Serikali yaanzisha kodi mpya kwenye miamala ya fedha kupitia Benki

Serikali yaanzisha kodi mpya kwenye miamala ya fedha kupitia Benki

Hii definetely ni double taxation. Mshahara wangu mushaukata makato zaidi ya 30% ndio munauingiza bank kwenye account yangu. Napokea (natoa) mshara wangu munanikata tena. This is straight upon the bullshit level. Its insane. Mwigulu umesomea wapi mambo ya fedha? Munakamua watu kuliko hata Firauni alivokuwa akiwakamua wana wa Israil.
 
Hamna namna yani ni kama wewe unavyopambana kujenga nyumba yako, ukope, uibe, ukate mshahara wa dada wa kazi au usilipe kabisa, uue, ukimbie madeni n.k ndivyo wanaoongoza nchi nao wanaona hivyo...ni kwa faida yetu watanzania hata hata hivyo nchi za ulaya watu wanakatwa mpaka 40% ya mshahara, halafu zinaletwa huku kama Aid, lakini haikuzuii kuhonga
 
Hapa huwezi kumuona yule CHIZI WA UBELGIJI akibwabwaja.

Kashapewa mafao anakula taratibu huku akiuguza MADONDA YA RISASI alizopigwa na MBOWE.

Hii ingelikuwa enzi za awamu ya tano, angeshatoka hadharani kubwabwaja na kutoa mapovu huku AMEJITWIKA MAGONGO.

Chezea pesa wewe! Njaa tupu.
 
Kodi ni lazima
Omba mungu wewe sio mfanyabiashara unaezunguka mikoani na gari lako vinginevyo mikeka yote mliotandikiwa barabarani Mwigulu anafikiria kuiwekea toll charge.

Utatia akili

Kodi ni muhimu lakini tozo hapana.

Jukumu la waziri wa fedha ni kukuza uchumi, kuboresha maisha ya wananchi na kuongeza furaha kwa wananchi.

Sio Mwigulu yaani ana hakikisha people are worst of today kuliko jana yao; yeye anawaza tozo tu.

Halafu wizara zingine hizo tozo wanazichezea kwa matumizi ya ovyo. Watu wametenga 500 million ya kununua majiko ya gas kwa madai ya promotion ya kubadili tabia.

Majiko yenyewe yananunuliwa kupitia kampuni moja mwenye biashara ana historia ya ufisadi na rafiki wa karibu wa godfather na baba yake waziri. Kibaya zaidi majiko yanachapa ya muuzaji sasa hiyo ni promotion ya wizara au taifa gas.

Kuna sababu wenzenu wanampenda ‘bi tozo’ kila muhuni anaangalia lake, wenyeviti wa mkoa na wilaya CCM wanaangalia kutafuna hela za miradi na vitega uchumi vya chama, mawaziri wanaangalia deals, civil servants kutafuna hela za miradi ya serikali, OC na rushwa, wafanyabiashara kukwepa kodi and so forth kila mtu na urahisi wa kupata asali iliyo mbele yake.

Mzigo wa kuendesha hiyo serikali anabebeshwa mtanzania maskini tozo kila kukicha, wengine kati yao wanaishi kwa mlo mmoja kwa siku.

Hizi ndio kodi za ku support kweli.
 
Waziri wa fedha na wataalamu wamekosa ubunifu wa kupata mapato na wanakimbilia njia rahis
Ukishakushiba ubongo haifanyi kazi vizuri unakuwa kamaa umelewa.mpaka nyumba ya tembe iwe na umeme ulipe Kodi. Ngoja turudi tuishi maporini
 
ingelikuwa enzi za awamu ya tano, angeshatoka hadharani kubwabwaja na kutoa mapovu huku AMEJITWIKA MAGONGO.
Mkuu njaa mbaya mno,huoni saivi wamepewa shavu na wao wanakula keki mpaka mama atoke madarakani.
Eti na wao Ni Kama wamejipatia Ajira yaani mama akaongea,eti tunafuatilia kuratibu katiba mpya,Kuna mkakati wa muda mrefu. Yaani saivi kimya walitaka kula tu. Na wao Ni njaa tu zilizokuwa zinawasumbua ujue. Aise Mungu nipate billions kadhaa nihame afrika umasikini Ni mbaya mno. Ukila kuku asiyekuwa na uwezo anaumia kiasi kwamba ukipata majanga anafurahi Tena anatoa fungu la kumi kuwa Mungu naye akamuona
 
CCM wameamua liwalo na liwe,wanatunyonya wapendavyo na tumekosa mbinu ya kuwafanya watuhurumie Wananchi wenye nchi.

Hakika wenzetu wamekosa Utu,Tozo hizi zinaenda kuishia kuwahudumia watawala wa CCM,Maendeleo yetu yote yanategemea wahisani,mikopo na misaada.Tumeendelea kuwa omba omba wa Dunia.

Tunahitaji Katiba Mpya itakayoweka uongozi wa nchi kwa matakwa ya Wananchi.
Hiyo katiba itasinamiwa na kina nani, hivi unzani watajielekeza kisu kwao!
 
Mfumo mbovu wa Ujamaa umeharibu uchumi ndiyo maana watu wanashindwa kuhimili kodi, tozo, mfumuko wa bei. Wa kulaumiwa ni Nyerere aliyeleta Ujamaa Tanzania.
 
Yaani mfano umelipwa mshahara na hio hio serikali ukaingia benki halafu unaenda benki au atm kutoa hela serikali tena wanakukata TOZO(Hapo kama bank nao huwa wanatoza unaliwa huku na huku)
Siku ambayo Mwigulu atang'olewa Wizara ya fedha NITAIADHIMISHA MILELE , huyu hafai
 
Hii definetely ni double taxation. Mshahara wangu mushaukata makato zaidi ya 30% ndio munauingiza bank kwenye account yangu. Napokea (natoa) mshara wangu munanikata tena. This is straight upon the bullshit level. Its insane. Mwigulu umesomea wapi mambo ya fedha? Munakamua watu kuliko hata Firauni alivokuwa akiwakamua wana wa Israil.
Tuanze kudai mishahara dirishani kwa cash kama zamani.
 
Back
Top Bottom