Serikali: Sasa ni ruksa kusafirisha wanyama nje ya nchi

Sasa ile royal tour ilikuwa ya kazi gani kama hao wanyawa mnaotaka waje wawaone na mpate hela mnawauzia huko

Waje huku kwa kazi gani!?

Unajua sisi wa waafrika wapumbavu sana

Kuna mambo huwa yanakera

Tukiwahoji hivi mnasema tunapinga pinga kila kitu.

Nauliza royal tour ilikuwa kwa kazi gani!?

Nafikiri kuwa muafrika ni kazi ngumu!?
 
Wakitangaza kuuza visiwa mnitag wazee maana hela zipo
Najua ntauzia kwa bei kama bure maana wapo wenye tamaa ntawapata tu
Hata hao Twiga watapelekwa kwa makaratasi kuwa wameuza Kasuku
 
Mimi mwenyewe najiuliza hili!?

Nchi ya ovyo sana hii.

Wanawaza hela tu hawajui kuna vitu ni national treasure na generational wealth
 
Ipo siku Kuna mtu atakuja kulipua hii nchi kwa huu upuuzi maana hii serikali imetuona wananchi hatuna athari yoyote wanatuona kama maiti, nasisi vijana tumezubaa mnooo mpaka najiuliza usomi wetu uko wapi sasa kama uhuni huu tu nakaa kimya yaani
 
Unaijue effect yake kwenye sekta ya utalii nini? Royal Tour ilikuwa basi ni kupaka upepo rangi tu!!
Inaweza kufanyika cost benefit analysis kuona kama ina athari zozote japo watalii lazima waje huku kipindi cha baridi kule kwao.
 
Kwa Nini wasisafirishe Mbuzi na ngombe lakini wasafririshe wanyama wetu ambao ni urithi wetu Kwa vizazi vyote.

Kwa Nini wasiwachinje hapa hapa nchini? Yani tunauza wanyama hai lakini mabeberu wanatuzuia kuuza pembe za wanyama waliokufa.
 
Maneno mazito sana. Hawa Wahindi wanaojiita WaTZ naona kama wanatuhujumu hivi? Na ndiyo hao wafadhili wa vyama, wapo kila sekta nyeti. Hivi kwa nini wanaaminiwa kijinga hivi?
 
ni kweli,...
Wengi wanapinga kwa kigezo cha utalii bila kufanya utafiti wowote. Watalii huku lazima waje kwao kunapokuwa majira ya baridi au joto kali (middle east)

Inaweza kufanyika cost benefit analysis kuona kama ina athari zozote.

Kama kuuza kunaleta fedha za maana hakuna tatizo kama wanyama wapo wengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…