Serikali: Wanaoanza Biashara kutolipa Kodi ya Mapato kwa muda hadi wa mwaka mmoja

Serikali: Wanaoanza Biashara kutolipa Kodi ya Mapato kwa muda hadi wa mwaka mmoja

Mambo kama hayo inabidi umsikilize waziri mwenyewe sio waandishi wa habari makanjanja.

Mabadiliko yoyote makubwa ya kikodi kama hayo lazima yapite bungeni, yawasilishwe na waziri wa fedha na yawe sehemu ya finance act.

Raisi hana mamlaka hayo na kodi ni sheria sio swala la mtu kujiamulia tu.
 
Kwanza hii biashara ya kuuza mashine za EFD Ina ukakasi. Kwa Nini zisiwe ni Mali za TRA na wafanya biashara wanazichukua kutoka kwako na wanaingiziwa gharama yake katika makadirio Yako ya mwaka na utalipa kidogo kidogo mara nne kama ulipavyo Quarterly Provisions?
Ni upuuzi mwingine huu
 
Mambo kama hayo inabidi umsikilize waziri mwenyewe sio waandishi wa habari makanjanja.

Mabadiliko yoyote makubwa ya kikodi kama hayo lazima yapite bungeni, yawasilishwe na waziri wa fedha na yawe sehemu ya finance act.

Raisi hana mamlaka hayo na kodi ni sheria sio swala la mtu kujiamulia tu.
Kwani aliyeongea ni kanjanja au Waziri wa Biashara? Kwenye Bajeti ijayo litatungiwa Sheria na Wizara itaweka utaratibu
 
Watanzania ni pasua kichwa pengine mama Samia hajawasoma vizuri,watakuwa wanaanzisha biashara mpya kila mwaka
 
Wowww wowww
Nani kama Mama
Basi waitangaze zaidi
Kuboost urasimishaji wa biashara
Nakumbuka tulivyofungua Kampuni
Tax clearance laki 6 na hapo hujaanza chochote

Ilinikera vibaya mnoo
Sawaa ni presumptive rate ndio on 0 sales and profits??!
 
Kwani aliyeongea ni kanjanja au Waziri wa Biashara? Kwenye Bajeti ijayo litatungiwa Sheria na Wizara itaweka utaratibu
Kwa ivyo unakubali sio sahihi kusema raisi ametoa kibali kwa jambo ambalo aliwezekani kutekelezeka bila ya bunge. Sasa ukisoma hiyo habari uoni huo ukanjanja kwa kusema raisi ametoa kibali?

Na hata Dr Kijaji hana mamlaka ya maamuzi ya kodi ni waziri wa fedha tu ndio anaeweza tolea huo ufafanuzi kwa hatua ambazo sera bado aijawa sheria rasmi.

If anything uwezi toza kodi kwa biashara mpya inapoanza sasa kama wanabadili ni kwenda sambambamba na dunia tu. Pili kusamehewa kodi kwa miezi sita au mwaka kuna maana gani, kutakuwa na threshold ya income ambayo itasamehewa, hakuna limit ya kiwango au watacheleweshewa tu muda wa kulipa kodi.

Halafu kodi utasemehewa ni ipi income tax, vat or both, sio swala la kushabikia bila ya maelezo ya waziri ni habari iliyoandikwa na kanjanja ambayo hakuna mtu mwenye uelewa wa maswala ya kodi inaweza make sense kwake.

Otherwise kodi ata huku kijijini kwetu mwaka ukiisha kwa biashara ndogo wanaolipa mara moja kwa mpigo deni lao awalipi hapo hapo unapewa miezi tisa na siku moja baada ya kufunga hesabu za mwaka. Biashara kubwa wanaolipa kwa makadirio na quarterly wanaanza baada ya miezi sita na siku kumi na every quarter after that, sasa huo sio msamaha ni kucheleweshewa muda tu wa kulipa deni.

Serikali inakusudia lipi hapo nikukuuliza huna majibu, halafu unabisha allieandika sio kanjanja kwa sababu nina uhakika alichosema waziri akiwezi kuwa jumla jumla ivyo.
 
Utaratibu ni kwamba unasajiliwa, na unakua kwenye rekodi baada ya miezi sita au mwaka ndio makadirio huanza sasa
Kuna ule mchezo wa kusema biashara imefilisika kisha inaanza kwa jina jipya, nadhani waliutumia Sheraton, Moven pick Serena etc
 
RAIS SAMIA: WANAOANZA BIASHARA HAKUNA KULIPA KODI MWAKA MZIMA.

Na Bwanku M Bwanku.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa kibali cha kuwawezesha Watanzania wote wanaoanza biashara kutolipa kodi kwa kipindi cha mwaka mzima mpaka biashara zao zitakapoanza kukua.

Uamuzi huo wa Rais Samia umetangazwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika wilayani Kondoa.

Dkt. Kijaji amesema adhima ya Serikali ya Rais Samia ni kuwainua Wananchi kiuchumi na kukua kibiashara na ndio maana ameendelea kutoa mikopo isiyo na riba kwenye Halmashauri zote nchini pamoja na kutoa fedha kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) huku akiwataka Watanzania kumuunga mkono Rais Samia kwenye dhima yake ya kumkomboa Mtanzania.

255679293705_status_0809f00a9f27431c8806ae010e405e4a.jpg

1150583791.jpg
 
Si kama makampuni yanavyofanya wanapopewa kipindi cha matazamio
Tecknolojia inakua. Tofauti na zamani Kuna link kati ya Brella na TRA na kila siku inaboreshwa. Ni risk sana kuwa na makampuni mengi yasiyofanya kazi. Na kufunga kampuni kuna gharama. Kwa mfumo wa sasa biashara ya kufungua na kufunga kampuni ni biashara kichaa. Itakugharimu tu, bora kama unaona hukui uachane na biashara.
 
RAIS SAMIA: WANAOANZA BIASHARA HAKUNA KULIPA KODI MWAKA MZIMA.

Na Bwanku M Bwanku.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa kibali cha kuwawezesha Watanzania wote wanaoanza biashara kutolipa kodi kwa kipindi cha mwaka mzima mpaka biashara zao zitakapoanza kukua.

Uamuzi huo wa Rais Samia umetangazwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika wilayani Kondoa.

Dkt. Kijaji amesema adhima ya Serikali ya Rais Samia ni kuwainua Wananchi kiuchumi na kukua kibiashara na ndio maana ameendelea kutoa mikopo isiyo na riba kwenye Halmashauri zote nchini pamoja na kutoa fedha kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) huku akiwataka Watanzania kumuunga mkono Rais Samia kwenye dhima yake ya kumkomboa Mtanzania.
Mods unganisha huu uzi
 
Back
Top Bottom