Serikali yapiga marufuku matumizi ya vitabu 16 vikiwemo Wimpy Kid ili kulinda mila, desturi na tamaduni za Kitanzania

Serikali yapiga marufuku matumizi ya vitabu 16 vikiwemo Wimpy Kid ili kulinda mila, desturi na tamaduni za Kitanzania

Wamekurupuka.

Hivyo vitabu tumenunua kwa watoto wetu na tumevisoma.

Havina hizo content.
Prof alidanganywa na kuna uwezekano yeye na kamati yake hawajavisoma hivyo vitabu
 
gays mmechefukwa na kupanic
Adhominem attack, mimi si gay, nakueleza hoja unaleta viroja.

Wizara imepiga marufuku vitabu kwa fake news za Whatsapp.

You are the laughingstock of the world!
 
Achaga ujuaji wa kisengerema kwenye mambo mazito. Kama una asili ya kubinuliwa, usitake kuambukiza vizazi vijacho.
Hujatoa hoja ya kukanusha hoja yangu, unakuja na matusi tu.

Hiyo ni alama ya mtu asiye na hoja na asiyeweza kujadiliana kwa mantiki.

Ni hivi, serikali yako imepiga marufuku vitabu kwa kuangalia fake news za Whatsapp.

Haiko makini.

Ni hilo tu. Fact.

Hayo mengine ni matatizo yako ya kisaikolojia na ya kukosa uwezo tu.
 
Msiwe na ujuaji sana Mazee.


Wizara haiwez kukulupuka kupiga marufuku kitu Kwa Hisia tu.

Hapo wamepitia vitabu vyote kupitia tume iloundwa na Wizara na wakajiridhisha
Hapa umeweka mahaba tu bila fact.

Wizara yako hata haijaeleza specifics kwa nini imepiga marufuku vitabu zaidi ya the awkwardly banal mila na utamaduni clause ambayo it is so overused and vague that it could mean anything.

Yani hata JF inaweza kufungwa kwa sababu uzi wa kula tunda kimasihara unakiuka mila na utamaduni za Mtanzania.

Hogwash!
 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda leo February 13, 2023 kwa Mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 59 cha sheria ya Elimu Sura 353 amepiga marufuku matumizi ya vitabu 16 vya ziada katika Shule za umma na binafsi nchini.

Vitabu vya 16 vilivyopigwa marufuku vimekutwa katika baadhi ya Shule si kama vitabu vya kiada wala ziada ambapo maudhui yake yanakizana na mila, desturi na utamaduni wa Mtanzania na yanahatarisha ukuaji wa Wanafunzi ikiwemo vinavyofundisha mapenzi ya jinsia moja.

Vitabu vilivyopingwa marufuku kutumika na kuwepo shuleni ni Diary of a Wimpy Kid, Diary of a Wimpy Kid -Rodrick Rules, Diary of Wimpy Kid - The Last Straw, Diary of Wimpy Kid-Dog Days, Diary of a Wimpy Kid The Ugly Truth, Diary of a Wimpy Kid -Cabin Fever.

Vingine ni Diary of a Wimpy Kid - The Third Wheel na Diary of a Wimpy Kid - Hard Luck, Diary of a Wimpy Kid - The Long Haul, Diary of a Wimpy Kid -Old School, Diary of a Wimpy Kid -Double Down, Diary of a Wimpy Kid-The Gateway, Diary, Diary of a Wimpy Kid-Diper Overlode.

Vitabu vingine vilivyopigwa marufuku kutumika shuleni ni Is for TANSGENDER ( you know best who you are!), Is for LGBTQIA ( find the words that make you you) na Sex Education a Guide to life.

View attachment 2516384

Prof.Mkenda amesema, uwepo wa vitabu hivyo pia unahatarisha malezi bora ya watoto na kwa shule ambayo itabainika kuendelea kutumia vitabu hivyo mara baada ya katazo la Serikali itachukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu na kisheria ikiwemo kufutiwa usajili wake.

“Nahimiza wazazi mkague mabegi ya wanafunzi kuhakikisha vitabu hivi havitumiki nyumbani; ukaguzi na ufuatiliaji huu ni endelevu ili kubaini kama vitabu kama hivi hipo katika shule tuweze kichukua hatua,".Profesa Mkenda”

Prof. Mkenda ametoa rai kwa watanzania kupiga namba 0262160270 ya mezani na 0737 962965 ya mkononi ili kutoa taarifa ya uwepo wa vitabu hivyo shuleni na kwamba hatua kali zitachukuliwa kwa shule yoyote itakayokutwa na vitabu hivyo ikiwemo kufutiwa usajili
Waziri gani aliviruhusu kuingizwa na kusambazwa kwenye mashule hayo kinyume na maadili na utamaduni wa Kitanzania?

Huku ndio kufungua nchi kuruhusu watu wenye tamaa ya kujamiiana jinsia moja?

Huu utawala ukiondoka kuna mtu ni lazima aondolewe kinga na kushitakiwa period!
 
Nimejikuta nakumbuka kitabu changu cha kiswahili na chapter zake
Siku ya gulio katerero
Simba mla watu
Kibanga ampiga mkoloni
Manenge na Mandawa

Hapo ndo tuanzie kama nchi wapi tulikwama tukaja na tamaduni za western?

kwa hasira siku moja nilisafiri mpaka kuona kijiji cha nanjilinji karibu na msola ili kujionea simba alipoandikwa na mwandishi akila watu
na siku moja akauwawa.
 
Mila, desturi na tamaduni za Tanzania sio sheria.

Marufuku ya Waziri pia sio sheria.

Nchi inapaswa kuongozwa na utawala wa sheria.

Tunataka sheria.
Sheria inatoa muongozo wa kipi na vipi kifanyike, na sheria ndio imempa mamlaka na kuongoza kuwa avifute. Hadi hapo sheria imefuatwa.

Kuna hapo umesema, mila, desturi na tamaduni za Tz sio sheria, Mkuu umejidanganya sana. Tambua kuna sheria ya kimila nchi hii na inafanya kazi huko kuna mila, desturi na tamaduni za jamii/makabila ya Tz hadi mambo ya kuchinja yapo huko.

Ukiacha hiyo kuna Kanuni ya adhabu, sura ya 16 inataja makosa ya kimaadili, ambayo yanatokana na hizomila, desturi na tamaduni. Pia zipo kesi za Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa.

Kubwa kuliko zote ipo katiba ya Jamhuri, ambayo ndiyo sheria mama na imetamka bayana hayo mambo ya mila, desturi na tamaduni zetu Tanzania.

Umesemamarufuku ya waziri sio sheria, ni kweli marufuku ya waziri hata raisi mwenyewe sio sheria bali huwa ni amri halali paletu itakapokuwa marufuku hiyo imetolewa kwa mujibu wa sheria fulani. Kwa kuwa sheria ya elimu imempa waziri mamlaka ya kupiga marufuku aina fulani ya vitabu kwenye mtaala wa elimu basi marufuku hiyo ni amri halali.

Mkuu, sheria imefuatwa na hiyo ndiyo sheria unayoitaka.

Ukiwana swali niulize tujifunze pamoja
(NB: Usilete ubishi usio na tija)

Karibu.
 
Mwenye softcopy atuwekee hapa tusome hivyo vitabu ili tujue yaliyomo.
Nimepata page moja katika kitabu kimoja.
Screenshot_20230215-124617~2.jpg
 
Habarini wana JF popote mlipo.

Jana moja ya habari zilizotawala kwenye mitandao na vyombo vya habari ni juu ya kuondolewa kwa vitabu 16 ambavyo haviendani na maadili ya kiTanzania.

View attachment 2516622

Ndugu waziri, nidiriki kusema kwamba mti umeukata ili hali bado shina na mizizi haijatolewa.

Kwanini?
Hapa naongelea hii alphabet R ambayo katika mashule mengi hapa nchini wanaitumia kuwakilisha huu upinde wa mvua, au kwa kimombo ni Rainbow.

Konsonanti hii R haijapotosha uwakilishi huo wa upinde wa mvua, bali maana iliyo huko duniani na inavyotumika ndio kinyume cha maadili na tamaduni zetu.

View attachment 2516627
View attachment 2516628


Sasa niweke wazi maana na uwakilishi wa upinde wa mvua kwa tafasiri ya huko duniani kulinganisha na suala la vitabu 16 ulivyokataza.

Upinde huu wa mvua unasimama kama alama ya jumuiya ya watu wa jinsia moja wanaoshirikiana kimapenzi, [yani mwanamme na mwaname, au mwanamke na mwanamke]

Pili, washiri wa mapenzi wa jinsia zaidi ya moja na kwa mtu zaidi ya mmoja.

Tatu, Watu waliobadili jinsia aidha alikua mwanamke akajibadili kuwa mwanamme, au kinyume chake.
Hii alama aligundua Gilbert Baker baada ya kuombwa kubuni alama kwa ajili ya washiriki wa kimapenzi wa jinsia moja, ambapo Harvey Milk anaesadikiwa kuwa mshiriki wa kwanza kujitangaza waziwazi kufanya ivo mnamo miaka ya 1970.

View attachment 2516630

How Did the Rainbow Flag Become a Symbol of LGBTQ Pride?

Swali langu linakuja, baada ya kutoa hivi vijitabu, Je watoto wetu bado wapo salama?
Jibu ni Hapana.

Hivyo basi ndugu Waziri mwenye dhamana, nikuombe umalizie hiki kisiki na mizizi yake ili kuondoa kabisa hili swala sio tu vichwani hata machoni ambapo ni njia ya kwanza ya mapokeo.

Naamini wewe ni kikngozi mweledi na mchapakazi, na hili sio jambo gumu kwako.
Moderator sijafurahishwa na kilichofanyika. Headings na kilichoandikwa humu ni vitu viwili tofauti. Why mme merge huu uzi? Ni nia yenu kuififisha ama?
 
Bora hata wangefuta topic ya circle kwenye maths, the earth as a sphere. Nilikuwa sizielewi. Tena bora hiyo sphere, circle sijawahi ielewa
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Sasa wewe ndugu hizo nazo ni hesabu? Just petty mathematics,kuna vyuma, abstract Mathematics science [emoji137][emoji137]
 
Serikali ya Tanzania imeingia mkenge kukubali fake news ya "Diary of a Wimpy Kid" kilichobadilishwa na wahafidhina na kusambazwa Whatsapp?

Kama ni hivyo, Wizara ya Elimu itakuwa kichekesho kikubwa sana.

Kuna siku page moja ya moja ya hivi kitabu ilikuwa inasambazwa Wwhatsapp, ina maandishi ya kushawishi watoto kufanya ngono.

Sasa mwenzetu mmoja akashangaa sana, kwa sababu mtoto wake anavipenda sana hivi vitabu (yupo Uingereza).

Akakichukua kile kitabu, akatafuta ule ukurasa, akakuta ukurasa wa kwenye kitabu na ukurasa ulele unaosambazwa Wwhatsapp ni vitu viwili tofauti.

Tukajua hizi ni kampeni za fake news.

Sasa najiuliza sana, kama habari hizi ni kweli, je, wizara imefanya uhakiki kwenye vitabu?

Au imetumia maandishi yaliyoonekana Whatsapp na kukurupuka?
Mtoto anaelia ,hii imetosha kuvikimbia
 
Kulikuwa kuna education material approval committee (EMAC), hiyo kamati ipo au waliishaifuta? Maana hiyo kamati ilikuwa na jukumu la kupitisha zana na vifaa vya kufundishia. Ina maana siku hizi watu wanaingiza vifaa hivyo bila kupitishwa na mamlaka za elimu? Sasa kama serikali imepiga marufuku vitabu hivyo mbona haijasema ubaya wake zaidi ya kusema vinaenda kinyume na utamaduni wetu? Au vina ushoga ndani yake? Au usagaji? Kama ni novel tu ingeacha watoto wakuze msamiati wa lugha iliyotumika kuandika. Halafu serikali ingehamasisha waandishi wazawa waandike vyenye utamaduni wetu
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Sasa wewe ndugu hizo nazo ni hesabu? Just petty mathematics,kuna vyuma, abstract Mathematics science [emoji137][emoji137]
Nilimaanisha kwa level ya secondary mkuu. Mimi zilinichemsha hasa circle
 
Watoto wadogo wa miaka minne hadi nane walikuwa wanafundishwa kut*mbana huko international schools😁😁😁
2023021908.jpg
2023021943jc.jpg
202302190.jpg
20230219.jpg
2023021.jpg
202302.jpg
 
Back
Top Bottom