Serikali kutodhibiti idadi ya wageni wanaoingia nchini kwa kisingizio cha Utalii, inahatarisha Usalama wa Taifa dhidi ya virusi vya Corona

Hivi kwanini wapinzani hamuendi WHO kuomba tunyimwe vipimo vya korona kama mlivyofanya kwa fedha za world bank.
 
Yani hapa nina hasira nahisi kupasuka kwann wamefanya uzembe kiasi hiki? taifa masikini linaangamia hili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uwezo wangu wa kuwajibisha ni huyu waziri. Kwa sababu ilikuwaje mashine au watu aliowaweka Airport KIA hawakuweza kumtambua mkonjwa? Wsngapi wamepita bila kugundulika? Na hao wazungu wa leo waliogundulika wamepita wapi? Maafisa wa afya walikuwa wapi?
 
Hujui usemalo, mwenye mamlaka ya kufynga mipaka ni rais peke yake, Ummy ana kazi yake ya kupambana na gonjwa na kutoa elimu.
Unafikiri kwani Majakiwa amefunga shule na si Ymmy?
Kila mamlaka ina mipaka.
Ummy hatatumbuliwa kwa hili labda patokee uzembe katkika kudhibiti humu ndani au namna wanavyo handle wagonjwa na sio Ishu ya mipaka. malisoka,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Apishe watu wengine. Na jukumu la kudhibiti corona airport la waziri mkuu au la Ikulu.

yeye ndiye mwenye dhamana ya afya ya watanzania.

Ajitokeze atolee ufafanuzi basi.
 
Kulikua hakuna haja ya kupoteza mda kwa kusubirii case ziongezeke sema wanahofia uchumi ila kwenye afya za watu ni kuamua a tu

Kinachofanyika nchi zilizo athirika sana ndo cha kufuata kwa sisi ambao athari bado hazijawa kubwa sio kusubirii

Waziri mkuu najua unasoma hii comment na zingine embu funga viwanja vya ndege na bahari na mpaka iwekwe uangalizi wa hali ya juu pia vichochoro vipo vingi tanzania hasa mipakani kuna fake entries nyingi kuliko hata iyo halali tafadhali ongezeni surveillance

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe dogi koko, unafanya mzaha kwenye janga kama hili!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna jambo dogo inapokuja swala la maslahi ya Taifa, ni wakati sasa wapinzani mkajifunza kufanya siasa za kistaarabu na sio kupenda kutafuta sifa kwa mambo yasiyokuwa na tija.
 
ummy hana shida katika hili, hao wakubwa zake ndo wakulaumiwa zaidi na ikiwezekana wajitumbue kabisa
 
Lakini kumbuka kuna watu wanatoka ktk nchi ambazo hazijagundua uwepo wa coronaV lakini wananchi wake tayari wameambukizwa na wakija Tz wanatuletea! Kama ni kufunga ilitakiwa siku ya kwanza tu china walipogundua uwepo wa corona, na tena ni mipika yote bila kujali chochote. sasa kama nchi, tunaweza kweli kujipiga pin wenyewe kiasi hicho kwa muda mrefu! Hamtaanza tena kulalama na kumtukana Magufuli?
Ninyi haohao mnaojidai kuwa mafundi wa kushauri mipaka ifungwe ndio walewale ambao mngeanza kukashifu hatua za kufinga mipaka yote. Kwa maana ninyi mnajiona mnajua vyote na hivyo wa wakosoaji wa vyote! Mungu tunaomba utunusuru sisi watanzania na taifa letu ktk janga hili la coronaV, amen!
 
Usilolijua n sawa na usiku wa Giza. Huwezu kuzuia kuingia watu kisa umepata watu watatu...huu ugonjwa upo Kama upepo tu kunawakat utakatka wenyewe na sio kisa kufunga mipaka...saiv nchi nying n msimu wa barid na hata huko dubai saiv bard ipo kwaiyo huku kwetu hao waliopatikana ni ngumu Sana kusambaza kwa watu wengine Kama ilivyo nchi nyingne

Ebola ilitokea Africa na bado dunia haikuzuia waafrika kwenda kwenye nchi zao walichofanya ni kuimarisha upimaji wa wasafr
 
Serikali zingatia huu ushauri kabla hayajawa makubwa
 
Hata wewe unaweza ukaenda
Nawakumbusha wahusika wajibu wao, wanafahamu ila wanajifanya kusahau, kwa bahati mbaya sisi hatusahau tunakumbuka matendo yao ya kifedhuli. Wasijifanye kutupenda sasa.
 
Wahusika wa usafirishaji ndo wanatakiwa wasimamie hili,nadhani hii hoja hata wao washajadili na wakaamua waache tuukwae huo ugonjwa,ila ummy hausiki moja kwa moja kwenye mamlaka ya anga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ummy nafkiri anaingizwa kwenye lawama zisizomuhusu hata chembe! Mfano anapata wapi mamlaka ya kuzuia wasafiri kuingia ilhali yeye ni waziri wa afya tu? Au hujui mamlaka hayo yupi ni muhusika? Ni kama kumlaumu mkeo kwa nini hajapika chakula na hali hujaacha fedha ya manunuzi ya chakula hicho!!! Ahsante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtanzania gani ameuawa au amekufa!?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…