Serikali: Sasa ni ruksa kusafirisha wanyama nje ya nchi

Serikali: Sasa ni ruksa kusafirisha wanyama nje ya nchi

Acha ujinga. Wanyama huwa wanaongezeka Sana hivyo huhitaji kuvunwa. Wakivunwa wakauzwe huko duniani. Wewe wa Kantalamba huko huna hata faida kwenye mbuga kwenyewe huwa huendi
Wanyama wakiongezeka - maduka ya nyama pori yamepotelea wapi? Ulaji wa nyama pori unaweza kuwa kivutio cha utalii nchini, huko wanakopelekwa nje ya nchi - labda wanaenda kuliwa kama chakula adimu na kivutio cha utalii huko nchi za wenzetu! Hii iwe fursa kwa Watanzania kula nyama pori.
 
Sheria ilitugwa 2009 wewe unaona imetugwa Leo?.Na unaelewa nini ukisikia ruhusa ilitolewa ni ya miezi 6 tu?.Ulitaka hao wafanya biashara ambao tayari zuio la Magufuli lilikuja wakati tayari kwenye vitalu vyao kuna wanyama, wawapeleke wapi na ili hali serikali haikuwa tayari kuwachukua wanyama na kuwarudishia wafanya biashara gharama zao?.
Hata kinana alipata hasara kuvuna tembo naye apewe kibali amalizie kusafirisha mzigo wake
 
Mpaka sasa ni hofu na mashaka tu maana ni kama yale yeliyotokea kipindi cha awamu ya nne kiasi cha Twiga ambae ni alama ya taifa letu kusafirishwa mchana kama anasafiri kumbe anaibiwa sasa yanaanza kurejea

Mbaya zaidi yanatengenezewa mazingira ya nguvu ili yawezekene kufanyika. Sasa vibari vya kusafirisha wanyama pori vitaanza kutoka na hapa ndipo taifa letu litaukizwa.[emoji116]View attachment 2250732
Huko nyuma Twiga walipanda ndege mchana kweupe na sasa ndio huenda yakaenda kujirudiahttps:

[emoji116]
Mwananchi › kitaifa
Maige asisitiza kutohusika wizi wa twiga - Mwananchi
Sheria ilitugwa 2009 wewe unaona imetugwa Leo?.Na unaelewa nini ukisikia ruhusa imetolewa ya miezi 6 tu?.Ulitaka hao wafanya biashara ambao tayari zuio la Magufuli lilikuja wakati tayari kwenye vitalu vyao kuna wanyama, wawapeleke wapi na ili hali serikali haikuwa tayari kuwachukua wanyama hao na kuwarudishia wafanya biashara gharama zao?.
 
Sheria ilitugwa 2009 wewe unaona imetugwa Leo?.Na unaelewa nini ukisikia ruhusa imetolewa ya miezi 6 tu?.Ulitaka hao wafanya biashara ambao tayari zuio la Magufuli lilikuja wakati tayari kwenye vitalu vyao kuna wanyama, wawapeleke wapi na ili hali serikali haikuwa tayari kuwachukua wanyama hao na kuwarudishia wafanya biashara gharama zao?.
Hujaelewa nina maana gani.
 
Dah! Sasa mbona tena mama anatuvua nguo watetezi wake? Maana nilianza kumpenda kumbe dah yajayo yanafurahisha.
SGR dar - moro iko asilimia 98 itaanza kaxi mwaka 2025.
Bwala la nyerere liaanza kazi mwaka 2030.
Daraja la busisi litaanza kazi mwaka 2027.
Riziwani kikwete atakuwa waziri mkuu mwaka 2025.
Mbowe atakuwa makamu wa pili wa Rais mwaka 2025.
Kuwa mpole mkuu bado maza ajakuvua nguo ndio anaanza sasa
 
Hata kinana alipata hasara kuvuna tembo naye apewe kibali amalizie kusafirisha mzigo wake
Ndiyo apewe.Ingekuwa wewe ni sehemu ya muhathika wa hili,ungeona ni sawa tu kupoteza milioni zako kadhaa ili hali ilifuata sheria ya kupata hicho kibali?.
 
Huyo mjinga hajui hata hao tausi na sisi pia tulipewa zawadi? Hii mitoto inayotokana na zao lakifisadi imelaaniwa haijitambui kabisa
MATAGA mna shida mmeumia kusafirisha wanyama huku hamuoni upumbavu mnaofanya wa kuiba kura mchana kweupe.

Cursed minds.
 
J
Meli yake ishafanyiwa service ya nguvu ipo tayari kwa utekelezaji
Jamaa ni shida sana kwenye tembo. Kuna kundi la wasomali liko arusha na linaishi njiro karibu na kwa bwana yule.
Ila wana sura inayofanana naye bwana yule. Sasa kuna makontena yanafungwa huko njiro serikali fuatilieni.
 
Ngoja mama watafutie hela
Mkiongezwa posho mnashangilia
Wakiajiri mnashangilia
Mkiongezwa mishahara mnashangilia
Wanafunzi wote wakipatiwA mikopo ya elimu ya juu mnashangilia

Sasa pesa zinatoka wapi?

Je ni bora kuwa na wanayama maporini huku mnakufa njaa?
Kwamba Mnyamapori azeeke hadi ajifie ndo tufurahi?

Wauzwe tupate pesa!
Hii ni biashara na watu watapata pesa.

Maisha ni biashara, biashara yenye akili.
Siyo kupinga tuu under Emotional attacks.

Mama piga kazi
 
J

Jamaa ni shida sana kwenye tembo. Kuna kundi la wasomali liko arusha na linaishi njiro karibu na kwa bwana yule.
Ila wana sura inayofanana naye bwana yule. Sasa kuna makontena yanafungwa huko njiro serikali fuatilieni.
Wasomali kwa biashara za magendo ndo wenyewe wanazijua border zote za kupitisha magendo.

Kariakoo niliwaona wanatumia school bus wamejaza lap top na computer equipments wanapakua kwenye store zao
 
Re- again
Duh, namkubali mama kwa mambo mengi ila hili lakuuza wanyama wetu nje hapana kwa kweli, huu ni urithi wetu tunatakiwa kuulinda kwa hali na mali,!!

Wazungu wakitaka kuona wanyama wa asili fulani ijulikane wapo Tanzania na sii vinginevyo!!

Hii sijaelewa kwa nn wameamua kufanya hivyo, ila siyo sahihi hata kidogo!! They should re think about it again!!
 
View attachment 2250921Hali iko hivyo, tunaelekea kule 7kule tulipotoka, sasa ni rasmi twiga wetu wataanza kupandishwa ndege tena kwenda Ughaibuni.



_______________


Wafanyabishara sasa huru kusafirisha wanyama Pori kutoka Tanzania

Marufuku hiyo imeondolewa kwa muda wa miezi sita ambapo wafanyabiashara watakuwa huru kusafirisha nje wanyama pori kuanzia Juni 6 hadi Desemba 5

Tanzania imeondowa kwa muda marufuku ya usafirishaji wanyama pori iliyokuwa imewekwa miaka sita iliyopita kwa lengo la kuwalinda wanyama pamoja na ndege katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Uamuazi wa kuondolewa marufuku hiyo kwa kipindi cha miezi sita kumewaibua watetezi wa mazingira na wanyama pori kutowa mwito kuwepo michakato ya ufuatiliaji kuwalinda wanyama dhidi ya ujangili ambao umepunguwa kwa kiasi.

Mamlaka ya wanyama pori nchini Tanzania ijumaa ilitowa taarifa ikisema serikali imekuwa ikitathmini biashara ya usafirishaji wanyama pori hai tangu ilipowekwa marufuku hiyo na hivi sasa imeamua kuondowa marufuku hiyo.

Taarifa hiyo imebaini kwamba wafanyabiashara watakuwa na kipindi cha miezi sita kuanzia Juni 6 hadi Desemba 5 kumaliza kuuza wanyama waliokuwa wamebakisha walioshindwa kuwauza wakati marufuku hiyo ilipokuwa ikitekelezwa.

Tanzania iliweka marufuku ya kusafirisha wanyama pori mnamo mwaka 2016 chini ya utawala uliopita uliokuwa ukiongozwa na hayati rais John Pombe Magufuli ambaye namna yake ya uongozi ilimfanya apachikwe jina la ''Bulldozer''.

Wakati huo serikali ilihalalisha marufuku hiyo kwasababu ya dosari zilizokuweko kwenye biashara,ikiwemo usafirishaji nje wa wanyama wanaolindwa.

Rais wa sasa wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan ameamua kujitenga na baadhi ya sera zilizokuwa zikifuatwa na mtangulizi wake,tangu alipoingia madarakani mwaka jana kufuatia kifo cha ghafla cha Magufuli.

WWF: Uamuzi huo usifute mafanikio yaliofikiwa

Shirika la kutetea mazingira na wanyama pori la WWF limetahadharisha kwamba kuondolewa kwa marufuku hiyo hakupaswi kuyaondowa mafanikio yaliyopatikana katika kuwalinda wanyama pori,na kuchochea kurudi hatua kama ujangili ambao umeonekana kupungua.

Amani Ngasuru ambaye ni mkurugenzi wa WWF nchini Tanzania ameliambia shirika la habari la AFP kwamba mifumo ya uhakika ya ufuatiliaji inahitajika pamoja na data kuenda sambamba na maamuzi kama yaliyofanyika.

Tanzania inafahamika kwa fukwe zake za kuvutia katika visiwa vya Zanzibar,lakini pia matembezi ya safari ya kutazama wanyama pori pamoja na mlima mrefu barani Afrika,Kilimanjaro,yote hayo yakiwa vivutio vikubwa kwa watalii.

Mnamo mwaka 2010 kiasi wanyama 116 pamoja na ndege 16 baadhi wakiwa ni wanyama wanaotakiwa kulindwa walisafirishwa kutoka uwanja wa ndege wa Kilimanjaro,huko kaskazini mwa nchi hiyo kwa ndege ya shirika la ndege la Qatar.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani ya Tanzania, miongoni mwa wanyama hao walikuwemo twiga wanne, aina chungunzima ya paa,na ndege aina ya Tai.

Mwandishi:Saumu Mwasimba

Mhariri:Hawa Bihoga
 
View attachment 2250921Hali iko hivyo, tunaelekea kule 7kule tulipotoka, sasa ni rasmi twiga wetu wataanza kupandishwa ndege tena kwenda Ughaibuni.



_______________


Wafanyabishara sasa huru kusafirisha wanyama Pori kutoka Tanzania

Marufuku hiyo imeondolewa kwa muda wa miezi sita ambapo wafanyabiashara watakuwa huru kusafirisha nje wanyama pori kuanzia Juni 6 hadi Desemba 5

Tanzania imeondowa kwa muda marufuku ya usafirishaji wanyama pori iliyokuwa imewekwa miaka sita iliyopita kwa lengo la kuwalinda wanyama pamoja na ndege katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Uamuazi wa kuondolewa marufuku hiyo kwa kipindi cha miezi sita kumewaibua watetezi wa mazingira na wanyama pori kutowa mwito kuwepo michakato ya ufuatiliaji kuwalinda wanyama dhidi ya ujangili ambao umepunguwa kwa kiasi.

Mamlaka ya wanyama pori nchini Tanzania ijumaa ilitowa taarifa ikisema serikali imekuwa ikitathmini biashara ya usafirishaji wanyama pori hai tangu ilipowekwa marufuku hiyo na hivi sasa imeamua kuondowa marufuku hiyo.

Taarifa hiyo imebaini kwamba wafanyabiashara watakuwa na kipindi cha miezi sita kuanzia Juni 6 hadi Desemba 5 kumaliza kuuza wanyama waliokuwa wamebakisha walioshindwa kuwauza wakati marufuku hiyo ilipokuwa ikitekelezwa.

Tanzania iliweka marufuku ya kusafirisha wanyama pori mnamo mwaka 2016 chini ya utawala uliopita uliokuwa ukiongozwa na hayati rais John Pombe Magufuli ambaye namna yake ya uongozi ilimfanya apachikwe jina la ''Bulldozer''.

Wakati huo serikali ilihalalisha marufuku hiyo kwasababu ya dosari zilizokuweko kwenye biashara,ikiwemo usafirishaji nje wa wanyama wanaolindwa.

Rais wa sasa wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan ameamua kujitenga na baadhi ya sera zilizokuwa zikifuatwa na mtangulizi wake,tangu alipoingia madarakani mwaka jana kufuatia kifo cha ghafla cha Magufuli.

WWF: Uamuzi huo usifute mafanikio yaliofikiwa

Shirika la kutetea mazingira na wanyama pori la WWF limetahadharisha kwamba kuondolewa kwa marufuku hiyo hakupaswi kuyaondowa mafanikio yaliyopatikana katika kuwalinda wanyama pori,na kuchochea kurudi hatua kama ujangili ambao umeonekana kupungua.

Amani Ngasuru ambaye ni mkurugenzi wa WWF nchini Tanzania ameliambia shirika la habari la AFP kwamba mifumo ya uhakika ya ufuatiliaji inahitajika pamoja na data kuenda sambamba na maamuzi kama yaliyofanyika.

Tanzania inafahamika kwa fukwe zake za kuvutia katika visiwa vya Zanzibar,lakini pia matembezi ya safari ya kutazama wanyama pori pamoja na mlima mrefu barani Afrika,Kilimanjaro,yote hayo yakiwa vivutio vikubwa kwa watalii.

Mnamo mwaka 2010 kiasi wanyama 116 pamoja na ndege 16 baadhi wakiwa ni wanyama wanaotakiwa kulindwa walisafirishwa kutoka uwanja wa ndege wa Kilimanjaro,huko kaskazini mwa nchi hiyo kwa ndege ya shirika la ndege la Qatar.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani ya Tanzania, miongoni mwa wanyama hao walikuwemo twiga wanne, aina chungunzima ya paa,na ndege aina ya Tai.

Mwandishi:Saumu Mwasimba

Mhariri:Hawa Bihoga
 
Back
Top Bottom