Wanajamvi, kama heading inavyojieleza, naona kuna mizaha sana kwenye hili suala la Corona! Na zaidi ni kwenye kuhusiana na lockdown.
Kiukweli naona tumechelewa sana. Lakini bado haina maana tuendelee na utaratibu huu wa sasa. Kwasababu mataifa ya hao wenzetu yanaanza kupata unafuu. Wamepambana, lakini wamepoteza watu!
Tukiendelea hivi, maambukizi yakizidi, nchi yetu itatengwa na hao watalii hawatakanyaga zaidi ya kubeba rasilimali tu. Pia watauzungumzia uzembe wetu.
Natoa tahadhari tu. Kuhusu ya kufanya tumeshauri sana.