Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

FEBRUARY kaona jamiiforums itamfanya akose urais.kwa mawazo yake anadhani watanzania wanamfahamu kama wanavyomfahamu lowasa,kwa hili amebugi na ndio mwanzo wa kuwafanya watu wazidishe imani kwa lowasa. yeye akae na waganga wake washauriane njia nyingine lakini kwa hii tutamdharau sana,mtoto mdogo anakuwa na sheria za kikoloni utafikiri zee la miaka 152. makamba hatukupi urais ng'o hata ufanyeje

Labda huyu ni puppet wa Joseph Makamba
 
Tunafuata nyayo za China ambayo iliwahi kuingia mgogoro na kampuni ya GOOGLE.
 
Acha kukuza mambo ili kuhalalisha ubakaji wa demokrasia of expression. Hiyo escrow inawauma sana, si mlisema ni uzushi? Huo mswada wako una haraka gani mpaka uletwe kwa dharura? Wacha u-ccm wako hapa.

jibu hoja niliyoitoa kuhusu masuala yalioko kwenye mada hii ya habari. Kama unataka ya Escrow nenda huko kwenye mada ya escrow. Hapa ni mada nyingine kabisa
 
Yericko ameumia, anavyo penda kutungia watu habari za uongo uongo. Ni lazima atanyea debe.
 
Hao police wenyewe wana utaalamu na vitendea kazi vya kusimamia hii sheria? Kwanza kama una vihela kidogo unatengenza kimtandao chako kidogo cha vikompyuta kadhaa halafu unawapiga pini wote na hizo website zao za joomla ambazo ziko wazi mno.
 
Matusi sasa mwisho, wenye kutumia majina bandia na picha za ajabu wataondolewa kwenye blogs. Safi sana
 
Huu mwaka wa uchaguzi tutaona mengi sn......ngoja tuone.
 
Huu muswada sijui unataka kuja rekebisha nini?

Mbona yapo matatizo mengi ambayo yanahitaji ufumbuzi wa hsraka zaidi ya hili....kuna matatizo ktk elimu,afya na hata huduma za maji nchi nzima yenye watu zaidi ya milioni 40,kwanini wasijadili hayo?

Wanaoteza muda ltk kuwadhibiti watumia mtandao 'wachache' labda ni 0.008%ya watanzania wote!!wakati wagonjwa wanalala sakafuni,pia wanafunzi wengi nchini hana madawati/vyoo,maji ubungo tu ni miska zaidi ya 20 ya shida sijui vijijini hali ikoje!? Matatizo ni mengi na mazito zaidi ya huu muswada.
 
Ukwel kama upo huwez kuuficha kama wanafanya maovu watabainika tu
 
This is indeed a ridicule point of view, Having a single side oriented thoughts about someones flaws without having self assessment and assurance on those perception can generally be regarded as EATING A FRESH OF A LIVING MAN.
In safeguarding their personal interests they ruin that of majority.
Most of them are lost sheep...! LOST BLACK SHEEP.
 
Sasa kama napokea picha nyingi za marais, wabunge, wachungaji, maaskofu nk ina maana nina hatia hata kama sikuitaka hiyo picha. Mimi naona kama tutafungwa wengi wasiokuwa na hatia. Asanteni
 
wao waweke sheria zao,sisi tutazivunja tu,nasema barazani kweupee.ngoja niweke bajeti,nanunua laptop maalum,natengeneza kitambulisho maalum,naenda kusajili simcard malum,nanunua modem maalum,nafungua account maalum,na ID nyengine maalum kwa ajili ya kuwalipua mafisadi,na hivyo vitu sivitumii kwa matumizi mengine yoyote zaidi ya hiyo ID maalum,na wala sitaitumia hiyo ID nikiwa na vifaa vyangu vya kawaida.Mumenisikia nyie sijui TRA sijui TCRA sijui nini!mtatafuta kerubi hadi musinzie kwene keyboard,you'll meet with ghosts,na wewe mod wakikuomba IP yangu wape tu,wala usiumize kichwa,tena wape huku umebanwa na kicheko,nyambaf!wanatutafuta kidijitali,tutajificha kianalojia,tuone kipi ni more secure.

mkuu kerubi,umenifurahisha sana kwa kweli.
Hawa jamaa kama huo uchafu utapitishwa na kuwa sheria,wajue kabisa ndio watakuwa wanamwagia petroli kwenye moto,maana kama ulivyoelezea,kuwa "ghost" kwenye mtandao ni rahisi sana,na tutafundishana humu humu,na hapo sasa ndio tutaweka madudu yote hadharani.
 
Naomba frequency ya radio inayotangaza bunge leo. Ningependa kujua wanachojadili huko juu ya huu mswada. Huku nilipo umeme wamekata na nategemea radio tu sasa frequency sina
 
Naomba frequency ya radio inayotangaza bunge leo. Ningependa kujua wanachojadili huko juu ya huu mswada. Huku nilipo umeme wamekata na nategemea radio tu sasa frequency sina
 
Hii imelenga kulinda maslahi ya wanaojiita watawala na si vinginevyo, lakini sisi kama raia tuna haki kuwasema wazi pale wanapokwenda kinyume na maadili ya uongozi na pale wanapolenga kutetetea maslahi binafsi kwakuwa nje ya uongozi nao ni raia kama sisi na wanaweza kusema kama raia wengine wasemavyo
 
Back
Top Bottom