Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Safi Sana aise,Tukiacha unafiki huyu Mama ni levels zingine kabisa,
Hata bwana Mbowe na Tanzania Daima yake atakubaliana na Mimi,
Hongera sana Ndg Shaka Hamdu Shaka,View attachment 2193845
===
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi & Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka amempongeza Rais wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuwa na kifua cha kuvumilia kukosoa na kukosolewa.
Aidha Ndg Shaka Hamdu Shaka amempongeza zaidi Rais pamoja na Waziri aliyemteua Mhe Nape Moses Nauye kwa kushusha gharama za kusajili "Online TV" kutoka TZS 1,000,000 ( milioni moja) ya awamu iliyopita hadi TZS 50,000 ( elfu hamsini ) ya sasa kwa kutambua kuwa kwasasa duniani " Mitandao ni Ajira".
Wakati huohuo, Amempongeza sana Rais wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan Pamoja na Waziri Nape Moses Nauye kwa kuvifungulia vyombo mbalimbali vya Habari vilivyofungiwa kwa muda mrefu kwani Vimerudisha ajira kwa Watanzania wanyonge na vimeongeza wigo wa kupata habari na wanahabari.
Aidha, Shaka Hamdu Shaka ameipongeza Serikali ya awamu ya Sita kwa kutekeleza kisawasa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020|25 hasa kifungu cha 125,kinachosisitiza Uhuru wa habari na wanahabari kwa WATANZANIA wote "Na ndio sababu leo watu wanakosoa na wanabaki kuwa salama " alilisisitiza bwana Shaka Hamdu Shaka.
Ndg Shaka Hamdu Shaka ameyasema hayo katika Uzinduzi wa Jengo la Studio za kisasa za Televisheni ya TBC2 pamoja na kipindi kipya cha "Jambo Tanzania", Mikocheni Jijini Dar es Salaam Jumanne 19 Aprili, 2022.
Shaka ni jembe sana,Hongera sana Ndg Shaka Hamdu Shaka,
Unafanya Kazi nzuri sana katika Taifa hili,
Appreciated 🙏🙏🙏🙏
CCM hakuna mtu mwenye shida nikusaidie tu,Je nyinyi wapiga mapambio mnaupiga mwingi majumbani kwenu?
Hivi ni ukosefu wa ajira ndio unawaletea UCHAWA au Njaa iliyopitiliza?
Mkuu upo?Ahsante kwa taarifa na inapendeza...
Mbio za Panya
Wafuasi wa Lumumba mm hapo ndio huwa siwaelewi... Yaani tozo ya awali mliweka nyie(Mkashangilia),,Leo tena nyie wenyewe mmeifuta(Mnashangilia)... as if kuna kitu kipya mmeongeza..
Mnatengeneza tatizo,, halafu mnalitatua.. then mnajiona Wakombozi...
Mtazamo tu...
😁😁😁Karibu CCM Chama cha uhakika
Wakitaka michango ya join the chain wanakimbilia kwa bodaboda na wachoma mahindi.
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Ilani yao ndio inatekelezwa.... waliahidi kujenga mazingira rafiki na wezeshi kwa ustawi wa tehama ili iajiri watu wengi zaidi ndicho kilichotokea....sasa unawaondoleaje pongezi...ikiwa wameahidi na kutekeleza!!!
Je nyinyi wapiga mapambio mnaupiga mwingi majumbani kwenu?
Hivi ni ukosefu wa ajira ndio unawaletea UCHAWA au Njaa iliyopitiliza?
Hizo ni tabia za ufipaHao ccm ndio wale " mmeshiba ndio, mnanjaa ndio"
Ahsante kwa taarifa na inapendeza...
Uko vizuriHongera sana Ndg Shaka Hamdu Shaka,
Unafanya Kazi nzuri sana katika Taifa hili,
Appreciated 🙏🙏🙏🙏
😍😍🙏🙏🙏Hapana Mkuu,, hakuna ubaya wowote kwa kilichofanyika....
Nilichosema ni kwamba aliyeweka watu walipe Millioni Moja,, ndio leo aliyetoa na kubaki Elfu hamsini..
Nani wa kusifiwa hapo na ni nani wa kumchukia..???
😀😀😀😀Naona sukuma gang Msoga line wanakutesa vibaya! Safari hii mabush star kazi mnayo kwa maborn town.