Kuna ukweli hapo kwenye watoto kuwa 'soft'
Mimi nimesoma hizo shule kwanzia primary mpaka sekondari, kiufupi kuna mtazamo flani tunakua nao, unakua hujazoea shida, unakua mlalamikaji sana, unaona maisha ni marahisi.....
Ni tatizo kwa kweli mimi mwenyewe najaribu kujibadilisha baada ya kufika chuo na kuanza kuona uhalisia wa maisha....
vitu vidogo vidogo kama kupika, kubudget hela vinatushinda kwa kweli.....
Ni vyema mtoto apitie ugumu kidogo ila awe 'flexible' kwenye maisha, kudekezwa raha ila unachelewa kukua....
Haya ni maoni yangu tu....
Kuna kitu mnashindwa kukielewa huo usoft wa mtoto mnaosema au kuona maisha rahisi au kuona kuwa yeye ana anapaswa kuwa na priviledge kuliko wengine anakuwa mlalamikaji sana belive me msingi wake sio shule
Mentality ya mzaz wa kitanzania alielewa kwenye shida au maisha ya kawaida ambaye ana uchu wa Maisha bora akija kuyapata utasikia mie nimeishi kwa shida sitak mwanangu apate shida mtoto au watoto wanageuzwa mboni za jicho haguswi na anapewa na kufanyiwa kila kitu..
Mwisho wa siku ndo ukubwan anapata shida huko kwenye mashule ya private sababu huo mfumo wa kulea watoto kama mboni za jicho upo nao wanaoanzisha hizo shule wanajaribu kuwaridhisha wazaz ili wapate ada
Ila amini nakwambia shule bora kabisa ya maisha kwa mwanao inaanzia kwenye malez yako.. kutokana na utakavyomlea ndio kutamfanya awe group leader ama
Follower.. hata huko kwenye hizo shule za soft utaona kuna watoto wana influence tabia kwa watoto wengine maana yake malez ya huyo mtoto yanakwenda kuathiri watoto wengine mashulen iwe in posotive au negative way so kama mtoto wako utamlea kuwa independent automaticaly yeye ndo atainfluence tabia kwa wengine hata copy za wengine
Mwisho kwenye jamii zetu za ngozi nyeusi circle ya maisha iko hv... babu kama alitaabika ujanan baba yako atajua kupambana na maisha na atatoboa ww utaishi maisha ya usoft maana maisha bora umeyarithi mwanao ataishi maisha ya tabu baada ya kutapanya mali maana hukumfundisha kuwa mpambanaji sababu ww hukufundishwa so matokeo yake mjukuu wako ataanzia moja kwenye maisha kama
Babu yako ..
kwa kifupi kwa alieshi maisha ya tabu akitoboa mali zake zitadumu kwenye generation zake mbili tu si zaid ya hapo sababu tunawalea vizaz vyetu kama Mboni.. mwisho wanashindwa kujimudu..
Huoni wazungu na watu wa asia kampuni
Ilianzishwa 30 years ago bado ipo mikonon mwa Familia
Kwa wabongo utakura historia babu yako au baba alikuwa anamiliki kampun x au biashara x