Serikali yatangaza awamu ya pili ya ajira 5000 za Walimu

Serikali yatangaza awamu ya pili ya ajira 5000 za Walimu

Habar zenu mabibi na mababu.

Mwaka jana 2020 mnamo mwezi wa tisa Mheshimiwa Rais John Magufuli alitoa kibali cha ajira mpya za walimu 13,000 kwa shule za Sekondari na Msingi, ambapo katibu wa tamisemi alitangaza majina elfu 8 mwezi wa kumi na moja mwishoni na walimu hao kutakiwa kuripoti kuanzia December 1 mpk 14.

Baada kama wiki moja mbeleni walikuja tena kwenye press kwa waandishi wa habari kueleza sintofahamu zilizotokea katika awamu ya kwanza ya majina 8000 ya walimu, press ile ilihudhuriwa na makatibu wakuu wa wizara tatu yani kulikuwepo na katibu mkuu wa tamisemi, katibu mkuu wizara ya elimu pamoja na katibu mkuu wizara ya utumishi. Kupitia press hiyo walitoa tamko la wazi kuwa majina elfu 8 ilikuwa ni awamu ya kwanza hivyo imebaki majina elfu 5000 awamu ya pili ambayo wataitoa muda si mrefu, wakatoa sababu za kutoa ajira hzo kimakundi eti ni katika kupunguza kusiwe na malimbikizo ya madeni kwa walimu hao.

Baada ya wiki tatu tena mbeleni kulikuwa na tukio la katibu mkuu wa tamisemi kukutana na wakuu wa shule za msingi ambapo katika hutuba yake alisisitiza kuwa kuna shule zaidi ya 2500 hazikupelekewa walimu awamu ya kwanza hivyo watapeleka na hiyo awamu ya pili ya majina 5000 yaliyobaki watawapangia walimu maeneo yenye uhaba zaidi hasa vijijini.

Majuzi hapa Mheshimiwa Raisi Magufuli akapigilia nyundo wakati yupo katika ziara yake huko bukoba akasema wazi kuwa zimetolewa nafasi za walimu elf 8 hivyo watamalizia elfu 5 ili kupunguza changamoto za ufundishaji.

Sasa imeshatimia miezi mitatu lakini Tamisemi bado wako kimya tu, kwako Mheshimiwa Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Suleiman Jaffo ni lini utaachia hayo majina elf 5 ajira za walimu awamu ya pili?? Vijana mtaaani wanateseka sana mpaka wanatia huruma, vijana wanaongoza kuwa na msongo wa mawazo utafikiri ni wazee kwa kukosa kazi.

Mbaya zaidi leo bunge limeanza wawakilishi wetu huko bungeni (wabunge) wanauliza maswali mengine ya miundombinu, umeme, afya, maji, lakini wanasahau kuhoji hili la ajira ambalo kibali chake kimeshatolewa na mhe Raisi??!!

Mh jafo aachia hayo majina ili walau keki ya taifa vijana waifaidi wote.


~Gai da Seboga
IMG_20210202_200845_463.jpg
 
Kunaa mchezo unaendelea huko dunian kunaa baadhi wamepata barua toka TAMISEMI kuripot kazini, then kunaa routine kwa wanaojitolea baada yaa rushwa kali kwa wale 8k round hii wanaojitolea wataula zaid maana UHAKIKI ushamalizika kwa mtu alyeko street tuu n boraa kuandaa mashamba mvua za mwez huu maharage alizeti znafika TRUST ME.
 
Niliwasikia katibu mkuu-utumishi na katibu mkuu-elimu wakisema wanatoa nafasi kwa wizara ya tamisemi kurekebisha mfumo wao wa maombi ili makosa yaliyojitokeza kwenye ajira zilizopita yasijirudie tena. Kwahiyo mleta mada tuendelee kuvuta subira mfumo ufanyiwe maboresho punde yakikamilika tutatangaziwa kuomba.
 
Kunaa mchezo unaendelea huko dunian kunaa baadhi wamepata barua toka TAMISEMI kuripot kazini ...then kunaa routine kwa wanaojitolea baada yaa rushwa kali kwa wale 8k round hii wanaojitolea wataula zaid maana UHAKIKI ushamalizika kwa mtu alyeko street tuu n boraa kuandaa mashamba mvua za mwez huu maharage alizeti znafika TRUST ME
Kujitolea tena? Duh! Mbona uonevu maana serikali ilitwambia tusikae tu kusubiria ajira bali tuwe tunajishughulisha pia kwa kazi ndogo kujiingizia kipato, pato kwa serikali na kukuza uchumi wa nchi. Sasa sisi tuliojishikiza kwenye vikazi mbali mbali wakisema waajiri tu waliokuwa wanajitolea si watakuwa wanatuonea?

Rais tunusuru
 
Siku hizi wenye konnekshen na watumishi wa Jaffo wanapigiwa simu wakaripoti vituoni. Ni mwendo wa kimya kimya
 
Niliwasikia katibu mkuu-utumishi na katibu mkuu-elimu wakisema wanatoa nafasi kwa wizara ya tamisemi kurekebisha mfumo wao wa maombi ili makosa yaliyojitokeza kwenye ajira zilizopita yasijirudie tena. Kwahiyo mleta mada tuendelee kuvuta subira mfumo ufanyiwe maboresho punde yakikamilika tutatangaziwa kuomba.
Kwa mujibu wa maelezo yao ni kutoka majina tu awamu ya pili na sio kutuma maombi tena. N vle nashndwa weka video yake yule katbu wa utumishi.
 
Mungu akupe hitaji la.moyo wako..ila tambua hizi ajira mara nyingi zinatolewa kisiasa sana..subiri 2025...wakiwa wanaomba mitano tena...chamsingi fovus kwenye mambo yako tu ya kujijenga kiuchumi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kunaa mchezo unaendelea huko dunian kunaa baadhi wamepata barua toka TAMISEMI kuripot kazini ...then kunaa routine kwa wanaojitolea baada yaa rushwa kali kwa wale 8k round hii wanaojitolea wataula zaid maana UHAKIKI ushamalizika kwa mtu alyeko street tuu n boraa kuandaa mashamba mvua za mwez huu maharage alizeti znafika TRUST ME
Hili Kama Kuna ukweli fulani haswa kwa wanao jitolea Nina jamaaa yangu ana jitolea anasema majina Yao yako wilayani wakuu wa shule walipelek rosta kule wilayani wapo barua za ajira bado mikoa wataenda wamepewa ronja baadh ya mikoa Wana weza kwenda Ila lini bado hawajajua
 
Kwa mujibu wa maelezo yao ni kutoka majina tu awamu ya pili na sio kutuma maombi tena. N vle nashndwa weka video yake yule katbu wa utumishi
Sasa wakitumia database si makosa kama yale ya mwaka jana yatajirudia tena?
 
Ninaskia kla mtu anasema kuna wanaopigiwa cm, n kwel hili jambo??
Yaaa ninao wawil nawafaham mmoja n dem nazan ana ndg huko juu kaambiwa aende musoma week hii kuaza kazi sooo kusubir hiz mambo wanazengo n kama kusubil embe chini ya mbuyu
 
Back
Top Bottom