Shibuda: Magufuli aliniahidi kunipa mil 5 nikalipe ada ya watoto lkn nilipompinga akanigeuka

Shibuda: Magufuli aliniahidi kunipa mil 5 nikalipe ada ya watoto lkn nilipompinga akanigeuka

Si unatuona tumerudi JF, ulituona wakati wa "bwana yule"? Tuliingia "mitini" wote.

Hata wafanya biashara wenye mitaji mikubwa waliihama nchi, lakini sasa wamerudi na AlhamduliLlah pesa zinazunguka tena mitaani. Huyajuwi hayo?
Wafanyabiashara Wenye biashara chafu ndiyo walikimbia,Sasa wanarudi tena na biashara zao chafu,but time will tell!!
 
Umeona eeh? Ben mwana JF mwenzetu tukibishana nae sana kisiasa humu JF yuko wapi? Tuliogopa sana na tulikuwa na haki ya kuogopa. Nchi ilifikia mpaka mawaziri wanatolewa bastola hadharani na hakuna linalofanyika.

Miaka ya bwana yule ilikuwa migumu sana kwa kila Mtanzania na hata wageni waaliopo Tanzania, yaliwakumba. Hata waliokuwa wanamtetea walikuwa katika hali ngumu, wakijikaza kisabuni tu. Tumeyaona.
Lakini wenye chama, wanasema alikua anakijenga chama chao kwa kuufutilia mbali upinzani. Maana bwana yule alihakikisha vyama vya upinzani havipandi majukwaani na vilikanyagwa hasa. Angalia uchaguzi wa 2020 ulivyoiacha nchi imepasuka (bunge la chama kimoja na kulazimika kuwatengeneza Covid-19), ambayo sasa mama anajitahidi kuiunganisha.

Ingawa kazi bado anayo, kwa sababu wateule wa mwendazake ambao baadhi bado anao, kuna maeneo wanamshauri vibaya au kutenda vibaya na kujikuta mama analazimika kurekebisha kwa gharama kubwa za kisiasa. Mfano kesi ya ugaidi ya Mbowe na walinzi wake watatu.
 
Nilivyosoma mimi ni kuwa Shibuda hajaomba, alipewa ofa.


Kasome tena uzi, usisome bichwa la habari tu ukaanza kuhukumu.
Ebu jiongeze akili kidogo,za kuambiwa changanya na zako,Magu alijuwaje Kama Shibuda ana shida ya ada za Watoto kama si Shibuda mwenyewe kueleza matatizo yake!? Shibuda kapindisha maelezo ili yeye aonekane mzuri na kumchafua Magu!!
 
Hata wewe muoga. Nani asiyeogopa Tanzania? Tanzania tulianza kutishwa ilipoanzishwa "presidential detention act" Uliza wajuzi wakujulishe ni nani aliianzisha na nani akaifuta? Na wajanja wengine walipoona hiyo haipo wakajitungia sheria zilizopendekezwa na USA za kukandamiza watu, mfano sheria ya "ugaidi" iliyomfunga Mbowe. Au sheria za utakatishaji fedha na sheria ya uhujumu uchumi. Umeshawahi kujiuliza kwanini hizo hazina dhamana? Mimi nasema sheria hizo ni ukandamizaji, anakutuhumu kwa sheria hizo kaamua kukumaliza kwa mateso, kidogo kidogo, hatafuti haki wala hataki kujuwa haki iko wapi. Ni mateso tu ya kuhukumiwa bila ya hatia.

Ni wachache sana wasioogopa. Wasioogpa ni wale wanaokuja humu JF kwa majina yao na kutoa mawazo yao kinaga ubaga. Wengine tunaokuja na id za kujipachika ni waoga ytu.
Umeeleza ukweli kabisa. Tuweke pembeni mambo ya itikadi, tuungane na tujenge nchi yetu. Nchi imepita kipindi kigumu sana kwa miaka 5+
 
Basi mtindo wake wa kuwasilisha mada upo katika style ya masihara.
Shibuda anajua sana kiswahili. Anatumia misemo na lugha zenye misamiati migumu kufikisha ujumbe. Wengi wanaweza wasimuelewe. Ni Msukuma aliyekielewa kiswahili vizuri sana na hata matamshi yake, huwezi kuamini kwamba ni Msukuma.

Cc FaizaFoxy
 
Viongozi wa upinzani wakipata nafasi ya kuzungumza na Rais huwa wanakuwa na hoja nyepesi na maswala binafsi tu.

Hata Lisu aliomba mambo binafsi mengi tu.
Na yote hayo binafsi yanatokana na risasi 38 mlizommiminia kama mnataka kuua tembo.
 
Akizungumza kwenye kongamano la kuenzi falsafa ya hayati Magufuli ya tanzania ya viwanda, ndugu Shibuda amesema siku moja alipata nafasi ya kumtembelea rais Magufuli ikulu.

Anasema siku hiyo Magufuli alimkaribisha ikulu na kumuuliza vipi watoto hawajambo? Akajibu hawajambo akamwambia nataka kuchangia ada yao shilingi mil5

Shibuda akajibu asante lakini sijaridhishwa na namna unavyoendesha demokrasia katika utawala wako ndipo rais akasema sasa hata hiyo hela sikupi.

Kwa nini Shibuda hakuyasema haya Magufuli akiwa hai?
Pumbavu we, unatamka mwenzako apotee?
 
Hata wewe muoga. Nani asiyeogopa Tanzania? Tanzania tulianza kutishwa ilipoanzishwa "presidential detention act" Uliza wajuzi wakujulishe ni nani aliianzisha na nani akaifuta? Na wajanja wengine walipoona hiyo haipo wakajitungia sheria zilizopendekezwa na USA za kukandamiza watu, mfano sheria ya "ugaidi" iliyomfunga Mbowe. Au sheria za utakatishaji fedha na sheria ya uhujumu uchumi. Umeshawahi kujiuliza kwanini hizo hazina dhamana? Mimi nasema sheria hizo ni ukandamizaji, anakutuhumu kwa sheria hizo kaamua kukumaliza kwa mateso, kidogo kidogo, hatafuti haki wala hataki kujuwa haki iko wapi. Ni mateso tu ya kuhukumiwa bila ya hatia.

Ni wachache sana wasioogopa. Wasioogpa ni wale wanaokuja humu JF kwa majina yao na kutoa mawazo yao kinaga ubaga. Wengine tunaokuja na id za kujipachika ni waoga ytu.
Point mama. Umenena, wote humu ni kunguru tu. Ujasiri wetu unakomea pale majina yetu feki yanapoishia nyuma ya simu janja zetu.
 
Akizungumza kwenye kongamano la kuenzi falsafa ya hayati Magufuli ya tanzania ya viwanda, ndugu Shibuda amesema siku moja alipata nafasi ya kumtembelea rais Magufuli ikulu.

Anasema siku hiyo Magufuli alimkaribisha ikulu na kumuuliza vipi watoto hawajambo? Akajibu hawajambo akamwambia nataka kuchangia ada yao shilingi mil5

Shibuda akajibu asante lakini sijaridhishwa na namna unavyoendesha demokrasia katika utawala wako ndipo rais akasema sasa hata hiyo hela sikupi.

Kwa nini Shibuda hakuyasema haya Magufuli akiwa hai?
Ayaseme hayo Magufuli akiwa madarakani, kwani hajipendi?.Mwandosya aliwahi kumkosoa , akamvua u Vice Chancellor MUST na Chuo cha Mwalimu Nyerere.
 
Magufuli alikuwa mtu wa matani Sana kwa wale tuliyemzoea haitupi shida, tatizo linakuja kwa wale ambao siyo waelewa ukutute Rais alimtania yeye akayaweka moyoni hapa ndipo wabongo tunafail

Note; Kuna watu hawataniwi yaani kitu kidogo wanakikuza ila nimejifunza usiweke matani penye userios ila weka matani penye matani over
Kwani kuna tabu gani mkinyoosha kuwa alikua na roho mbaya mpaka mjifiche kwenye kivuli cha utani huku wenzenu wanaumizwa?
 
Back
Top Bottom