Serikali yamrejeshea Pascal Mayalla Press card yake iliyozuiliwa kwa takriban miaka 3 ataanza kuonekana Saba Saba!

Pascal Mayalla chapa kazi mkuu. Maneno ya wivu na kejeli kutoka JF yanafahamika wala yasikusumbue, Tanzania kwanza mengine baadaye. Nyota ya Tanzania inazidi kuwaka na mwisho wa siku Watanzania wengi wataneemeka na rasilimali za nchi hii ambazo zilikuwa zinakwapuliwa na wachache ambao hawataki kufanya kazi. Timiza wajibu wako.
 
Ni wakati wake sasa...nchi yetu imebadilika hilo halina ubishi....ni kuitangaza nchi tuu.mambo ya ufisadi yalikoma 2015...
 

Hakuna mwenye msimamo mbele ya njaa. Manjaa walimtia njaa akashika adabu,amejikomba mpaka wamemuonea huruma.
 
Mayalla aliweka wazi kabisa humu kuwa tangu aitwe Bungeni kujibu lile sakata, mambo yalibadirika sana. Shughuri zake za kuingiza kipato zilipigwa pini, uchumi ukayumba mno. Hakuwa na njia ya kujinasua zaidi ya kuanza kuimba mapambio asubuhi, mchana na usiku kutetea ugali wake na watoto wake.

Ndivyo ilivyo katika Taifa lenye serikali isiyotaka kuambiwa ukweli mchungu. Bora Mayalla hajafa wala kutekwa, amechagua kusimama upande wa WAONEVU na WATESI.
 


Tuna timiza wajibu wa kusifu na kuabudu lakini bado tunalimia meno tu,hali ikiendelea hivi tutaongea lugha muda moja muda si mrefu.
 
Ila Pasco kwenye huu utawala wa JIWE kanyooshwa kweli kweli. Mara aitwe bungeni, mara azuiwe kufanya kazi zake dah.

Ndiyo maana alianza kusifia sana bila break
...na hapo angekuwa MKAIDI akajimwambafy kuendelea kukaza zaidi ungesikia katekwa na watu wasiojulikana!.
 
Itabidi ahamie ofisi kubwa sasa atoke kwenye kale kajichumba kama choo,

Yote yote kwa yote asiwasahau wale wasaidizi wake kule Sabasaba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…