Serikali yakiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudi tena

Serikali yakiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudi tena

Mm nimetembelea mbuga nying sn ila serenget sijawah fika kinachofanya watalii wasirud ni management mbovu mfano ukienda ruaha mapokez ni pa kiswahili vyoo ni vya kiswahili refreshment ndio kabisa uswahili swahili tu afu mbuga kubwa wanyama wachache yaan mnatafuta wanyama kwa mbinde chui .simba ndio balaa hawapatikan kuna haja ya kujenga good management wagen wasipate usumbufu mbuga pekee ambayo angalau niliifurahia ni manyara ipo poa sn japo na penyewe pana changamoto yake ilaa kwa serenget naamin ipo juu maana ndio best of all in africa
Je tarangire nilienda nikiwa mdogo pa ukweli Sana
 
Juzi hapa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii alikutana na wafanyakazi wa wizara hiyo katika kujadili masuala ya utalii na changamoto zake alikiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudu tena, wakishakuja mara moja wengi wao huwa hawarudi tena.

Maana yake ni kuwa sisi Tanzania kila mwaka tunategemea watalii wapya, hatuwezi kuwatuliza(keep) ama kuwahakikishia watalii wa zamani kurudi tena Tanzania kufurahia vivutio vyetu vya utalii.

Retention yetu ya watalii ni chini ya 20%. Maana yake ukuaji wa utalii wetu bado una changamoto kubwa sana.

Nikitoa my personal experience, nilitembelea Kisiwa cha Saa Nane, Mwanza, tukakutana na tour guide wa kike, wote tuliofika pale siku hiyo hatuwezi kutamani kurudi tena, mimi na wenzangu siku hiyo tulikuwa disappointed, siwezi kutamani hata kwa bunduki kutembelea tena hiyo hifadhi.

Nimewahi kwenda Serengeti National park mara 2, kwa pale niko tayari kurudi maana mategemeo yangu yalikamilika kwa zaidi ya 80%.

Je, unadhani ni kwanini watalii wa nje hawarudi tena baada ya kutembelea Tanzania.

Hicho kiingereza cha hicho kifungashio cha maandazi aisee! Daah, aibu naona mimi kutoka Kayumba!
 
Watalii wengi wanapenda kutembelea sehemu nyingi tofauti ambazo hawajawahi kufika.

Sehemu za utalii ziko nyingi sana duniani na gharama kubwa; badala ya kurudia sehemu ile ile mara nyingi watu wanaenda sehemu/nchi nyingine.

Mie binafsi sipendi kurudia sehemu niliotembelea, mara chache narudia kama imetokea watoto wamepapenda na wameomba kwenda tena.

Njia rahisi ya kuwatumia(wageni) kuweza kutuongezea utalii ni uduma nzuri ili wakawashawishi marafiki, ndugu na wafanyakazi wenzao waje kutembelea nchi yetu. Pia sehemu za utalii pamoja na hotels wanaweza kutoa punguzo la bei kwa safari ijayo. Kwa mfano siku ya kuondoka wanawapa voucher itakayotoa punguzo la bei wakirudi tena. Voucher ambayo wanaweza kumpa ndugu au rafiki aje kuitumia kama hawataki kurudi tena.

Muhimu zaidi ni usalama, uduma nzuri na mazingira safi kwenye vivutio vyetu. Kwa mfano, ni muhimu sana kusafisha fukwe za bahari. Wenzetu wana magari maalum ya kusafishia fukwe , serikali inaweza kufanya hivyo pia.
 
Juzi hapa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii alikutana na wafanyakazi wa wizara hiyo katika kujadili masuala ya utalii na changamoto zake alikiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudu tena, wakishakuja mara moja wengi wao huwa hawarudi tena.

Maana yake ni kuwa sisi Tanzania kila mwaka tunategemea watalii wapya, hatuwezi kuwatuliza(keep) ama kuwahakikishia watalii wa zamani kurudi tena Tanzania kufurahia vivutio vyetu vya utalii.

Retention yetu ya watalii ni chini ya 20%. Maana yake ukuaji wa utalii wetu bado una changamoto kubwa sana.

Nikitoa my personal experience, nilitembelea Kisiwa cha Saa Nane, Mwanza, tukakutana na tour guide wa kike, wote tuliofika pale siku hiyo hatuwezi kutamani kurudi tena, mimi na wenzangu siku hiyo tulikuwa disappointed, siwezi kutamani hata kwa bunduki kutembelea tena hiyo hifadhi.

Nimewahi kwenda Serengeti National park mara 2, kwa pale niko tayari kurudi maana mategemeo yangu yalikamilika kwa zaidi ya 80%.

Je, unadhani ni kwanini watalii wa nje hawarudi tena baada ya kutembelea Tanzania.

View attachment 1666303
Mtalii mwenye akili timamu aliyetafuta pesa yake kwa jasho na damu hawezi kukubali kurudi kwenye nchi iliyojaa sera mbovu za utalii.

Kama mimi ni mtalii, hiyo pesa ya kurudi tanganyika bora nikanywee K-Vant
 
Sijui ndo uzalendo ama Ni Nini lakini kiukweli sisi tunaona Tanzania Kama nchi ya kipekee Sana duniani kitu ambacho sio kweli, Wala si kweli kuwa Tanzania ni nchi pekee ya kuvutia watalii duniani. Kuna nchi nyingi duniani Zina vivutio vya kutosha hasa wanyama wa mwitu. Hapa Afrika tu Kuna nchi Kama Botswana, Namibia na south Afrika Zina wanyama wengi na vivutio vingi hata nje ya wanyama.

Kitu mingine ni sera mbovu za utalii. Tunachikulia watalii Kama Matajiri Sana hivyo gharama ni kubwa Sana.

Roma ,ugirigi na uturuki Kuna Majengo Yana miaka zaidi ya 800 na bado hapo Hadi leo sisi huko Zanzibar jengo la miaka 200 linaanguka, serikali mbovu isiyojali.

Kikubwa tuboreshe mazingira ya kuvutia watalii hasa usafiri na makazi ikiwemo vyoo. Pia tupunguze kodi.

Kuna nchi Kama Marekani, India, Amerika kusini na hata baadhi ya nchi za ulaya Zina vivutio vizuri Sana vya utalii kuzidi kwetu. Lakini sisi tunajiona Kama Ni wa pekee zaidi duniani.
 
Hakuna mtalii anayeweza kurudi sehemu ileile wakati Kuna nchi nyingi Hajaenda tena zenye vivutio tofauti au vinavyofanana na vyetu lazima kuwe na creativity
 
TUNA SAFARI NDEFU SANA YA KUITANGAZA TANZANIA KATIKA UTALII , WAKATI RWANDA WANATANGAZA NCHI YAO KUPITIA JEZI ZA ARSENAL SISI TUNAWANANGA
 
Hiyo ndio sababu ya utalii. Ukishafanya utalii huna sababu ya kurudi tena kwa sababu tayari sehemu umeshafika kama huna interest kwa nini urudi tena? Mfano ukishawaona wanyama Serengeti huwezi kila mwaka kupanga safari ya Serengeti tena? Utaamua kwenda kuangalia mfano Victoria falls. Pengine utaamua kwenda Thailand au Canada, Australia nk.

Mtalii kurudi sehemu ile ile tena ni kwa sababu ana interest na pengine anawaleta rafiki zake etc. Kumbukeni ni gharama kubwa kufanya utalii sio bure. Mimi binafsi nimeshafanya utalii Northern Tanzania na rafiki zangu kama mara mbili kwa sababu nafahamu hayo maeneo na marafiki zangu waliomba niwasindikize. Sehemu za vivutio ni nyingi sana hapa duniani ndio sababu watu katika maisha yao huwa wanapanga sehemu za kutembelea.

Tanzania tuamke tuanze kwa nguvu kubwa kukuza utalii wa ndani. Baada ya uhuru 1960 nakumbuka mfano wafanyakazi wa serikalini walikuwa wanapewa hati za kusafiria wanapokuwa likizo pamoja na familia zao kwenda kwenye vivutio vyetu. Sio vibaya Serikali ikaliangalia swala hili hasa kwa wafanyakazi wa serikalini pamoja na familia zao.
 
Hapo land cruiser ili ziingie zitengenezwe kwa ajili ya kubeba watalii Kodi yake ipo juu tunabaki kuwa na gari chakavu kwa wageni wanaolipa Kodi kubwa...punguzeni Kodi kwa vifaa vinavyohusiana na utalii ili kuweka mazingira mazuri ya kupata wageni wengi mimi ninapata wageni wanaoenda table mountain nikiwashawishi baadhi wanakuja Tanzania mwaka unaofatia wanarudi Cape hawataki kusikia kuhusu Tanzania tena maana Cape gharama za kawaida mno au hapo Botswana gharama zao zinaeleweka sio kama sisi na tunasahau kuwa wanyama wapo na wataendelea kuwepo tuu ni sisi kuweka mazingira rafiki kwa wageni...
 
Hiyo ndio sababu ya utalii. Ukishafanya utalii huna sababu ya kurudi tena kwa sababu tayari sehemu umeshafika kama huna interest kwa nini urudi tena? Mfano ukishawaona wanyama Serengeti huwezi kila mwaka kupanga safari ya Serengeti tena? Utaamua kwenda kuangalia mfano Victoria falls. Pengine utaamua kwenda Thailand au Canada, Australia nk.

Mtalii kurudi sehemu ile ile tena ni kwa sababu ana interest na pengine anawaleta rafiki zake etc. Kumbukeni ni gharama kubwa kufanya utalii sio bure. Mimi binafsi nimeshafanya utalii Northern Tanzania na rafiki zangu kama mara mbili kwa sababu nafahamu hayo maeneo na marafiki zangu waliomba niwasindikize. Sehemu za vivutio ni nyingi sana hapa duniani ndio sababu watu katika maisha yao huwa wanapanga sehemu za kutembelea.

Tanzania tuamke tuanze kwa nguvu kubwa kukuza utalii wa ndani. Baada ya uhuru 1960 nakumbuka mfano wafanyakazi wa serikalini walikuwa wanapewa hati za kusafiria wanapokuwa likizo pamoja na familia zao kwenda kwenye vivutio vyetu. Sio vibaya Serikali ikaliangalia swala hili hasa kwa wafanyakazi wa serikalini pamoja na familia zao.

Nilitaka kusema haya uliyoyasema.

Watalii wa ndani ndio wanaoweza kurudia kutembelea vyanzo vyetu vya utalii.

Watalii toka nje kwa kawaida wana orodha ndefu [ bucket list] ya vivutio wanavyotaka kuvitembelea ktk maeneo mbalimbali duniani.

Unaweza kukuta mtalii toka nje amejiwekea malengo ya kutembelea mabara yote, na ktk kutembelea Afrika ndio amechagua Tanzania.

Watalii toka nje ambao wanaweza kurudia kutembelea vyanzo vyetu ni wale wanaofanya shughuli za UWINDAJI.

Kwa hiyo naunga mkono hoja yako kwa 100% kwamba serikali wa-target watalii wa ndani.
 
Tatizo hasa ni masomo ya watanzania wanayofundishwa darasani. Unakuta darasa la uchumi degree kuanzia mwaka wa kwanza hadi mwisho wanafundishwa aina za kodi, left kodi, right kodi centre kodi. Tatizo ni elimu.

Ukimwambia mchumi wa Tanzania uchumi wa nchi haujengwi kwa kodi za kichwa hakuelewi kabisa. Kumbuka hizi kodi zote tunazokatana ni kodi za kichwa ktk jina jingine.
 
Hapo sijaongelea mminyo wa online content creators wa Kitanzania.

Wahusika hata hawakujiuliza utaathiri vipi idadi ya content nzuri zilizokuwa zinatengenezwa na Watanzania za kuitangaza vyema Tanzania.

Kiufupi tatizo ni gharama kuwa juu sana, customer care mbovu, hatujaongeza thamani na creativity ya kutosha katika vivutio vyetu na pia marketing effort bado iko chini sana.
Nakubaliana na wewe mkuu, hasa kwenye kuongezea thamani vivutio vyetu.

Kwa takribani miaka sita nimekuwa nikifanya matembezi angalao mara moja kila mwaka kutembelea sehemu mpya. Nilishatembelea northern circuit (Manyara, Ngorongoro, Tarangire na Serengeti) mara kadhaa nikaamua kwenda Southern circuit. Kwa kuwa ninapenda hiking na long trails nikaenda Udzungwa, Mbamba Bay, Kitulo na kufanya trail ya Kitulo mpaka Matema.

Nilishukuru kwa kuwa ni mtanzania gharama zilikuwa rafiki na ninaelewa lugha ya kiswahili. Ila kwa wageni, gharama zilizowekwa na thamani yake ni vitu viwili tofauti. Southern Circuit ina potential kubwa sana ya kudiversify aina za utalii. Ila inahitaji uwekezaje na usimamizi mzuri. Hapa ndio serikali ingetakiwa kushirkiana na Sekta binafsi kuwekeza kwenye hii circuit.

Kwa mfano, Udzungwa unaweza kuweka picnic spots kwenye vituo mbali mbali, vyoo visafi angalao katika vituo vitatu kwa kila trail na kwenye camping sites. Hivyo ni vitu basic sana na muhimu. Unaweza kuweka zipline hasa kwa wale wasio na uwezo wa kupanda lakini wanataka kuona maporomoko na sunrises. Unaandaa special packages za vyakula na burudani kwa wanaofanya camping...

Huwa sijui tunakwama wapi...
 
Hiyo ndio sababu ya utalii. Ukishafanya utalii huna sababu ya kurudi tena kwa sababu tayari sehemu umeshafika kama huna interest kwa nini urudi tena? Mfano ukishawaona wanyama Serengeti huwezi kila mwaka kupanga safari ya Serengeti tena? Utaamua kwenda kuangalia mfano Victoria falls. Pengine utaamua kwenda Thailand au Canada, Australia nk.

Mtalii kurudi sehemu ile ile tena ni kwa sababu ana interest na pengine anawaleta rafiki zake etc. Kumbukeni ni gharama kubwa kufanya utalii sio bure. Mimi binafsi nimeshafanya utalii Northern Tanzania na rafiki zangu kama mara mbili kwa sababu nafahamu hayo maeneo na marafiki zangu waliomba niwasindikize. Sehemu za vivutio ni nyingi sana hapa duniani ndio sababu watu katika maisha yao huwa wanapanga sehemu za kutembelea.

Tanzania tuamke tuanze kwa nguvu kubwa kukuza utalii wa ndani. Baada ya uhuru 1960 nakumbuka mfano wafanyakazi wa serikalini walikuwa wanapewa hati za kusafiria wanapokuwa likizo pamoja na familia zao kwenda kwenye vivutio vyetu. Sio vibaya Serikali ikaliangalia swala hili hasa kwa wafanyakazi wa serikalini pamoja na familia zao.
You are quite right, Sir. Kwenda kutalii si sawa na Simba na Yanga, inahitaji matayairisho. As you say, ukishaenda Ngorongoro mwaka huu, kwa nini uende tena? Ila kuna usemi Tanzania Unforgettable, kuna namna ya kutumia nafasi hii vizuri: wote waliokuja mara moja watarudi tu tena, maybe 3 or 4 times kabla hawajazeeka mno, na watakuja na familia.

Mie ni mfano mzuri. Tulienda mara ya kwanza Seronera tukiwa Form IV (Shy Bush, bure, tulilala sehemu za wanafunzi tukitumia malori ya Bwiru, Headmasters are very smart). Nikapenda sana. Hii ni lazima tuifanyie kazi Shule zote F2, F4 na F6 waende, kila mtoto aende walau mara moja. Hata kama tutamlipia au tutakula "hasara" inakupa addiction ni lazima tu utarudi tena na tena.

Next nikaenda after 8 years nishaajiriwa. Nikaenda tena 5 years later baada nilipooa, then after 3 nikiwa na familia nzima. Yote ilikuwa ni Seronera, ila ujanjani na kipato kupanda niliongeza Ngorongoro na Lobo.

Mtalii wa kweli atarudi every 4 or years, siyo kila mwaka.
 
Hakuna kitu kisichohitaji ubunifu na akili.

Kama huduma za utalii zingekuwa contracted, nina hakika sekta binafsi ingefanya vizuri maradufu ya jinsi mambo yalivyo leo.

Serikali yetu hakuna inachokiweza. Kwenye biashara na uchumi, ndiyo sifuri kabisa. Ushahidi upo, jinsi mashirika mbalimbali na viwanda namna vilivyokufa.

Na mahali ambapo Rais Magufuli amefeli kabisa, ni kufikiria Serikali, tena Serikali ya Tanzania inaweza kufanya biashara. Na akitaka aangamize kabisa uchumi mdogo uliopo aendelee kuweka shughuli za biashara kuwa controlled na Serikali.

Tanzania, pamoja na vivutio vyote tinavyotamba navyo, kwa mwaka mapato ni $3 billion. Misri mapiramidi yanaingiza $5 billion, Jiji la Paris $80 billion.

Serikali inafikiria utalii ni mikia tu ya fisi, pundamilia na tembo! Wanaofanya utalii, wanataka ku-enjoy na relaxation, sasa ukishaona mikia ya pundamilia, ndiyo basi. Hakuna cha ziada.

Tunazidiwa na nchi kama Thailand inayofanya sex tourism. Utajiri mkubwa hapa Duniani ni akili, siyo madini wala twiga na fisi. Ukiwa na akili halafu ukawa na madini, gas, wanyamapori, unapaa. Lakini hata ukapewa vyote hivyo, kama huna akili, utaendelea kudumu kwenye ndoa ya umaskini.

Nilienda Serengeti kwa kupitia lango la kule Magu, ni hovyo kabisa. Hiyo anayeandikisha mnapoingia unadhani amesoma shule ya ngumbaru. Hata ywezo wa kuandika ni hoi. Mtu mwenyewe ni goigoi, hajua thamani ya muda na wala hajitambui. Pale langoni tu, unaanza kukatishwa tamaa.

Tuna wanyama na mbuga lakini hatuna watu wa kuvipa thamani vitu hivyo!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo letu kubwa ni kujifanya tunajua Kila kitu au tunaweza Kila kitu kwa vile na sisi tuna certificate kama wao....!!

Ili kuinua quality tunahitaji kuruhusu a lot of expatriates in this sector.
 
aya ebu tupe average cost on a trip to dubai, kenya, south africa and tanzania then tujue yupi prices zake zpo low!
Mkuu, swala siyo gharama tu, swala ni thamani ya gharama anazolipa. Ukiacha vivutio kama hifadhi za Serengeti, Ngorongoro, Gombe na Mlima Kilimanjaro, au visiwa vya Zanzibar, Mafia, nk...vivutio vingine huduma zake ni za chini sana.

Tanzania ina vivutio vingi sana ukiacha wanyama pori, Mlima Kilimanjaro na Visiwa vya Zanzibar. Kila Mkoa una kivutio angalao kimoja. Kwa mfano, Tanzania tuna Maporomoko ya Kalambo, ambayo ni maporomoko ya pili yasiyokatika Afrika nzima (second uninterrupted falls), lakini kuyafikia ni kadhia..tuna Bustani ya Mungu ya Kitulo ambayo ikiongezewa thamani tutavutia wapenzi wa flora, maana ina aina ya mimea ambayo haiko sehemu nyingine duniani. Lakini haitunzwi ipasavyo mwisho wa siku kuna majangili wanawashamoto ile milima ili wavune wild orchids zinazopatikana kwenye hifadhi, mwisho wa siku wanaua mimea muhimu

Tukubali tu, inabidi kuongeza thamani ya vivutio vyetu na kuwekeza kwenye aina mbalimbali za vivutio.
 
Mimi naona watanzania tunahitaji elimu kwa kiwango cha hali ya juu sana.
Wala hatuna sababu ya kwenda mbali kama Ulaya au hats South Afrika, tuje kwa jirani zetu was Kenya.

Ukimwajiri mkenya kama mhudumu wa hotel, mgahawa ama bar utaona tofauti kubwa sana na Mtz, kwa sababu anawapokea wageni kwa haraka na kwa ukarimu.

Pili, lugha wanayotumia wafanyakazi was TRA no ngumu, kwa sababu wanamchukulia mfanyabiashara kama mkwepa kodi, na hii no Sera ya serikali yetu.

Tens kodi zetu so rafiki kwa watalii na hats kwa wafanyabiashara, hii inapelekea kuwe na gharama kubwa sana zinazotozwa kwa watalii kwa sababu ya wingi na ukubwa wa kodi zetu.
Hivi, kutokana na kodi zetu kuwa nyingi na kubwa unatozaje kodi za vitanda wakati unataka watalii wake kwa wingi?
 
Kwanza nitoe kheri za mwaka mpya kwa wana jamvi. Pili nilitaka kidogo kutoa maoni yangu kutokana na habari hii :

This' why most tourists do not return to Tanzania after first visit -> This' why most tourists do not return to Tanzania after first visit.
Nikubaliane na hoja kuwa kuna eneo la maboresho katika sekta ya utalii. Hii ni general rule kama kila kitu lazima kiboreshwe, maana kwangu naamini ukiona hakuna maboresho basi ujue kitu kinakufa! Lakini si kwa hoja hizi za kuwa kuna wizi ndio maana watalii hawarudi!

Nadhani tunatafuta mchawi, hii ni tabia ya kawaida kwa mtalii kila siku kutafuta nchi ambazo hajawahi kufikia na kwenda huko. Ni mara chache sana kumuona mtalii anarudia nchi ambayo alishakwenda. Nayasema haya sio kama napotosha, binafsi nikichagua nchi ya kwenda kutembea basi kila mwaka nachagua nyengine. Sio kama nimekosewa wala!

Tanzania nachagua kila baada ya miaka 3-5 kurudia matembezi, lakini hii inakuwa ni special treatment kutokana na kuwa nina kwetu nataka kutembelea na wazee, ndugu, marafiki n.k. Sitashangaa kumuona mtalii aliekuwa na mahusiano na mtanzania kumuona anarudia matembezi yake Tanzania kwa sababu hii ambayo inafanana na hio ya kwangu hapo juu.

Nadhani tujikite kuboresha utalii lakini sio kunyosheana vidole na kuanza kumtafuta mchawi. Kama suala la usafiri wa anga ni kweli Tanzania haina connection nzuri, sina uhakika tatizo ni nini. Hili linanisumbua hadi leo kufahamu, tena miaka ya hivi karibuni ndio kumeiprove kidogo. Zamani ilikuwa ticket za TZ ni ghali zaidi kutokana na uhaba wa airlines zinatua. Tutazame vizuri kama taifa jinsi ya kufanya partnerships na airlines na mataifa yenye watalii ili kuwe na urahisi wa haswa ticket za ndege.

Maasalaam
 
Back
Top Bottom