Sheria mpya ya TISS tusijifanye vipofu wakati kumbe tunatawaliwa ama tunaenda kutawaliwa kijeshi

Sheria mpya ya TISS tusijifanye vipofu wakati kumbe tunatawaliwa ama tunaenda kutawaliwa kijeshi

Kwa mujibu wa bandiko hili, TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
muswada huu ni majibu ya hoja zangu za bandiko hili, yale mambo niliyoaulizia humu ambayo TISS hawaruhusiwi, kuteka, kutesa na kuua, kwa muswada huu, sasa TISS wanaruhusiwa!.
P
Wewe Mayalla wewe,kuna wakati unajidharirisha,vitu vingine uwe una kaa kimya,sio kile kitu ukiandikie.Nani alikuambia Tiss hawaruhusiwi kuteka?!.Nani alikuambia Tiss hawaruhusiwi kuua?.
Mayalla,kogano nosse ulita shiballa.
 
Hao jamaa hata sheria isipobadilishwa haithiri chochote Ben amepotezwa na wao wao(Zitto alithibitisha baada ya kufanya upelelezi) hakuna aliyekamatwa wala kushitakiwa.

Zakaria aliwapiga risasi hao majamaa walivyotaka kumteka lakini hawakushitakiwa kwa UTEKAJI kwahiyo mimi sioni hata faida ya kwenda kuwalipa wabunge wakae kujadili amendments ni kupoteza muda na fedha za posho haisaidii kitu maana kwa sheria hii wanaua /wanateka/wanajeruhi lakini hawaguswi.
Ili taifa liweze kuwa na amani,ni lazima kuna washenzi ni lazima waumie,
 
Op zote zinaenda kuwa rasmi sasa....

Siyo unaona mkonga kitaani kwako unaanza kurecord na kutuma kwa mitandao...

Kile kimbelembele cha polisi kuingilia mishe za za watu kinaenda kuisha....

Hii ni nzuri, wapewe huo uwezo na siyo kutegemea polisi

Mfanyakazi anawajibika kwenye majukumu yake ya kazi unamletea mambo ya JINAI..

Pigeni kelele, Itapitishwa!
Lengo kuu la Idara ni kutafuta taarifa, kuchakata na kutoa ushauri kwa wafanya maamuzi.

Nyenzo ya kufikia hayo hapo juu ni usiri katika kusaka taarifa hizo.


Sina hakika hilo la kinga ya jinai na kubeba silaha lina mchango mahiri sana kuyafikia malengo. Kulinda jinai kunaindoa nguvu ya usiri katika kusaka taarifa. Jinai haifichiki, hasa hiyo inayosamehewa ndio itasambaa kama moto wa nyika mifano ya matukio hayo yapo, na yamechafua hasa sifa za vyombo.

Tafasiri ya taarifa za kiusalama ni zipi sasa, maana unachorwa sasa mstari mwembamba kati ya Idara, Polisi-CID
 
Sasa kwa sheria hii hii si wanaua ,wanateka na wanajeruhi na hawashitakiwi sasa nini kinaenda kubadilika?
Tanzania imerithi kila aina ya unyama ambayo ilipambana nao against during ilipokuwa mstari wa mbele kupambania afrika

Watu wetu walienda kupambana na wakarudi wameiga namna ya kukandamiza badala ya kuendeleza
 
Ili taifa liweze kuwa na amani,ni lazima kuna washenzi ni lazima waumie,

Si kweli ,hao unaosema washenzi mara nyingi ni wasema kweli ,Lissu kilichomponza ni kufichua ukweli kwamba mkulima styne kachukua ndege....Ukweli haufichiki hata kama ukichelewa.

Serikali za kidikteta mara nyingi hazipendi kuambiwa ukweli ,mbona kwasasa mikutano ya wapinzani inaendelea na wanasema ukweli mbona hawatekwi? Yule Dikteta alikuwa hataki kuambiwa ukweli kwasababu alikuwa anawaongopea watanzania.
 
Kwa hiyo endapo TISS ndio hivi inatik, halafu POLISI qanafanikiwa kupenyeza Boss kutokea TISS na JWTZ hali kadhalika, maana yake itakuwa TIFWILI,yaani watakachoamua wao hichohicho, aaahaa, jamani, mbona maisha haya walau twaishi kwa upendo tu, why mnajiandae saaana jamani! Sio vizuri.

Sent from my SM-G977B using JamiiForums mobile app
 
Lengo kuu la Idara ni kutafuta taarifa, kuchakata na kutoa ushauri kwa wafanya maamuzi.

Nyenzo ya kufikia hayo hapo juu ni usiri katika kusaka taarifa hizo.


Sina hakika hilo la kinga ya jinai na kubeba silaha lina mchango mahiri sana kuyafikia malengo. Kulinda jinai kunaindoa nguvu ya usiri katika kusaka taarifa. Jinai haifichiki, hasa hiyo inayosamehewa ndio itasambaa kama moto wa nyika mifano ya matukio hayo yapo, na yamechafua hasa sifa za vyombo.

Tafasiri ya taarifa za kiusalama ni zipi sasa, maana unachorwa sasa mstari mwembamba kati ya Idara, Polisi-CID

Mkuu

Unaposema wafanya maamuzi....

Unamaanisha nini...?!
 
Sheria kandamizi zote zimetungwa kipindi cha mzilankende akidhani ataishi milele, Sasa kuna watu serikalini wanataka kumwingiza bi mkubwa king alafu baadaye wafanye yao kupitia hao wavaa miwani
Kwanini asiukatae labda unathibitisha mastori ya kitaa kuwa
Bint kirembo yupo pale kama MC tu
 
Wanataka nchi iwe chini ya deep state moja KWA moja kiuongozi yaani hao jamaa wawe na mkono wa mmoja KWA moja KWA watawala namna ya kuiongoza nchi!

Kama hili au lile hawataki bas ukilazimisha unaenda na maji!

SASA Bas;

Kama ikitumika ku vema kuwabana viongozi waliopo madarakani Bas check and Balance itafanikiwa KWA asilimia zote! Elimination method itakua common KWA sana na imehalalishwa!!

Lakini kama just kama ikitumika vibaya,Aiseh hapatoshi kupotea nje nje kama kuku au kifaranga, jamaa wana malengo yao ya kuonyesha makucha wazi wazi hasa katika kipindi cha mabadiliko ya kimfumo ya kiutawala nchini!!!

Ngoja tuone!!
wanalenga kuwalinda waliompiga risas Lisu
 
View attachment 2643253

Nimeweka hii snapshot inayoonesha muswada wa mabadiliko ya sheria ya chombo chetu cha Intelejensia.
Kwenye mapendekezo hususan kifungu cha 19 wanasema hapo kuwa, jinai inaweza kufanywa na TISS personels wakiwa wanatekeleza majukumu yao kwa uaminifu....

Jambo linalonistua ni kwamba, wengi hudhani jeshi kutawala ni mpaka pale jeshi linapopindua serikali ya kiraia. Huu muswada umeleta tafsiri mpya ya utawala wa kijeshi. Tufuatilie kwa akili kubwa sana haya mambo yanavyopangiliwa kwa uangalifu kuelekea imla ya kijeshi...

Nipate elimu kutoka kwenu wanaJF

  1. Kuna ukamilifu gani kwenye jinai?
  2. Kuna uaminifu gani kwenye jinai
  3. Kipimo gani kinatumika kufahamu kuwa jinai fulani imefanyika during utekelezaji wa majukumu kwa uaminifu
  4. Aina gani ya jinai inayoombewa mabadiliko? Ya kutesa au kuua?
  5. TISS ni jeshi au kitengo cha uraia kinachofanya shughuli za kijeshi? Sheria za kimataifa zinasemaje kuhusu utendaji wa jeshi kwa raia?
  6. Huu muswada nani wameomba hayo marekebisho yaani ni TISS au Rais (taasisi/sponsor)?
Lengo na dhumuni la uzi huu siyo kubeza ama kuponda kazi kubwa wanayofanya TISS kwa nchi yetu, bali ninalengq kuangalia motive ya huu muswada ambao umekuja kana kwamba ni by the way lakini uzito wa sentensi zilizotumika kuuandaa ni wake up call kurecall matukio ya kijinai ambayo chombo chetu kitukufu kimehusishwa ama kunyooshewa vidole.

Kwa mahaba mema kwa nchi yangu, I submit

CC: Mzee Mwanakijiji Pascal Mayalla Retired raraa reree Extrovert Bujibuji Simba Nyamaume Mshana Jr zitto junior lumumbai Kiranga Erythrocyte mwanamwana MwanaWA Ebrania Gily Demi
Chukua mfano wa Raila, tangu Kenya wapate uhuru yeye na baba yake ni wapinzani tu. Walitaka Uhuru wakapata uhuru ,(akiwamo Rais).

Wakataka majimbo wakapata majimbo (wao khasa walitaka ukabila, Dholuo wajitawale wamejitawala). Baadaye wakataka katiba mpya wakapata katiba mpya. Wakataka mahakama huru Wakataka kura huru wakapiga kura huru wakashindwa. Wakakata rufaa wakashindwa . Sasa wanaandamana kupinga bei ya mtori. Huyu utamchekea mpaka lini?

Na hapa tunaelekea huko, kumbuka migomo ya Muhimbili na vikundi vya UAMSHO. Kumbuka wasaliti wa makanikia.

Hivi utawachekea hadi lini? Sometimes, it's best to use other ways.
 
Back
Top Bottom