DOKEZO Shule ya Precious Pre, Primary and Secondary Goba ifanyiwe uchuguzi, kuna mambo yanaendelea si afya kwa watoto

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hii tabia ni karibu shule zote za dar zimejitungia utaratibu wa kumlazimisha mzazi amweke mwanae boarding anapofika darasa la nne.Kikubwa ni kuwakatalia tu.Ikiwezekana waziri wa elimu atoe mwongozo wa kuzuia huu uhuni maana mtoto wa darasa la nne anakuwa Bado mdogo sana .
 
Kiongozi mtoe boarding tu aende day gharamikia usafiri wa kwenda na kurudi atateseka ulisema umuamishe shule hazipokei watoto darasa la mitihan saiv washaanza sajiliwa bila ivyo mwanao atateseka tu
 
Mhamishe!
 
Kabisa mkuu. Huyu mzazi ni katili na anakimbia majukumu ya kumlea mtoto ktk umei ambao anatakiwa kuwa beneti na mzazi. Std4??? Huyo mtoto anatakiwa awe anatokea nyumbani kwa level hiyo.
Mtoto anapitia unyanyasaji na kutokuoga wiki 2 na joto lote hili la dar! Mzazi amekaa nyumbani anajua mtoto anasoma, hii ni huzuni kuu! Enyi wazazi mnaosomesha watoto kwenye hivi vi English medium, mtapelekeshwa na hao wamiliki wa hivyo vishule mpk lini? Kwa nn mmekuwa kama misukule kila kitu nyie ni kuitikia na kutekeleza bila kuhoji? ACHENI UNDEZI.! MNATESA WATOTO BILA SABABU ZA MSINGI...KWA ELIMU GANI SASA HAPO? HIYO GRADE 4 NDIO YA KUTESA WATOTO HIVYO?
 
Wait....mtoto wa grade 4 unamuweka boarding?

Am sorry kam aswali langu ni kali, mimi nimehamisha mtoto shule fulani akiwa grade 7 kwa sababu wametulazimisha boarding, Principle yangu namba moja ni kwamba sitopeleka mtoto boarding mpaka amalize form 4

By the way pole sana, mtoto wa grade 4 bado ni mdogo sana anahitaji uangalizi wa karibu wa mzazi na muongozo, usikwepe jukumu ndugu, toa mtoto boarding msimamie mwenyewe, huyo bado anahitaji malezi yako kwa karibu

Hizi shule zisitufante watumwa, pesa tunawalipa nyingi bafo wanatunyima haki ya kuwalea watoto

Trust me, usiamini katika malezi ya boarding, unaweza kukaa na mwanao nyumbani na bado akafauku kuliko wale wa boarding
 
Ila unajishangaza unavyolaumu shule, kwani ulifungwa kamba kupeleka mtoto boarding? Grade 4 unapeleka boarding? Huoni unamfanyia mtoto ukatili na kukwepa wajibu wako wa kumlea huyo mtoto?

Mambo mengine huwa tunayataka wenyewe, kaa chini jitafakari na uchukue jukumu la kumlea huyo mtoto, boarding itakurudishia mtoto mwenye malezi ambayo hayajatoka kwako wala kwa mama yake
 
Shida Iko kwa hawa wamiliki wa hivyo vishule, wamejitungia sheria zao wenyewe za kulazimisha watoto walio ktk madarasa ya mitihani kukaa boarding ilhali miundombinu yao ni hafifu na mibovu kuweza kuaccomodate hao watoto! Wazazi pia bila kutafakari athari wanazozipata watoto wanaitikia na kufuata kama misukule!
 
Hili jambo limenikwaza sana maana mwanangu yuko grade 4 na tayari nimeshaskia fununu kuna utaratibu wa shule kulazimisha watoto wakae boarding kipindi cha likizo...najiandaa kupambana nao vikali.
 
Wazazi WA dar ni viazi mno.hivi mikoani kuna hizi Sheria?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…