Sheria ya Ndoa: Maswali na majibu mbalimbali

Sheria ya Ndoa: Maswali na majibu mbalimbali

Fanza hivi
1. Peleka malalamiko yako kwenye Baraza la Usuluishi linalotambulika kisheria (Ofisi ya ustawi wa Jamii, Kiongozi wa Kanisa mwenye mamlaka ya kufungisha ndoa)
2. Baraza/Kiongozi husika atawasikiliza wanandoa wote na kuona kama anaweza kuwashauri ili msamehane na kuendelea kuishi pamoja. Kutengana kisheria/makubaliano huwa ni mbadala katika hili.
3. Endapo usuluishi utashindikana Baraza/Kiongozi husika atakupatia Barua/Hati ya kushindwa kusuluishwa. Barua/Hati hiyo itaandikwa ikielekekzwa kupelekwa katika Mahakama husika.
4. Ukifika Mahakamani unatakiwa kulipia gharama za kufungua Kesi ya Ndoa ili kuomba TALAKA na Kuvunja Ndoa yenu rasmi kisheria ukipenda na mgawanyo wa mali za ndoa plus matunzo ya watoto kama wapo. Kumbuka kuambatanisha Madai yako na Cheti cha ndoa
5. Mahakama itasajili Kesi yako ya Madai ya Talaka na kukupa Hati ya kumwita Mkeo Mahakamani ili kujibu madai dhidi yake
Angalizo;
Sababu kubwa ya kuvunja ndoa na kutoa Talaka huwa ni KUWEZA KUITHIBITISHIA MAHAKAMA KUAMINI KUWA NDOA YAKO IMEVUNJIKA KIASI AMBACHO HAIWEZI KUREKEBISHIKA TENA.
Aidha Mahakama uangalia mambo muhimu/vigezo vifuatavyo ili kujiridhisha
(a) Ugoni
(b)Ukatili
(c)Kulawiti
(d)Kichaa
(e) Kuzembea wajibu kwa makusudi
(f) Uasi/Utoro
(g) Kutengana - kusiko pungua miaka 3
(h) Kifungo
(i) Dhana ya Kifo
(j) Tofauti za Dini/Kubadili Dini

Anyway huo ndo ushauri wangu faster lakini kwanini uvunje ndoa Bana, gangamala maisha sio mchezo etiii.

Kwa vile ndoa ni makubaliano ya watu wawili, vipi kama hao watu wakiamnua by mutual consent kuvunja makubaliano yao ya kuishi pamoja? Kwani ni lazima kuwe na ugoni, ukatili, kulawiti, nk? Si wanaweza kukubaliana tuu hata kama hayo uliyootheresha hapo juu hayapo? Mahakama inaweza kukataa?
 
KIBONGOMKUTI

Mbona huo mlolongo mkubwa mno hivyo?!

Unaweza kukuta watu wanakuwa emotional abused kwenye ndoa wanashindwa kutoka kwa sababu hawawezi kuonyesha wazi mateso, na mmoja kati ya wana ndoa hajakubali kuwa ndoa hiyo haiwezi kuendelea tena.

Something needs to be done, kulegeza masharti hayo.

Hii haijakaa sawa

Ndo maana hata mie nilitaka kujua vipi kama wanandoa wamekubaliana by mutual consent kuachana. Kuna haja ya kupitia mlolongo wote huo? Kuna haja gani hapo kuwahusisha baraza la usuluhishi? Si wamekubaliana kuachana by mutual consent?
 
Ndo maana hata mie nilitaka kujua vipi kama wanandoa wamekubaliana by mutual consent kuachana. Kuna haja ya kupitia mlolongo wote huo? Kuna haja gani hapo kuwahusisha baraza la usuluhishi? Si wamekubaliana kuachana by mutual consent?

Hapa wajuzi wa sheria wanahitajika. Haiingii akilini kuwa nyie wenye ndoa mmeamua kuvunja uhusiano wenu kwa sababu zenu wenyewe mlazimishwe kusuluhishwa.

Ni kupoteza muda na resources nyengine tu.
 
Hebu jaribu kucheki na Dr Katibu mkuu wa chama chetu nadhani anaweza kukusaidia katika hili maana anaka-experience kidogo.
 
Ujue ndoa za kikristo kimsingi hazivunjwi, ni mpaka kifo kiwatenganishe wanandoa. Nadhani inategemea pia umefunga ndoa ya kikristo ktk madhehebu gani. Kuna madhehebu ambayo kukiwa na matatizo fulani mazito ktk ndoa, yanaweza "kuivunja" ndoa hiyo na kukupa nafasi ya kufunga. Lakini kuna madhehebu ambayo nafasi hiyo ni finyu mno-mno.

Mkuu Babuyao huo ndio ukweli wa ndoa za KIKRISTO.
 
Mahakama yaweza kuvunja ndoa ya aina yoyote ile iwayo. Hatahivyo,kikanisa utafungiwa sakramenti...
 
Unfortunately hii sababu yako jaikidhi kuachana. Kama wewe mkristo muombee.
Tatizo kubwa ni mke kabadili kabisa muelekeo kiimani kitu ambacho kinakingana na ile imani iliyokuwapo awali wakati wa kutoa kiapo cha ndoa kanisani. Licha ya kuonywa na kukatazwa mume, pia ndugu, jamaa na hata kasisi wamemshauri aondokane na hiyo imani yake mpya, bila mafanikio. Hii inaleta hali ya kutoaminiana na kuvunjika kwa amani nyumbani.
 
Kwahiyo ukishaoa kikristo ndoa ikakushinda,basi hutoki,utazini tu mpaka ufe,na ikifahamika kuwa umemtenga mkeo na unamwanamke mwingine unaishi nae hautazikwa kikristo??
 
Tatizo kubwa ni mke kabadili kabisa muelekeo kiimani kitu ambacho kinakingana na ile imani iliyokuwapo awali wakati wa kutoa kiapo cha ndoa kanisani. Licha ya kuonywa na kukatazwa mume, pia ndugu, jamaa na hata kasisi wamemshauri aondokane na hiyo imani yake mpya, bila mafanikio. Hii inaleta hali ya kutoaminiana na kuvunjika kwa amani nyumbani.
ulokole @ work...........hivi mie najiuliza kwanini akina mama ndio wanao hamaga dini sana? yaani utakuta mama kazaliwa mlutheri akaolewa Rc so akabadili( of which is not bad) huko nako akaona hakuna Mungu kwa imani utamkuta kwa mwingira kesho akiona nako hakuna dini utamkuta Agape sasa najiuliza ivi sisi wanawake tumelogwa ama ni ujinga wa kuzaliwa? kwanini sisi kila siku ni chanzo cha matatizo kwa kupenda kuyumbisha misingi ya familia?

naumia kwa hili sana tu halafu utakuta mama akiingia kwenye haya makanisa ya siku hizi kutwa kucha anakesha kanisani kusali na kutumikia kanisa anasahau familia kabisa siriaz niliona mama mmoja anamuhudumia mch kuliko mumewe hadi mume akamwambia sasa ama uende ukaish na huyo mch ama ubaki hapa nyumban na penyewe bado mama akagom ukawa ugomvi wa ajabu hadi padri kuingilia kwani mama alianza kumyima mumewe unyumba kisa tu hajaokoka jamani jamani acheni tu dunian kuna mambo........
 
Asante kwa maoni yako. Nachotaka kufahamu ni sheria imekaaje kuhusu tatizo hili. Isitoshe jee kiapo cha ndoa kilichotolewa dhehebu moja bado kitaendelea kuwa halali kama mmoja wa wanandoa baadaye aamue kujitoa kwenye dhehebu lake na kuingia dhehebu lingine?

Ni kama ulivoelezwa na wadau kadhaa..hoja ya kubadilika imani ni dhaifu.. haitasababisha talaka. Nijuavyo mimi madhehebu yote huwa yanatambua ndoa ambazo tayari zimefungwa sehemu nyingine. na ndio maana hata kama watu hawakuwa na ndoa lkn wana watoto na waliishi kama mume na mke madhehebu mengine huwa yanabariki tu..
ushauri wangu ni kuwa achana na talaka jipange kutatua hilo tatiz la kiimani.. labda kama kuna ishu nyingine hujasema
 
wewe tafuta njia ya kuimarisha ndoa upewe ushauri ila kuvunja mmmh binadamu hatakiwi kuwatenganisha
 
ili kuweka mambo sawa weka dhehebu mlilofungia ndoa, taratibu za kuvunja ndoa zinatofautiana sana sana kati ya dhehebu moja na lingine. Kisheria mkikubaliana na mwenzi wako manavunja ndoa mara moja haina tatizo lakini ndio hivyo kama ni mkatoliki utakosa huduma zote za kiroho i.e hautaruhusiwa hata kwenda kanisani na hata ukifa utazikwa na manispaa.
kama ni mkatoliki tatizo linaanza kushughulikiwa kwa masuluhisho kuanzia jumuiya.. parokia...jimbo... mpaka pope. Mchakato wake mpaka kukamilika nilisikia unaweza kuchukua miaka 30
 
Hii nimesoma kwenye mtandao. Mwenye kufahamu tafsiri yake halali tafadhali niwekee hapa.

Vinginevyo nashukuru kwa michango yenu wote mliochangia.

http://rita.go.tz/laws/History%20Laws/Marriage%20Ordinance,%20%28cap%2029%29.pdf


91. Recognition of decrees of foreign courts

Where a court of competent jurisdiction in any foreign country has passed a
decree in any matrimonial proceeding, whether arising out of a marriage contracted in
Tanzania or elsewhere, such decree shall be recognised as effective for all purposes of
the law of Tanzania–

(a) if the petitioning party was domiciled in that court or had been resident there for
at least two years prior to the filing of the petition; or

(b) being a decree of annulment or divorce, it has been recognised as effective in a
declaratory decree of a court of competent jurisdiction of the parties or either of them.

92. Recognition of extra-territorial divorces
Where any person has obtained a divorce, otherwise than by decree of a court in
Tanzania, in any foreign country, the divorce shall be recognised as effective for all
purposes of the law of Tanzania if–


(a) it was effective according to the law of the country of domicile of each of the
parties at the time of the divorce; or


(b) it has been recognised as effective in a declaratory decree of a court of
competent jurisdiction in the country of domicile of the parties or either of them.
 
Mkuu, ndoa haimuzuii mtu kubadili dini kwani kuabudu ni moja ya haki msingi za mwanadamu. Wewe mwanandoa una haki kwa mkeo/mumeo katika mengi mf. tendo la ndoa, kuishi pamoja, kusaidiana. Lakini huna haki ya kumiliki maisha yake ya kiroho (ila haki na wajibu wa kumsaidia kuishi imani yake lakini si kummiliki kiimani). Unachotakiwa wewe kukidai kutoka kwake ni huduma zake, yaani haki zako wewe za kindoa. Huna haki za kiimani kwake.

Sawa, lakini hata sheria (inaonekana) imetambua umuhimu wa tofauti za kidini katika ndoa iwapo mmoja wa wanandoa ataamua kubadili dini katika ndoa. Huwezi kuendelea kuishi na mkeo kama hamuelewani kutokana na imani mpya za kidini alizokumbatia.
 
ulokole @ work...........hivi mie najiuliza kwanini akina mama ndio wanao hamaga dini sana? yaani utakuta mama kazaliwa mlutheri akaolewa Rc so akabadili( of which is not bad) huko nako akaona hakuna Mungu kwa imani utamkuta kwa mwingira kesho akiona nako hakuna dini utamkuta Agape sasa najiuliza ivi sisi wanawake tumelogwa ama ni ujinga wa kuzaliwa? kwanini sisi kila siku ni chanzo cha matatizo kwa kupenda kuyumbisha misingi ya familia?

naumia kwa hili sana tu halafu utakuta mama akiingia kwenye haya makanisa ya siku hizi kutwa kucha anakesha kanisani kusali na kutumikia kanisa anasahau familia kabisa siriaz niliona mama mmoja anamuhudumia mch kuliko mumewe hadi mume akamwambia sasa ama uende ukaish na huyo mch ama ubaki hapa nyumban na penyewe bado mama akagom ukawa ugomvi wa ajabu hadi padri kuingilia kwani mama alianza kumyima mumewe unyumba kisa tu hajaokoka jamani jamani acheni tu dunian kuna mambo........

Hapa umezungumza ukweli mtupu. Iweje mke aende kusali/kufanya maombi kila siku, siku saba kwa wiki? Na mbaya zaidi hata watoto hawahudumii vilivyo kama ilivyokuwa awali?
 
Imekula kwako kama vp badili dini kama chamelleone then oa muke mwingine!
 
Kuna tofauti za msingi kati ya madhehebu mbalimbali ya kikristo. Kwa hiyo ile kwamba wote ni wakristo siyo hoja.

Mbona umpe talaka jamani?MUNGU ANACHUKIA KUACHANA,usichoke kuongea nae ili arudi RC mwambie MUNGU haangalii dhehebu hata ukiwa katoliki anabariki tu.
 
Back
Top Bottom