Serikali: Wanafunzi waliopata mimba kuendelea na Masomo katika mfumo rasmi

Serikali: Wanafunzi waliopata mimba kuendelea na Masomo katika mfumo rasmi

Watakuwa kwenye mfumo wa elimu ya watu wazima na shule zao zimeshaandaliwa na walimu wanaajiliwa Sasa ila naona wametumia kauli hiyo Ili wasijione wametengwa ila shule watakazosoma ni elimu ya watu wazima watakuwa wanaelekezwa wakifika shule.
Waziri kashasema, wewe nani mpaka uanze kuediti?
 
Kumbe jiwe alikuwa anawaudhi watu wa karibu yake., leo alichokisimamia kinapingwa wazi waz dadadeki
 
Nafikiri sera ya elimu nazo zitabadilishwa ili kutoa ruhusa ya Mama mwanafunzi kupewa ruhusa ya kwenda kunyonyesha au kuja na yaya wao shuleni hii ni kwa ajili ya welfare ya mtoto na haki ya mtoto ambazo hazijali mama kaolewa, ni mfanyakazi, mwanafunzi au hana kazi ila mtoto anahitaji huduma na upendo wa mama na kuondoa adhabu ya viboko kwa mama mwanafunzi
Itungiwe sheria
 
Tunatumia muda mwingi kupromote na kutetea mambo ya hovyo kwenye jamii.

Yani asiyefuata maadili anaenda kuchanganywa na wanaofuata maadili baada ya miaka 10 wote unakuta wameoza.

Wamemwandaa nani wa kuacha shughuli zake alee hao watoto watakao zaliwa na kuachwa na wazazi wao? Maana baba ataenda jela miaka 30 na mama atarudi shule.

Muda si mrefu na haki ya vilainishi itaruhusiwa
 
Hayati Magufuli akifufuka leo atahisi alikufa miaka 100 ilopita..mana hii U turn inayopigwa na wapambe zake hawezi amini.

Siasa za bongo bila unafiki huwezi ziishi.

#MaendeleoHayanaChama
Mabinti sasa Ngono kama ubuyu, hawatakuwa na wasiwasi tena.
Ruhusa hii inahitaji Tahadhari sana
 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari watakaokatisha masomo yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro, mimba na changamoto mbalimbali za kifamilia watapewa fursa ya kurejea Shuleni katika mfumo rasmi.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hii leo akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya Sekta ya elimu katika kipindi cha miaka 60 "leo natoa waraka wa elimu ambao utaelezea ni lini Wanafunzi watakaokatisha masomo kwa sababu ya mimba na changamoto nyingine watapaswa kurejea Shuleni, leoleo natoa waraka hakuna kupoa, zege halilali"

Wizara ya Elimu inaelezea mafaniko yake ndani ya miaka 60 ya Uhuru kwa kutumia hashtag ya "Tunaboresha Elimu yetu"

My Take
Kama mnakumbuka tuliishauri sana serikali na maamuzi haya ya hovyo,ikakaza shingo. Waziri Ndalichako alikuwepo, mama Samia alikuwepo. Kwa mantiki hii Waziri anatakiwa ajiuzuru kwa kutokuwa na msaada wowte katika nchi ukizingatia kuna wanafunzi wameshaadhirika.
Unawaonea bure, nchi hii ilikuwa ni mali binafsi ya shetani kutoka Chato.

Huyu Mama Samia alitaka kujiuzuru wazee wakamsihi avumilie, ndio sababu leo ana mamlaka kamili ndio anarekebisha damage iliyofanywa na yule chizi mjaalaana.

Mwacheni mama arekebishe nchi, tena swala hili lilisababisha tunyimwe fund za elimu kwa ajili ya ukaidi wa mpuuzi mmoja tu.
 
Hayati Magufuli akifufuka leo atahisi alikufa miaka 100 ilopita mana hii U turn inayopigwa na wapambe zake hawezi amini.

Siasa za bongo bila unafiki huwezi ziishi.

#MaendeleoHayanaChama
Peleka ujinga wenu huko na Mwendazake,iweje mimba imnyime mtu elimu?

Alafu alikuta watoto wenye mimba wanasoma akaja kufuta Kwa upuuzi wake kwa hoja za kijinga..

Safi Sana Samia kwa kuwaheshimisha na kuwajali wanawake wenzio.
 
Tunatumia muda mwingi kupromote na kutetea mambo ya hovyo kwenye jamii.

Yani asiyefuata maadili anaenda kuchanganywa na wanaofuata maadili baada ya miaka 10 wote unakuta wameoza.

Wamemwandaa nani wa kuacha shughuli zake alee hao watoto watakao zaliwa na kuachwa na wazazi wao? Maana baba ataenda jela miaka 30 na mama atarudi shule.

Muda si mrefu na haki ya vilainishi itaruhusiwa
Mbona sisi tunakubali kuchanganywa na watu msiokuwa na akili na hamtuambikizi ujinga wenu?
 
Hii ndo nimeisikia leo tangu nizaliwe.
Hao walimu walitakiwa wachukuliwe hatua kali sana.
Hii ilikuwepo mkuu , walimu si huwa wanapewa zawadi wakifaulisha vizuri wanafunzi, vilaza wengi waliwafukuza shule kwa case za mimba za uongo, Saiz hata takwimu za mimba zitapungua
 
Hebu tuache ushabiki wa kinafki. Je zuio lile lilikuwa halali? Tusimsakame tu Waziri tujiulize wewe ukiwa na binti yako akabakwa akafukuzwa shule unalionaje wewe tuache unafki hili ndio tatizo la Watanzania. Kwani Mwendazake alikuwa saint? no alikuwa binadamu alifanya makosa Mungu atamsamehe huko aliko.
Sikuwahi kukubaliana na lile zuio tangu awali..ila nacho shangaa ni jinsi hawa mawazir walivyokua wanafiki kipindi hicho..na wanachokifanya sasa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom