwemo Dar Es Salaam, Mwanza, Arusha na kwingineko?

Serikali imekuwa ikipiga kelele nyingi eti wahaya wameshindwa kujenga soko na kituo cha mabasi mjini Bukoba, ikijifanya haijui kwamba jukumu hilo ni lake na vyombo vyake, ikiwemo TAMISEMI. Kwani vituo vya mabasi na masoko ya Dodoma, Morogoro, Dar Es Salaam, Mwanza na kwingineko vimejengwa na nani kama sio Serikali? Nimalizie kwa kuishauri Serikali kwamba iwekeze mkoani Kagera kama ambavyo imekuwa ikiwekeza sehemu nyingine nchini.

Ikiwekeza Kagera, kama ambavyo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imepanga kufanya kwa kujenga kitengo cha Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM), mkoani humo, basi itarajie kwamba maprofesa na PhD holders kutoka mkoani Kagera watarudi nyumbani kufaidi fursa za uwekezaji wa serikali. Ni matumaini ya wengi mkoani Kagera kwamba Mkuu mpya wa mkoa wa Kagera, Mhe. Chalamila ataelewa chanzo cha "umasikini wa mkoa wa Kagera."
 
Kinachosikitisha ni kwamba kila anayepanda jukwaa kuelezea kinachoitwa umaskini wa Mkoa wa Kagera anakuja na ngonjera za wingi wa maprofesa na ma-PhD holders kutoka mkoani mwetu. Lawama zote zinarundikwa kwa watu hao na Wanakagera kwa jumla.

Huo ndio ukasuku na unafiki wa watawala wetu ambao tumezoea kwa miaka mingi sasa. Watawala wanajifanya kama hawajui chanzo halisi cha kile wanachokiita umasikini uliokithiri mkoani humo. Bila tafakuri yoyote ya "tafiti" zinazodaiwa kufanywa na Serikali, wanakuja tu na porojo za jumlajumla kuhusu "umasikini" huo. Tafiti hizo za kimangumashi hazielezei chanzo cha tatizo la mkoa wa Kagera.

Haziangalii matokeo ya vita vya Kagera na uharibifu wa usalama na miundombinu uliosababishwa na ugomvi wa Serikali na Iddi Amin. Kwamba shughuli za uzalishaji na kiuchumi zilikufa kabisa kutokana na vita hiyo.

Hawaoni kwamba serikali ilikosea (kwa makusudi) kutotangazwa kwa hali ya hatari mkoani humo, kwa maana ya kujenga miundombinu upya na kuwasaidia wanakagera kurudia maisha yao ya kabla ya vita. Hawasemi Serikali ilifunga mpaka na Uganda, hivyo kusitisha shughuli zote za kiuchumi, ambapo soko kuu la mkoa wa Kagera lilikuwa Uganda. Baada ya vita Ukimwi uliotokea Uganda ulimaliza nguvukazi kubwa ya mkoa huo kwa kupuputisha maisha ya maelfu ya nguvukazi wa Kagera.

Wanajifanya hawajui kwamba MV. Bukoba ilizama na kuua mamia ya watu, wengi wao wakiwa Wanakagera. Hapohapo, MV. Victoria "iliharibika" na kufanya Wanakagera kukosa kabisa usafiri wa kuwaunganisha na nchi yao, huku mazao yao ya kiuchumi yakishindwa kusafirishwa kwenda kwenye masoko makubwa ya kibiashara ya hapa nchini kama Mwanza na Dar es Salaam. Serikali haikuona umuhimu wa kuwapa Wanakagera vyombo vingine vya usafiri ili wajimudu kiuchumi.

Ndipo pia ulipoingia "Ugonjwa wa Mnyauko" wa migomba uliopigilia msumari wa mateso na umasikini wa wanakagera. Yapata sasa zaidi ya miaka 15. Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwasaidia wakulima wa kilimo cha migomba mkoani Kagera? Hakuna! Wakati huohuo Wanakagera walikatazwa kuuza kahawa yao nchini Uganda ambako walikuwa wanapata bei nzuri kulingana na gharama za uzalishaji. Waliopatikana na uvushaji wa zao hilo waliadhibiwa, ikiwemo vifungo au kufilisiwa, huko kahawa ikilimbikiziwa "tozo" lukuki bila kutilia maanani gharama za wakulima za uzalishaji.

Hiyo ni mifano michache tu ya hujuma ya serikali dhidi ya mkoa wa Kagera kwa miongo mingi sasa. Matokeo yake ni nini, Wananchi wa mkoa wa wa Kagera waliona serikali ilikuwa haiwataki, haiwapendi. Wakasema isiwe taabu, wakaamua kuhamia mikoa nyingine nchini na kuwekeza huko. Je, serikali inajifanya haioni uwekezaji wao mkubwa na uliotukuka katika mikoa mingine nchini, ikiwemo Dar Es Salaam, Mwanza, Arusha na kwingineko?

Serikali imekuwa ikipiga kelele nyingi eti wahaya wameshindwa kujenga soko na kituo cha mabasi mjini Bukoba, ikijifanya haijui kwamba jukumu hilo ni lake na vyombo vyake, ikiwemo TAMISEMI. Kwani vituo vya mabasi na masoko ya Dodoma, Morogoro, Dar Es Salaam, Mwanza na kwingineko vimejengwa na nani kama sio Serikali? Nimalizie kwa kuishauri Serikali kwamba iwekeze mkoani Kagera kama ambavyo imekuwa ikiwekeza sehemu nyingine nchini.

Ikiwekeza Kagera, kama ambavyo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imepanga kufanya kwa kujenga kitengo cha Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM), mkoani humo, basi itarajie kwamba maprofesa na PhD holders kutoka mkoani Kagera watarudi nyumbani kufaidi fursa za uwekezaji wa serikali. Ni matumaini ya wengi mkoani Kagera kwamba Mkuu mpya wa mkoa wa Kagera, Mhe. Chalamila ataelewa chanzo cha "umasikini wa mkoa wa Kagera."
Punguzeni vikundi vya kuchangiana misiba, harusi , rushwa na sifa za kufekii . Fanyeni kazi kwa bidii muuondoe huo umaskini wenu.

Vitu vya ajabu sana unaviona hapo Kagera. Mashoga wengi sana wa kihaya, umalaya na uvivu wa kujikweza

Mfanye kazi na huyo mkuu wenu wa mkoa msonge mbele
 
Mkuu tatizo mnadanganywa na tafiti za Twaweza, wenda mnazungumzia tu kipi kinapatikana kule katika changia kwenye mfuko wa serikali kuu, kisa hivyo viwanda vichache vinavyofanya kazi

Maana vingi ni maghofu,

Pili utazungumzia labda kilimo Cha mkonge ambacho nacho kinasuasua, mashamba yale yaliyokua yakiajili watu wengi mengi yamebaki Kama sanam,ila wachache pitia hatimiliki walishachukulia mamikopo wanakula KWA urefu wa kamba zao,

Utazungumzia kilimo Cha machungwa, ambapo wengi wenye mashamba pale sio wazawa ni Wakinga, wazawa walisha uza

Bandari pia utaizungumzia lakin je imeajiri watu wanagapi?

Pale katika uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja ni wakimaskini wa kutupa,ndo maana linaitwa jiji ila bodaboda za baiskeli ni Kama zote,

Sasa niambie nyie kipimo Cha umaskini katika mkoa mnaangalia kile mkoa inachangia katika mfuko wa serikali kuu au pato kwa mwananchi mmojammoja
We ndo unajidanganya Tanga Haina umaskini kama unavyodhani labda uniambie maendeleo ila sio umaskini kwamba ipo kweny danger ,kwa nn usisime lindi, rukwa, kigoma ,kama unabisha leta takwimu zako nimekaa mikoa kiboa uache kutaja mtwara ...acha kusumbua kaangalie mikoa yenye watu weny kipato

Hata Arusha umaskini upo wa kumwaga ukitoa pale mjini, nenda mwanza ndo usiseme we unaropoka kama umekunywa maji ya chooni
 
Punguzeni vikundi vya kuchangiana misiba, harusi , rushwa na sifa za kufekii . Fanyeni kazi kwa bidii muuondoe huo umaskini wenu.

Vitu vya ajabu sana unaviona hapo Kagera. Mashoga wengi sana wa kihaya, umalaya na uvivu wa kujikweza

Mfanye kazi na huyo mkuu wenu wa mkoa msonge mbele
Ukiona mtu anazungumzia Umalaya,mashoga, na uvivu kwamba ni sifa ya mkoa flan ndani ya tz, jua
1.akili yake kaifungia kwenye sanduku, alipo anatembea yeye tu,.
Hakuna mkoa haya Mambo hayapo
 
Punguzeni vikundi vya kuchangiana misiba, harusi , rushwa na sifa za kufekii . Fanyeni kazi kwa bidii muuondoe huo umaskini wenu.

Vitu vya ajabu sana unaviona hapo Kagera. Mashoga wengi sana wa kihaya, umalaya na uvivu wa kujikweza

Mfanye kazi na huyo mkuu wenu wa mkoa msonge mbele
Sasa wew unachuki na wahaya huna hoja...
 
We ndo unajidanganya Tanga Haina umaskini kama unavyodhani labda uniambie maendeleo ila sio umaskini kwamba ipo kweny danger ,kwa nn usisime lindi, rukwa, kigoma ,kama unabisha leta takwimu zako nimekaa mikoa kiboa uache kutaja mtwara ...acha kusumbua kaangalie mikoa yenye watu weny kipato

Hata Arusha umaskini upo wa kumwaga ukitoa pale mjini, nenda mwanza ndo usiseme we unaropoka kama umekunywa maji ya chooni
We ni mpuuzi sio kawaida yangu jibiza na wapuuzi,unamtisha nani umekaa Mikoa mingi na kuja na matusi hapa mwanaharam mkubwa, Kama ni laana zako za ukoo kaa nazo huko,binfsi sio mtu wa matusi
 
Ndiyo ni kweli, ila maprofesa hao na PhD holds wa Kagera ndio wana waelimisha watu wa Kigoma, Mara, Mtwara na kwinginko! Hawahudumii Kagera tu! Ni Tanzania nzima na kwingine duniani.
Kwao wamekushindwa

Wakitoa ushauri darasa la saba anainuka kupinga
 
Mkuu tatizo mnadanganywa na tafiti za Twaweza, wenda mnazungumzia tu kipi kinapatikana kule katika changia kwenye mfuko wa serikali kuu, kisa hivyo viwanda vichache vinavyofanya kazi

Maana vingi ni maghofu,

Pili utazungumzia labda kilimo Cha mkonge ambacho nacho kinasuasua, mashamba yale yaliyokua yakiajili watu wengi mengi yamebaki Kama sanam,ila wachache pitia hatimiliki walishachukulia mamikopo wanakula KWA urefu wa kamba zao,

Utazungumzia kilimo Cha machungwa, ambapo wengi wenye mashamba pale sio wazawa ni Wakinga, wazawa walisha uza

Bandari pia utaizungumzia lakin je imeajiri watu wanagapi?

Pale katika uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja ni wakimaskini wa kutupa,ndo maana linaitwa jiji ila bodaboda za baiskeli ni Kama zote,

Sasa niambie nyie kipimo Cha umaskini katika mkoa mnaangalia kile mkoa inachangia katika mfuko wa serikali kuu au pato kwa mwananchi mmojammoja
We unahitaji kwenda kusoma kwa vile mshamba sana wa magorofa kaangalie kilimanjaro magofu kibao ila wananchi wake Wana kipato kizuri na ni WA pili kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja..

Umaskini upi? Life la Tanga lipo chini ambayo watu wanaaffoid ndo maana wanaita Tanga raha kwa mshahara wa laki na nusu unaishi.. unachoshindwa kuelewa hujitambui nn unaongea unasema bodaboda na baiskeli ndo uwezo wao huo ulifikia kaangalie na mkoa Kuna watu hWana hata chakula kabisa

Kule chakula sio shida nenda handeni ukaone mahindi ,vitu Bei chee umekariri kupiga picha kweny magorofa punguza ushamba umaskini haupimwi kiivyo nenda Kilimanjaro hakuna magorofa kaangalie standard ya Maisha ya watu ipo juu kwa mmoja mmoja

Huwezi nidanganya Tanga hata Ukitaja mikoa 20 maskini haipo! Kwa takwimu nnilizo nazo huwezi kuacha shinyanyaz lindi, kagera, mara,mtwara,katavi,singida,tabora,manyara,singida, mwanza,simiyu eti uje kutaja Tanga kuwa na akili timamu
 
Ila Chalamila kaongea kiti kizito hilo.la kupenda kulala lina ukweli kuna mitaa ya akina mama wahaya Dar es Salaam maeneo ya mwananyamala na Tandika nk wana vyumba vingi vidogo vidogo ivina kitanda kimoja kazi wanayofanya kutwa ni kulala tu.Hawana kazi nyingine
 
Back
Top Bottom