Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015: Kwa mkakati huu wa Serikali, Watumiaji wa Mitandao tutapona?

Wacha tu tushike adabu kwanza maana watu wengi wanatumia mitandao isivyo sahihi kabisa. Pamoja na kwamba yaweza kuwa hii sheria inaibeba serikali ila kwa upande mwingine hata sisi wananchi wa kawaida itatusaidia. Haiwezekani hata hapa Jf watu wanatukana matusi ya nguoni bila kuogopa chochote eti kisa tu ni uhuru wa mitandao. Leo hii mtu akikikuchukia basi anaingia photoshop na kutengeneza picha ya kukudhalilisha kisha anaisambaza mitandaoni. Ifike mahali watu tuheshimiane. Ukienda Instagram watu wanachafuana utadhani hii nchi haina sheria wa vyombo vya dola. Demokrasia bila utii wa sheria ni bure kabisa, na uhuru usiokuwa na mipaka ni fujo. Pengine hii sheria itasaidia kurudisha heshima ya Jambo Forum.
 
Nimemshangaa mleta Uzi kwa kujaribu kutuaminisha ndivyo sivyo,sasa ulitaka kupost habari za uzushi ili ikusaidie nini mkuu ama napata mashaka kidogo yawezekana na wewe ako ndo katabia kako ...kama uko smart why worry?

Anza kwa kuweka picha yako halisi hapa na jina lako kama kweli unaunga mkono kwa dhati hilo pendekezo. Au wewe ni ccm, wanajua kusema na sio kutenda.
 
Ukifanya mambo ya kipumbavu tutasema bila kufinya macho kwamba wewe ni mpumbavu. Hivi ni tusi kubwa kiasi gani serikali kufyonza sh bilioni 300 na kudanganya wananchi. Hivi mwizi akiingia nyumbani kwako akapora hazina yako unamuitaje, rafiki au mheshimiwa. Mafisadi hawana hadhi ya kupata heshima yoyote, hao wanataka kufunga vinywa vya watu. Hao wanao umbuana na picha za uchi ni vichaa, hakuna nchi inayokosa vichaa. Unafikiri serikali imewa target hao, NO. Targeted guys are those who speak the truth, maana ukweli unawauma sana. Serikali ya ccm haitaki kuusikia ukweli ukizungumzwa na watu wa kawaida. Imagine jinsi serikali ya JK ilivyo vurunda, unategemea nini kama sio kufungia mitandao yenye mawazo chanya. Sitashangaa hizo blogs za matusi ndio zikaachiwa na kushamiri maana wakubwa wengi wako huko.

huna hoja umechemsha. Nikupe mfano mmoja tu atokee mtaalam mmoja wa kutengeneza picha kwa kutumia computer akachukua picha ya mtu mwingine analiwa tg kisha akachukua sura ya mama yako akaibandika pale kuwa yeye ndio analiwa tg. Wewe utajisikiaje? Sio kila kitu mnapinga tu. Hapa mada ni mswada wa vyombo vya habari wewe unaleta escrow
 
Vijana wanasambaza picha zao za Uchi kwa kasi that's why...
Acha tu wabebe maji kwenye chujio na ndoto zakujaza Pipa...

Angekuepo Marehemu Komba lazma angetilia mkazo sana suala hili.
 
Acha uongo banaaaa sasa hivi kuna thread inaonyesha mtume wenu Gwajima kafariki mbona mmeiweka bila kuthibitisha? Na huko nyuma mlikuwa mnaminya sana habari za mnaowapigia chapuo lakini teknoligia imekuwa challenge kwenu. Na nyie ondoeni ban,maana haina maana inanyima uhuru wa maoni
Kweli kiongozi
 
Ndo maana sheria inasema kama una taarifa basi uwe na ushahidi wa kutetea taarifa yako.

Ninaposema upotoshaji sina maana ya mambo ya aikina chenge mkuu, kuna upotoshaji mwingi sana kwenye mtandao wengine mpaka wanazushiana vofo n.k

Kwa hiyo nadhani sheria ya namna hii itaongeza credibility ya habari na taarifa zote mtandaoni.

Kwa hiyo kama kuna viashiria vya ufisadi tusiseme mpaka vitokee? Mfano usiseme kuwa ikulu inahusija na ufisadi wa escrow mpaka mnikuru Gurumo atakapopasua jipu! Hivi sisi waTZ tuko sayari ipi?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
WATANZANIA TUUNGANE KuMPINGA JANUARY MAKAMBA,NI MKANDAMIZAJI WA WANANCHI ANATAKA KUTUNYANG'ANYA UHURU WETU. PIA VILEVILE TUSIMSAPOTI KWENYE MBIO ZAKE ZA URAIS.TANZANIA SIO YA MAMA YAKE KUTUAMULIA KILA KITU ANAVYOTAKA YEYE.NDO MAANA KAPEWA KAZI YA KUANDAA HOTUBA ZA RAIS ,WATANZANIA TUMPINGE KWA HALI ZOTE HUYU MSALITI WA BUMBULI ARUDI KWAO MPONDE NA MB 8 ZAKE. NA KUANZIA LEO TUNAJIUNGA NA LOWASA RASMII NDO MAANA ALIKUWA HAMTAKI LOWASA SASA TUMEMSHTUKIA ,MTOTO MDOGO LAKIN ANAMAMBO YA KIZEE

Kama ni kuachana na Makamba, then niende kwa Fisadi Lowassa, kawaulize AICC aliwafanya nini? Bora nibaki Team Membe ~ Mwana Usalama wa Taifa Mstaafu
 
Enyi wabunge wetu,tunaowachagua kwa kura zetu,tunaomba hili lisipite.Sheria hii inawalenga hata nyinyi na watu wengine nyeti serikalini ambao kwa uzalendo wao kwa taifa,na kukerwa na maovu ya wenzao serikalini, wanaamua kutumia fake ID'S even sometimes fake names and profile details ili kuizindua jamii.

Sote tu mashahidi mtandao kama JF umechangia kiasi gani ishu kama za escrow etc. Serikali yenyewe inapata habari nyingi humu na kuelewa mitazamo ya watu juu ya mambo mbalimbali, jambo linalowasaidia kufanya maamuzi sahihi. Juzi juzi tu hapa JF kulitolewa information na ID fulani kuhusu uwepo wa magari yanayofanana namba za usajili,siku chache baadae tukasikia TRA ikitoa tangazo kuita wahusika wakajieleze. Tayari raia huyu mwema ametoa taarifa ambayo dola ikifanyia kazi itaokoa mamilioni ya kodi zinazokwepwa.

Tena ni suala lenye faida kwa serikali,wala mtoa mada kama ni raia wa kawaida hafaidiki na chochote binafsi. Sasa mtu ukijua JF inaweza kubanwa kutoa IP address yako, mnafikiri watu watatuma vitu vya aina hii? Mmefikiria upande wa ufisadi unaowaumizeni tu, hamjafikiri kuwa nyie ndio wanufaika wakubwa wa info zilizomo humu. Mimi mwananchi wa kawaida utanibana nitakaa kimya,but remember, watoaji wakubwa wa habari nyeti mitandaoni ni nyie nyie watu wa serikali kwa kutoridhika na mambo huko juu. Hawa hamuwawezi,mkiwabana wasitoe nyongo zao humu,they'll give you a direct fight, wala hawatakubali.

Kupenda mabadiliko pale asiporidhika ni nature ya binadamu.You can't fight nature,you have to live with it.The only way ni kumridhisha.Kama wananchi hawaridhiki na uongozi wao, mabadiliko ni lazima. Hata mfungie hadi tv stations,we will find another way to communicate and give you a fight. Hii fight hamtaikwepa kwa kubana media, itakuwepo tu, suala si mimi kumiliki pc yenye net,bali suala ni mimi kurudi nyumbani na kukuta wanangu wana njaa huku sina hela,na huku natumikia kazi kikamilifu bila kupata ninachostahili.Suala ni kuniridhisha,nitulie. Vita iko mioyoni mwetu, sio kwenye server za JF.

Open up your mind nyinyi viongozi vipofu msiojua maamuzi sahihi ni yepi.Always mnarukia kuficha matatizo badala ya kutibu.Wabunge kataeni huu mswada kwa manufaa yenu wenyewe. Watanzania wenzangu October tusichague mgombea yeyote mwenye any connection na uongozi huu wa awamu ya nne. Naukataa sana utawala huu, unaiharibu nchi sana, haufai, si rais, waziri, rc, e.t.c yaani vitu ambavyo sijawahi kuvifikiria vitatokea, vinatokea kwenye awamu hii. Hivi hakuna think tanks huko serikalini? Mbona serikali hii ya kienyeji enyeji hivi? Hekima ya kuona mbali iko wapi?

Jamani, hivi watz tulichaguaje hawa watu? Jesus Christ!
 
Nilichosoma katika utaratibu na taratibu za serikali ya ccm ni kulinda uchafu,kuhalalisha uchafu na kuendeleza uchafu.

Sheria ina lenga kuwabana watu wasiweze kujieleza,kupata habari na kushea.
Ahsante kikwete ila habari sio lazima iwe kwenye mitandao.
Mdomo kwa mdomo ni njia tosha zaidi ya speed ya mwanga.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mkuu kwa serekali kuamua kudhibiti taarifa au habari tunazozipata sisi wananchi ni suala la kawaida kabisa.hii ni kuepuka kiliingiza taifa kwenye machafuko.china wameblock facebook,twiter,youtube na links nyingine nyingi tuu ili ku control taarifa wanazopata wananchi.and believe me,kwa sisi wananchi wa kawaida kuna mambo mengi ambayo ili kuishi kwa amani na furaha ni vizuri kama hatutayajua.serekali haziendeshwi kwa namna tunavyofikiria.be blessed!

Mbona husemi china wanawanyonga watuhumiwa wa madawa ya kulevya au kwamba wao wanakula vyura. Kwani sisi tunafuata siasa za uchina? Usiige kunya kwa tembo ... hakuna swala la kawaida hapa! Kwa nini wamelifungia gazeti la -----------? Kwa nini wanawakamata watu wanao andamana kutaka kuzungumza ukweli kweupe mchana, kwa nini wanawapiga wanaharakati, Ulimboka? Msijifanye vipofu au mmevaa miwani za mbao kutoona lengo la ccm na serikali. Kwa nini mswada uwe wa dharura?
 
Tatizo kuna watu wanaharibu sana jf kwa mada mbovu mbovu!

Jifunze kuishi na watu walio chini ya kiwango chako. Mfano ukiwa raisi hata vichaa ni wananchi wako unawajibika kuwalinda. Hii JF ni shule pia, wengine watabadilika na wengine watahalibika jali unachokisema wewe. Unajua hili janvi sio dini, mod akiruhusu thread itoke basi ikubali na una uhuru wa kupita tu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Sheria inasema atakayeandika habari za uongo na uzushi atapata adhabu............. Sasa mnaogopa nini kama mnaandika habari za kweli? Kumbe mlikuwa kazi maalum ya uzushi humu Jf kuchanganya watu? Raia mwema hana hofu na polisi. Kwa hii naunga mkono 100%

Serikali nzima ilisema scandal ya escrow ni uzushi, yako wapi leo! Sasa wanataka kuzikana hata methali zao, kila panapofuka moshi pana moto. Sisi tukiona moshi (call it uzushi) tutasema ili aliyewasha moto ajulikane, sasa sheria inataka mpaka tuone moto! Moshi unapanda juu ni rahisi kuuona.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ukifanya mambo ya kipumbavu tutasema bila kufinya macho kwamba wewe ni mpumbavu. Hivi ni tusi kubwa kiasi gani serikali kufyonza sh bilioni 300 na kudanganya wananchi. Hivi mwizi akiingia nyumbani kwako akapora hazina yako unamuitaje, rafiki au mheshimiwa. Mafisadi hawana hadhi ya kupata heshima yoyote, hao wanataka kufunga vinywa vya watu. Hao wanao umbuana na picha za uchi ni vichaa, hakuna nchi inayokosa vichaa. Unafikiri serikali imewa target hao, NO. Targeted guys are those who speak the truth, maana ukweli unawauma sana. Serikali ya ccm haitaki kuusikia ukweli ukizungumzwa na watu wa kawaida. Imagine jinsi serikali ya JK ilivyo vurunda, unategemea nini kama sio kufungia mitandao yenye mawazo chanya. Sitashangaa hizo blogs za matusi ndio zikaachiwa na kushamiri maana wakubwa wengi wako huko.

Mkuu hivi unajua mimi naweza kamata picha yako nikamtumia shigongo akaweka kwneye magazeti yake ya upuuzi. Hakuna sheria inayombana yeye wala wanao tuma picha za watu tupu online.
 
Kuna watu humu wanaifurahia hii sheria bila kujua kwamba, imetengenezwa mahsusi ili kuifungia kama siyo kuifuta kabisa Jamii Forums.

Huu ni mkakati maalum wa kuzuia uhuru wa kupata habari hasa ktk kuelekea uchaguzi mkuu.

Hatma ya hili suala liko mikononi mwa wabunge wazalendo na wapenda maendeleo.

JF live long.......

mkuu hajalengwa mwananchi wa kawaida hapo ambaye hana mambo mazito ya kuilipua serikali humu.Hawa wamelenga kubana wamiliki wa mitandao pamoja na watumiaji wanyetishaji toka serikalini.pamoja na wabunge,viongozi,wanausalama wanaotumia fake ids kuilipua govt humu.Wanadhibiti watu wao wasilete nyeti humu kwani hao ndio wanaozidisha awareness ya wananchi kwenye mambo ya kiserikali.It means kuna umafia mzito unapangwa uchaguzi huu.
 
huna hoja umechemsha. Nikupe mfano mmoja tu atokee mtaalam mmoja wa kutengeneza picha kwa kutumia computer akachukua picha ya mtu mwingine analiwa tg kisha akachukua sura ya mama yako akaibandika pale kuwa yeye ndio analiwa tg. Wewe utajisikiaje? Sio kila kitu mnapinga tu. Hapa mada ni mswada wa vyombo vya habari wewe unaleta escrow

Acha kukuza mambo ili kuhalalisha ubakaji wa demokrasia of expression. Hiyo escrow inawauma sana, si mlisema ni uzushi? Huo mswada wako una haraka gani mpaka uletwe kwa dharura? Wacha u-ccm wako hapa.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kama ilivyokuwa kwa SOPA (Stop Online Piracy Act) na PIPA ( Protect IP Act) Marekani, mwaka 2012,sheria hii si rafiki kwa watumiaji wa mtandao. Ni kweli kumekuwa na matumizi mabaya sana ya mtandao lakini sheria hii haitamaliza hilo tatizo,Kamwe!

Mtandao wa internet uliundwa uwe huru na watu wanapigania sana uwe huru lakini uhuru huo utapotea mara moja tukisharuhusu ''censorship". Kila siku sisi hulalamika kuhusu matumizi mabaya ya madaraka katika mamlaka tofauti tofauti za serikali na hii sheria inaongezea madaraka zaidi mamlaka hizohizo. Na hapo tusisahau kwamba mtandao ndio jukwaa lililobakia huru ambalo hata "mwananchi wa kawaida" anaweza akatoa mawazo yake kwa sasa.

Kwahiyo wakati tukifurahi kwamba picha za utupu na habari za uzushi zitakoma mtandaoni (kitu ambacho si kweli), ni vyema tukiliangalia hili swala kwa upana wake kujua kwamba malengo hasa ya muswada huo ni nini na huku tukifahamu wazi kabisa;

1.Sheria hiyo haitasaidia kutokomeza yanayotukera mtandaoni kwa sasa
2.Lugha iliyotumika ni tatanishi na pana kiasi cha kuruhusu kutumiwa au kutafsiriwa vibaya
3.Kuweka vidhibiti kwenye Mtandao ambao ni haki uwe huru na wazi

Naamini kuna namna nyingi tofauti za kuweza kutoa kero na kuweka mambo sawa katika mitandao lakini huu muswada si mojawapo. Nina imani ukipita tutakachokipoteza ni kikubwa kuliko tutakachokipata.
 
jf na nyinyi mbadilike,hii tabia ya kutoa ban/kufuta thread/ wakat mwingne mnaangalia mtu na mtu sio fair
 
Dah kweli Noma wanaacha kukomaa na mafisadi wanakuja kuonea wanyonge aagh kama vipi nchi Yenyewe tuuze kila Mtu adake chake tutembee manake co poa mzawa unaish kama mkimbizi
 
Back
Top Bottom