Ni hatari sana Mkuu.
 
Tanzania hakuna corona. Tuongeze uzalishaji wa mazao ili tuwauzie hao wenye kuteseka na nafaka kwa sasa maana hawatakuwa na chakula mwakani
Akili za kuambiwa changanya na zako, corona ipo chukua tahadhari wewe na familia yako, vueni mashuka ya upumbavu.
 
Inawezekana kabisa nia ya Magufuli ya kufungua uchumi pamoja na kuwa na Corona ni uamuzi mzuri lakini makosa yanayofanywa ni kijiaminisha kwamba huu ugojwa haupo na hauwezi kuingia Tanzania kwasababu huu sio ukweli.

Kuuwaambia Watanzania wanawe mikono, wasishikane mikono ovyo na kuwa mita moja wakati wa kuongea ni muhimu sana. Watanzania ni lazima tujue huu ugojwa ni mbaya zaidi kwa watu wenye kisukari, pumu na wazee wote wenye umri zaidi ya miaka 60. Kibaya zaidi mwezi wa kumi na mbili walikuwa diaspora na wenzetu wengine walisafiri na wakaleta hii Corona inayo enea haraka. Tusifanye hili swala la kisiasa maana hawa wazee ni wetu wote. Imekuwa kisirisiri lakini Agha khan hospital pekee ndiyo wana dawa za majaribio pale oxygen za kutosha na habari nazopata kwa marafiki Madaktari wa pale wagojwa wameongezeka sana hasa wazee na kwa siku kuna wanaolipa milioni mbili kwa kulazwa. Ndugu yangu mmoja wazazi wake wawili walilazwa mama pekee alidaiwa milioni 36 na mzee wake bado yupo kwenye oxygen na inaweza kuwa milioni 40 nyingine na nilijua kwasababu wanapitisha bakuli la kuomba pesa.

Sababu moja wapo tuna wagojwa wacheche wanaojulikana kwetu ni umri Tanzania umri wa kati ni miaka 17-18 wakati US kwa mfano ni karibu miaka 43-44. Huu ugojwa kwa vijana wadogo wanaweza kuumwa mpaka kupona bila hata ya mtu kujua. Watanzania wenye umri wa miaka zaidi ya 64 ni asilimia 3 tu!! hivyo tusishangae wagojwa wanaozidiwa kuwa wachache. Asilimia zaidi ya 80 ya Watanzania ni chini ya miaka 30 na hawa wengi watakuwa sawa hata kama wakipata Corona. Lakini wito wangu ni kulinda wazee wetu.
 
corona hakuna Tanzania, labda useme NEMONIA.
 
Let's call a spade as it is suppossed to be, and not a big spoon of its own kind as per value judgment of some ignorant people.

Madktari wanaongea kwa uwazi na kuthibitisha kisayansi kuhusu kuongezeka kwa tishio na changamoto hii ya gonjwa la mapafu hapa nchini hivi sasa. Wataalamu wa wizara ya afya wanaogopa na kukosa ujasiri wa kufanya hivyo. Sijui tatizo hata ni nini!

Hivi kuna heshima gani ktk kuficha maradhi? Je! Ni uzalendo kuficha maradhi yanatunyemelea kama taifa ili kimmfurahisha mtu mmoja mwenye mamlaka ya kikatiba juu yetu?
 

Kwa kusema haya umetimiza wajibu wako kama binadamu.

Ni bahati mbaya kuwa ugonjwa huu hatari kama ulivyo, umefanywa kuwa ni mtaji wa siasa na mijamaa ya chama fulani pasipo na kujali maisha yanayopotea.

Mijamaa hiyo imejikita katika kuhalalisha hata watu kufa ili tu kumpendezesha bwana mkubwa wao.

Utu umeyatoka kiasi kuwa hawajali maisha ya watu kabisa.

Hadi pale gonjwa hili litakapo mtembelea bwana yule vilivyo kila mwenye domo ana lake la kusema.

Walisema waungwana: "Mwenyezi Mungu si Athumani."

Yetu yanabakia kuwa ni macho hadi siku muafaka itakapofika.
 

Unajua unaruhusiwa kuvaa barakoa na kubakia ndani mwako hadi utapoona hali ni shwari kwa mtazamo mwenyewe? Wengine tushasahau story za corona.
 
Leo nimeona jamaa fulani wakiwa katika gari na wamevaa barakoa..........nilishangaa sana😳😳😳
 
Wakiisha ndio Safi si ni wanaccm hao sasa kuna shida gani wakipukutika na wao ndio wamesema hakuna corona au
 
 
Unajua unaruhusiwa kuvaa barakoa na kubakia ndani mwako hadi utapoona hali ni shwari kwa mtazamo mwenyewe? Wengine tushasahau story za corona.
Unajua unaruhusiwa kuvaa barakoa na kubakia ndani mwako hadi utapoona hali ni shwari kwa mtazamo mwenyewe? Wengine tushasahau story za corona.
Utakumbuka tu ukipitiwa na upepo wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…