Serikali impe angalizo Jerry Silaa, namuona anaiingiza Serikali katika mgogoro mkubwa wa kulipa fidia!

Serikali impe angalizo Jerry Silaa, namuona anaiingiza Serikali katika mgogoro mkubwa wa kulipa fidia!

Yupo sahihi sana mkuu. Kuna mfumo corrupt hata uende mahakaman ni zero. Sasa njia nzur unacheza nao kwa style hiyo hiyo waliyonayo.
Nimemuonesha hapo KESI TATU zinazomhusu huyo kiumbe anayemtetea na zote ni za ardhi, na hizo ni zile zilizo kwenye public domain tu. Sasa by total sijui atakuwa na kesi ngapi.
 
Hili ni funzo,
Tuache kununua maeneo na kujenga mahala kwa uvamizi.

Uko Fanya hivyo ujue itakuja kula kwako ni swala la muda tu utakula hasara.

Kisicho riziki huwa hakiliki.

Tuache kulaumu mkwezi maana nazi imeliwa na mwezi.

Siłaa Ana Hoga ya ni ku enforce sheria na kufanya maamuzi mwenye haki apate haki yake.
Na sio hao Mawaziri wengine wanafiki wasokuwa na maamuzi.
Kwa nini watu wavamiie maeneo?ina maana wizara ya ardhi kuna uzembe sana bado,
 
Katika kitu rahisi sana na cha nafuu ni kupima ardhi,sijui kwa nini hadi leo wanashindwa
 
Siamini mtu akajenge gorofa na nyumbq kali kama ile bila kufatuta kwanza base nzuri ya kisheria kwa kiwanja chake ukizingatia kwa Bongo kila kitu kinawezekana.
Hizo kesi ni nyingi sana nchi nzima ambazo kwa macho yangu ni complex sana. Ile clinic yake ikae kiushauri saidi ya kutenda. Mahakama iachwe kutekeleza wajibu wake.
 
Kiukweli katika waziri ambaye ataiweza hii wizara ni Jerry Silaa. Sababu kibwa anafuata sheria na amesoma sheria. Nimeona mfano wa sheli pale mikocheni kwa Rupia, Sayore na Mama Tibaijuka pale kuna suala la rushwa mpaka kibali kikatoka kisheria cha kujenga sheli.

Jerry ilikuwa ni kuionesha mamlaka kwamba rushwa imefanyika mamlaka zingine zichukue hatua kama Takukuru.

Kuna suala la Tarura kukodisha road reserve na wafanyabiashara kuje ga majumba, showroom za magari, baa, majiko ya chips hii imetokea Msikiti road mikocheni maarufu kama kwa Warioba. Jerry amemuambia mkurugenzi ashirikiane na Tarura waondoe wale waru kwenye road reserve ambayo ilipaswa kuwa njia ya waenda kwa miguu kuna mtu kaweka car wash, baa, chips na takataka zinhinie ikiwemo showroom ya magari.

Jerry silaa anapaswa kuungwa mkono atusafishie mipango miji. Kuna barabara ya tegeta inahitajika iwe na service road kuanzia mwenge mpaka bunju lakini pale kwa ndevu watu wamejenga mpaka mbele ya mawe na notice walishapewa na Tanroad miaka 7 iliyopita ni utekelezaji tuu unakwama wa kuvunja na kupata nafasi ya barabara mana inasemekana mwendokasi inakuja na washaanza kujenga ofisi pale vilima vya Lugalo kambini.

Barabara ya kawe inahitajika NHC anapomaliza ujenzi wa magorofa ya mama samia housing projects basi na kawe isafishwe yote iwe na setvice roads waliojenga mbele ya road reserve wavunjiwe wote bila huruma.

Suala la kumpa mwamposa aende kule nyuma ya shule ya msingi kawe B halikubaliki kwani ataenda kuleta kelele kwa wanafunzi wa shule za serikali na feza kwa ujumla. I efika wakati mwamposa anajiweza atafute eneo lake hata lile alilojimilikisha waziri mabula na mwinyi angepewa mwamposa upande wa Kawe club akatoka kanisa moja kama St peterburg cathedral.

Matumizi ya atdhi ni suala inabidi lizingatiwe bila huruma haiwezekani sasa hivi mbezi ya chini mpaka bahari beach kote ni fremu tuu. Huu sio ukuaji wa uchumi ni uharibifu wa mazingira. Hatuwezi kuwa na eneo moja ni maduka ya nguo tuu kila wilaya na sio kila anayejisikia anajenga fremu mbele.
 
Leo katika taarifa ya habari ya ITV nimemuona Jerry Silaa akisimamia kubomoa ghorofa, na bila shaka kwa kujifanya yeye
Kweli Mkuu,jamaa ajikite kwenye core competency ya kazi yake kusimamia sera.
How come Waziri anazurula mitaani yaani hakimu na jaji ni yeye!
 
Kweli Mkuu,jamaa ajikite kwenye core competency ya kazi yake kusimamia sera.
How come Waziri anazurula mitaani yaani hakimu na jaji ni yeye!
Yaani yeye ni mtuhumiwa wa kutoa hati zote mbili, yeye mwenyewe anaendesha mashtaka, yeye anatoa hukumu, na anaenda na greda kutekeleza hukumu!
 
Nimeona nimeshangaa sana halafu watu wapo ndani yeye anabomoa nje ingekua amri ya Mahakama watu na vitu vitolewe ndio zoezi liendelee nimeona yule mama mwenye nyumba anatia huruma sana,
Hivi viwanja ni vina migogoro kwa sababu ya madalali kufanya yao na hasara unakuja kupata wewe huhusiki na una hati toka serkalini ovyo kabisa!
Kwa nini hadi mishipa inamsimama kichwani wakati kiwanja si chake na yeye anasimamia tu
 
Back
Top Bottom