SGR Mchakato wa Nauli ndiyo huu hapa, mtoto hadi Moro kulipa Tshs 12,400

SGR Mchakato wa Nauli ndiyo huu hapa, mtoto hadi Moro kulipa Tshs 12,400

Dar Zenj tu hapo, tena umbali chini ya maili 40, nauli ni kati ya 30k hadi 100k, kwanini tunaona shida 20k kwa Morogoro kama safari itachukua saa 1.30 kweli?
Bahati mbaya unatolea mfano eneo ambalo hulijui na hata ukijua bado unaweza kubisha.

Hapo baharini kuna makampuni zaidi ya mawili yanayotoa huduma ya usafirishaji abilia, zinazofahamika ni mbili tu, Azam marine na Zanzibar fast faries, sababu ndizo zilizopo.

Nauli (mimi) nilianza kulipa 15,000/- ilipanda hadi leo 30,000/- sababu ni uendeshaji na eneo hilo, hakuna ushindani ni hao wawili na hata mtetezi wa abilia hamna.

Mwaka jana wakati wa uzinduzi wa boat ya Kilimanjaro VIII, mmiliki aliomba serikali ifikilie kuwapunguzia kodi sababu ya uendeshaji ila majibu waliyopewa ni kuwa mbona hamjawahi kuacha kuangiza boat mpya kila baada ya miaka kadhaa, ina maana mnapata faida ila mwananchi hapati haueni.

So unatakiwa uelewe hakuna mfanyabiashara mwenye undugu na mteja, bado nauli ya 30,000/- ni kubwa na inawalipa sana hata ingekuwa 20,000/- ila kwa sababu hakuna namna nyingine lazima tutumie vyombo vyao, kuna meli za mizigo zinasafiri usiku kwa usiku hizi nauli ni 20-25,000 bado watu ni wengi wanazipanda.
 
Tatizo muda....Unapanda basi saa tatu asubuhi Magufuli stand mpaka utoboe Chalinze saa Sita mchana.....Moro unaingia saa Nane mchana..
Happy Easter 😂, umepotea sana mwamba!.

Sasa issue ya muda kwa hili dubwasha sidhani kama itakuwa same like hiki wanachotuhubilia sidhani abadani.


Nina hakika siku rasmi likianza kazi in one week litaenda speed ya farasi kuwakonga nyoyo zenu ila mkishazubaa wenye mabasi wanakuja kwenye makubaliano wenyewe huko sasa ''mzee umesahau tuliongea nini... hebu punguza speed tunakosa abilia huku"

Kumbuka buses owner wanalipa kodi, ushuru, staff nk, na kumbuka wana nguvu huko ndani, hawawezi kukubali kampuni zao zisiinzie kisa dubwasha, ndipo itakuja komwe la kutaka libinafsishwe kwa mwerarbeu!.
 
Ulitaka wakuchukulie na wewe?
NO binti yangu!.

Ndiyo maana unamsomesha kijana wako ili aje awe vile atataka ukubwani na siyo unamuacha aje ajisomeshe mwenyewe, ndivyo hata mali za nchi inapaswa iwe hivyo.
 
Dunia nzima usafiri wa train ni rahisi kuliko usafiri wowote na sababu ziko wazi kwakuwa train inabeba watu wengi na mizigo mingi inapunguza gharama za uendeshaji, sasa ni lazima waweke bei chini ya usafiri wa ndege au magari hii itachochea sana wingi wa abiria na mizigo na hata parcels ndogo ndogo waweke utaratibu wa mzuri watabeba soko lote wafanye wepesi bila urasimu yaani service bora kuliko waliopo. Itasaidia kuwa na train kwa siku hata mara 4 na kila trip zikiwa nyingi gharama za operation zinashuka. Wasiliuwe shirika kama walivyofanya reli ya kati na Tazara.
Mawazo mazuri sana especially hapo kwenye parcels lkn nani anajali
Hao kina kadogosa au genge la mafisi wa ccm
Kazi Bure tu
Labda wajenge halafu waruhusu watu binafsi wanunue train kama ilivyo kwenye mabasi
 
Ni sahihi ndio maana hata hoteli za kitalii soda ambayo uswahilini inauzwa elfu moja hoteli ya kitalii soda hiyo hiyo unakuta inauzwa elfu 12 kupunguza vibaka na wachafu wachafu kuingia hoteli za kitalii
Sidhani kama lengo ni kupunguza wateja. Gharama ya uendeshaji wa hospitality services yoyote ni kubwa na ndiyo maana gharama ya kupata huduma yoyote inakuwa ipo juu.
 
Back
Top Bottom