Sheria mpya ya TISS tusijifanye vipofu wakati kumbe tunatawaliwa ama tunaenda kutawaliwa kijeshi

Totalitarian state iliyikuwa ikizuga zuga kujifanya nchi ya Democracy.
Karibuni ktk ulimwengu wa kunyatiana na sheria bubu.

Sasa mjiandae kweli kweli mana hata wao wataadhibiwa endapo watafeli Maagizo na kuonekana wamekaidi maagizo...... Afande sio rafiki
 
Huu muswada uliandaliwa kipindi Cha mwendazake, sijui bi mkubwa kaupendea nn aisee... yaani tunaenda kuunda majambazi watakaokuwa wanafanya ujambazi kisheria... Wakikupora sawa tu, wakikuua sawa tu..wakikuteka sawa tu... yaani kiukweli cjui sasa kama polisi watakuwa na kz gn sasa... Mmmmhhhh hii nchi ngumu sana aisee
 
Kabisa system ikikutaka inakupata kwa style yoyote ile

Ova
 
Kumekuwa na marekebisho ya kisheria yakifanyika na kupitishwa bungeni kwa nyakati tofauti tofauti pasipo wananchi au wadau kuanzishia mijadala kama hili la TISS sasa hivi ambavyo imekuwa maana.

TISS wamelipa nguvu kwenye mitandao ya kijamii kusambaaa na baadhi ya wana habari kufahamika na lipingwe, kwasababu wao wenyewe ndani ( wenye akili timamu wameona hii sheria kimeo itakuja waumiza hata wao wenyewe kama sio familia zao etc ). Kama wangekuwa wanalitaka ( wanaitaka iyo sheria ipite ) jamaa walikuwa wana uwezo wa kucheza nalo kimya kimya mkashangaa tu sheria imepitishwa..

Kwa ufupi hii sheria hata TISS wenyewe wameona ya kidwanzi ndio maana wanatumia hizi media kuisanua jamii, hatimae mabunge yataona soo waifanyie marekebisho
 
Yah, inawezekana ikawa hivyo na wao huenda hawajaikubali lkn ikifika bungeni tena kwa Tulia Akson ujue ataipitisha tu, wabunge wenye uwezo wa kuizuia hiyo sheria hakuna na kibaya zaidi cku hz wanahongwa ili mambo yaende
 
Wanakamatwa mbona
 
Yah, inawezekana ikawa hivyo na wao huenda hawajaikubali lkn ikifika bungeni tena kwa Tulia Akson ujue ataipitisha tu, wabunge wenye uwezo wa kuizuia hiyo sheria hakuna na kibaya zaidi cku hz wanahongwa ili mambo yaende
Jamaa wameichomoa hii, haitakaa ipite. Ndio maama wanatumia media kuwasanua watu mbali mbali.. kelele ikiwa nyingi bungeni wataona nomaaa, itarudishwa tu. Haiwezi pita, wangekuwa wanataka ipite usinge ona hizi harakati za kusanua watu
 
[emoji625][emoji625]
 
Ulishaona wanakamatwa kama wanavyokamata wanajeshi au polisi? Lini uliona mfanyakazi wa "teeth" amepelekwa mahakamani kwa kosa la kijinai ,sabaya "andakava igo sirii" alivyodakwa hata kama ni wa kwao lakini walimkana.
Msala binafsi wanakutemaa tu mazimaaa.. ila kama msala wa kikazi mbona inaishaga kimya kimyaaa
 
Hata sasa hawafanywi lolote kwa chochote......sheria inawapa power zaidi kisheria Yaani wana nguvu zaidi vyombo chochote nchini ....kuliko hata mahakama na bubfd sasa kama mhimili....wa 4
wana nguvu tu kwasababu hawafahamiki. Wakiondoa usiri wa kutofahamika makali yanapungua maana wanaishi kitaa hata kwao itakuwa hatari
 
wana nguvu tu kwasababu hawafahamiki. Wakiondoa usiri wa kutofahamika makali yanapungua maana wanaishi kitaa hata kwao itakuwa hatari
Sasa watakuwaje juu ya sheria ? Wataua...kwa visasi ...watajificha utekekezaji ....na interest ya nchi ....hiyo haiwezekani ....Lazima uwajibikaji uwepo ili sheria iwe one guide kwenye utendaji m....itakuwa fujo sasa ...nani alieomba hayo mabadiliko ? Tiss kama taasisi kutokana research ....yao ugumu kutengeneza Majukumu au Rais kama taasisi ??
 
Kikawaida TISS wasingetakiwa kuwepo lakini hali halisi si kawaida. Kuna elqaeda walitikisa dunia kuna uamsho walitikisa zanzibar kuna raila na askofu mackenzie wanatikisa Kenya. Sheria zote haki zotezote taratibu zote zipo yeye hataki. Huna jinsi. Au mko vitani na mabeberu msaliti anatoa siri zenu. Huna jinsi. Kama si hivo walactusingehitaji TISS.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…