Shura ya Maimamu Tanzania: Mlinzi Mwanamume wa Rais kuvaa Hijabu na kuingia Msikitini

Shura ya Maimamu Tanzania: Mlinzi Mwanamume wa Rais kuvaa Hijabu na kuingia Msikitini

Maana bila andiko (surah) wakija BAKWATA wakasema PSU walikuwa sahihi kuingiza mwanaume msikitini, hapo utazuka utata.

Ili kusiwe na utata ni lazima mtizamo wa kuunga mkono ama kupinga ujengwe juu ya Quran tukufu ama hadithi inayokubalika kwa wote.
Na wewe uwe unaelewa

Shura ya Maimamu hajasema Qur'an imekataza Wanaume na Wanawake kukaa pamoja bali tatizo ni kukaa kwa kificho ambako unaweza kuwachungulia maungoni bila Wao kujua
 
Bismillahir Rahmanir Rahiim

SHURA YA MAIMAMU TANZANIA

KAMATI YA MAADILI

WARAKA WA WAZI KWA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI

JUNI 18, 2024.

‘MLINZI MWANAMUME WA RAIS KUVAA HIJABU NA KUINGIA MSIKITINI’

Shura ya Maimamu imeona malumbano yanayoendelea katika Mitandao ya Kijamii kuhusiana na picha inayomuonesha mtu anayekisiwa kuwa ni mwanamume akiwa amevaa mavazi ya kike ya Kiislamu.

Picha hiyo inamuonesha mtu huyo akiwa pamoja na wanawake wa Kiislamu akiwa nyuma ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Msikitini

Picha hiyo inasemekana ilichukuliwa katika Swala ya Idd Adh-Ha iliyo swaliwa juamatatu Juni 17, 2024, katika Msikiti wa Mikocheni (kwa Warioba), jijini Dar es Salaam.

Katika malumbano hayo inaelezwa kuwa mtu huyo ni miongoni mwa timu ya walinzi wa mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na alikuwa Msikitini hapo kikazi.

MAKOSA MAKUBWA

Shura ya Maimamu imo katika juhudi ya kupata hakika ya mtu huyo kama ni sehemu ya ulinzi wa Rais Samia Suluhu Hassan au laa. Hata hivyo ikiwa tukio kama hilo litaihusisha serikali yoyote ile tunasema ifuatavyo:

Ifahamike kuwa Wanawake wa Kiislamu huvaa mavazi ya stara kusitiri aura zao mbele ya wanaume wasio waume zao.
Lakini wanapokuwa sehemu ya wanawake Msikitini huwa huru kupunguza stara zao kwa kuamini kuwa hakuna mwanamume atakaye waumbua.

Kwa hiyo mwanamume kuingia sehemu hiyo tena kwa kificho, ni kudhamiria kuwaona utupu wanawake hao wachamungu wenye tabia ya kujistiri. Na hiicho ni kitendo kibaya cha kuwadhalilisha na kuwafedhehesha wanawake wachamungu.

Vilevile Wanawake wa Kiislamu wanapo swali hujipanga katika safu peke yao mbali na wanamume. Kitendo cha kumuweka mwanamume miongoni mwao kisha wakagusana tena ndani ya swala kinaharibu swala zao.
Pia ni kutendo cha kukiuka sheria zinazolinda uhuru wao wa kuabudu. Kitendo hicho pia kinavunja utukufu na heshma ya nyumba takatifu ya Mwenyezi Mungu, Msikiti.

Turejee kusema iwapo mwanamume atajitanda kwa mavazi ya wanawake kisha akaingia Msikitini upande wa wanawake basi hicho ni kitendo kibaya kabisa kinachofedhehesha dini na hata usalama wa taifa.

Shura ya Maimamu inakemea vikali kitendo hicho kisifanywe na ikiwa kimefanywa mfanyaji, na walioidhinisha wanapaswa kuwaomba radhi Waislamu.

Iwapo wahusika hao ni Waislam, wanapaswa kutubu kwa Allah (SW) kwa kutothamini dini yao.

WITO KWA SERIKALI

Shura ya Maimamu inatoa wito kwa vyombo husika vya Dola Tanzania kutoa ufafanuzi iwapo ni kweli kwamba msafara wa Rais Samia Suluhu Hassan ulijumuisha mlinzi mwanamume aliyeingia Msikitini sehemu ya wanawake na kwamba alifanya hivyo akiwa amefichama kwa kuvaa hijab, vazi la stara la wanawake wa Kiislamu.

Shura inasisitiza kuwa ufafanuzi huo ni muhimu sana kupatikana kwa haraka kwa sababu zifuatazo:

1. Kuondoa taharuki miongoni mwa jamii, na hususan wanawake wa Kiislamu.

2. Ikiwa serika ya Tanzania imehusika, ni muhimu Umma ufahamishwe tukio hilo ni la mara ya kwanza au ndio utaratibu wa kiulinzi toka Rais mwanamke alipokuwa Makamu wa Rais na sasa Rais.

3. Umma ufahamishwe iwapo mlinzi huyo ni yeye pekee au wapo wengine wanaume wanaoingia na Rais Msikitini upande wa wanawake wakiwa wamevaa hijabu.

4. Umma ufahamu mlinzi huyo kuvaa hijabu na kuingia kwa kificho Msikitini kwa wanawake ni utashi wake au ni utaratibu wa kazi aliopangiwa.

5. Wananchi wana haki ya kupata ufafanuzi kwa serikali yao pindi linapotokea jambo lenye kutatiza katika jamii.

Katika kuhitimisha, Shura ya Maimamu inarejea wito wake kwa kuhimiza vyombo husika kitoa ufafanuzi wa suala hili kwa muktadha wa nukta tulizoainishwa hapo juu .

Imetolewa Dar es Salaam leo tarehe 18 mwezi wa 6 mwaka 2024.

USTADHI MUSTAFA M. ABEID
KATIBU KAMATI YA MAADILI
Takhbiiiirrrr
 
Na wewe uwe unaelewa

Shura ya Maimamu hajasema Qur'an imekataza Wanaume na Wanawake kukaa pamoja bali tatizo ni kukaa kwa kificho ambako unaweza kuwachungulia maungoni bila Wao kujua
Hakuna Aya kama hiyo inayokataza wanawake na wanaume kuswali pamoja bila kutenganishwa
 
Andiko...!??
Kabla ya kuitekeleza ibada ya swala miiongoni mwa mambo inakubidi ujue ni udhu. Kabla ya kujua udhu inakubidi ujue sharti zake. Na ukijua sharti zake inakubidi ujue sunna zake na fardhi zake.

Kwenye Fiqh mlango wa udhu kuna mlango unazungumzia "nawaaqidhul udhui" kwa maana vitenguzi vya udhu/vinavyotengua udhu. Kutengua kwa maana unafanya udhu wako unakuwa tena si halal kwako. Kwa maana hiyo hutoweza kutekeleza ibada ya swala.

Bakwata ni madh-heb ya Shafii.
Kwenye Fiqh madh-heb ya Shafii miongoni mwa vitu au mambo yanayotengua udhu ni kugusana kwa ngozi baina ya mwanaume na mwanamke. Zikigusana ngozi imma za mikono au miguu kwa sababu kwenye uislam mkiswali ni lazima mpange swafu (mstari) na vidole vya miguu vitakutana na kwa kufanya hivyo ngozi zenu zinagusana.

Kwa mujibu wa madh-heb ya Imam Shafii hapo unakuwa hauna udhu. Kama hauna udhu hauna swala. Kwa mantiki hiyo haifai mwanamke na mwanaume kuswali pamoja.

Swali; kama huyo mlinzi ni mwanaume kwa nini kaenda kuwaharibia watu swala zao? Ina maana anafanya mchezo?

Kingine uislam unaheshimu faragha za jinsia mbili tofauti na ndiyo maana wanaume wana sehemu yao na wanawake wana sehemu yao. Ikiwa kama huyo ni mwanaume kivipi anaingilia eneo la wanawake wenye faragha yao?
 
Kabla ya kuitekeleza ibada ya swala miiongoni mwa mambo inakubidi ujue ni udhu. Kabla ya kujua udhu inakubidi ujue sharti zake. Na ukijua sharti zake inakubidi ujue sunna zake na fardhi zake.

Kwenye Fiqh mlango wa udhu kuna mlango unazungumzia "nawaaqidhul udhui" kwa maana vitenguzi vya udhu/vinavyotengua udhu. Kutengua kwa maana unafanya udhu wako unakuwa tena si halal kwako. Kwa maana hiyo hutoweza kutekeleza ibada ya swala.

Bakwata ni madh-heb ya Shafii.
Kwenye Fiqh madh-heb ya Shafii miongoni mwa vitu au mambo yanayotengua udhu ni kugusana kwa ngozi baina ya mwanaume na mwanamke. Zikigusana ngozi imma za mikono au miguu kwa sababu kwenye uislam mkiswali ni lazima mpange swafu (mstari) na vidole vya miguu vitakutana na kwa kufanya hivyo ngozi zenu zinagusana.

Kwa mujibu wa madh-heb ya Imam Shafii hapo unakuwa hauna udhu. Kama hauna udhu hauna swala. Kwa mantiki hiyo haifai mwanamke na mwanaume kuswali pamoja.

Swali; kama huyo mlinzi ni mwanaume kwa nini kaenda kuwaharibia watu swala zao? Ina maana anafanya mchezo?
Acha porojo weka aya
 
Bismillahir Rahmanir Rahiim

SHURA YA MAIMAMU TANZANIA

KAMATI YA MAADILI

WARAKA WA WAZI KWA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI

JUNI 18, 2024.

‘MLINZI MWANAMUME WA RAIS KUVAA HIJABU NA KUINGIA MSIKITINI’

Shura ya Maimamu imeona malumbano yanayoendelea katika Mitandao ya Kijamii kuhusiana na picha inayomuonesha mtu anayekisiwa kuwa ni mwanamume akiwa amevaa mavazi ya kike ya Kiislamu.

Picha hiyo inamuonesha mtu huyo akiwa pamoja na wanawake wa Kiislamu akiwa nyuma ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Msikitini

Picha hiyo inasemekana ilichukuliwa katika Swala ya Idd Adh-Ha iliyo swaliwa juamatatu Juni 17, 2024, katika Msikiti wa Mikocheni (kwa Warioba), jijini Dar es Salaam.

Katika malumbano hayo inaelezwa kuwa mtu huyo ni miongoni mwa timu ya walinzi wa mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na alikuwa Msikitini hapo kikazi.

MAKOSA MAKUBWA

Shura ya Maimamu imo katika juhudi ya kupata hakika ya mtu huyo kama ni sehemu ya ulinzi wa Rais Samia Suluhu Hassan au laa. Hata hivyo ikiwa tukio kama hilo litaihusisha serikali yoyote ile tunasema ifuatavyo:

Ifahamike kuwa Wanawake wa Kiislamu huvaa mavazi ya stara kusitiri aura zao mbele ya wanaume wasio waume zao.
Lakini wanapokuwa sehemu ya wanawake Msikitini huwa huru kupunguza stara zao kwa kuamini kuwa hakuna mwanamume atakaye waumbua.

Kwa hiyo mwanamume kuingia sehemu hiyo tena kwa kificho, ni kudhamiria kuwaona utupu wanawake hao wachamungu wenye tabia ya kujistiri. Na hiicho ni kitendo kibaya cha kuwadhalilisha na kuwafedhehesha wanawake wachamungu.

Vilevile Wanawake wa Kiislamu wanapo swali hujipanga katika safu peke yao mbali na wanamume. Kitendo cha kumuweka mwanamume miongoni mwao kisha wakagusana tena ndani ya swala kinaharibu swala zao.
Pia ni kutendo cha kukiuka sheria zinazolinda uhuru wao wa kuabudu. Kitendo hicho pia kinavunja utukufu na heshma ya nyumba takatifu ya Mwenyezi Mungu, Msikiti.

Turejee kusema iwapo mwanamume atajitanda kwa mavazi ya wanawake kisha akaingia Msikitini upande wa wanawake basi hicho ni kitendo kibaya kabisa kinachofedhehesha dini na hata usalama wa taifa.

Shura ya Maimamu inakemea vikali kitendo hicho kisifanywe na ikiwa kimefanywa mfanyaji, na walioidhinisha wanapaswa kuwaomba radhi Waislamu.

Iwapo wahusika hao ni Waislam, wanapaswa kutubu kwa Allah (SW) kwa kutothamini dini yao.

WITO KWA SERIKALI

Shura ya Maimamu inatoa wito kwa vyombo husika vya Dola Tanzania kutoa ufafanuzi iwapo ni kweli kwamba msafara wa Rais Samia Suluhu Hassan ulijumuisha mlinzi mwanamume aliyeingia Msikitini sehemu ya wanawake na kwamba alifanya hivyo akiwa amefichama kwa kuvaa hijab, vazi la stara la wanawake wa Kiislamu.

Shura inasisitiza kuwa ufafanuzi huo ni muhimu sana kupatikana kwa haraka kwa sababu zifuatazo:

1. Kuondoa taharuki miongoni mwa jamii, na hususan wanawake wa Kiislamu.

2. Ikiwa serika ya Tanzania imehusika, ni muhimu Umma ufahamishwe tukio hilo ni la mara ya kwanza au ndio utaratibu wa kiulinzi toka Rais mwanamke alipokuwa Makamu wa Rais na sasa Rais.

3. Umma ufahamishwe iwapo mlinzi huyo ni yeye pekee au wapo wengine wanaume wanaoingia na Rais Msikitini upande wa wanawake wakiwa wamevaa hijabu.

4. Umma ufahamu mlinzi huyo kuvaa hijabu na kuingia kwa kificho Msikitini kwa wanawake ni utashi wake au ni utaratibu wa kazi aliopangiwa.

5. Wananchi wana haki ya kupata ufafanuzi kwa serikali yao pindi linapotokea jambo lenye kutatiza katika jamii.

Katika kuhitimisha, Shura ya Maimamu inarejea wito wake kwa kuhimiza vyombo husika kitoa ufafanuzi wa suala hili kwa muktadha wa nukta tulizoainishwa hapo juu .

Imetolewa Dar es Salaam leo tarehe 18 mwezi wa 6 mwaka 2024.

USTADHI MUSTAFA M. ABEID
KATIBU KAMATI YA MAADILI
Akili imetumika ya hali ya juu sana kutoa ujumbe! Maadili lazima yazingatiwe na hakuna uchawa hapo! Hongereni sana!
 
Maana bila andiko (surah) wakija BAKWATA wakasema PSU walikuwa sahihi kuingiza mwanaume msikitini, hapo utazuka utata.

Ili kusiwe na utata ni lazima mtizamo wa kuunga mkono ama kupinga ujengwe juu ya Quran tukufu ama hadithi inayokubalika kwa wote.
Yapo mambo Aya za Qur'an zipo na hadithi zipo ila bado yana utata, na yapo mambo hayana utata wote wanakubaliana. Hili la mwanaume kujichanganya katikati ya wanawake na kuvaa mavazi ya kike hata kwa akili tu ya kawaida ni jambo ambalo halipo sawa.
 
Nimetafuta kama kuna andiko limewekwa linalokataza wanaume kuswali na wanawake sijaona.

Wangeweka hilo andiko bila ya shaka lingeongezea uzito wa habari yenyewe
Kwani Papa aliporuhusu mashoga kubarikiwa vatican aliweka andiko?

Wewe hujui kua wanawake hawachanganyiki na wanaume kwenye misikiti?

Kwahiyo hao watu wa ulinzi wameingia kwa wanawake coz hawajui hilo andiko? Ingekua hawajui kua wanawake hawachanganyiki na wanaume,wasingejificha kwa kuvaa hijabu.
 
Mimi binafsi siyo muislam ila niseme tu kuwa ikiwa kitendo hicho kimefanyika basi ni makosa makubwa mno yaliyofanywa na waliompangia kazi huyo jamaa na hata kumshauri avae nguo za kike.

Huo ni udhalilishaji kwa akina mama wachaMungu walioingia Msikitini kusali.

Kitendo hiko kitapotezewa kwa kuwa tu Rais ni Muislam ila angekuwa Mkristo, sipati picha ingekuaje.

Ikiwa ni kweli basi serikali iwaombe radhi waislamu wote na watu wachukue tahadhari ili watu wasiendelee kujificha kwa mavazi hayo ambayo hayamtambulisha mtu.
 
Back
Top Bottom