Shibuda: Magufuli aliniahidi kunipa mil 5 nikalipe ada ya watoto lkn nilipompinga akanigeuka

Shibuda: Magufuli aliniahidi kunipa mil 5 nikalipe ada ya watoto lkn nilipompinga akanigeuka

Eti wanao hawajambo? Hawajambo
Nataka kuchangia ada

Yeye aseme alisema hawajambo mkuu ila hawa wawili wako nyumbani sina ada mkuu okoa jahazi ndipo mzee akasema atamchangia kabla hajayatinyanga akanyimwa

Hakuna mwanasiasa anayependa kuchanwa ukweli, Huyu mama gazeti liliandika hana nia kugombea akalifungia
 
Kuna Kamanda Mmoja alipopata tu fursa ya kuonana na Rais akaanza kuomba sijui pesa za matibabu sijui marupurupu ya Bunge yaan anawaza pesa tu na akitoka hapo anasema Muhimili wa Bunge unaingilia na Rais wakati yeye mwenyewe kamshawishi Rais aingilie
Viongozi wa upinzani ni omba omba sana.

Freeman Mbowe pekee ndio tajiri.
 
Yaani ndo mjue nguvu ya chadema sasa...millions tanoooo ya ada inatia aibu hivi kweliiii?
 
Jiwe alikuwa na roho mbaya sana, na ndiyo maana Mwenyezi Mungu alimtwaa haraka haraka!
Jamaa alikuwa anakusimanga hata wakati wakula,huoni hata mwili unakuja kwa retired 1 reeeede
 
tutasikia mengi shibuda bado anazalisha tu eti watoto wanasoma achangie milion 5 ,mtu sahihi wakuendesha democrasia baada ya kifo Cha maalim seif kabakia pekee Freeman aikael mbowe ,huyo mzee milion tano

Zito kabwe itakua shinga?
 
Ulitaka aseme magu akiwa hai ili amiminiwe mvua ya risasi kama lissu?

Mtu unamuona kabisa kakaa kinyamelanyamela ujitokeze tu useme.

Haiwezekani lazima uufyate tu.
Hapana mkuu angesema tu hayati akiwa hai mashaka yangu ni kwamba isije kuwa marehemu anasingiziwa tu kwa sababu hana nafasi ya kukanusha
 
Ayaseme wakati yupo hai! kwani hajipendi yeye?

Sote tuliufyata wakati wa "bwana yule".
Angalau angekufa amesema ukweli kuliko kuongea sasa maneno mazito kama haya ambayo yangesaidia kuwafungua macho watanzania waliokuwa hawajui tuna rais wa namna gani. Kwa mfano ikiwa shibuda ndiye alienda kulia njaa akaambulia patupu nani atatusaidia kubalance hii habari?
 
Akizungumza kwenye kongamano la kuenzi falsafa ya hayati Magufuli ya tanzania ya viwanda, ndugu Shibuda amesema siku moja alipata nafasi ya kumtembelea rais Magufuli ikulu.

Anasema siku hiyo Magufuli alimkaribisha ikulu na kumuuliza vipi watoto hawajambo? Akajibu hawajambo akamwambia nataka kuchangia ada yao shilingi mil5

Shibuda akajibu asante lakini sijaridhishwa na namna unavyoendesha demokrasia katika utawala wako ndipo rais akasema sasa hata hiyo hela sikupi.

Kwa nini Shibuda hakuyasema haya Magufuli akiwa hai?
Mwanaume mtu mzima aina ya Shibuda unalilia mil 5 kweli. Huu ni ujuha.
 
Magufuli alikuwa mtu wa matani Sana kwa wale tuliyemzoea haitupi shida, tatizo linakuja kwa wale ambao siyo waelewa ukutute Rais alimtania yeye akayaweka moyoni hapa ndipo wabongo tunafail

Note; Kuna watu hawataniwi yaani kitu kidogo wanakikuza ila nimejifunza usiweke matani penye userios ila weka matani penye matani over
 
Na yeye Alimpinga baada ya kuona pesa yenyewe ndogo,Angeambiwa mil.50 Angeongea tena.
 
Shibuda tutakuamini vipi ikiwa wamsema marehemu?
 
Back
Top Bottom