Serikali msijisahau katika hili la daktari kumtibia mtu wa jinsia tofauti na yeye

Serikali msijisahau katika hili la daktari kumtibia mtu wa jinsia tofauti na yeye

Mkuu ili haya yasiwe madai tuwekee ushahidi hapa wa hayo uliyoyasema ili tupate faida isiwe inaishia kwemye kudai tu mkuu
Mimi nimeenda kupima vipimo na dr wa kiume pembeni yangu alikuwepo nurse mwanamke, na Hadi kwenda theatre hyo ni lazima nurse wa kike awepo na hyo ya kuchunguliwa haina mashiko
 
Ulikuwa wap kumuelekeza ndugu yetu mpka anakurupuka ivooo
Atakuwa hajui labda hajawahi kwenda hospital na anasikiliza story za vijiweni Ila Dr akiwa anafanya Jambo la vipimo, kupima sijui nini nurse wa kike yupo pembeni
 
Kigezo kinachoangaliwa pale ni ujuzi na sio jinsia.

Anaweza akawa daktari jinsia ya kiume ndio ana weledi na hiyo kazi kuliko hawa assistant nurse ambao kazi yao ni kufuata maelekezo nini wafanye kutoka kwa huyo daktari bingwa.

Sasa We utakubali kumuacha dada yako au mama yako asifanyiwe operation azae eti kwasababu ya daktari kua ni mwanaume?
 
Aisee mi napenda kuhudumiwa dr wa kike....

Nakumbuka mwaka 2010 nilienda hospitali moja kkoo nko na ishu flani sehemu nyeti kavaa gloves zake akawa ananikagua mnara ukaanza kusoma kwa mbali akaniambia acha umalaya wewe[emoji23][emoji23]
Ulikuwa Unaumwa Kweli? Hisia Zinatoka Wapi Hapo..Hahaha Dada Alikuwa Sahihi
 
Hivi umeelewa hoja ya mtoa mada?

Mtoa mada analalamika mgonjwa kutibiwa na dk asiye wa jinsia wa jinsia yake wewe unasema sheria zipo zinataka kama mgonjwa ni ke na dr ni me basi awepo na dr/nesi wa kike,sasa huyo nesi wa kike atazuia vp dr wa kiume kumchungulia mgonjwa?

Hio sheria kama ipo basi itasaidia unyanyasaji wakijinsia ila mambo mengine kama kuchungulia hio sheria itasaidia vipi?

Nikuulize swali,hivi endapo ikitokea mama wa dr wa kiume ni mjamzito je huyu dr wa kiume anaweza kumzalisha mama yake chini ya uwepo wa dr/nesi wa kike?

Kwavyovyote dr ataomba ma dr wenzake wamzalishe mama yake kwani kwa utamaduni wakiafrika sio heshima.

Sasa inakiwaje vi dr vidogo vinapata ujasiri wakuchungulia wamama wenye rika sawa na mama zao?
Hiyo ni conflict of interest.Atakuja dr mwengine wa kiume atamzalisha mama wa huyo dr.
 
Atakuwa hajui labda hajawahi kwenda hospital na anasikiliza story za vijiweni Ila Dr akiwa anafanya Jambo la vipimo, kupima sijui nini nurse wa kike yupo pembeni
Dr ndo wanaongoza kupendwa na wamama wanaokuja kujifungua .hawapendi manurse coz wana lalama hawana huruma, wanawafinya na mengineyo ambayo sina ushahidi kama kesi ya mzazi ikiwa ngumu wakati anajifungua mama mjamzito lazima aitwe daktari kuisolve tatizo sasa huyu ana bwabwaja ovyo na dada yake kakimbia sayansi kaenda arts anataka ifanyike anavyo waza yy
 
Hata tubishane mpaka kesho, nasema "DAKTARI/MUUGUZI WA JINSI TOFAUTI HASA MWANAUME, AMUHUDUMIE MGONJWA PALE INAPOLAZIMU SAAAAANA." Binafsi nafurahia pale napohudumiwa na mwanaume mwenzangu (ila isiwe ile ya kutafuta mshipa wa damu kwenye makalio[emoji3][emoji3][emoji3]) kuliko mwanamke. Japo kwa utafiti usio rasmi, wanawake ndio wanaonyanyasika katika hili. Sisi wanaume wengi wetu hufurahi pale anaposhikwashikwa na nesi "ke" hasa kama nesi amejaziajazia tabia.
 
Mimi nimeenda kupima vipimo na dr wa kiume pembeni yangu alikuwepo nurse mwanamke, na Hadi kwenda theatre hyo ni lazima nurse wa kike awepo na hyo ya kuchunguliwa haina mashiko
Kuwepo nesi wa kike pembeni bado sio ishu.

Mbona polisi wa kike anapomkagua mtuhumiwa wa kike haitakiwi polisi wa kiume awepo bali huwa ukaguzi unafanyikwa wakiwa wawili tu ?
 
Atakuwa hajui labda hajawahi kwenda hospital na anasikiliza story za vijiweni Ila Dr akiwa anafanya Jambo la vipimo, kupima sijui nini nurse wa kike yupo pembeni
Mkuu sio kweli kwamba hospitali zote hufanya hivyo.

Lakini hata kama wanafanya bado sio suluhisho zuri kwa jambo hili
 
Kigezo kinachoangaliwa pale ni ujuzi na sio jinsia
Hilo ni tatizo,haiwezekani kwenye kazi zingine jinsia ziangaliwe alafu katika udaktari jinsia isiangaliwe it's totally wrong.

Iamagine katika upolisi jinsia hutazamwa ndio maana polisi wa kike atamfanyia upekuzi mtuhumiwa wa kike pekee,mbona hapa haisemwi kuwa kinachoangaliwa ni ujuzi wa kupekua tu hivyo hata mwanaume apekue tu pale na jinsia inaangaliwa ?

Ujuzi lazima uendane na jinsia huu ndo ustaarabu,linapofika suala la kutibu jinsia lazima iangaliwe nayo.
Anaweza akawa daktari jinsia ya kiume ndio ana weledi na hiyo kazi kuliko hawa assistant nurse ambao kazi yao ni kufuata maelekezo nini wafanye kutoka kwa huyo daktari bingwa.
Solution ya kudumu ni kuzalisha madaktari wengi wa kike ambao nao watakuwa na ujuzi.
Akini hasa hasa uzi wangu ulilenga hospitali ambazo madaktari wa kike wapo lakini wanaume ndo huwa wanatibu hata wale wagonjwa wa kike.

Ikiwa ugonjwa huo anaeweza kutibu ni dokta wa jinsia tofauti na mgonjwa basi uzi wangu wala haukukataa kutibiwa.
Sasa We utakubali kumuacha dada yako au mama yako asifanyiwe operation azae eti kwasababu ya daktari kua ni mwanaume?
Labda niseme kuwa hukuelewa uzi,na hili ni tatizo la sisi wana jf.

Kumbuka niliposema 👇👇
Yani utakuta hospitali kuna madaktari wa jinsia nyingi lskini mwanamke anatibiwa na mwanaume au kinyume chake.

Serikali isomeshe watoto wengi wa kike ili kuja kuepusha hii aibu,ipunguze vigezo vya kusomea udaktari kwa mwanamke hasa kwa mambo ya kawaida haya ambayo hayahitaji kujitoa sana wanawake wasomeshwe waje kuzalisha wanawake wenzao.
Hapo ukisoma utagundua nimemaanisha kuwa hospitali ama sehemu ambazo hazina daktari jinsia sawa na mgonjwa basi sijasema kuwa asitibiwe.

Na kusomesha watoto wa kike wengi ni solution ambayo nimeitoa ili hata mama yangu au ndugu yangu akitaka kufanyiwa operation basi amkutedaktari wa kike ambaye yuko na utaalamu huo.

Kuna hospitali moja iko ilala pale kuna mama mmoja ni mtaalamu mzuuri tu anazalisha na kufanya operation kubwa tu,huyu kaweza kuwa mtaalamu na wengine pia wanaweza ni jambo la kuwekeza juhudi tu
 
Wakuu naomba niipongeze serikali kwa jitihada zake inazofanya katika kuhakikisha ile heshima ya jinsia zote inalindwa.

Tukiangalia katika majeshi hasa jeshi la polisi utakuta kuna askari wa kike ambao kama itatokea muhalifu ni mwanamke basi askari yule hakuajiriwa kwa bahati mbaya bali hiyo itakuwa ni kazi yake kumpekua sehemu za mwili wake.

Hali kadhaalika mwanaume atapekuliwa na askari wa kiume katika kulinda heshima.

Hata mashuleni kuna waalimu wa kike kibao ambao wao watashughulikia masuala mbali mbali ya wanafunzi wa kike.

Mbona sioni suala hili la kuheshimu jinsia na kulinda heshima ya mtu likifanyika na kusisitizwa katika kada ya afya ?

Kwa nini isiwe kosa daktari wa kumtibia mgonjwa wa jinsia tofauti na yeye ikiwa katika hospitali hiyo ama maeneo hayo kuna daktari mwenye jinsia sawa na mgonjwa ?

Kama ambavyo polisi haruhusiwi kumfanyia upekuzi wa mwili mtu wa jinsia isiyekuwa yake wakati wa jinsia yake wakiwa pale hii ni kosa,vipi isiwe kosa katika hii kada ya afya ?

Yani utakuta hospitali kuna madaktari wa jinsia nyingi lskini mwanamke anatibiwa na mwanaume au kinyume chake.

Serikali isomeshe watoto wengi wa kike ili kuja kuepusha hii aibu,ipunguze vigezo vya kusomea udaktari kwa mwanamke hasa kwa mambo ya kawaida haya ambayo hayahitaji kujitoa sana wanawake wasomeshwe waje kuzalisha wanawake wenzao.

Chumba cha kuzalisha kuna madaktari wa kike watano na wa kiume mmoja,huyu wa kiume anatafuta nini,kwa nini isiwe kosa kisheria?
Wewe ni mtu mpumbavu sana kuwahi kutokea.
Kama unaona una wivu na mwenzi wako mtibu wewe.
Nirudie tena wewe ni bogus.
 
Tumechelewa Sana Ndugu Zangu
Nasema Uongo Ndugu Zangu
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Mimi nimeenda kupima vipimo na dr wa kiume pembeni yangu alikuwepo nurse mwanamke, na Hadi kwenda theatre hyo ni lazima nurse wa kike awepo na hyo ya kuchunguliwa haina mashiko
Waeleze hawa vilaza wa nchi ya Tanzania
 
Kama mteja/mgonjwa wa kike wa hao madaktari, Basi nachagua kuhudumiwa na daktari mwanaume, unakuwa mikono salama zaidi kuliko hizo za kujiita madaktari wa kike, kifo nje nje Yani sitaki kuwasikia kabisaaa
 
kama umeliona hilo basi acha kugegeda na kuwapa mimba wanafunzi wa kike, waache watimize ndoto zao.
 
Back
Top Bottom