Serikali wekeni ruzuku kwenye Mafuta, hizi bei kwa sasa hazivumiliki tena

πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ . Na bado mpaka tuite maji mma. Uongozi bora sio kitu cha kufanyia masihala.
Maana unatugusa wote.
Nashangaa kila kitu kinaposemwa kwa nia nzuri kuwa kinahitaji marekebisho mapema, huwa kinachukuliwa kama ni kupinga maendeleo
 
Wahini fursa, mama anakuja na wawekezaaji kibao wa kilimo.

Mambo ya mafuta yasikupe shida, Mwarubaini wake upo njiani, umeshamsikia Biteko hivi karibuni? Yuko jikoni anakaangiza mambo huko.

Hao wawekezaji toka aanze kuwaleta wamefika wangapi? Haya mambo muhimu tuwe tunatanguliza hekimaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
hii ni habari njema sana kwa wakulima aise,
na sisi tupate kafaida kidogo mmetunyonga vya kutosha kwakweli.

Wala hakuna haja ya kuweka ruzuku kwenye mafuta ama hata kwenye uzalishaji wenyewe
 
BEI YA MAFUTA IPO JUU KWA AJILI YA UTITIRI WA KODI ULIOPO KWENYE MAFUTA...

NA HIZO KODI NDIO ZINAZOHAKIKISHA MISHAHARA YAO HAO WANASIASA...

USITEGEMEE...LAITI WANGEKUWA HAWAWEKEWI MAFUTA NA SERIKALI KWENYE MAGARI YAO...HII BEI ISINGEFIKA HUKU...ILA KWAKUWA WAO HAWANUNUI MAFUTA NA HATA BEI YAKE HAWAIJUI...
 
Kodi zilikuwepo Toka awamu ya Mkapa na ndio alianza kuziweka na mafuta yalikuwa bei nafuu.

Muwe mnaelewa mkiambiwa wazalishajo wamepandisha bei
 
Si tulikubaliana hela za ruzuku tuwape Taifa stars na tununue magoli !!
 
Halafu tunasimamisha miradi na kukopa kila uchao. Sasa hela zinaenda wapi kama zinakusanywa?

Hii inanikumbusha mwaka huu Tanesco ilitangaza kupata faida ya kufa mtu. Baada ya miezi michache wanasema umeme upo ila hautoshi na hakutakuwa na mgao. Nikagundua kama labda tumeanza ku implement mipango kabambe ya Bulicheka πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚
 
Pitia tovuti inayohusiana na uwekezaji: TIC | Home
Uwekezaji mkubwa uko kwenye mining. Na sababu iko wazi, kuwa tafiti zake zimeshafanyika muda mrefu umepita. Wanataka uwekezaji sasa.
Hawa wa bandari nao ni wawekezaji? Au kilimo, wamewekeza wapi? Siasa ni kitu kimoja...na uhalisia ni kitu kingine. lets be practical maana hii ni nchi yetu sote. Sio vizuri kudanganyana
 
Wewe una akili finyu sana,kwanza nitajie mradi uliosimama.

Pili Bajeti ya Nchi ni zaidi ya Trilioni 41 ,Kwa mapato hayo ya TRA hayazidi Trilioni 26 Kwa mwaka.

Sasa Kwa akili zako za kuku unadhani hizo za Juu zitatoka wapi?

Mwisho kukopa ni sehemu ya management ya uchumi yaani kiufupi kukopa ni lazima Ili ku regulate money supply kwenye uchumi.
 
Wabunge wakati wa kuchaguliwa, huwa ni wawakilishi wa wananchi.

Wakishachaguliwa, wanakuwa wawakilishi wa serikali.
 
Endelea na siasa...watanzania wanaamka.Ipo siku utajikuta kumbe wewe ndio una akili finyu.Unatakakutueleza nini kuhusu kuchelewa kufanya kazi kwa SGR toka Dar mpaka Dodoma?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…