DOKEZO Serikali isipoingilia kati, kuna siku yatatokea Maafa ya kutisha Mbagala

DOKEZO Serikali isipoingilia kati, kuna siku yatatokea Maafa ya kutisha Mbagala

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Wewe ni mpotoshaji sana!

Hapo wapo kwenye barabara ya mwendo kasi ambayo bado haijaanza kutumika.
Unamtukana bure huyu mleta uzi...kimsingi wafanyabiashara wa Mbagara wengi wao hufanya biashara barabarani kiasi kwamba, magari na vyombo vyengine vya moto hulazimika kutumia njia moja badala ya mbili. Kwakusema ukweli mbali na usumbufu wanaouleta kwa watumiaji wa barabara lakini pia usalama wa wafanyabiashara hawa na watembea kwa miguu upo hatarini.

Kwa upande wangu nadhani, kuna umuhimu wa serikali kuandaa utaratibu mzuri zaidi ili kuondoa changamoto hii. Kwa ujumla, katika eneo hili kuna watu wachache wenye nguvu ni kama wamejianzishia utawala wao. Kikundi hiki cha watu wachache, hukusanya ushuru na kodi kutoka katika vizimba vya wafanyabiashara. Kwa mfano, ile kona ya zamani kuelekea Charambe, pale kila meza ya biashara unayoiona tena ipo barabarani hulipiwa kati ya 3000 hadi 5000 kwa siku (fedha hizi huingia mifukoni mwa watu wachache)

Aidha, Kikundi hiki cha wachache waliojipa madaraka (Godfathers) ndio huwahakikishia ulinzi na usalama wafanyabiashara hawa kwa kutumia sehemu ya fedha wanazokusanya kuzuaia hatari yoyote inayoweza kujitokeza. Kwa mfano, serikali ilipoamua stendi ya magari ya kusini ihamishiwe kijichi, Kikundi hiki kilitumia ushawishi na nguvu walizonazo stendi iliweza kurudishwa Mbagara. Aidha, watu wa Mkuranga walikaribia kunufaika na mvutano huu, hadi kufikia stendi yao (Mwandege Azam) kupata magari mengi sana. Lakini, lilikua suala la muda tuu kabla stendi kurudi Mbagara.

Soko zuri limejengwa pale Zakhem lakini hadi sasa wafanyabiashara wanasuasua kuhamia. Za ndaaani zinasema kwamba, kikundi hiki cha wanufaika wametengeneza mazingira ya kutofunguliwa na hatimaye kutumika (kumbuka kuna kiongozi alikuja kwa ajili ya ufunguzi bila mafanikio).

Sina shaka juu ya utendaji wa Serikali hususani vyombo vya ulinzi na usalama (Ni Imani yangu kwamba, vyombo hivi vimeweza kupandikiza watu kwaajili ya kuendeleza tunu yetu adhimu ya usalama na amani). Lakini wasiwasi wangu ni kwamba, ikiwa vikundi vya namna hii vikiendelea, basi ushawishi wa vikundi hivi unaweza kuhatarisha usalama wa amani.

Katika hali na mazingira tuliyonayo, baadhi ya watu wasiolitakia mema taifa hili wanaweza kutumia vikundi vya namna hii kuhatarisha usalama wa nchi. Hivyo basi, Serikali iendelee kuwa macho na hai wakati wote ili kuzuia mambo ya namna hii kutokea. Aidha, Serikali iwekeze nguvu kubwa kuhakikisha kwamba, biashara hazifanywi katikati ya barabara.
 
Hivi we umewahi kwenda mbagala mbona watu hovyo namna hii, anapotosha nini? Mbagala Zackiem hadi Rangi 3 kwote wafanyabiashala wametapakaa barabarani foleni haiishi yamagali pale iwe j3 hadi j2 foreni yani kutoka Zackiemu hadi Rangi 3. unaweza kutumia saa zima sehemu ya umbali mita kama 400 tu.
Ajabu siku nyingine foleni hadi saa 6 usiku kisa watu wamepanga bidhaa barabarani.
 
Hawa ni wamachinga wakifanya biashara zao barabarani bila kujali hatari inayoweza kutokea.

Ni kweli kwamba kila Mmoja wetu ana haki ya kujitafutia riziki, lakini riziki ya namna hii yaweza kuleta Maafa ya kukumbukwa milele.

View attachment 2792653View attachment 2792670View attachment 2792655


Baada ya Maafa Chalamila ataunda Tume ya Uchunguzi .
Mimi naona wagongwe wafe tuu. Yani wasted life ningekuwa na uwezo ningewatoa kafara niendelee kuneemeka na utajiri ama kuwageuza watumwa kwa kuwafanyisha kazi bure bila malipo.
 
Barabara ya mwendokasi ni kichanja cha kuuzia bidhaa ?

Halafu kuniita Kima ndio kuonyesha wewe ni Mjanja eeeeh ? huku kwetu Tandika matusi ni sehemu ya salamu , ila sasa tukijibu usimlilie mtu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Unamtukana bure huyu mleta uzi...kimsingi wafanyabiashara wa Mbagara wengi wao hufanya biashara barabarani kiasi kwamba, magari na vyombo vyengine vya moto hulazimika kutumia njia moja badala ya mbili. Kwakusema ukweli mbali na usumbufu wanaouleta kwa watumiaji wa barabara lakini pia usalama wa wafanyabiashara hawa na watembea kwa msi, Serikali iendelee kuwa macho na hai wakati wote ili kuzuia mambo ya namna hii kutokea. Aidha, Serikali iwekeze nguvu kubwa kuhakikisha kwamba, biashara hazifanywi katikati ya barabara.
Nina uhakika viongozi wa hilo kundi watakuwa makada wa chama tawala na wanakitumia chama kama ngao yao wafuatiliwe
 
Hawa ni wamachinga wakifanya biashara zao barabarani bila kujali hatari inayoweza kutokea.

Ni kweli kwamba kila Mmoja wetu ana haki ya kujitafutia riziki, lakini riziki ya namna hii yaweza kuleta Maafa ya kukumbukwa milele.



Baada ya Maafa Chalamila ataunda Tume ya Uchunguzi .
Mtu hana hata mia unadhani anawaza kuhusu maisha yake wakati ana njaa. Ukimgonga kwake ni bingo. Mkiandika vitu jiwekeni kwenye viatu vya walengwa sababu Serikali ya CCm haina ubunifu wala uwezo kufanya chochote zaidi ya kulalamika kama mwananchi yoyote.
 
Back
Top Bottom