Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Pole hii stage inaoneka na umeiruka mpira unapatikana katika mazingira tofaut yasiyo fanana.mnaweza kufuma wote au mtu akaja nao inategemea
 
Marufuku kupiga mpira kwa dole la mguu utamua mpira

Ukipiga penat ya funua kama kipa ni mwenye shut likawa kali unatolewa uwanjani
 
Tujikumbushe sheria za mpira za zamani, enzi zetu, nitaanza na ya golikipa, ilikuwa ni marufuku kuingia eneo la golikipa yaani ndani ya 12 na ukiingia basi golikipa anaruhusiwa kukufanya chochote ikiwamo kukukanyaga popote pale, nakumbuka mimi niliwahi kukanyagwa kichwani.
 
Kona ya tatu mfululizo inazaa penati
 
Timu ikizidiwa mchezaji mmoja basi golikipa wao anakuwa kipa na beki, yani anacheza nafasi zote mbili.. sasa anaweza kudaka mpira hata katikati ya uwanja bila tatizo lolote
 
1.Mwenye mpira Lazima acheze ata kama hajui mpira
2.Dogo mnene lazima awe golikipa
3.Mwenye mpira ataamua nani acheze na nani asicheze
4.kama haujashiriki kufuma mpira unaweza usipate namba
5.Ukichaguliwa mwishoni ujue uwezo wako ni mdogo kuliko wote
6.Mwenye mpira akikasirika mpira umeisha
7.Inaruhusiwa kubadili golikipa kama ikitokea penati na baada ya apo ataendelea kudaka yule yule
8.Mechi itaisha pale giza linapoingia
9.wale ambao wamekosa namba kazi yao ni kufata mpira ukitoka
10.yule mtaalam wa soka {kama mimi } huwa hakosi namba hata siku moja!
Ukiikumbuka lazima utabasamu!
 
penalty hadi mtu aumie na atoke damu.

ni kawaida match kuisha goal zikiwa 20-27 etc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…