Serikali yakiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudi tena

Serikali yakiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudi tena

Asante kwa mrejeshonyuma.

Binafsi napenda kufahamu: Mambo yapi hayakukuvutia ulipotembelea kisiwa cha Saanane:ni huyo mwongoza watalii wa kike?Kipi alifanya kinyume na matarajio yako(yenu)?

Ama kisiwa cha Saanane hakina mandhari au vivutio vyenye kuridhisha hata uone thamani ya pesa yako (value for money)?
Mimi huwa nawashangaa wanaoenda kisiwa cha saa nane,maana kuna pimbi tu na vi swala vya kuhesabu.bora hata zamani kulikuwa kuna cage wanafuga wanyama mfano simba, sokwe, chui, fisi hii iliwavutia watu wengi kulipia na kwenda kuwaona mi naomba warudishe huo utaratibu.

lakini vile vile wanaweza kuongeza na mabwawa ya kufuga mamba itakuwa ni kivutio tosha maana kuna wakazi wengi wa mwanza japo wamezungukwa na ziwa ila hawajui mamba anafanana vipi.
 
Kwa maoni ya wadau hapa, inaonyesha kodi kubwa ndio changamoto kubwa.

Ninachojiuliza ni kuwa mbona suala la kodi bongo ni kaa la moto?

Kwenye biashara kodi kubwa, viwandani kodi kubwa, kwenye kilimo tozo kibao, kuagiza bidhaa nje e.g. magari ndio balaa kabisa. Kumbe kwenye utalii nako hali nin gumu pia?

Ilitakiwa tuwe mbali sana kiuchumi kwa kodi hizi.
 
Sekta ya utalii nikama imekuf inajiendea tu bora liende.Changamoto zake ni nyingi sana na hakuna mwenye ujasiri wakuziweka wazi nakuzifanyia kazi.ndo maana kuanzia wazir hadi watendaji ndani ya wizara ni porojo tu siku ziende.

Sasa kama kuna waziri kateuliwa juzi yeye badala yakukaa na wadau wahiyo sekta kujadiki changamoto zilizopo ili apush kuleta tija na ufanisi yeye anaongelea watumishi kukariri ilani ya chama wakati wizara ina mambo chungu mzima yakuyajadili.

Kwahiyo sidhani kama tuko serious na hii sekta.Kwahiyo hao watalii kutokurudi sio kosa lao ni letu.Sasa hivi watendaji wamejificha kwenye kichaka cha corona.
 
Labda waongeze vivutio vingine vya mapumziko; kwa sasa asilimia kubwa ya tourism destination zetu ni ‘special interest tourism’ usually it has a niche market. Udhani kila mwaka familia itakuja kutembelea simba at the minimum cost of $5000 per head au kupanda mlima Kilimanajaro kila baada ya miaka mitatu.

Ni aina ya utalii ambao ukishamuona fisi anavyowinda mara moja inatosha ukizingatia bei zenyewe. Wajiongeze ili watu warudi inabidi wapewe sababu zingine. Mtu kabla ajaondoka labda anapitishwa Arusha au Kilimanajaro anapata sababu zingine za kurudi.

Sitoshangaa kusikia asilimia kubwa ya watalii wanaorudi ni wale waliotembelea Zanzibar kufuata beach resorts ambazo kwa sasa wanajaribu kutengeneza mazingira to rival anywhere in the world.
 
Napendekeza

1. Sisi Watanzania Tujifunze na Tuwe Vivutio.
2. Sisi Tukivutia kwanza na Vivutio vingine vitavutia zaidi wavutiwaji.
3. Taifa Zima kila mtu avutie kwa upekee wa eneo husika.

Mfano Ukija Arusha watu Wote tuvae na Tuwe na muonekano wa Kimasai, Kibarghaidu, Kihadzabe n.k. Tusivae Kama wavutiwaji maana sasa hakutakuwa na tofauti.

Nyumba Tujenge za Kisasa katika muonekano wa Kiasili.

Ni kutengenezwa upya kwa Utaifa na Utalii Policy Mpya.
 
ili kuvutia watalii wa kigeni zaidi, nadhani tozo za kuingia hifadhi ingepunguzwa ili wengi wao waweze kumudu na kuongeza mapato ya nchi.
Hili limekuwa tatizo kubwa. Kuna hifadhi moja kubwa. Wageni wanakuja pesa kiasi fulan ila wanaishia getini na malalamiko kibao.

Embu tujaribu kushusha tozo ziko juu sana sana sana
 
Inasikitisha kiwango cha inefficiency katika nchi hii. Halafu wahusika wala hawajali.

Mimi kuna biashara hata hapa Dar tu niliamua sirudi tena kwao. Pesa yangu nataka niitumie sehemu nitakayoheshimiwa kama mteja, bila kutapeliwa au kuchukuliwa poa. Na hili ndiyo ninaloliona kwenye suala hili.

Hakuna anayejali.
 
Hapo sijaongelea mminyo wa online content creators wa Kitanzania.

Wahusika hata hawakujiuliza utaathiri vipi idadi ya content nzuri zilizokuwa zinatengenezwa na Watanzania za kuitangaza vyema Tanzania.

Kiufupi tatizo ni gharama kuwa juu sana, customer care mbovu, hatujaongeza thamani na creativity ya kutosha katika vivutio vyetu na pia marketing effort bado iko chini sana.
 
Napendekeza

1. Sisi Watanzania Tujifunze na Tuwe Vivutio.
2. Sisi Tukivutia kwanza na Vivutio vingine vitavutia zaidi wavutiwaji....
That thing haita work 100%. Eti wote wavae rubega? Nani kasema inavutia watalii?

Mgeni anapotaka kuja tz asianze kulalamika bei.. apate hile customer care top notch.
Bei iwe rafiki. Mfano wageni wanaopanda mt.klm wanalalamika tozo ni kubwa sana. Halaf service wanazopata ndani si zenye value hizo.

Ndio kusema kwamba wachaga hawakai kitalii.. nope? Service.. na gharama ziangaliwe upya.

Kipindi hiki cha corona..wenzetu uchumi wao ume shake. Tungepunguza tozo tuweze kuwa accomodate. Kama wanavyofanya maiafa mengine.
 
Hii topic ingefundishwa darasani ,tunaita repetitive purchase ina maana kuna shida kwenye service quality au overall customer satisfaction

Walimu wa marketing Udbs wamejaa wangeenda wakafundisha how to bridge 4 gaps za service quality ambazo ni Tatizo ku retain customers -defensive marketing ,otherwise ku attract a new customer (tourists) costs 5 times than keeping existing customer.

So topic italenga ku attract new customers (acquisition strategies e.g marketing communication tools e.g advertising and other promo mix) then ku defend existing customers' retention strategies kama relationship marketing ,service failure recoveries ,marketing research etc
 
H

Watalii hawarudi kwa sababu zifuatazo:-
1. Gharama za utalii sio rafiki mfano kupanda mlima Kilimanjaro mtalii mmoja ni usd 1000 . Bila malazi ya hoteli alikoshukia na chakula na unakuja kila mtalii anapanda mlima kea gharama tofauti mwisho watalii wakikutana na kujadiliana wanaomba watanzania ni watu wasio waaminifu...

1. most places ukishaenda mara moja ukirudi mara mbili inakua sio adventure tena, hata kama ni dubai ukishaenda mara moja ukienda the second time it doesnt add up

2.ebu fanya comparison na sehem zingine za utalii utajua tanzania bei ni che sana, mfano kupanda tu mlima everest andaa mil 300 tanzania ni $1000 sasa nan ana nafuu apo
 
Hii topic ingefundishwa darasani ,tunaita repetitive purchase ina maana kuna shida kwenye service quality au overall customer satisfaction...
Nimeipenda idea yako. Wakatoa seminar. Au hov iwape access waje na model itakayo changia kuongezeka kwa watalii
 
ili kuvutia watalii wa kigeni zaidi, nadhani tozo za kuingia hifadhi ingepunguzwa ili wengi wao waweze kumudu na kuongeza mapato ya nchi.
Alitarajia kukuta kipusa akakuta kipussy......hahahahaha
 
Juzi hapa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii alikutana na wafanyakazi wa wizara hiyo katika kujadili masuala ya utalii na changamoto zake alikiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudu tena, wakishakuja mara moja wengi wao huwa hawarudi tena.

Maana yake ni kuwa sisi Tanzania kila mwaka tunategemea watalii wapya, hatuwezi kuwatuliza(keep) ama kuwahakikishia watalii wa zamani kurudi tena Tanzania kufurahia vivutio vyetu vya utalii.

Retention yetu ya watalii ni chini ya 20%. Maana yake ukuaji wa utalii wetu bado una changamoto kubwa sana.

Nikitoa my personal experience, nilitembelea Kisiwa cha Saa Nane, Mwanza, tukakutana na tour guide wa kike, wote tuliofika pale siku hiyo hatuwezi kutamani kurudi tena, mimi na wenzangu siku hiyo tulikuwa disappointed, siwezi kutamani hata kwa bunduki kutembelea tena hiyo hifadhi.

Nimewahi kwenda Serengeti National park mara 2, kwa pale niko tayari kurudi maana mategemeo yangu yalikamilika kwa zaidi ya 80%.

Je, unadhani ni kwanini watalii wa nje hawarudi tena baada ya kutembelea Tanzania.
Huyo katibu mkuu siyo mzalendo kwa kweli.
 
Back
Top Bottom